Nyumba ya Oscar Kambona sasa ni Feza Primary. Nini kimetokea?

Nyumba ya Oscar Kambona sasa ni Feza Primary. Nini kimetokea?

Wazoefu wa mitaa ya Mikocheni, kwa Nyerere, kwa Mwinyi, kwa Warioba haya ni majina ya vituo vya daladala. Lakini pia Kuna nyumba ya Oscar Kambona mitaa hiyo ila kwa sasa naona imekuwa shule ya msingi Feza.

Nini kilitokea? Iliuzwa? Je Kambona hakuacha familia? Mke na watoto wake wako wapi? Baba akiwa muasi hadi familia yake inachukuliwa kama waasi?

Je, ilikuwa ni nyumba ya serikali au alijenga mwenyewe Oscar?
Kambona aliasi Nini !??? Hivi Hawa waliogeuka wote na walikuwa na Magufuli SI ndio waasi !!?? Kambona alisema mwenendo wa nchi Kwa sera za kijamaaa tutachelewa maendeleo hana uasi wowote zaidi ya kusema ukweli wake .
 
Oscar Kambona ana mtoto wa kike ni Askari Magereza gereza la Karanga Moshi. Kama sikosei anaitwa Witness.
Huwezi amini mtoto wa Kambona analipwa mshahara usiozidi TSH laki tano.
Huyo mtoto hatambuliki katika familia hebu muulize vizuri..
 
Kambona aliamini siasa za ubepari na akiwa Waziri akishaingia mikataba mingi na wawekezaji wa Kiingereza na walimpa cha juu chake. Kwenye account yake alikua na pesa nyingi sana.

Wakati Nyerere aliamini katika Ujamaa, hakuwa na tamaa ya pesa na mpaka anastaafu hakuwa na hekalu alilojimilisha.
Umewahi sikia upande wa Kambona mwenyewe?
 
Kwa msiolijua, Rashid Mfaume Kawawa alikuwa mjomba wake Oscar Kambona na ndiye aliyesimamia harusi yake Kambona, wote asili yao Wanyasa. Enzi hizo miaka ya sitini kila mwanaume na mwanamke alipenda afanane muonekano wa Oscar Kambona, the guy was extremely smart.
Kutoka mkoa mmoja sio undugu...
Nyasa na Tunduru Kuna umbali Sana
Zamani zile Wilaya ya Mbinga Jimbo la mbinga magharibi ndio Nyasa huko kwao Bambo Kambona, Namabengo/ Namtumbo wilaya ya Songea vijijini uelekeo wa Tunduru ndio kwao Mzee Kawawa, hawana huo undugu uusemao

Wewe itakuwa Chirwa wa mchongo imeshindwa tofautisha Mnyasa mwenzio na myao.
 
Oscar Kambona ana mtoto wa kike ni Askari Magereza gereza la Karanga Moshi. Kama sikosei anaitwa Witness.
Huwezi amini mtoto wa Kambona analipwa mshahara usiozidi TSH laki tano.
Kumbe mshahara wa askari magereza unategemea wadhifa wa mzazi
 
Ile nyumba ilichukuliwa na Serikali. Ilipokuwa guest house ya Serikali mimi niliishi pale muda mrefu. Halafu baadaye ikarudishwa kwa Familia ya Kambona. Yule binti yake akaigeuza kuwa shule ya English Medium. Ah,yes. Kuna shule moja hapa naona kila asubuhi magari mengi yanakwenda pale, very heavily fortified, nadhani ndio shule hiyo.
 
Kwa msiolijua, Rashid Mfaume Kawawa alikuwa mjomba wake Oscar Kambona na ndiye aliyesimamia harusi yake Kambona, wote asili yao Wanyasa. Enzi hizo miaka ya sitini kila mwanaume na mwanamke alipenda afanane muonekano wa Oscar Kambona, the guy was extremely smart.
Hawa watu hawakuwa ndugu.kambona ndio mnyasa.kawawa sio.
 
Kwa msiolijua, Rashid Mfaume Kawawa alikuwa mjomba wake Oscar Kambona na ndiye aliyesimamia harusi yake Kambona, wote asili yao Wanyasa. Enzi hizo miaka ya sitini kila mwanaume na mwanamke alipenda afanane muonekano wa Oscar Kambona, the guy was extremely smart.

