NYARAKA: Katiba Inayopendekezwa Oktoba, 2014 (Tanzania's Proposed Constitution)

NYARAKA: Katiba Inayopendekezwa Oktoba, 2014 (Tanzania's Proposed Constitution)

Kama kwenye eneo la maadili umeona kitu kizuri kilichoandikwa na Chenge, basi huu ni ushahidi tosha kuwa hukuisoma Rasimu ya Pili ya Tume ya Marekebisho ya Katiba. Ukisoma rasimu halafu ukasoma Katiba pendekezwa, ndipo utaona jinsi gani Ile ya Sitta na Chenge ilivyo ya hovyo hovyo tena haistahili kupigiwa kura ya ndiyo.

Katiba Pendekezwa haitoi dawa ya kuinua uchumi bali inadidimiza uchumi wa Nchi. Kwa kuruhusu watu/watawala kujiwekea utaratibu wa kuhamisha uchumi wa nchi bila soni. Hivi ww unakubaliana na katiba inayoruhusu viongozi tena wa umma kufungua account za benki nje ya Tanzania. Tume ya Maadili kuwa toothless dog. Mawaziri wa nchi maskini kama Tanzania kuwa arobaini. Katiba kutotaja majina ya Wizara stahiki katika nchi, madaraka kurundikwa kwa mtu mmoja (Rais), mawaziri kuwa wabunge, kuwepo kwa haki zisizodaiwa mahakamani. TUMEISOMA hiyo katiba na rasimu yake, mambo ya msingi kwa Taifa letu yameondolewa, umebaki upuuzi tu. Please give me a break!!!!!!!!!!!



MAJIBU YAKO HAYA HAPA:
Nenda kaisome tena hasa hasa SURA YA TATU, Sehemu ya 3; MALENGO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KIUTAMADUNI.

Pia kasome SURA YA NNE; IBARA YA 29-(1) vifungu (a) hadi (h) kisha utakuwa umepata majibu yako.

Kuhusu idadi uliyoisema ya Mawaziri kuwa 40 nadhani umeweka kinyume ama hujaielewa Katiba hiyo, kwasababu SURA YA NANE ya Katiba Inayopendekezwa katika kipengele (b) Baraza la Mawaziri IBARA YA 115-(1) hadi (5) kimefafanua wazi wazi kuwa "Kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (1), Idadi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano HAITOZIDI AROBAINI". sasa wewe idadi hiyo ulosema wanazidi 40 umeisoma katika Katiba gani? ndo mana nakushauri uipitie kwa makini na kuielewa.
 
Nenda kaisome tena hasa hasa SURA YA TATU, Sehemu ya 3; MALENGO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KIUTAMADUNI.

Pia kasome SURA YA NNE; IBARA YA 29-(1) vifungu (a) hadi (h) kisha utakuwa umepata
majibu yako.

Kuhusu idadi uliyoisema ya Mawaziri kuwa 40 nadhani umeweka kinyume ama hujaielewa Katiba hiyo, kwasababu SURA YA NANE ya Katiba Inayopendekezwa katika kipengele (b) Baraza la Mawaziri IBARA YA 115-(1) hadi (5) kimefafanua wazi wazi kuwa "Kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (1), Idadi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano HAITOZIDI AROBAINI". sasa wewe idadi hiyo ulosema wanazidi 40 umeisoma katika Katiba gani? ndo mana nakushauri uipitie kwa makini na kuielewa.

hiyo katiba ni takataka .mambo muhimu mmeyatoa yani ni katiba ya kishenzi kabisa
 
Suala la miiko na maadili ya Viongozi na Watumishi wa Umma, Katiba Inayopendekezwa imeanisha vizuri sana katika Sura ya Nne, ambapo sehemu ya kwanza inaongelea maadili ya uongozi na utumishi wa umma na sehemu ya pili inagusia miiko ya uongozi wa Umma.

