Nini tafsiri ya Megawatts 2,115 za umeme wa bwawa la Mwalimu Nyerere (Stiegler's Gorge)?

Nini tafsiri ya Megawatts 2,115 za umeme wa bwawa la Mwalimu Nyerere (Stiegler's Gorge)?

Haikuwepo na haja ya kujenga bwawa jipya Hali ya zamani yangeweza boreshwa, kwa kuondoa michanga na matope mabwawani pia kubadili injini za zamani na kufunga za kisasa maji kidogo speed kubwa umeme mwingi
Kufanya maintenance ya jengo au mradi huwa ni gharama zaidi kuliko kununua kitu kipya na kufanya Installation. But all in all uko sahihi kwa maana marekebisho ni muhimu
 
Ok, soon utaupata uchambuzi. Hii ni baadhi ya mitambo ya gesi asilia (Methane) inayopatikana Tabata Kinyerezi inayopokea gesi asilia kutoka Madimba Natural Gas pPocessing Plant, Mtwara na Songosongo, Lindi. Gesi asilia imeshaanza kutumika maeneo mengi mkoani mtwara na Lindi na Dar es salaam ikiwa ni pamoja na Serena Hotel, kiwanda cha saruji cha Dangote. Lakini pia mfumo wa Magari yanayotumia gesi asilia yaana CNG - Compressed Natural Gas upo pale DIT na magari mengi yanatumia mfumo wa CNG. CNG inatumia gharama ndogo sana ukilinganisha na diesel au petrol. Mfumo huu wa CNG hauondoi mfumo wa zamani wa gari yako kutumia diesel au petrol isipokuwa unakuwa na mifumo yote na unachagua kwa wakati huu utumie upi.
Kwanza nianze tu kwa kukupongeza unastahili PHD ya uongo na siasa sasa twende chin
Kwanza kabisa mrad huo pesa nying zimekopwa na sio pesa zetu za ndan zaid ya 60% ni pesa za mkopo

Sasa tuje kwenye technical specification MEGAWATTS ww umeongea kisiasa siasa tu ila kwa ma ELECTRICAL ENGINEET wanakuchora tu unaposema MEGA means million kwaio unaposema 2115 MW maana yake ni 2115000000 watts
Sasa tuje kwenye watts watts ni S1 unit ya power na neno power lina maana kubwa sn kwenye physics maana mbali na umeme linatumika mpaka kwenye mechanics na thermodynamics

Sasa ili tusilete sound hapa tulete formula ya power kwenye umeme

Ohm's law equation (formula): V = I × R and the power law equation (formula): P = I × V. P = power

Kifaa chochote kile cha umeme lazima kiandikwe kinatumia nishati kiasi gan mfano TV kubwa sn inatumia 400watts
Kwa maana km bwana linazalisha 2115 watts basi litaweza kuwasha tv 5287500 au tuseme TV million 5

Kwa hesabu hzo tu nan kakudanganya km mgawo utaisha nan kakudanganya km umeme utashuka bei

Niliitaka nikuumbie pia kwenye swala bei ila nimeona bora nikukaushie tu maana sio ww ni buku 7 io
 
Mwambie uyo naenda kukojoa narud
Mh Rais Dr. John Pombe Magufuli leo akiwa Kinyerezi, Dar es salaam amesemasualala ajira kwa vijana awamu ijayo litatatuliwa tu. Lakini pia hii miradi itaajiri sana ndiyo maana kwa sasa serikali inapambana kutengeneza miradi mikubwa ya kudumu yenye kutoa ajira za kudumu
 
Kwanza nianze tu kwa kukupongeza unastahili PHD ya uongo na siasa sasa twende chin
Kwanza kabisa mrad huo pesa nying zimekopwa na sio pesa zetu za ndan zaid ya 60% ni pesa za mkopo

