Nisaidieni wanajamiiforum wenzangu nipate kibarua chochote, hali yangu ni ngumu sana mpaka nimekata tamaa ya kuishi

Mayelee

Member
Joined
Oct 13, 2021
Posts
53
Reaction score
80
Proffessionally mimi ni mwalimu, masomo ninayofundisha ni Kiswahili na Historia. Nilibahatika kuajiriwa serikalini mwaka 2013. Kutokana na matatizo ya kifamilia nilikazimika kuacha kazi 2019, matatizo yamekuwa yakiniandama bila suluhisho na nimejaribu kutafuta ajira sehemu mbali mbali bila mafanikio.

Kwa sasa nipo tayari kufanya kazi yoyote, iwe sheli, barmen au hata kuhudumia mahotelini nipo tayari ndugu zangu. Familia inanitegemea nikiwaangalia watoto wangu huwa najifungia ndani na kutoa machozi. Najua wapo humu wenye uwezo wa kunisaidia kwa hili. Pia kama nitamkwaza mtu nitaomba kusamehewa, kichwa na akili yangu havipo sawa kwa sasa.

Asanteni
 
Ilikuwaje ukaacha kazi na una level gani ya elimu.
Matatizo ndugu yangu, ni historia ndefu. But kwa ufupi kwetu nipo peke yangu katika familia yetu. Baba yangu alishafariki nikiwa mdogo hivyo nikabaki na mama. Mama yangu nae alipararaizi ikanibidi niende kumuuguza maana sikuwa na pa kumuweka nilipokuwa naishi, nilijaribu kuomba likizo hata ya bila malipo kazini kwangu lakini afisa elimu na mkurugenzi wangu hawakutaka kunielewa. Sikuwa na namna mama yangu nilimpenda sana japo mwenyezi Mungu alimchukua ila nilichagua kwenda kumpambania afya yake.
 
Jifunze kuwa mkweli usaidiwe.

Serikalini watu hawafukuzwi kazi kirahisi hivyo.

Unless ufukuzwe kazi na Rais.

Sasa kama kweli Ni kumuuguza mama yako, kwanini usingemchukua na kumuuguza nyumbani kwako unqkofanyia kazi?
 
Dah pole sana mkuu ila amini Mungu nafasi yako ipo
 
Pole sana mkuu. Mungu ni wetu sote, tutafika tu kaka usijali. Mungu akufanyie wepesi mkuu.
 
Natafuta kazi nimesomea health systems management...ukatibu wa afya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…