Nyumba ya Oscar Kambona sasa ni Feza Primary. Nini kimetokea?

Nyumba ya Oscar Kambona sasa ni Feza Primary. Nini kimetokea?

Nadhani nyumba mikocheni inayojulikana Mama Kambona ameishi muda mrefu na kuimiliki ni ilipo Dsm International School (DIS).

Mwanae anayejulikana ni Neema aliyekuwa anafanya kazi British Council na baada ya kumaliza ndoa yake na Mchaga Masika akaamua kurudi Uingereza. Sidhani kama Kambona ana mtoto mwingine. Nadhani Kambona ana asili ya ugenious maana hata huyo neema ni kama akili zimezidi na kuwa fyatu kidogo in a good way.
Fytu kidog in good way wee jamaaa wee nimechek tu
 
Oscar Kambona ana mtoto wa kike ni Askari Magereza gereza la Karanga Moshi. Kama sikosei anaitwa Witness.
Huwezi amini mtoto wa kambona analipwa mshahara usiozidi TSH laki tano.
Ttzo liko wapi mkuu
 
sio kweli... labda kamaa ni mjukuu, kitukuu au kilembwe, kining'ina
Oscar Kambona ana mtoto wa kike ni Askari Magereza gereza la Karanga Moshi. Kama sikosei anaitwa Witness.
Huwezi amini mtoto wa kambona analipwa mshahara usiozidi TSH laki tano.
 
Nyerere alikuwa dikteta uchwara,hojs zake zote alizompinga nazo kambona zilikuja 'kuprove failure',kambona alikuwa anaona mbali kutokana na exposure na elimu,nyerere alikuwa amemezwa na wachina,akaishia kufeli kwnye kila kitu,azamio la Arusha lilifeli,vijiji vya ujamaa vilifeli,ujamaa wenyeww ulifeli aliachia nchi kwa aibu watu wakiwa hawana chakula Wala mavazi!!
Mtazamo wa nyerere haukuwa sahihi ila nia yake haikuwa mbaya kwa watanzania.
 
Oscar Kambona ana mtoto wa kike ni Askari Magereza gereza la Karanga Moshi. Kama sikosei anaitwa Witness.
Huwezi amini mtoto wa kambona analipwa mshahara usiozidi TSH laki tano.
Unataka alipwe shilingi ngapi??

Si kila mtu analipwa kulingana na kazi yake?
 
Kawaida ya binadamu Hana shukrani. Anapenda kulaumu vitu vidogo na kuacha mambo makubwa. Unasema mwaka 1961 tungeruhusu ubepari leo Tanznia ingekuwaje?. Unaongea hivyo kwa sababu hujayajua madhara ya ubepari. Mimi nashukuru Nyerere kukataa ubepari maana leo tu tunadaiwa trillion 82, je tungeruhusu wazingu wake mapema ingekuwaje?. Tungekuwa tunadaiwa trillion 200. Unapopinga Jambo Rudi nyuma ujiulize Ni kwa nini huko nyuma serikali iliamua ilivyo amua?.
sawa, lakini angalia mataifa mengine yaliyo opt ubebari tangu mwanzoni, madeni yao yakoje?
 
Mtazamo wa nyerere haukuwa sahihi ila nia yake haikuwa mbaya kwa watanzania.

Hii inatufundisha kuwa tujifunze kuvumiliana pale inapotokea tunatofautiana kimitazamo!
Sijafurahishwa na namna OSCAR KAMBONA alivyoikimbia nchi na kuishi ughaibuni Kama mkimbizi,Familia yake haieleweki iko wapi mpaka sasa!😞😞
Cha kushangaza hata familia ya Nyerere nayo wanaishi utadhani siyo royal family 🙄.MAISHA HAYANA MAANA,TUJIFUNZE KUHESHIMIANA.
 
Kama tu nchi ina wasomi wengi kwa sasa lakini UBEPARI unaitafuna nchi sijui miaka ile nyerere angekimbilia ubepari nchi ingekuwa na hali mbaya kiasi gani yani mali nyingi zingekuwa chini ya wazungu na mambo ya vita ya madini yanayoendelea CONGO yangekuwepo hadi leon tz maana wazungu wasingekubali kutolewa kiboya na kwa umaskini wa enzi zile tungeuzwaa aisee so NYERERE alitumia akili sana kuukataa ubepari ila kilichomuangusha ni UJAMAA kufail...!! NYERERE angkuwa na ubepari bhasi amini hakuna Rais wa afrika angemfikia utajiriii hata nusu ila ajabu mzee yule hakuacha hata hisa yoyote sio kwamba alishindwa ila alifanya alichokihubiri UJAMAA jambo waliloshindwa viongozi asilimi 98 wenye asili ya kiafrika.
 
