Nini chanzo cha ugomvi wa January Makamba na Musukuma?

Nini chanzo cha ugomvi wa January Makamba na Musukuma?

Kwa aliyefatilia kikao cha Jana cha Bunge atakuwa amepata picha kile ninachojaribu kuelezea hapa.

Musukuma anamtupitia mashambulizi makali Mh Makamba kwa kutoa ushahidi wa kile alichokuwa anakiona wakati akiwa mjumbe wa kamati ya nishati kwa miaka 6 sasa.

Na Makamba anajibu mashambulizii kisomi na kitaalamu zaidi lakini mwisho wa majibu yake anamwambia Musukuma

"Kama una shida na uwaziri, sema mengine ila kama shida ni ukatikaji wa umeme ilo sio tatizo langu."

Kwa kauli ya Makamba na Musukuma inaonesha hawa watu hawako kwenye good term Liko jambo linafukuta kati ya watu hawa wawili.

Ikumbukwe Makamba ni Waziri kwa miezi minne tu, ila Musukuma ni mjumbe wa kamati kwa miaka 6, kwanini anayoelezea Makamba kamati haiyajui? Au ni makusudi ya wasukuma kujiziba masikio?

Au ni chuki maana nasikia Makamba hatoi bahasha kwa wajumbe wa kamati wakija. Kumtembelea?

Musukuma anasema Makamba anapanda Elikopita kukagua mabwawa wakati yeye anaendaga na baiskeli.

Nini kinaendelea kati ya Musukuma na Makamba?
Ikumbukwe tu, Musukuma ni PhD holder, msiulizeulize
 
Sijaona kasoro kwenye maswali ya msukuma!
Amekaa kwenye kamati ya Nishati kwa miaka 6 anasema tangia project haijaanza kamati ilikuwa inafika mpaka inaanza walikuwa wanaenda na wlaikuwa wanaona kabisa kitu kinafanyika na mkandarasi hadai certficate mkandarasi anadai mpaka sasa, ila ujenzi hauonekani ukisonga shida nini? Waziri mwanzo alisema hakuna crane yakubeba tani 26 sawa crane imefika zinatolewa sababu nyingine kuwa yale mahandaki yalijengwa substandard ndiyo msukuma anahoji wasomi wenzake vipi mbona mnamuangusha?

Swali jingine ni kukatika kwa umeme, kwa mujibu wa kwenye kamati hawakuona sababu yoyote ya msingi ya kukatika kwa umeme ovyo, na waliiomba Tanesco ilete taarifa ambayo inaonesha huko nyuma miaka mi5 walikuwa wanatumia mbinu gani kufanya umeme usikatike ovyo huku wakifanya maintenance tofuti na sasa? Maana tulibiwa sababu mitambo haikufanyiwa maintanance sababu watu waliogopa kutumbuliwa, mara tukaambuwa mabwawa yamekauka na Waziri kachukua mpaka Herkopta mpaka Mtera pale ila mkurugenzi wa lile bwawa akatoa ukweli kuwa mpk miezi saba mbele wanaweza kuzalisha megawati 80 kama kawaida ata mvua isiponyesha ila mvua zimenyesha baada ya Chief Hangaya kuomba mvua, wakaja maintenance ya siku 10 sawa ila bado kuna tatizo la kukatika kwa umeme ovyo! Shida nni?

Ndo maswlai yasukuma hayo wala hajamlenga mtu kuwa anataka Uwaziri
Halafu kuna mtu anasema eti Msukuma ni mfitini; si wajibu hayo maswali? Hapa mbona wala halingwi mtu, kuna issue hapa, ijibiwe issue wala sio mtu. January ajibu maswali ya Msukuma, baaasi
 
Ulivyoandika tu kwa mtu ambae ana akili kidogo tu anajua uko biased tayari . Unamtetea makamba, toka awe waziri umeme ni kukatika tu ana faida gani?, pia anaonekana wazi kuhujumu bwawa la Nyerere kwa visingizo visivyokuwa na maana yoyote...hamna waziri hapo zaidi ya hisani.
Nailed; ukweli watu wanamtetea tu jamaa but ukweli kachemka mbaya kwenye UMEME, mbayazaidi Magufuli aliisha twambia kwamba kwenye umeme, wahuni walikua wakifanya yao, tunao sasa na bado watu wana ujasiri kabisa wa kutetea jambo hili. Kalemani alivyotolewa tu, hata mwezi haukuisha, mgao wa umeme ukaanza, till todate bado umeme sio stable. Sasa hata hili watu wanataka kumtetea mtu kwa maslahi ya nani!?
 
Kwa aliyefatilia kikao cha Jana cha Bunge atakuwa amepata picha kile ninachojaribu kuelezea hapa.

Musukuma anamtupitia mashambulizi makali Mh Makamba kwa kutoa ushahidi wa kile alichokuwa anakiona wakati akiwa mjumbe wa kamati ya nishati kwa miaka 6 sasa.

Na Makamba anajibu mashambulizii kisomi na kitaalamu zaidi lakini mwisho wa majibu yake anamwambia Musukuma

"Kama una shida na uwaziri, sema mengine ila kama shida ni ukatikaji wa umeme ilo sio tatizo langu."

Kwa kauli ya Makamba na Musukuma inaonesha hawa watu hawako kwenye good term Liko jambo linafukuta kati ya watu hawa wawili.

Ikumbukwe Makamba ni Waziri kwa miezi minne tu, ila Musukuma ni mjumbe wa kamati kwa miaka 6, kwanini anayoelezea Makamba kamati haiyajui? Au ni makusudi ya wasukuma kujiziba masikio?

