Nini kilipelekea 1 Us dollar kubadilishwa kwa shilingi za kitanzania 7 mwaka 1960 mpaka shilingi 2600 mwaka 2024 ?

Nini kilipelekea 1 Us dollar kubadilishwa kwa shilingi za kitanzania 7 mwaka 1960 mpaka shilingi 2600 mwaka 2024 ?

Kwa hiyo ndiyo kusema Wachumi wote waliojazana serikalini wamekosa kabisa suluhu ya kuirejesha thamani ya shilingi yetu!! Yaani miaka inavyozidi kwenda na thamani nayo inazidi tu kushuka!!
Ni ngumu Sana kurekebisha hali Kama hiyo, ni suala mtambuka.
Je, Wananchi wenyewe kwanza wanazo akili (elimu) nzuri na zilizo stable sawa sawa katika kufanya Utafiti, Ugunduzi Mpya, Uvumbuzi na Bunifu mbali mbali zitakazosaidia katika kuzalisha bidhaa mbali mbali ambazo pia zitasaidia kuongeza Pato la fedha za kigeni hapa Tanzania????

Nguzo Kuu kabisa ya Uchumi wa nchi yoyote ile hutegemea zaidi na Ubora wa akili (elimu) walizonazo Wananchi wake katika nchi husika.
Kama Wananchi/Watu wengi katika nchi Wana AKILI NZURI Zaidi, basi upo uwezekano mkubwa sana wa nchi husika kuwa na Uchumi mkubwa, and vice versa is also true.
 
Kwa hiyo ndiyo kusema Wachumi wote waliojazana serikalini wamekosa kabisa suluhu ya kuirejesha thamani ya shilingi yetu!! Yaani miaka inavyozidi kwenda na thamani nayo inazidi tu kushuka!!
Mtaka cha uvunguni sharti ainame !
Ndivyo wanavyotaka wakubwa wa Dunia kwa sababu tuna shida na ni lazima tukope !

Mwalimu alikataa kugeuka jiwe akaamua ni bora akae pembeni !
 
Mtaka cha uvunguni sharti ainame !
Ndivyo wanavyotaka wakubwa wa Dunia kwa sababu tuna shida na ni lazima tukope !

Mwalimu alikataa kugeuka jiwe akaamua ni bora akae pembeni !

Alikataa kufuata IMF ili kutupiga changa la macho kwani nchi aliifilisi yeye kwa sera zake mbovu za uchumi na siasa yake ya Ujamaa wake usio mashiko
 
Jibu ni uongozi legelege wa mama.viwanda vyote vimekufa,Kila kitu tunaagiza nje kuanzia magari ya viongozi v8GXR Hadi chumvi.mahitaji ya dolla lazima yapande.wazawa wakitaka kuwekeza kama kujenga viwanda Kodi yake inakuwa ni nafuu uagize nje.hadi mama amalize muda wake Dola Moja itakuwa sana tsh 5000 maana kapokea 2021 ikiwa Dola Moja ni sawa na 2200 ndani ya miaka miwili tu imefika 2690
 
Karibuni wataalamu wa Siasa na Uchumi .
1960 - 1 US dollar ilikuwa shilingi 7 za kitanzania .

2024 -1 us dollar ni shilingi 2600 za kitanzania.

View attachment 3049955

Hapa inaelezwa thamani ya shilingi ya Zanzibar kwa kipindi hicho

View attachment 3049959
Source yako siyo sahihi. Mpaka mwaka 1979, shillingi ya Tanzania ilikuwa imebebeshwa kwenye pauni ya kiingereza ikiwa ni pauni moja kwa Sh 20, ambayo ilikuwa Sawa na dola moja kwa shillingi 5 siyo Sh 7 kama ulivyoandika. Neno dala dala lınatokana na nauli kuwa shillingi tano tano wakati huo
 
Alikataa kufuata IMF ili kutupiga changa la macho kwani nchi aliifilisi yeye kwa sera zake mbovu za uchumi na siasa yake ya Ujamaa wake usio mashiko
Ile vita ndio ilituletea shida zaidi ndipo mabeberu wakawa wamempata Mwalimu pale walipomtaka awepo !

Wakubwa wa magharibi walikuwa wanajua kama sera za Ujamaa zitapata mafanikio Nchi nyingi Africa zitafuata zile policy na wao mirija yao ya unyonyaji itakuwa imefikia mwisho wake !!

Baada ya ile vita wakajua sasa Mwalimu hana tena ujanja mwingine na ndipo wakashikilia hapo hapo, kwamba kama unataka mikopo shusha thamani ya pesa yenu !

Ujanja wetu ukaishia hapo 😳🙌
 
Karibuni wataalamu wa Siasa na Uchumi .
1960 - 1 US dollar ilikuwa shilingi 7 za kitanzania .

2024 -1 us dollar ni shilingi 2600 za kitanzania.

View attachment 3049955

Hapa inaelezwa thamani ya shilingi ya Zanzibar kwa kipindi hicho

View attachment 3049959
Kipindi hicho ndiyo tulikuwa na maisha magumu kuliko sasa kwa sababu hela yetu haikuwa na thamani sana ukilinganisha na dollar.

Ni kwa sababu purchasing power ya TZS 7/= mwaka 1960 kwa sasa inaweza kulingana na purchasing power ya shillingi laki saba (TZS 700,000/=)

Kwa hiyo ukiangalia kwa mtizamo huu, dola moja ya Marekani mwaka 1960 ilikuwa ni sawa na laki saba za hela ya sasa ya Tanzania
 
Ile vita ndio ilituletea shida zaidi ndipo mabeberu wakawa wamempata Mwalimu pale walipomtaka awepo !

Wakubwa wa magharibi walikuwa wanajua kama sera za Ujamaa zitapata mafanikio Nchi nyingi Africa zitafuata zile policy na wao mirija yao ya unyonyaji itakuwa imefikia mwisho wake !!

Baada ya ile vita wakajua sasa Mwalimu hana tena ujanja mwingine na ndipo wakashikilia hapo hapo, kwamba kama unataka mikopo shusha thamani ya pesa yenu !

Ujanja wetu ukaishia hapo 😳🙌
Vita ya mwaka 1979 siyo chanzo cha matatizo ya leo. Tatizo ni sera za tawalazilizofuatia baada ya hapo. Rwanda walipigana vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa muda mrefu na Kuuana wenyewe kwa wenyewe sana lakini mbona baada ya Vita hiyo uchumi wao ukawa stable wakati sisi bado Tunayumba tu.
 
Kipindi hicho ndiyo tulikuwa na maisha magumu kuliko sasa kwa sababu hela yetu haikuwa na thamani sana ukilinganisha na dollar.

Ni kwa sababu purchasing power ya TZS 7/= mwaka 1960 kwa sasa inaweza kulingana na purchasing power ya shillingi laki saba (TZS 700,000/=)

Kwa hiyo ukiangalia kwa mtizamo huu, dola moja ya Marekani mwaka 1960 ilikuwa ni sawa na laki saba za hela ya sasa ya Tanzania
Elaborate more please.
Naona kama kuna Conflicting Contradictions kwenye Maelezo yako
 
Source yako siyo sahihi. Mpaka mwaka 1979, shillingi ya Tanzania ilikuwa imebebeshwa kwenye pauni ya kiingereza ikiwa ni pauni moja kwa Sh 20, ambayo ilikuwa Sawa na dola moja kwa shillingi 5 siyo Sh 7 kama ulivyoandika. Neno dala dala lınatokana na nauli kuwa shillingi tano tano wakati huo
Kabisa kabisa 👍
 
Back
Top Bottom