NMB Tanzania Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri

Ushauri wa bure NMB, mimi nilifungua akaunti Mtwara nikiwa Mwalimu nimehama Mtwara tokea 2013. Kadi yangu ya ATM iliisha matumizi 2015.

Nilipoenda NMB Arusha ku renew nikaambiwa fuata kadi yako ipo Mtwara au nilipe 15,000 ili itumwe Arusha. Mimi pia ni mteja wa NBC lakini u
NBC wanatoa ATM card popote Tz. Hivi ni sahihi NMB Kuendelea na ukritimba huu wa kizamani? Nini maana ya teknolojia ya mtandao?

Kama naweza kutoa/kuweka fedha tawi lolote la NMB kwa nini kuhuisha ATM card iwe lazima kurudi tawi ulilofungulia?
 
Kati ya umaku wa huduma ni ile huduma kwa wateja,imenibidi niseme tu hivyo maana uvumilivu umenishinda sasa,mtu nina siku takribani 4 napiga tu more than 3 times per day lkn hakuna mhudumu anayepokea simu,nikajisemea huenda ni sikukuu na leo mtakuwa kazini lakini,leo nimeshapiga zaidi ya mara 8 hakuna mhudumu yeyote anayepokea simu.

Maswali yangu kwenug
1.Hicho kitengo cha huduma kwa wateja mmekifuta/mmekisimamisha kwa muda usiojulikana/wahudumu hawataki tu kuhudumiwa baada ya kuvimbiwa pilau na togwa za pasaka na hangover za viroba?
 
Kwanini huwa madirisha ya ma TELLERS nimengi Bt yanayotoa Huduma nimachache?
 
Utaratibu wenu wa kupeleka kadi kwenye branch ni mmbovu mtu anaweza kuomba kazi akakaaa mpaka miezi kadhaa hajapata tena kwa wale wale wanaoombea kadi kwenye branch tofauti na walizofungulia account yaani hamjari kabisa mpaka inaboa sana tambua huduma zenu za ndani ghalama iko juu sasa sijui mnafanya kusudi ili muendelee kukata zaidi sijui mnataka tupeleke haya mambo kwa mkuu wa nchi
 
NMB mnazingua na advance salari yenu,kama mlikuwa hamuiwezi kulikuwa na haja gani ya kuianzisha huduma hii?
vigezo ninanvyo ila nikiomba naambiwa muamala umeshindikana jaribu tena baadae mpaka salio limeisha,,
halafu custamer care yao ya ajabu sanaaa unaweza kukaaa hata saa zima ukisubiri KWENYE foleni simu ipokelewe daaah
SIO KILA KITU LAZIMA MKOPI NA KUPEST,,,MNATUTIA HASARA
 
Nmb kwanini nanunua salio kwa nmb mobile toka kwenye akaunti yanguhela inakatwa lakini sipati muda wa maongezi nilioomba? Imetokea mara mbili weekend iliyopita,majibu tafadhali
 
Boresheni system ya ATM pesa inayogoma kutoka kwenye machine iwe yarudu automatically kwenye account isiwe mpaka mtu ajaze claiming form
 
Nimetoka kuongea na customer care wenu hivi punde, ni washenzi sana yaan huyu dada ananikaripia wakati mi ni mteja? Shenzi.
 
Vipi NMB mna master card au VISA Kwa ajili ya online transaction
 
Swali kwenu nmb

Fedha kutoka nje ya nchi inachukua muda gani..Masaa mangapi kuingia nchini kwa ikitumia nmib swift code yenu?
 
Nahitaji kufahamu gharama za Makato kwa kila sms moja mnayomtumia mteja wenu anapo fanya credit au derbit?
 
Mimi imenitokea mara mbili nikitoa pesa kwenye ATM inatoka pungufu zaidi (wakati mwingine nusu) ya kiasi nilichoingiza wakati wa muamala. Na kama nisingehesabu pesa papo hapo kama wengi wetu tulivyozoea kwa kuziami ATM, ningesingizia uchawi.

Maana hata baada ya kupeleka malalamiko kwenye uongozi wa benki nilitakiwa kujaza fomu halafu nisubiri baada masaa 24 ndipo kiasi cha pesa kilichozuiwa na ATM kitarejeshwa kwenye akaunti.

Sasa maswali:-
Kwanza, je nisingegundua kuwa ilikuwa tatizo la ATM ingekuwaje?
Pili, je, kama ni weekend mfano Jumamosi jioni halafu ninadharura, au ninasafiri ningefanyeje?

Tatu, je, pesa iliyokatwa kwenye ATM hamwezi kuirejesha kwenye akaunti yangu bila kujaza fomu?
Nne, je tatizo hili hamwezi kulitatua? Maana kwa upande wangu limenitokea kwa nyakati mbili tofauti, tena kwenye matawi mawili tofauti.

Tano, nina akaunti kwenye baadhi ya benki pia lakini mbona kwenyewe hakuna risk kama hii?
 
NMB Magomeni Branch. Dar es Salaam. Kuna mwanamke anaitwa Joyce. Huwa anawazunguusha sana walimu wanaoomba mikopo hapo NMB. Walimu tumechoka kiasi kwamba wengi sasa wanakwenda benki ya walimu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…