Njia gani ni bora kwa mtumishi kuhama kutoka halmashauri (local government) kwenda Taasisi zingine?

Njia gani ni bora kwa mtumishi kuhama kutoka halmashauri (local government) kwenda Taasisi zingine?

Au pambana ukapige m.a ya kitu fulan ukipata g.pa nzur hamia vyuo kufundisha
Ukipata g.pa nzur unaanza na assistant tutorial badae unaunga phd saf
 
Serikali ina mkono mrefu, usijichanganye kamwe.

Kuhama Taasisi nyingine ni jambo linawezekana wala halihitaji hata kusoma tena degree ya pili hapa ni connection na uthubutu wako.


USIJICHANGANYE KUACHA KAZI UKAENDA KUSOMEA JAMBO JINGINE BILA KUFUATA TARATIBU.

UKISHAINGIA KWENYE SYSTEM YA GVT HATA UKIACHA KAZI YAKO UKAENDA KUSOMEA KITU KINGINE KUAJILIWA TENA NI NGUMU KWENYE MFUMO HUWA INASOMEKA KUWA VYETI HIVI VIMESHAAJILIWA SEHEMU FULANI.


Njia sahihi kwa 100% soma degree nyingine ukiwa kazini hlf omba kubadilishiwa kazi au cheo RECATEGORIZATION hii inafanya kazi bila shida.


Mambo siyo rahisi kama unavyowaza kuhamia Taasisi ni rahisi lakini kuna taratibu zake siyo kukurupuka na kwenda haraka kama unavyotaka wewe.

Unaweza kuanzia halmashauri ukahamia Taasisi.

Siwezi kueleza mengi hapa JF ila ukiweza fanya tuongee live nina mengi ninayoyajuwa kuhusu hii michakato coz mimi pia ni mhanga wa mishe hizi,

Taasisi kuna maisha kuliko serikali za mitaa so kutokana na kuhaso sana nilijifunza mengi kwa vitendo.

Yaani mimi nililianzisha kweli kweli mpaka NIKAFIKA KWA DE (Director of Estblishment) Huyu ndiyo anacontrol watumishi wote nchini ukitaka kutoka sehemu moja kwenda nyingine, kumuona tu ni issue ofisini kwake.

Akitoka Waziri wa UTUMISHI, ANAFUATIA KATIBU KIUENDAJI NA BAADA YA KATIBU ANAFUATIA HUYO ED.

Huyo akisema hamia pale unakwenda akisema NO hata katibu mkuu anamsikilizia huyu kiutumishi.

Kwanza kujishusha ni lazima kuna inabidi uwe mpole ili jambo liende zaidi ya hapo labda uwe na ndugu vigogo serikalini.
Mwamba umemamaliza. Kwel we mhanga.
 
Kama watu wakihama wote unadhani jamii ita hudumiwa na nani kikubwa kumshukuru mungu hapo ulipo na tengeneza mazingira kuwa fursa mm nilikuwa na mawazo kama Yako ila saiv nalima na mshukuru mungu fursa ya kilimo imenifanya niondokane na mawazo ya mshahara mkubwa sijui sehemu nzuri hata ulipwe milioni 10 kma huna nidhamu na fedha bado utaona ndogo na utataman ten kuhamia taasisi nyingine
Fursa iliyopo ni labda awe na bot karema huko zivue dagaa.au kulima mpunga ifinsi huko kuna wal mpaka wa jero
 
Mkuu kwanza mimi nakutahadharisha kwamba unachokitafuta ni UTAJIRI WA PESA kitu ambacho kwenye UTUMISHI WA UMMA hutokuja kukipata kamwe. Unachokitafuta wewe ni siku moja kuja kuwa mwizi au fisadi.
Uko kikazi Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi halafu unalalamika???????
Mwili wangu umesisimka ujue kwa mfano uko Sibwesa, Karema, Mishamo nk popote ulipo umezungukwa na Utajiri mdogo wangu.
Fuga Ng'ombe anza na mtaji wa Mil 2 nenda mnada wa Sibwesa nunua ng'ombe wako 5 wa laki 4@ baada ya miaka 3 utaanza kula matunda.
Lima Mpunga pale Sibwesa kodi shamba tandika ekari zako 5 mwisho wa msimu una gunia zako 180 na sasa guni ni 120k@.
Nunua Ng'ombe zako 2 na jembe lake anza kukodisha hii kwa siku hukosi 50k umekosa sana.
Lima Pamba ambalo ni zao jipya hapo Tanganyika na kiwanda kipya kimefunguliwa pia na ardhi inakubali kinyama.
Nunua Mpunga wakati wa Mavuno hifadhi uza wakati wa njaa Januari.
Naongea haya yote nimeyapitia na kuyaishi. Usidanganye watu jwamba Tanganyika ni pabaya, mimi nipo ndaaaaani huku Kijijini MWESE nafanya maisha yangu na BATA LANGU nikiamua kwasababu Mpunga ninao nakamata zangu pipa nazama Dar nafanya UNYAMA MWINGI. Ukitaka ushauri njoo inbox acha kupaparika na kukimbilia mjini au Taasisi. Askari wa kweli hakimbiii Uwanja wa VITA.
Yaaani uko Tanganyika halafu unalia huna maisha???? Maajabu.
tukuyu 08 uko Sumbawanga unalia lia.
Ukitaka Utajiri usikubali kuajiriwa.
Unapoajiriwa tambua kwamba umrjisajili kwenye mnyororo wa Umaskini.
Tambua kwenye orodha ya Mabilionea Ilimwenguni kote halipo jina la Mfanyakazi aliyeajiriwa. So kama unatafuta utajiri acha kazi[emoji419]
Umesahau ifinsi aisee.wasukuma wanalima mpunga huko. Wali sahan jero aisee.
 