Hivyo kuna haja kubwa ya Watanzania kuzisoma kwa makini Sura mbalimbali za Katiba hiyo badala ya kutoa kasoro ama hoja zisizo na mashiko, kwani itakuwa jambo la aibu kudanganya Umma kuwa suala fulani halimo au limetolewa pasipo kuisoma vizuri na kuielewa kwasababu naamini mtu yeyote ambaye ameisoma kwa makini atakuwa na majibu ya hoja mbalimbali zinazoendelezwa na watu mbalimbali, mimi binafsi yangu mwanzo sikuielewa vizuri lakini nimejitahidi kuipitia kwa makini tena mara mbili mbili mpaka nimepata kugundua mambo kadha wa kadha yenye tija kwa maendeleo ya nchi yetu.

Ebu acha umburula wewe katiba hiyo inapatikana duniani hapa„„„„?
 
Nenda kaisome tena hasa hasa SURA YA TATU, Sehemu ya 3; MALENGO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KIUTAMADUNI.

Pia kasome SURA YA NNE; IBARA YA 29-(1) vifungu (a) hadi (h) kisha utakuwa umepata majibu yako.

Kuhusu idadi uliyoisema ya Mawaziri kuwa 40 nadhani umeweka kinyume ama hujaielewa Katiba hiyo, kwasababu SURA YA NANE ya Katiba Inayopendekezwa katika kipengele (b) Baraza la Mawaziri IBARA YA 115-(1) hadi (5) kimefafanua wazi wazi kuwa "Kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (1), Idadi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano HAITOZIDI AROBAINI". sasa wewe idadi hiyo ulosema wanazidi 40 umeisoma katika Katiba gani? ndo mana nakushauri uipitie kwa makini na kuielewa.
Ndg UFO nimeisoma na kuielewa, ndiyo maana nakwambia kuwa haitufikishi popote zaidi ya kuendelea kudidimiza Taifa. Malengo, malengo malengo yatabaki kuwa malengo, Malengo bila maadili thabiti ni kutwanga maji kwenye kinu, malengo bila uzalendo, uwazi na uwajibikaji kama tunu za Taifa ni kutwanga maji kwenye kinu tukitarajia kupata pumba za mahindi. Kuruhusu baraza kuwa na mawaziri Arobaini na kuogopa kuziweka wizara kwenye Katiba tena kwa majina ni ujinga uliopitiliza. Katiba inatakiwa izibe mianya iliyopo kwa kuweka majina ya wizara na kufunga ukurasa kwa kuandikwa idadi kamili ya wizara rejea rasimu ya Tume uone jambo hilo lilivyokuwa limwekwa vizuri/

bila maadili tuko chaka, ndg yangu mtanzania mwenzangu, Katiba pendekezwa haifai kabisa
 
Mimi siangalii umati, mimi naangalia content ya katiba. Hao waliokusanyika hapo wengi wamesombwa kwa malori, wengine wana maslahi na CCM, na wengine wamekuja kushanga farasi.
Moja ya matatizo makubwa ya nchii ni viongozi kujirundikia mali wananchi wa kawaida kuwa mafukala.

Mfano nimetoa hapo juu.
Mkuu wa mkoa anafanya madudu lakini mwananchi hana mamlaka ya kumwajibisha kwa kuwa yeye ni mteule wa Rais
Wakurugenzi wanaiba pesa lakini wako mwajiri wao ni Waziri mkuu, ambae ni mteule wa Rais
Rais anateua watu wasio na kiwango au marafiki zake anavyotaka yeye bila kudhibitishwa na wabunge
Wabunge wameongezwa zaidi

Haina tofauti na hii ya sasa

Bongo lala hakuna kitu hapa.....hivi wewe cant u imagine the impact of giving much power to citizen...we unataka machafuko wewe hivi upewe rungu la kumuwajibisha mtu unategemea nini....Jamani tunaamini hao wakurugenzi wapo watu wanaowaoongoza wanaoitwa wafanyakazi ambao in other sense ni wananchi kumbuka moja kati ya haki za wanafakazi wanahaki ya kugoma sasa unadhani kwa kufanya hivyo hamuwezi kumuondoa wasiowajibika halafu ndugu yangu kumbuka Katiba Inayopendekezwa imezungumzia suala la Maadili ya viongozi wa umma au labda ni quote hapo kwenye kipeperushi tena kwa Lugha nyepeeeeesi Kabisaa

KATIBA MPYA14.jpg

" AU HUYO MKURUGENZI AU MKUU WA WILAYA SIO MTUMISHI WA UMMA"
 
KATIBA INAYOPENDEKEZWA NI BORA KULIKO YA SASA, HONGERA MH. RAISI, HONGERA WATANZANIA.

