Nisaidieni wanajamiiforum wenzangu nipate kibarua chochote, hali yangu ni ngumu sana mpaka nimekata tamaa ya kuishi

Nisaidieni wanajamiiforum wenzangu nipate kibarua chochote, hali yangu ni ngumu sana mpaka nimekata tamaa ya kuishi

Kila tatizo Huwa Lina utatuz wake, hebu eleza kwanini uliacha Kazi Unaweza saidiwa na wadau hapa ukarudisha Kazi yako. Jpo asilimia kubwa MTU kusema uliacha Kazi Kwa matatizo ya kifamilia ni ngumu kueleweka. MM naamin Kazi yako hyo ukitaka kupambana unaipta lkn Elza why uliacha..
Proffessionally mimi ni mwalimu, masomo ninayofundisha ni Kiswahili na Historia. Nilibahatika kuajiriwa serikalini mwaka 2013. Kutokana na matatizo ya kifamilia nilikazimika kuacha kazi 2019, matatizo yamekuwa yakiniandama bila suluhisho na nimejaribu kutafuta ajira sehemu mbali mbali bila mafanikio.

Kwa sasa nipo tayari kufanya kazi yoyote, iwe sheli, barmen au hata kuhudumia mahotelini nipo tayari ndugu zangu. Familia inanitegemea nikiwaangalia watoto wangu huwa najifungia ndani na kutoa machozi. Najua wapo humu wenye uwezo wa kunisaidia kwa hili. Pia kama nitamkwaza mtu nitaomba kusamehewa, kichwa na akili yangu havipo sawa kwa sasa.

Asanteni
 
Matatizo ndg yangu, ni historia ndefu. But kwa ufupi kwetu nipo peke yangu ktk familia yetu. Baba yangu alishafariki nikiwa mdogo hivyo nikabaki na mama. Mama yangu nae alipararaizi ikanibidi niende kumuuguza maana sikuwa na pa kumuweka nilipokuwa naishi, nilijaribu kuomba rikizo hata ya bila malipo kazini kwangu lakini afisa elim na mkurugenzi wangu hawakutaka kunielewa. Sikuwa na namna mama yangu nilimpenda sana japo mwenyezi mungu alimchukua ila nilichagua kwenda kumpambania afya yake.
Ndugu Kwa maisha ya kawaida na ninavyoifahamu hii sekta kiukwel naamin Hii haikuwa Sababu, Japo Unaweza itumia kupata Kazi yako upya. Coz ulikuwa Unaweza kumleta Kule uliko... Hukukopa ukaondoka??? Nakushauri ndugu hyp Kazi Bado uko nayo endapo utaamua kurudi Kwa mwajili wako na kukiri.

Kubali kujirudi ndugu. TSC ipo yawezekana hata baraza la madiwani hawajui suala Lako. Usikate tamaaa. Kazi hyo uko nayo Rudi Kwa mwajili wako japo Sasa itakubidi usubiri kwa muda mrefu kupata salary.
 
Kumbe hiki kinawezekana?
Ndugu Kwa maisha ya kawaida na ninavyoifaham hii sekta kiukwel naamin Hii haikua Sababu, Jpo Unaweza itumia kupta Kazi yako upya. Coz ulikuwa Unaweza kumleta Kule uliko... Hukukopa ukaondoka??? Nakushaur ndugu hyp Kazi Bado uko nayo endpo utaamua kurudi Kwa mwajil wako na kukir. Kubal kujirudi ndugu. TSC ipo yawezkana hTa baraza la madiwan hawajui suala Lako. Usikate tamaaa. Kazi hyo uko nayo Rudi Kwa mwajil wako Jpo Sasa itakubid usubir Kwa muda mrefu kupta salary.
 
Kumbe hiki kimawezekana?
Kinawezekana kufutwa Ajira Kwa serikali Hasa za mitaa kuna vitu Huwa vinapuuzwa tofauti na mashirika ya umma. Unakuta toka atoke hkuna hatua yoyote ilyochukuliwa hivyo akirudi anafanikiwa vizuri tu. Arudi Kwa mwajiri ila atasota kupata salary
 
Jifunze kuwa mkweli usaidiwe.

Serikalini watu hawafukuzwi kazi kirahisi hivyo.

Unless ufukuzwe kazi na Rais.