Sasa tuje kwenye technical specification MEGAWATTS ww umeongea kisiasa siasa tu ila kwa ma ELECTRICAL ENGINEET wanakuchora tu unaposema MEGA means million kwaio unaposema 2115 MW maana yake ni 2115000000 watts
Sasa tuje kwenye watts watts ni S1 unit ya power na neno power lina maana kubwa sn kwenye physics maana mbali na umeme linatumika mpaka kwenye mechanics na thermodynamics

Sasa ili tusilete sound hapa tulete formula ya power kwenye umeme

Ohm's law equation (formula): V = I × R and the power law equation (formula): P = I × V. P = power

Kifaa chochote kile cha umeme lazima kiandikwe kinatumia nishati kiasi gan mfano TV kubwa sn inatumia 400watts
Kwa maana km bwana linazalisha 2115 watts basi litaweza kuwasha tv 5287500 au tuseme TV million 5

Kwa hesabu hzo tu nan kakudanganya km mgawo utaisha nan kakudanganya km umeme utashuka bei

Niliitaka nikuumbie pia kwenye swala bei ila nimeona bora nikukaushie tu maana sio ww ni buku 7 io
Niambie kwa sasa nchi nzima Tanzania tunatumia MW ngapi kwa matumizi ya ndani,.. na MW ngapi kwa matumizi ya viwandani.

I rest my case here.
 
Mkuu huu uchambuzi wako ni wa kisiasa zaidi sio kitaalam Kwa sababu zifuatazo:-
1. Mikoa uliotolea mfano wako hawana matumizi ya umeme kabisa Kwa kuwa hawlkuna viwanda vingi wala migodi.
2. Wananchi wa mikoa hiyo wengi ni maskini na hawana umeme na matumizi Yao mengi ni kuwasha taa.
3. Jenho moja kubwa hapa Dar kama Viva tower au Mkapa tower lina matumizi sawa na mkoa wa Lindi.
4. Mgodi wa madini kama Bulyankulu unaweza kutumia Hadi megawat 300 au zaidi.
Hivyo mkuu wangu hizo hesabu zako zina ukakasi tu.
Hakuna Jengo lolote ambalo linaweza likatumia hata Megawatt moja duniani usitufanye sie wajinga . Kwenye jengo hilo na Mkapa kuna furnace za kuyeyushia dhahabu au chuma punguzeni uongo wewe unaonekana umesomea siasa tu na kukaa kwenye keyboard kuleta uongo huku ukibadili ID zako.
 
Anza hata leo gesi asilia kwenye gari

Ok, soon utaupata uchambuzi. Hii ni baadhi ya mitambo ya gesi asilia (Methane) inayopatikana Tabata Kinyerezi inayopokea gesi asilia kutoka Madimba Natural Gas pPocessing Plant, Mtwara na Songosongo, Lindi. Gesi asilia imeshaanza kutumika maeneo mengi mkoani mtwara na Lindi na Dar es salaam ikiwa ni pamoja na Serena Hotel, kiwanda cha saruji cha Dangote. Lakini pia mfumo wa Magari yanayotumia gesi asilia yaana CNG - Compressed Natural Gas upo pale DIT na magari mengi yanatumia mfumo wa CNG. CNG inatumia gharama ndogo sana ukilinganisha na diesel au petrol. Mfumo huu wa CNG hauondoi mfumo wa zamani wa gari yako kutumia diesel au petrol isipokuwa unakuwa na mifumo yote na unachagua kwa wakati huu utumie upi.
Wakati unakuja na mambo ya gesi taf pitia comment no. 3 tupate ukweli. Kwa kukumbusha tu mtungi wa kawaida unasimama Tshs 45,000/- mpaka 49,500/= (ORYX) kwa bei ya sasa.
 
