Mkuu nipe highlight ya vita vya kongo kiujumla, huwa naona speculations nyingi nashindwa kuelewa, ina maana madini yanayogombaniwa na westerns ndo yanafanya nchi isiwe na amani? Na hivyo vikundi vya waasi je? Kwa nini wanauliwa kikatili sana huko vijijini? Na je vita ipo ngapi ya sehemu ya nchi.
Nimetoa hayo maswali ili uelewe ninachoelewa na ujue utanifafanulia vipi na sio uyajibu, tumia mfumo wako kunielewesha mwanzo mpka mwisho.
Vita ya kongo ni mgogoro wa muda mrefu ambao umeanzia haswa kwene mauaji ya kimbari ya rwanda.
Mauaji ya kimbari kutokea 1994 na Uganda kushirikiana na watusi wa rwanda waliokua wanaishi ukimbizini kuvamia rwanda na kuangusha serikali ya habyarimana na kusimikwa kwa serikali ya kitusi ya PK.
Katika kile kinachodhaniwa kwamba PK alihofia kupinduliwa kama ambavyo yy alifanya kwa kutokea uganda kama waasi kisha kupindua au kutwaa madaraka .
PK alihofia kua wanajeshi wa kihutu ambao walikimbilia kongo watarudi tena kwa msaada wa mobutu na kuangusha serikali yake hivo waliingia kongo kuwawinda.
Ikumbukwe kua serikali ya mobutu ilikua ni imara si kama sasa ambapo vikundi kadhaa vya uganda,rwanda na waasi vinaishi ndani ya kongo.
Pk na mshirika wake mseveni waliona kizuizi pekee cha kutawala rwanda ilikua n mobutu kwan walishindwa kuingia kongo kuwita waasi hivo waliandaa mbinu ya kuvamia Kongo.
Wakati huo Laurent kabila mpinzani wa Mobutu alikua akiishi tanzania , Inasadikika kua serikali ya tanzania iliwashauri PK kua Lauren kabila angewafaa kwenda kuipindua serikali ya mobutu.
Kwa kua walihitaji sappot ya wakongo pia kuweza kufika kinshasa.
Hivo walimchukua laurent kabila ,vikosi vya rwanda,uganda plus vikosi vilivyokua vikipinga mobutu au vilivokua vinasapot laurent kabila.
Hapa kuna watusi wa kongo ambao selikali ya mobutu ilikua haiwatambui kwan waliwasili kongo miaka ya nyuma na kujiita ay kukaa vilima vya mulenge na wakajiita wanyamulenge pia wakaungana na hizi nchi wavamizi kuvamia nchi ya kongo.
******stori n ndefu lakin huu ndio ulikua mwanzo wa kongo yenye damu
Baada ya kupindua serikali Laurent kabila aliwageuka mseven na pk ndio mwanzo wa uasi wa m23.
Wakamuua akaridhi mtoto wa kambo ambae ni joseph kabila. huyu aliwaacha waibe wanavotaka hivo hawakua wanamsumbua.
lakini ukabila na machafuko ya kikabila yalianza baada ya first na second congo war.
Wakongo walikua washashuhudia usaliti wa watusi wa kongo na mauaji ya kinyama dhidi ya makabila mengine walipokua wanatimiza ajenda yao ya kumtoa mobutu lakini pia kwene 2nd congo war walipotaka kumpindua Laurent kabila.Kifupi wanawaona kama ni mamruki wanaotumiwa kuua na kupora.
Hivo vita ilianza kama kwenda kongo kuwasaka wahutu hadi kuingia kongo kuiba madini.
Lakini yote haya yaliwezekana vipi.
Marekani,Ufaransa na Uingereza zimekua zikihusika kuzilinda nchi hizi mbili uganda na rwanda ili ziendelee kuivamia kongo na kuiba.
Kwann kongo haipigani? Kongo iliwekewq arm imbago hivo ilikua haina uwezo wa kununua silaha za kisasa kupambana na haya makundi wakat huo nchi hzii zenywwe zimekua zikipewa silaha nzito za kisasa.
Vita ni silaha.
Kifupi kinachoendelea Kongo ni Aina nyingine ya ukoloni,,,,,
Ukoloni mpya ambao watu hawaujui kwakua wanatumia waafrica kutawala na kuchukua malighafi.
Na kwa kua wazungu wao ndo wameshikilia vyombo vya haki basi wanachagua wa kumhukumu
Na kwa kua wao ndo wenye vyombo vya habar bas wanachagua cha kutangaza.
inshort iko hivo