Sasa kama kweli Ni kumuuguza mama yako, kwanini usingemchukua na kumuuguza nyumbani kwako unqkofanyia kazi?
Sina sababu yakuongea uongo ndg yangu, mazingira ya kazi ya ualim hope unayafaham. Nilikuwa naishi kwenye chumba kimoja na sebule na familia yangu yenye mke na watoto wawili. Ningewezaje kumchukua mama na kuishi nae? Kiuhalisia nisingeweza ndg yangu. Ila asante pia kwa mawazi yako
 
Sina sababu yakuongea uongo ndg yangu, mazingira ya kazi ya ualim hope unayafaham. Nilikuwa naishi kwenye chumba kimoja na sebule na familia yangu yenye mke na watoto wawili. Ningewezaje kumchukua mama na kuishi nae? Kiuhalisia nisingeweza ndg yangu. Ila asante pia kwa mawazi yako
Unaishi wapi Mkuu? (Mkoa na Wilaya).
 
@gmail.com??
Ukituma maombi wanakukubalia, kisha wanakuandikia maneno marefuuuu na wanakwambia tuma pesa kwa ajili ya kugharamia accommodation na chakula kwenye training ya kufanya kazi itakayofanyika hotel xxx. Ha ha haa. Jamaa utapeli wao laini kweli. Ila unakuta kuna watu wanakamatika.
 
Sina sababu yakuongea uongo ndg yangu, mazingira ya kazi ya ualim hope unayafaham. Nilikuwa naishi kwenye chumba kimoja na sebule na familia yangu yenye mke na watoto wawili. Ningewezaje kumchukua mama na kuishi nae? Kiuhalisia nisingeweza ndg yangu. Ila asante pia kwa mawazi yako
Kwahiyo sasa hizi hauna kazi, wewe mama yako na familia yako mnaishi wapi?
 
Nam naungana na waliosema hiyo haikuwa sababu ya wewe kuacha kazi, haimake sense eti uache kazi ili ukamuuguze mama yako, hela ya matibabu, gharama ya chakula n.k ulitegemea utapata wapi? Wewe ni mtoro ulienda piga issue zako. Anyway kuhusu wanaosema yawezekana ajira yako ipo usiweke asilimia 100, siku hizi serikalini pia ukizingua unafukuzwa vilevile, ushauri wangu ambao ni professional kabisa sio wa kubahatisha iko hivi, nenda kwenye halmashaur uliyokuwa unafanyia kazi uulize hatma ya jambo lako ikiwa ulifukuzwa omba barua yako ya kufukuzwa kazi, then nenda ofisi ya TSC omba ushauri wa namna ya kuwasilisha maombi ya kurudi kwenye utumishi wa Umma, watakupa utaratibu then utaufuata, mchakato unachukua muda mrefu hata miaka zaidi ya miwili au kama unabahati kabla ya hapo. Ikiwa hukufukuzwa waombe msamaha kwa kuwaambia ukweli kabisa nao ni binadamu huenda wakakusikia kilio chako wakatafuta means ya kukusaidia
 
Nipo Dar es salaam ndg yangu, Kimara Stop over
Pole sana ndugu yangu, endelea kuweka juhudi katia kutafuta chakufanya huku ikikumbuka jitihada hazizidi kudra, hivyo kudra ya mwenyezi Mungu ikuwezeshe.
 
Wanajamii mimi forklift operator elimu kidato Cha sita pia ni dereva naombeni msaada yeyote anayejua kuna kiwanda au warehouse au kampuni yoyote ambayo nkienda kuomba naweza kupata kazi aniambie. Iwe Dar, Pwani, Tanga, Moro nafika 0623736996 mwenye connection
 
Ukituma maombi wanakukubalia, kisha wanakuandikia maneno marefuuuu na wanakwambia tuma pesa kwa ajili ya kugharamia accommodation na chakula kwenye training ya kufanya kazi itakayofanyika hotel xxx. Ha ha haa. Jamaa utapeli wao laini kweli. Ila unakuta kuna watu wanakamatika.
Yani sijui nipoje ila i can smell fishy far away from 1000km na sijawai na hawato wai kuniingiza mkenge wezi wa aina iyo..[emoji23]

Kitu kinacho wafanya watu kuingia mkenge ni kutokuwa na uelewa wa TEHAMA. Hapa ndio wengi wanaumizwa. Wakati mi i can smell the links with scams wengine wanatuma maombi ya kazi kwenye makampuni makubwa kupitia@gmail.com na bado wana ambiwa watume hela za kugharamia blah blah na still wanatuma.
 
Mi nilikuwa siamini lakini kumbe kweli wapiga debe wanajenga bhana.
 
Back
Top Bottom