Soma open university mkuu mambo yasiwe mengi nenda kasome environmental engineering uende EWURA au mashirika ya umma unapiga hela fasta.
Ataendaje EWURA? Kumbuka transfer hazifanyiki kizembe hivyo, anahamishwa mtu na kada yake. Labda kama EWURA wana uhitaji wa Education Officer mwenye sifa za Ualimu, sio za Environment Officer, maana unahamishwa kwenda kwenye kada kama uliyoajiriwa huko unakohama
 
Nj
Jamiiforums kisima Cha maarifa.

Mimi ni mtumishi Mwalimu, Nilisoma PCB advance nikapata division II point 12, nilichaguliwa computer and software engineering Lakini sikwenda, nikazamia Chaka la ualimu wa Physics Nilisoma kwa sababu ya kukosa washauri pamoja na umaskini wa home na nilitaka kuajiriwa mapema Ili nijitegemee , ni kweli baada ya kumaliza chuo nikaajiriwa, Niko na miaka 26 sasa.

Mwaka mmoja kazini sasa, nafikiria mambo mengi kuondoka hapa nilipo shida sio mshahara tulianza na Tgts D3 na Rais Mama Samia alijitahidi kuongeza ongeza (nimpongeze kwa ilo), pia anajitahidi kulipa walimu stahiki zao, kuwapandisha madaraja Pamoja na madaraja mserereko (anaupiga Mwingi) pia watumishi wengi wa halmashauri mishahara yao ni humo humo hakuna utofauti saana, Kwahiyo swala la Mwalimu kua na mshahara Mdogo kuliko watumishi wengine wa halmashauri sio kweli. labda utofauti ni kwamba Mwalimu hana Cha kuiba mpaka Mwisho wa mwezi, pia walimu hawana professional board yani mtu yoyote yule anaweza kumfanyia ujinga Mwalimu maana hana sehemu ya kuguswa mfano hao "Afsa utumishi" CWT na wenyewe wapo wapo tu kula hela ya Mwalimu wakinenepeana bila kazi yoyote Ile hiki chama kingefutwa labda ingeleta tija. Ukiwa wa tofauti wanakuona mkorofi na kukutafutia zengwe upuuzi.

Nafikiria kusoma degree nyingine kabisa mawazo yangu yakanipelekea kusoma meteorology au hiyohiyo computer and software engineering ambayo niliiacha au niende pale ATC nikapige bachelor degree in mechatronics and material engineer?

Nilianza kufanya application Mwaka huu changamoto niliyoipata ni ruhusa wanasema kupewa ruhusa kwenda kusoma degree nyingine ni ngumu, kwa mtu mwenye degree wanatoa ruhusa ya miezi 18 tu?, Hapo swala limekaaje?

Wengine wamenishauri nisome open university mambo ya procurement and supply Pamoja na mambo ya finance kitu ambacho naona kama nitarudi tu halmashauri kujipendekeza wanifanyie "recategorization" kitu ambacho sitaki. Nikifikiria kusoma masters degree ya Education au utawala Lakini naona kama aina faida yoyote kwangu, maana Kuna Mwalimu wa sekondari ana PhD Lakini njaa Kali tu.

Je nikifanikiwa kusoma degree nyingine uwezekano wa kuhamishwa kwenda wizara au Taasisi nyingine upo?
NB, Sina mtu yeyoye ambae naweza kusema Nikisoma kitu Kingine anaweza kunishika mkono hapana, au niachane navyo vyote niende VETA Nikachukue ujuzi mbali mbali nijiajiri Huku nikiwa Teacher?
NNje ya mada, kwa nyie walimu wa shahada, take home inafika shngp kwasasa ukitoa na bod ya mikopo nq michango yote
 
Mpaka sio poa mkuu, ningeajiriwa kwenye manispaa au hata halmashauri zilizochangamka tungejiajiri kwenye harakati mbalimbali, Lakini Sasa huku useme ujiajiri dah.
Huku unajiajiri kwa kilimo na ufugaji, kusingekuwa na ishu watu wasingeishi huko, hiyo ajira ya serikali kuna watu wanaililia wameikosa, angalia usije kujuta baada ya kuacha kazi.
 