Mh Rais Dr. John Pombe Magufuli leo akiwa Kinyerezi, Dar es salaam amesemasualala ajira kwa vijana awamu ijayo litatatuliwa tu. Lakini pia hii miradi itaajiri sana ndiyo maana kwa sasa serikali inapambana kutengeneza miradi mikubwa ya kudumu yenye kutoa ajira za kudumu
Kwani haukuwepo kwenye zile Ajira milioni 6 za miaka mitano iliyopita...Serikali imesema imetengeneza ajira milioni 6 kwa mwaka 2015 - 2020. Sasa kama umekalia vyeti vyako unasubiria yajayo yanayofurahishwaa shauri yako.. 😀 😀 😀 😀 😀 😀.

Alafu mdogo wangu usiwasikilize wanasiasa na kuamini wasemacho..nakumbuka ile ahadi ya kila kijiji aliyoitoa mgombea wetu October, 2015?? We waache waongee tu jitahidi ujiajiri kama wanavyotushauri wenyewe wanasiasa wakati wao wanapambana wapewe kura wapate ajira kwa kutumia midomo tuu..au teuzi kwa kusifia sanaa...kujiajiri hawawezi kamwee..
 
Kwa nyongeza zaidi kitakwimu, kwa wale maTomaso, wanaobeza kuwa huo mradi ni maendeleo ya vitu, mimi natumia wastani wa unit 420 kwa mwezi wa gharama ~ 150,000/-. Umeme wa Bwawa la Nyerere ukikamilika nitakuwa nalipa chini ya 20000/- kwa mwezi. Hii ina maana nitakuwa na salio la 130,000/- ambayo nitaitumia kwa maendeleo yangu (mtu). Hiki ni kiasi cha 1,560,000/- kwa mwaka ambacho si haba maana kinatosheleza kwa elimu ya watoto/wajukuu wangu (maendeleo ya watu) au kulipia bima ya afya (maendeleo ya mtu), na kadhalika
Halafu huu wa kinyerezi na vyanzo vingine vya maji tunaupeleka wapi?kama tunauza uhakika wa soko upo? Je wataumaliza wote au?...vyanzo vingine kama mtera,nyumba ya mungu nk vingeboreshwa je tusingeweza fikia megawatt hizo za stigler?..kama zingefikiwa hudhani kwamba ingekua busara kiuchumi hii hela ya stigler zingejengwa skimu za umwagiliaji vijana wangepata ajira huko?..ukiweka na viwanda vyepesi vya kuchakata hayo mazao yatokanayo na skimu huoni tungekua tumeyagusa maisha ya raia moja kwa moja na serikali ingepata kodi chapu?
 
Tuna safari ndefu kwa uelewa huu.
Palitakiwa pajengwe skimu za umwagiliaji kuajiri watu kwenye kilimo na viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo,ina tija kwa tra na raia kuliko kihangaika na umeme wakati wa vyanzo vingine upo,ile sgr sioni hata haja yake maana pana mtandao mkubwa barabara za lami
 
NINI TAFSIRI YA MEGAWATTS 2,115 ZA UMEME WA BWAWA LA MWALIMU NYERERE (Stiglers Gorge)?

Wengi tunaona na kusikia kuhusu habari ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa uzalishaji umeme wa maji wa Megawatts 2115 kutoka kwenye Mto Rufiji, mradi uliobuniwa na Mwalimu Nyerere toka mwaka 1975 na sasa unatekelezwa na Rais wa awamu ya 5 Dkt John Pombe Magufuli.

Tumesikia habari ya ukubwa wake huo mradi, gharama ya utekelezaji wa mradi wenyewe, umeme unaoenda kuzalishwa na mambo mengine mengi sana kuuhusu mradi huo wa Stieglers Gorge (Bwawa la Mwalimu Nyerere). Sasa leo ngoja tuumulike kidogo mradi huu wa umeme, tujue idadi ya namba zilizoko za gharama na Megawatts zinazoenda kuzalishwa hapo na tafsili yake kwa Watanzania na uchumi wetu.