Au ni chuki maana nasikia Makamba hatoi bahasha kwa wajumbe wa kamati wakija. Kumtembelea?

Musukuma anasema Makamba anapanda Elikopita kukagua mabwawa wakati yeye anaendaga na baiskeli.

Nini kinaendelea kati ya Musukuma na Makamba?
Mtu akisoma ulichoandika, anajua upande wako.
 
January Makamba ni another seti tupu ilioko kwenye system.. huyu na huyo mwingine aliesema aliekatwa makato kwenye simu ampelekee . yaani ma zero fulani hivi yapo kwenye uongozi kwa hisani ya msoga, ila kuna siku kitawaka: wafurahie uongozi kwa sasa. Makamba majibu aliojibu bungeni ni ya kisanii sana ila kwa wapumbavu ndio wanaweza sema kajibu kitu. Cheap politics kwenye mambo ya maana shenzi sana hawa akina kigogo2014 dawa yao iko jikoni.
 
Mkitumaliza sisi, mtaanza kumalizana wenyewe kwa wenyewe, nukuu ya Godbles Lema
 
Shida ya watu katika Tanzania yetu ni akili Huyo msukuma hata kama anaongea pumba katika kuhoji suala la umeme kukatikakatika hovyo anaweza akawa na akili zaidi kuliko Elimu,hivi waziri asiye na akili ila ana Elimu anaweza kusaidia nn kwenye wizara nyeti kama hii.waziri anatakiwa awe na akili kwanza alafu awe na Elimu,akiwa hivyo ataweza kusaidia sana kuitoa wizara hapa ilipo na kuipeleka kwenye hatua kubwa zaidi.Tunapaswa kujua kwamba Hii wizara imepata waziri mpuuzi ambae haelewi nn anatakiwa kufanya na hii yote inatokana na kuwa na Elimu alafu akili HAKUNA sasa hapo huwa lazima haya tunayoyashuhudia yatokee.NCHI INAHITAJI WAZIRI MWENYE VITU VYOTE VIWILI YAANI AKILI NA ELIMU,SASA MAKAMBA HANA KIMOJA YAANI AKILI NDIO MAANA NCHI INAJIKUTA KWENYE MKWAMO WA MGAO MKUBWA WA UMEME.
 
Kwa kifupi kabisa huyu mtu anaitwa Musukuma ni mtu wa hovyo sana na mpenda fitina za kijinga. Ameumiza watu wengi kwa fitina zake za hovyo. Naamini watawala wameelewa uhuni wake. Niishie hapo, inatosha.
Muombe radhi Dr.Musukuma kwa hichi ulichokiandika.
 
Wewe unataka kumtetea Makamba inaonekana.

Ni nani anafurahia utendaji wa Makamba? Utendaji ni kukata umeme kwa visingizio lukuki? Walisema maji, Mungu si Athumani, akaleta mvua. Sasa ndio wakaja na visingizio vya maintanance.

Anataka apewe miaka 4 kama vile ndio tumepata uhuru? Kwanini anataka kukata connection ya regime hii na nyingine?
Serikali haikatiki.

Halafu anadhani kila mtu anapenda madaraka kama yeye. Akiulizwa wajibu wake, anakimbilia kwenye madaraka.
Awajibu. Hakuna wa kudumu kwenye siasa.

Hakuna mwenye hati miliki ya uongozi. Uongozi ni dhamana.

Labda hujaelewa majibu ya Makamba...

Hoja yako na ya Msukuma ni kuhusu kukatikakatika kwa umeme...

Majibu ya Makamba ni kuwa, kama mashambulizi hayo yote ni kwa sababu ya kukatikatika kwa umeme, HILO SIYO TATIZO LAKE...

Binafsi nayaita "mashambulizi" kwa sababu, ukimsikiliza mbunge Msukuma vyema, utatambua mara moja kuwa haulizi kwa nia ya kutaka suluhu ya ishu ya umeme bali lengo lake ni beyond that, likely kutaka ku - undermine integrity ya Waziri Makamba. Watu wa namna hii huwa hawakubali wala kuridhishwa na jibu lolote unless nia yako imetimia. That's how Msukuma is...!

Mimi nadhani Msukuma angemuuliza tu waziri kuwa, kama siyo tatizo lake basi litakuwa tatizo la nani, then from there kama watu wwnye nia ya kuifikia suluhu wajadiliane na kuokoa wananchi na adha hii...?

By the way, kwani ni lini ishu ya umeme wa Tanzania iliwahi kuwa reliable & stable...?

Tatizo la umeme Tanzania ni ni sugu na ni la tangu Uhuru mpaka kesho. Siku zote CCM na serikali yao wamekuwa na short term solutions.

Magufuli hakuwahi kutatua kero ya umeme. Ni utamaduni uleule wa kutafuta suluhusho dogo na la muda mfupi...

And to be honest kabisa, Tatizo la umeme wa Tanzania siyo waziri January Makamba...

Tatizo la umeme wa Tanzania ni CCM na sera zake kuhusu nishati ya umeme kwa ujumla wake akiwemo yeye Kasheku Msukuma, Makamba, Samia na wengine wote...

Ni kuwa, CCM haiwezi kuleta suluhu ya umeme hapa Tanzania. Hawa walishashindwa, hawana mapya. Ni wanafiki na waongo tu...!

Suluhu ni CCM na Sera zake mbovu za nishati ya umeme kuondoka ama kufa kabisa ili kupisha watu wapya wenye mawazo mapya, mipango mipya na sera mpya zenye uelekeo mpya...!!
 
Back
Top Bottom