Ninahisi mpenzi wangu ana mwanaume mwingine

Ninahisi mpenzi wangu ana mwanaume mwingine

Sawa inawezekana nina makosa ... lakini kwao nilishaenda na nikajitambulisha... yote kwa yote sioni kwamba alichochagua ni sahihi

Wewe kama unampenda mke wako mpiganie. Kumbuka kizuri unachokiona kwake wanakiona wengi
Tuma mshenga, lipa mahari, funga ndoa
 
Mimi Sisyphus leo, nimeliona joto la jiwe ... mtu nilimuamini ameanza rasmi kuonyesha MAKUCHA yake ... ni miaka minne sasa niko na huyo mwanamke, ni muda mrefu sasa mwenzangu alikua anaomba ndoa mara nyingi sana..nimejaribu kumuelewesha asubiri tujipange kwanza (na najipanga kweli sio uhuni) .. maana tushamleta na mtu duniani, naona sasa muda wa uvimilivu wake umaenza kufika kikomo ....

Story inaanzia kati, leo alienda kutafuta chumba mana kuna short course alikua anataka kusomea kwahiyi ikambidi akatafute chumba sasa amefika dalali akamwambia asubiri mama mwenye nyumba arudi kwahiyo itambidi akae masaa matatu kumsubiri... akanipa taarifa mimi nikaona hakuna logic ya kumsubirisha mana anakoishi(siishinae) amecha mtoto ( 1.9 year) basi bwana nikampigia dalali , dalali akaanza kuropoka “ ooh bro msiondoke mana mkiondoka hiki chumba mtakikosa” ... la haula ikabidi ni muulize nisiondoke na nani, akajibu “ we si yule jamaa mumewe ambae uko nae” bila kufikiri mara mbili nikajibu hapana mimi ni mumewe ila sipo huko.

Dalali akaanza kuuma uma maneno mwisho akasema aaah basi ngoja kidogo nitaku-check ... nikamuambia embu subiri nipe maelezo kidogo huyo mwanamama amekuja na nani? ... kwa sababu alishaanza ikabidi aseme amekuja na jamaa akamtambulisha ni mumewe ( mimi nilipo ikabidi nikae chini kwanza ) ... lakini dalali akaendelea itakua basi boda... nikamwambia sawa fatilia hilo swala la mama mwenye nyumba kwanza.

Nikatulia kwanza alafu nikamtafuta vipi mwenzangu leo umeenda na nani? Mara ooh sijaenda na mtu mara oohh ni boda ndiye niliyemtambulisha mume wangu ... kwa kifupi taarifa aliyonipa dalali ni kwamba walienda wawili na aliwaacha wawili ukiacha boda.
Ikanibidi nimuulize vizuri boda ndio unamtambulisha mumeo ,? ( ...ghafla akaanza ule mchezo wao anakurudishia maswali kwani wewe huniamiani blah blah).

Baada ya haya ikabidi nianze ku-analyse wapi nilikosa umakini mpka nikashindwa kuona hili kwa hupitia uwezo wa roho mt. nikaanza kuona vingi nilivyokua sitilii maananini kwanza AMEACHA KUSISITIZIA NDOA , pili amepunguza wivu na anakaribia kuacha kabisa , tatu amekua na majibu ya mkato na kujifanya anajiamini( now days ana-vihela mana kuna-business nilimpa akaweza ku-make kwa kipindi kifupi).

Nne .. kuna mambo anayafanya mwenyewe mwenyewe na hua tunashirikishana kila kitu ila nimeanza kuona gap upande wa pili
NB: huyu mwana-mama nimefanya nae vitu vingi sana hata kipindi na mpiga tarehe anafaham hasa nini nilikua nafanya, nilivyofanya na naendelea kufanya . MAAZIMIO shetani amenijia na ujumbe wa kumpiga chini mapema maana nilivyokua nafanya nafanya kwa ajili yetu sote isingekua hivyo mi ningeenda zangu SHULE KITAAMBO nikabukue zangu masters ya masimulizi...

WAJAMENI ...nipeni ushauri mana shetani ananizonga na mawazo yake... ni chukue hatua gani easy way , hard way Au mixing
Narudi kusoma ili nijue tunaanzia wapi kukupa adhabu
 
Mwenzio atakua anakujua vizuri sana kakuona hueleweki.

Kwani kufunga ndoa sh ngapi? Vile vyeti vya ndoa vinalipiwa sh ngapi? Au wewe unataka kufanya karamu ya taifa??

Tena usikute unaishi na mtoto wa watu kihuni wala kwao hujaenda kwa kufuata taratibu halafu unamshikilia tuu muda unaenda kwa ahadi za subiri

Huyo nae ni binadamu na kama ametafuta mtu mwingine umeyataka mwenyewe
Baada ya kusoma comments roughly nimegundua wanawake wote waliochangia huu uzi wana side na mwanamke mwenzao.

So tatizo la huyu chali linaweza likawa ni tatizo la wengi katika jamii.
 
Ulifanya vibaya Sana mpka ukapata jina la kijana wa hovyo kabisa

Ni lazima ujiandae ndiyo uoe siyo utafute mwanamke harafu ndiyo ujiandae.


Anataka ndoa na mimba hiyo alipata kama mtego na yawezekana siyo wako , huyu mtoto anaweza kuw na Kadi tatu za kliniki moja ya jina lako mbili za majina ya Baba wengine .

Maana yeye anahitaji ndoa si mbali Sana anaweza kuolewa na mwanamme mwingine atakayekuwa tayari hata kama utamtema , kumbe naye ashakutema hapo ndo unajua Ngoma draw.
 
Baada ya kusoma comments roughly nimegundua wanawake wote waliochangia huu uzi wana side na mwanamke mwenzao.

So tatizo la huyu chali linaweza likawa ni tatizo la wengi katika jamii.

Mwanaume aspofanya mambo yake sawa anaweza zalisha shida nyingi sanaaaa
 
Ila mara nyingi ,mwanaume akishamzalisha mwanamke, huamini huyo mwanamke hana ujanja wa kupata mwingize zaidi yake yy, na kuamini kwamba mwanamke sokonlake ndo linakuwa limeishia hapo, kumbe ndivyosivyo.
Wanawake mnajitahidi kuteteana kwenye huu uzi
 
Kaa na mwenzio muyazungumze ,umepaniki mapema sana .Hakuna mahusiano yasiyo na changamoto na ukiona yamedumu ujue kuna mmoja amekubali kuwa chini .


Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
mimi naona maisha ya mahusiano hayana formular.. yaan mambo taflan
 
Wanaume tu wabinasfi sana:

1. Miaka 4 ya mahusiano.
2. Umemzalisha - anaweza asiwe wako.
3. Amedai ndoa sana.
4. Ameenda tafuta chumba mwenyewe!

Yeye mwanamke angoja tu utakuja muoa? Kweli? Kweli? Hana kosa huyo mwanamke hata Kama analiwa!
Sasa huyo aliekuwa naye ndiyo atamuoa? Aliemtambulisha una hakika atamuoa
 
Back
Top Bottom