Kwanza kuingia kwa Serikali ya awamu ya 5 kulifungua ukurasa mpya wa utekelezaji wa maono ya Baba wa Taifa ya toka mwaka 1975 ya kutaka kuzalisha umeme kwenye bonde la Mto Rufiji kupitia mradi huo mkubwa kabisa namba 4 wa uzalishaji wa umeme barani Afrika unaoenda kuzalisha Megawatts 2115 kwa gharama ya Trillion 6.5 tena kwa fedha zetu za ndani.

Adhima ya utekelezaji wa mradi huo inakuja wakati nchi ikiwa kwenye ujenzi wa uchumi wa viwanda ambao kwa kiwango kikubwa unategemea sana nishati umeme ya kuwezesha viwanda kupata nishati ya kutosha ili iweze kuzalisha vya kutosha na muhimu kwa gharama nafuu. Viwanda ni umeme na umeme ni viwanda.

Lakini licha ya yote ni wangapi tunaelewa tafsiri halisi ya Megawatts 2,115 za umeme zinazoenda kuzalishwa pale Mto Rufiji? kwa sisi watu wa kawaida ambao si wataalamu wala wahandisi tunaelewa nini kuhusu Megawatts 2115? twende sawa hapo chini.

Kuzielewa Megawatts 2115 na ukubwa wake ni rahisi ukipitia na kujua matumizi ya umeme na mahitaji ya umeme kwa taifa letu. Mfano mwepesi tu ni kwamba mahitaji halisi ya umeme kwa mikoa kama ya Mtwara na Lindi ili umeme usikatike hata sekunde ni Megawatts 22 hadi 30 tu, ina maana katika zile Megawatts 2,115 tunakuwa na chenji kama ya Megawatts 2,085.

Tanzania ina Mikoa 31, hivyo ukifanya kila mkoa upate Megawatts 50 tu kama makadirio ya juu kabisa hata kwa mikoa isiyozidi matumizi hayo maana yake ni sawa na kupeleka bahari ya umeme kila mkoa na bado matumizi tutaishia Megawatts 1,550 na bado zitabaki Megawatts 565 kama akiba ya umeme tuliyoiweka kibindoni. Bado hiyo Megawatts 50 kiwastani hata ukijumlisha mikoa yenye viwanda vingi na vikubwa kama Pwani, Dar es Salaam, Arusha, Tanga na Mwanza bado ni kubwa sana. Nimeweka kwa kiwango cha Juu saana usisahau matumizi ya Mtwara na Lindi ni Megawatts 22- 30 tu.

Ina maana hapo tunaenda kuua kabisa stori za mgao wa umeme na mambo ya umeme kukatikakatika. Hapo wenye viwanda vikubwa, vya kati na vidogo kabisa watazalisha bidhaa zao bila tatizo na zaidi kwa gharama nafuu kutegemea na urahisi wa gharama kwa umeme wa maji.

Umeme wa Kinyerezi ambao ndiyo tunaojivunia kwa sasa kuwa ni mradi mkubwa wa umeme kiwango chake cha mwisho cha kuzalisha umeme ni Megawatts 1,560 tu ina maana Bwawa la Mwalimu Nyerere pekee yake linaenda kutupa umeme wa uhakika tena wa maji ambao ni rahisi zaidi kuliko aina yoyote ile ya umeme duniani ukiachana na wa jua, upepo, nyuklia, makaa ya mawe, mafuta na gesi.

Tukumbuke umeme unaozalishwa na maji ndio umeme wa gharama nafuu na rahisi zaidi kuliko umeme wowote ule duniani. Kumbuka uniti 1 inayozalishwa na maji ni shilingi 36 tu wakati umeme wa nyuklia ni shilingi 65 kwa uniti, umeme wa jua shilingi 103.05, upepo 103.05, makaa ya mawe 118, gesi asilia 147 na mafuta ni 426. Hivyo tunaenda kushusha maradufu bei ya umeme kwa watumiaji hivyo kuhimili mfumuko wa bei wa bidhaa za viwandani.

