Nitaifichaje hii aibu ili niweze kurudisha heshima yangu

Nitaifichaje hii aibu ili niweze kurudisha heshima yangu

Habari zenu ndugu zangu ,

Mimi ni mtumishi idara Fulani sasa juzi tulikuwa na hafla fulani au tuseme ni ziara fulani nje ya mkoa sasa ikapelekea kunywa pombe kupitiliza na kuanza kuropoka yaani kila mfanyakazi mwenzangu alijua kwamba nimelewa na wengine kuwaweka wazi kuwa nawapenda sasa hii kwangu ilishangaza mno watu kiasi kwamba kuanza kunishangaa mno.

Mimi sio mnywaji wa pombe kabisa ila nilikuwa kama kichaa baada ya kulewa kupitiliza hivyo imekuwa aibu na fedheha kiasi kwamba mpaka nilipopanga wamejua kuwa nililewa na kuanza a kuongea maneno ya hovyo hivyo ni aibu kweli kweli na pia kabisa naona heshima yangu imeshuka mno

Nifanyaje ndugu zangu niweze kuirejesha heshima niliyokuwa nayo kazini, kwenye jamii na hata kwa wale niliowakosea japo sio wote wamenambia kuwa niliwakosea najua kuna ambao niliwakosea lakni hawawezi kusema

Hapa nina mawazo mno yani najiona mkosaji kuliko wakosaji wengine mana sijawahi kulewa na kudhalilika kiasi kile

HAPA NIMEANDIKA NIKIWA NA MAWAZO MENGI MNO KICHWANI YANI KILA NINAYE MUONA NAHISI ANANIZUNGUMZIA MIMI HASA KWA HESHIMA NILIYOKUWA NAYO

NISAIDIENI MAWAZO YANANITESA
#NIMEAPA POMBE SITOGUSA MPAKA NAINGIA KABURINI
Mimi nilijua tu kuwa utakuja kusema huku jf enhee je wale wengine?
 
Waombe tu msamaha ndugu wote unaofikiria uliwakosea, naamini watakusamehe na pia acha muda ufanye yake, binadamu Wana tabia ya kusahau baada ya muda fulani naamini watasahau na mambo yatakuwa sawa, ila USIRUDIE kunywa pombe kama imekukataa
 
Pole sana mkuu, na wacha nikupe hizi njia mbili, zitakusaidia sana.

Njia namba uno: Itabidi uendelee kulewa ili hao uliowakosea uendelee kuwakosea hadi washangae kiasi cha kuona si jambo la kawaida bali inawezekana kuna jambo limekupata na hapo wataanza kukufuata kwa upole ili wakupe ushauri wa hapa na pale kwa lengo la kukusaidia uondokane na hiyo hali.

Na wewe utajifanya kuzingatia ushauri wao then utakaa Kaa baadae utaacha utaona wote uliowakosea wanakupa pole kwa changamoto zilizokupata na hapo heshima yako itakua haijaguswa ila wataanza kulaumiwa watu walioko katika ulimwengu wa giza ilihali wao wenyewe hawana taarifa zozote na tatizo lako. 😅😅😅.

Njia ya pili jifanye haukumbuki chochote kilichotokea baada ya kulewa ila urudi uanze kuwaomba msamaha watu wote ambao walikua karibu na wewe wakati huo wa kulea uwaambie haujui kilichotokea baada ya kulewa ila kwakua unajijua wewe huwa pombe hazikufai kwa maana ukilewa huwa unaongea mambo mengi yasiyofaa(kuropoka, yaani unakua kiropo ropo), kwahiyo unawasiwasi inawezekana kuna jambo lolote la ajabu ulilifanya iwe la kukufedhehesha wewe au watu wengine kwa hali ya kutokujua basi unawataka wakuwieladhi kwa maana haikua dhamira yako, na isitoshe wanajua the really you ukoje.

Fanya hivyo kazini na kwa majirani zako hapo mtaani kwenu then acha yaliyopita yapite na maisha yaendelee kwa maana mwisho wa siku wewe ni binadamu tu na kimsingi hakuna mwanadamu aliyemkamilifu.
Ahsante ndugu
 
Jambo dogo sana Hilo kama nukta..... Kwanza hongera kwa kufungua mlango wa 7 ukitaka uishi amani na ujipate ishi maneno uliyoyaongea wakati umekunywa uliyemwambia unampenda mfuate mazima mwambie sio pombe nakupenda kweli ili asijue ni pombe au ukimwambia me
Sawa ndugu ahsante pia kwa ushauri ila pia niligombanisha wanawake wawili
 
Habari zenu ndugu zangu ,

Mimi ni mtumishi idara Fulani sasa juzi tulikuwa na hafla fulani au tuseme ni ziara fulani nje ya mkoa sasa ikapelekea kunywa pombe kupitiliza na kuanza kuropoka yaani kila mfanyakazi mwenzangu alijua kwamba nimelewa na wengine kuwaweka wazi kuwa nawapenda sasa hii kwangu ilishangaza mno watu kiasi kwamba kuanza kunishangaa mno.