Umri unaruhusu kapige masters nje viza ukiwa mtumishi ni rahisi kupata,nauli unakopa bank.
Huku unasoma ukiwa unachek michongo mingine nje mambo yakikaa sawa unawaforwadia email ya 24hrs juu kwa juu.Ngoma ikigoma unarudi bongo na elimu yako unalipwa mshahara wa masters Sio Haba Serikalini.
Ukikomaa nje unatunza pesa ukija bongo unanunua nyumba,unarudi nje hivyo hivyo
Au unajenga apartment,hotel, viwanja hizi ndizo pension zako,ukiwa Mzee.
Siku hizi mkuu Ukitaka kwenda kusoma wanakusainisha Mkataba utakaokuzuia kuacha kazi kipind ukiwa masomoni au muda mfupi baada ya kumaliza masomo..
kwahyo Ngoma ngumu 😀😀
 
Umri unaruhusu endelea kuomba majeshini pia kwa graduate mwisho miaka 28 ukipata unakula Kona.
Serikali inatambua masters siku hizi unavuta milion na laki saba
Majeshi hawataki watu wenye check number, wanataka watu ambao hawana ajira, Kuna kapata
 
Majeshi hawataki watu wenye check number, wanataka watu ambao hawana ajira, Kuna kapata
Sorry for typing error, Nilitaka kusema, kuna kapteni mmoja aliwafukuza waajiriwa wa Tamisemi pale TAU(kikosi cha mgulani) na imeandikwa kabisa ktk tangazo la ajira, siyo kwamba aliwaonea.
 
Mkuu kwanza mimi nakutahadharisha kwamba unachokitafuta ni UTAJIRI WA PESA kitu ambacho kwenye UTUMISHI WA UMMA hutokuja kukipata kamwe. Unachokitafuta wewe ni siku moja kuja kuwa mwizi au fisadi.
Uko kikazi Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi halafu unalalamika???????
Mwili wangu umesisimka ujue kwa mfano uko Sibwesa, Karema, Mishamo nk popote ulipo umezungukwa na Utajiri mdogo wangu.
Fuga Ng'ombe anza na mtaji wa Mil 2 nenda mnada wa Sibwesa nunua ng'ombe wako 5 wa laki 4@ baada ya miaka 3 utaanza kula matunda.
Lima Mpunga pale Sibwesa kodi shamba tandika ekari zako 5 mwisho wa msimu una gunia zako 180 na sasa guni ni 120k@.
Nunua Ng'ombe zako 2 na jembe lake anza kukodisha hii kwa siku hukosi 50k umekosa sana.
Lima Pamba ambalo ni zao jipya hapo Tanganyika na kiwanda kipya kimefunguliwa pia na ardhi inakubali kinyama.
Nunua Mpunga wakati wa Mavuno hifadhi uza wakati wa njaa Januari.
Naongea haya yote nimeyapitia na kuyaishi. Usidanganye watu jwamba Tanganyika ni pabaya, mimi nipo ndaaaaani huku Kijijini MWESE nafanya maisha yangu na BATA LANGU nikiamua kwasababu Mpunga ninao nakamata zangu pipa nazama Dar nafanya UNYAMA MWINGI. Ukitaka ushauri njoo inbox acha kupaparika na kukimbilia mjini au Taasisi. Askari wa kweli hakimbiii Uwanja wa VITA.
Yaaani uko Tanganyika halafu unalia huna maisha???? Maajabu.
tukuyu 08 uko Sumbawanga unalia lia.
Ukitaka Utajiri usikubali kuajiriwa.
Unapoajiriwa tambua kwamba umrjisajili kwenye mnyororo wa Umaskini.
Tambua kwenye orodha ya Mabilionea Ilimwenguni kote halipo jina la Mfanyakazi aliyeajiriwa. So kama unatafuta utajiri acha kazi📌
Mkuu umeongea point mpaka kero, haya ndo madini tunayoyatafuta.
 
Siku hizi mkuu Ukitaka kwenda kusoma wanakusainisha Mkataba utakaokuzuia kuacha kazi kipind ukiwa masomoni au muda mfupi baada ya kumaliza masomo..
kwahyo Ngoma ngumu [emoji3][emoji3]

[emoji28][emoji28] huo mkataba hauvunjiki mana wife naye walimsainisha ila kamaliza anata kuhama.
 
Back
Top Bottom