Nini kilibadili mfumo wangu wa maisha na kuanza kufanya mazoezi (Physical fitness)....

Hongera Sana mkuu. Wengine maisha yetu ni kusafiri kila week mpaka kuweka ratiba nzuri unashindwa.

Kwa mtu wa safari ukifika room ya hotel au lodge hakikisha japo push ups 50 hadi 100, then ruka ruka juu kama wamasai hata mara 50 , halafu fanya situps kama 20, halafu fanya pranks hata kwa dakika tatu humo humo chumbani utatoka jasho ni dakika kama 20 hivi lakini zina maana sana
 
nikipita goba na mbezi beach naona wanaofanya asubuh ni watu wenye kipato cha juu tu, masikini wengi maisha yetu ni mazoezi tosha.
Lakini pia wao ndio wahanga wakubwa wa magonjwa yasiyoambukiza.
 
Lakini pia wao ndio wahanga wakubwa wa magonjwa yasiyoambukiza.

Unamkubalia kua wafanya mazoezi wote duniani wana uwezo wa hali ya juu? Hapana tubase kwenye faida za mazoezi kwanza kuimarisha afya ya mwili, kuukinga mwili na maambukizi ya magonjwa, kuongeza kinga ya mwili, kupunguza au kuondoa kabisa msongo wa mawazo, lakini pia specifically kuimarisha utendaji kazi wa ubongo na kuukinga ubongo dhid ya maambukizi, lakini michezo au mazoezi hukupatia marafiki wengi zaidi. Kama una nia ya dhati hata chumbani unafanya mazoezi vizuri tu
 
Nadhani wameanzisha huu utaratibu kutokana na ukweli kuwa suala la Presha limekuwa underated ilhali ni Ugonjwa unaoshiriki kuua kwa kasi kubwa nowadays.. Na sababu kuu ni watu kutokuwa aware nao
 
Hawa ni madaktari wetu wa bongo..yaani ni full kumchamba mgonjwa...mi walinikutaga pressure imepanda hadi 240 ilikuwa balaa kabisa ....walikuja madokta kibao wametoa macho na kuanza kuuliza nani kanileta nikawaambia nimedrive mwenyewe...duh
 
Watakufukuza
 
Hawa ni madaktari wetu wa bongo..yaani ni full kumchamba mgonjwa...mi walinikutaga pressure imepanda hadi 240 ilikuwa balaa kabisa ....walikuja madokta kibao wametoa macho na kuanza kuuliza nani kanileta nikawaambia nimedrive mwenyewe...duh
Kama huna utulivu na ukiingiwa na hofu. Unapitiliza moja kwa moja. Wanaua sana wagonjwa wa Pressure kwa hofu na mishtuko (Heart attack). Mtu anakupiga zile picha zao sijui echo, sijui E.C.G na unaona na kusikia moyo wako unavyodunda then jamaa "anakuambia Sikia moyo wako unavyodunda kwa nguvu" yaani ni vitisho juu ya vitisho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…