Mimi sio mnywaji wa pombe kabisa ila nilikuwa kama kichaa baada ya kulewa kupitiliza hivyo imekuwa aibu na fedheha kiasi kwamba mpaka nilipopanga wamejua kuwa nililewa na kuanza a kuongea maneno ya hovyo hivyo ni aibu kweli kweli na pia kabisa naona heshima yangu imeshuka mno

Nifanyaje ndugu zangu niweze kuirejesha heshima niliyokuwa nayo kazini, kwenye jamii na hata kwa wale niliowakosea japo sio wote wamenambia kuwa niliwakosea najua kuna ambao niliwakosea lakni hawawezi
 
Hapana sio mimi
Oohh...pole sana yatakwisha mkuu!!omba Toba Kwa Mungu uwe na amani,watu watasahau tu.

Huenda pia ndiyo njia ya kufanya uache pombe kabisa hata kama haukuwa mnywaji kihivyo...😊
 
Kipindi ni mchanga kwenye sekta ya ulevi hiyo ilishanikuta sana , dawa ya wamatumbi ukishafanya vituko kama hivyo ni kufuata biashara zako tu , watazungumza mwishowe wakiona upo bize na mishe zako wataanza kujipendekeza wenyewe tu.
 
Habari zenu ndugu zangu ,

Mimi ni mtumishi idara Fulani sasa juzi tulikuwa na hafla fulani au tuseme ni ziara fulani nje ya mkoa sasa ikapelekea kunywa pombe kupitiliza na kuanza kuropoka yaani kila mfanyakazi mwenzangu alijua kwamba nimelewa na wengine kuwaweka wazi kuwa nawapenda sasa hii kwangu ilishangaza mno watu kiasi kwamba kuanza kunishangaa mno.

Mimi sio mnywaji wa pombe kabisa ila nilikuwa kama kichaa baada ya kulewa kupitiliza hivyo imekuwa aibu na fedheha kiasi kwamba mpaka nilipopanga wamejua kuwa nililewa na kuanza a kuongea maneno ya hovyo hivyo ni aibu kweli kweli na pia kabisa naona heshima yangu imeshuka mno

Nifanyaje ndugu zangu niweze kuirejesha heshima niliyokuwa nayo kazini, kwenye jamii na hata kwa wale niliowakosea japo sio wote wamenambia kuwa niliwakosea najua kuna ambao niliwakosea lakni hawawezi kusema

Hapa nina mawazo mno yani najiona mkosaji kuliko wakosaji wengine mana sijawahi kulewa na kudhalilika kiasi kile

HAPA NIMEANDIKA NIKIWA NA MAWAZO MENGI MNO KICHWANI YANI KILA NINAYE MUONA NAHISI ANANIZUNGUMZIA MIMI HASA KWA HESHIMA NILIYOKUWA NAYO

NISAIDIENI MAWAZO YANANITESA
#NIMEAPA POMBE SITOGUSA MPAKA NAINGIA KABURINI
Kawaida tuu mkuu,Bora umegundua Hilo!jipe moyo na heshimu maamuzi Yako.
 
Habari zenu ndugu zangu ,

Mimi ni mtumishi idara Fulani sasa juzi tulikuwa na hafla fulani au tuseme ni ziara fulani nje ya mkoa sasa ikapelekea kunywa pombe kupitiliza na kuanza kuropoka yaani kila mfanyakazi mwenzangu alijua kwamba nimelewa na wengine kuwaweka wazi kuwa nawapenda sasa hii kwangu ilishangaza mno watu kiasi kwamba kuanza kunishangaa mno.

Mimi sio mnywaji wa pombe kabisa ila nilikuwa kama kichaa baada ya kulewa kupitiliza hivyo imekuwa aibu na fedheha kiasi kwamba mpaka nilipopanga wamejua kuwa nililewa na kuanza a kuongea maneno ya hovyo hivyo ni aibu kweli kweli na pia kabisa naona heshima yangu imeshuka mno

Nifanyaje ndugu zangu niweze kuirejesha heshima niliyokuwa nayo kazini, kwenye jamii na hata kwa wale niliowakosea japo sio wote wamenambia kuwa niliwakosea najua kuna ambao niliwakosea lakni hawawezi kusema

Hapa nina mawazo mno yani najiona mkosaji kuliko wakosaji wengine mana sijawahi kulewa na kudhalilika kiasi kile

HAPA NIMEANDIKA NIKIWA NA MAWAZO MENGI MNO KICHWANI YANI KILA NINAYE MUONA NAHISI ANANIZUNGUMZIA MIMI HASA KWA HESHIMA NILIYOKUWA NAYO

NISAIDIENI MAWAZO YANANITESA
#NIMEAPA POMBE SITOGUSA MPAKA NAINGIA KABURINI
Pole sana, binadamu tumeumbiwa kusahau.
Hilo litapita tu na litaondoka vichwani mwa watu. Lipe muda!
 
Back
Top Bottom