Hakuna askar magereza anaelipwa chini ya laki 5 huyo ni muongo...........

Kama ishu ni kuambiana ukweli basi shika hii
Askari Magereza, askari Polisi, fire wanaoanza kazi salary ni laki 4+ kwa mwenye Form 4
Kwa degree ni laki 7+

Sijui Immigration wanalipwaje lakini bila shaka wanaendana kwenye salary wakatofautiana marupurupu na mishe mishe binafsi.
 
Kama tu nchi ina wasomi wengi kwa sasa lakini UBEPARI unaitafuna nchi sijui miaka ile nyerere angekimbilia ubepari nchi ingekuwa na hali mbaya kiasi gani yani mali nyingi zingekuwa chini ya wazungu na mambo ya vita ya madini yanayoendelea CONGO yangekuwepo hadi leon tz maana wazungu wasingekubali kutolewa kiboya na kwa umaskini wa enzi zile tungeuzwaa aisee so NYERERE alitumia akili sana kuukataa ubepari ila kilichomuangusha ni UJAMAA kufail...!! NYERERE angkuwa na ubepari bhasi amini hakuna Rais wa afrika angemfikia utajiriii hata nusu ila ajabu mzee yule hakuacha hata hisa yoyote sio kwamba alishindwa ila alifanya alichokihubiri UJAMAA jambo waliloshindwa viongozi asilimi 98 wenye asili ya kiafrika.
Naamini binadamu ni mbinafsi kwa asili... Ujamaa ndo maana umefail Dunia nzima.
 
Mtandaoni wakati mwingine muandishi anaweka yale anayoyajua tu. Je huko mtandaoni kuna taarifa kuwa watoto wake walirudi Tanzania au la? Kuna taarifa wako wapi kwa sasa?
Vilevile, kama wao - Kambonas - hawana shughuli nayo, je wakiwapangisha wengine ni dhambi?
 
Lakini Kambona kaonekana ndie aliyekuwa sahihi kuliko Mwalimu. Yafanyikayo sasa ni mawazo ya Kambona ya Nyerere yalishakufa kibudu
Kambona alikuwa mwanglikana dini ya uingereza iliyotawala Tanzania

Nyerere alikuwa mkatoliki ila hakuwa na ubaguzi wa kidini .Akamwamini sana mtu wa kusini mngoni muislamu anaitwa Rashid Kawawa mtu mwaminifu sana kwa Nyerere
aliyemwachia hadi Nyerere uongozi wa chama

Kawawa ndie aliyewaleta watu wa kusini waangilikana akina Kambona ,nk aliowaamini kuwa ndugu zake kutoka kusini walikuwa wengi sana kutoka Malawi hasa
Nyerere akawapa uongozi

Sasa wao wakawa huko makanisani Anglikana wanapanga kumpindua Nyerere katoliki!! Kilichofuata waangilikana wengi sana wakubwa walidakwa na kuswekwa ndani Kambona kiongozi wao akakimbia nchi!! Wamalawi Anglican kibao wakaswekwa ndani Miaka Nadhani Mwinyi ndie aliwaachia
 
Oscar Kambona ana mtoto wa kike ni Askari Magereza gereza la Karanga Moshi. Kama sikosei anaitwa Witness.
Huwezi amini mtoto wa Kambona analipwa mshahara usiozidi TSH laki tano.

Ulitaka alipwe shingapi?

Unataka watu waanze kulipwa mamilioni just cos ni watoto wa fulani? Kina Ridh, Pinda, Sokoine, Makongoro nk ni wabunge na nafasi zingine kadha wa kadha na yeye apambane ashike wadhifa hakuna free lunch.
 
amini tena ukiangalia marais walivyojimbikizia mali...
Hivi unajua baada ya tanesco office ya kinondoni mbele yake kuna kiwanja kikubwa kimezungushwa uzio,mmiliki ni mama Maria Nyerere....
Miaka nenda rudi hakiendelezwi
Sasa sijui hana mpango huo au ndiyo
Familia haina mawazo ya biashara kuwekeza

Ova
 
Back
Top Bottom