Hii tafsili yake kukamilika tu kwa Bwawa la uzalishaji wa umeme la Mwalimu Nyerere kutashusha kwa kiwango kikubwa sana gharama ya umeme mpaka shilingi 36 tu kwa uniti hivyo kutoa nafasi kwa bidhaa zetu za viwanda nazo kushuka sana. Hapo mpaka kwenye matumizi ya kawaida nyumbani yatashuka na hata kwa watanzania watakaofungua viwanda vidogo kwa vikubwa watanufaika sana na gharama ndogo ya uzalishaji wa bidhaa itakayoleta neema na nafuu mpaka kwa sisi watu wa hali ya chini kabisa, machinga, mama nitilie, wajasiriamali na makundi mengine.

Unapokuwa na umeme wa uhakika, lakini sio wa uhakika tu tena na wa gharama nafuu ya bei tayali unavutia wawekezaji wengi zaidi kuja kujenga viwanda hapahapa. Suala la uhakika wa umeme na nafuu yake ni mambo ya msingi sana kwa mwekezaji anayefikiri kwenda kuwekeza sehemu yoyote ile kwasababu kiwanda ni nishati.

Vipi umefikilia hizo Megawatts zingine zaidi ya 565 ambazo tunakuwa tumezitia kibindoni baada kujihakikishia uhakika wa umeme nchi nzima? hapo tunaweza kuamua kuuza kwa majirani zetu hapo Kenya, Malawi, Uganda au Msumbiji ambako tunajua bado hawana uhakika wa umeme. Hapo unazungumza kuhusu umeme wa Rufiji tu, hujaenda Kinyerezi, Kidatu, Mtera, Nyumba ya Mungu na kwingine ambako umeme unaendelea kuzalishwa.

Rais Magufuli na Serikali yake baada ya kugundua hatuna umeme wa kutosha na wenye bei nafuu kwa wananchi wake ndiyo ikaja na suluhisho hilo la Bwawa la Mwalimu Nyerere. Nini tena sasa? Tusiposema sisi kwa haya yanayofanyika basi hata mawe yatapiga kelele siku moja.
Kwani huo mradi una tofauti gani na kidatu? Je Kidatu imeishia wapi?
Je bwawa la Mtera limeishia wapi?

je gas ya Mtwara imeishia wapi?

tumechoka kudanganywa kila siku.
 
Kwa nyongeza zaidi kitakwimu, kwa wale maTomaso, wanaobeza kuwa huo mradi ni maendeleo ya vitu, mimi natumia wastani wa unit 420 kwa mwezi wa gharama ~ 150,000/-. Umeme wa Bwawa la Nyerere ukikamilika nitakuwa nalipa chini ya 20000/- kwa mwezi. Hii ina maana nitakuwa na salio la 130,000/- ambayo nitaitumia kwa maendeleo yangu (mtu). Hiki ni kiasi cha 1,560,000/- kwa mwaka ambacho si haba maana kinatosheleza kwa elimu ya watoto/wajukuu wangu (maendeleo ya watu) au kulipia bima ya afya (maendeleo ya mtu), na kadhalika

Mataga umechanganyikiwa
 
Umeme pekee hauwezi kumwagilia bila uwepo wa scheme hizo.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
Labda hukunisoma vizuri. Kushuka kwa bei ya umeme inaweza kuwa motisha kwa wanaotaka kuanzisha hizo scheme. Mimi ninayo micro scheme, gharama za umeme kuvuta maji toka kisima kirefu zinafanya mapato ya mradi kuwa kidogo sana hasa mikoa ya kanda ya kati yenye ukame mkubwa.

Umeme ukipunguzwa bei tukalipa kwa mfano sh 100/unit, itawavutia wengi ku-invest kwenye schemes ndogondogo za umwagiliaji kwakuwa zitalipa.
 
Back
Top Bottom