Katika historia ya uandishi wa katiba mpya duniani hakuna nchi yeyote ambayo iliwahi kuandika katiba mpya ikakidhi matakwa ya wananchi wote na taifa kwa 100%. Katiba si msaafu wala si biblia kwamba haiwezi kufanyiwa maboresho. Leo hii jambo ambalo tumeliona lina tija na manufaa kwa taifa na tukaliingiza kwenye katiba, kesho tutaliona halina tija na tutakubaliana kuliondoa au kuliboresha. Vilevile jambo ambalo leo tumeliona halina tija na kutoliingiza ndani ya katiba kesho tutaona umuhimu wake na tutakubaliana kuliingiza ndani ya katiba yetu.

Katiba inayopendekezwa imetambua haki za makundi mbalimbali kama vile wakulima, wafugaji, wafanyakazi, wasanii, vijana, wanawake na wengine. Pia katiba inayopendekezwa imetambua haki bunifu, mgombea, binafsi, maboresho katika muungano wetu sambamba na kuweka mfumo bora wa kusimamia rasirimali za taifa na kudhibiti mianya ya matumizi mabovu ya rasirimali. Kundi pekee ambalo linadhani halijatendewa haki katika katiba hii ni kundi la wanasiasa wachache ambao kwao tafsiri ya katiba bora ni ile inayokidhi maslahi yao ya kisiasa. Hili ni jambo ambalo watanzania hawana budi kulikataa.

Jambo la msingi ambalo kila mtanzania anapaswa kukubali ni kwamba katiba inayopendekezwa ni bora kuliko ile ya sasa. Wakati ambapo baadhi ya watu wakiipinga na kudai kwamba haiwezi kulivusha taifa letu, wapo watanzania tena asilimia kubwa ambao wanaiona katiba inayopendekezwa kuwa ni chombo madhubuti ambacho kitachochea maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hatuwezi kuwa na mtazamo mmoja, na ikifika wakati watanzania wote tukawa na mawazo yanayofanana basi tujue kwamba tunapaswa kujitazama upya. Kutofautiana kimtazamo ni jambo la kawaida na
hiyo ndiyo afya ya demokrasia iache ichukue nafasi yake. Tupingane kwa hoja bila kuhatarisha amani ya taifa letu.

Hongera Mh. Raisi Dr. Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa uliyoifanya. Hili ni jambo la kihistoria ambalo halijawahi kutokea katika historia ya Taifa. Hii ni mara ya kwanza kwa Taifa letu kuandika katiba yake kwa kushirikisha wananchi wake. Yapo mataifa ambayo yaliwahi kuandika katiba zao kwa kutumia Bunge la katiba pekee, wapo waliogeuza Bunge la kawaida na kuwa Bunge la katiba. Kwa taifa letu, mchakato umekuwa wa kidemokrasia zaidi kiasi kwamba wapo wanazuoni, wanasiasa na mataifa mbalimbali ambao wameishangaa Tanzania kwa kuruhusu demokrasia kwa kiwango hiki. Kwa hakika Mh. Rais anastahili pongezi na daima watanzania tutakukumbuka na jina lako haliwezi kufutika katika fikra zao.

Hakuna pongezi hapo
 
Siitaji hata kusikia huu ujinga.

ongeza kufuri la 2 kwenye avatar yako ili uendelee kuverify uwezo wako wa kuelewa jinsi ulivyo mdogo,subiri wenzako wenye akili uone watakavyofanya maamuzi sahihi hapamwakati wa kupiga kura!
 
Ndg UFO nimeisoma na kuielewa, ndiyo maana nakwambia kuwa haitufikishi popote zaidi ya kuendelea kudidimiza Taifa. Malengo, malengo malengo yatabaki kuwa malengo, Malengo bila maadili thabiti ni kutwanga maji kwenye kinu, malengo bila uzalendo, uwazi na uwajibikaji kama tunu za Taifa ni kutwanga maji kwenye kinu tukitarajia kupata pumba za mahindi. Kuruhusu baraza kuwa na mawaziri Arobaini na kuogopa kuziweka wizara kwenye Katiba tena kwa majina ni ujinga uliopitiliza. Katiba inatakiwa izibe mianya iliyopo kwa kuweka majina ya wizara na kufunga ukurasa kwa kuandikwa idadi kamili ya wizara rejea rasimu ya Tume uone jambo hilo lilivyokuwa limwekwa vizuri/

bila maadili tuko chaka, ndg yangu mtanzania mwenzangu, Katiba pendekezwa haifai kabisa

Mwakaboko kwa jinsi navyokujua hujaisoma yote na kwa mtindo huo huwezi kuielewa ndio maana unataka kila kitu kiwekwe kwenye katiba,unataka katiba iseme mkulima atalima heka 20 tu, mfugaji mifugo 100, wizara zitakua 5, mawaziri 4 etc hiyo siyo katiba ninayoijua mimi itakua barua ya posa hiyo au mahali, naomba upumzike ukipata mawazo mapya urudi tena!
 
MAJIBU YAKO HAYA HAPA:
Nenda kaisome tena hasa hasa SURA YA TATU, Sehemu ya 3; MALENGO YA KIUCHUMI, KIJAMII NA KIUTAMADUNI.

Pia kasome SURA YA NNE; IBARA YA 29-(1) vifungu (a) hadi (h) kisha utakuwa umepata majibu yako.

Kuhusu idadi uliyoisema ya Mawaziri kuwa 40 nadhani umeweka kinyume ama hujaielewa Katiba hiyo, kwasababu SURA YA NANE ya Katiba Inayopendekezwa katika kipengele (b) Baraza la Mawaziri IBARA YA 115-(1) hadi (5) kimefafanua wazi wazi kuwa "Kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (1), Idadi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano HAITOZIDI AROBAINI". sasa wewe idadi hiyo ulosema wanazidi 40 umeisoma katika Katiba gani? ndo mana nakushauri uipitie kwa makini na kuielewa.

Mwakaboko a jumping human being kwenye kila msafara hata wa siafu yeye analazimisha kuingia tu.
 
Watanzania wote hatuwezi kuwa na msimamo mmoja, ila ccm mna msimamo mmoja. Lazima mjitizame, kwanini ccm wote mna mtizamo mmoja?

Kama wewe mwenyewe sio raia wa Tanzania utajuaje msimamo wa watanzania, huna jipya kwani nini cha ajabu watu kukubaliana kwenye mambo ya msingi? Au hilo nalo hulijui wewe???wewe hata bunge huwa hufuatilii!!!
 
Mwakaboko kwa jinsi navyokujua hujaisoma yote na kwa mtindo huo huwezi kuielewa ndio maana unataka kila kitu kiwekwe kwenye katiba,unataka katiba iseme mkulima atalima heka 20 tu, mfugaji mifugo 100, wizara zitakua 5, mawaziri 4 etc hiyo siyo katiba ninayoijua mimi itakua barua ya posa hiyo au mahali, naomba upumzike ukipata mawazo mapya urudi tena!
Nadhani jambo la muhimu nikubali kuwa natofautiana nawe kimtazama, Udhaifu ninaouona mimi, ww unaona ni strength ya Katiba pendekezwa. Mambo ambayo mimi nayaona siyo ya muhimu kuwemo ww unaona ni ya muhimu. Yale ambayo mimi naona ni vema yakawekwa. Ww unaona hayana umuhimu. Tofauti zetu ni za mtazama, Ila Katiba itapita but It won't last longer as expected. Inapita au inapitishwa I don't care, remember the cry for new constitution will start afresh.
 
Back
Top Bottom