Kambona ndie alikuwa mnyasa.sio kawawa
 
Ulitaka alipwe shingapi?

Unataka watu waanze kulipwa mamilioni just cos ni watoto wa fulani? Kina Ridh, Pinda, Sokoine, Makongoro nk ni wabunge na nafasi zingine kadha wa kadha na yeye apambane ashike wadhifa hakuna free lunch.
Acha kukurupuka.... Soma taratibu uelewe acha kukaza fuvu.
 
Huyu Mzee Kambona alirudi early 90’s. Alipanga Sinza njia ya Lion Hotel kama waenda kwa Mwaibula. Alitaka kurudishiwa hiyo nyumba na akapewa. Wanadai familia waliiuza. Kiafya hakuwa vizuri na alikuwa amechoka sana. Hawakuwa na mapeni kama zamani.
Haieleweki baada ya kuuza wamejichimbia wapi. Mrs Kambona bado alikuwa fit cheupe dawa na uzuri ule ule pamoja na utu uzima wake.
 
Kambona aliamini siasa za ubepari na akiwa Waziri akishaingia mikataba mingi na wawekezaji wa Kiingereza na walimpa cha juu chake. Kwenye account yake alikua na pesa nyingi sana.

Wakati Nyerere aliamini katika Ujamaa, hakuwa na tamaa ya pesa na mpaka anastaafu hakuwa na hekalu alilojimilisha.
Aliyekwambia walimpa cha juu nani?? Acha kuamini propaganda za mchonga,aliamini ujamaa haukuwa mfumo sahihi na kweli ilikuja kuthibitika baadae baada ya kila kitu cha ujamaa kufeli na mchonga kulazimika kung'atuka kwa aibu!
 
Unatoka kijiji gani?
Ukirudi kijijini kwenu huwa unapotea njia?
Tambua mawazo ya kujenga vijiji ni Nyerere mwenyewe. Mawazo hai, bado yanaishi na utayaacha yakiboreshwa.
Ujamaa kama ilivyo via Tamu, watu watafanya biashara na watakopeshana kwa mtindo wa kijamaa (vikoba)
Tz vijiji vilikuwepo kabla ya nyerere,na aina ya ujamaa tunaouishi haukuanzishwa na nyerere ni historia yetu kabls ya ujio wa wakoloni,vijiji vya ujamaa vilianza pale nyerere alipotaka kuua vijiji halisi na kuanziaha vipya kwa minajili ya kuzalisha mali pasipo teknolojia wala nyenzo,watu wakusanywe wapelwkwe mwanalumango wakaanze maisha mapya ya kilimo cha jembe la mkono,hapo ndo failure ilipoanza!
 
Si vyema kumuita hivyo, fuatilia wenzake wengi waliojizipatia nchi zao uhuru hio miaka ya 60's, sidhani kama ulikuwa umezaliwa.

Angeweza kujilimbikizia mali na madaraka kwa familia yake mpaka leo hii isingeshindikana.

Ukizingatia ni wakati ambao waTanzania wengi hawakiwa na elimu.
So tumsifu kwa uzalendo wake, kwa mali iliyopo kwenye hii nchi sijui ingekiaje tungepata raisi mwenye tamaa.
Kwan kuna nchi gani ya maana tuliyopata nao uhuru tumeizidi kuuchumi licha ya mali tulizonazo?? Huyo mzee aliyeondoka nchi watu wanavaa magunia wanakula ugali wa njano kila kitu kwa foleni ndo wakumtukuza??? Hapana,miaka yake utawala ndo iliturudisha nyuma kama taifa!ilikuwa miaka 24 ya kupima marktime,ubaya zaidi waliomkosoa hakutaka kuwasikiliza mpaka aliposhindwa
 
Wasiwasi wa Nyerere angeruhusu ubepari nchi ingemshinda maana wazungu wangerudi mapema sana na kumiliki rasilimali kama Zimbabwe na South Africa
Hata ambapo hakuruhusu mbona nchi ilimshinda??chukua mfano wa wakati anakabidhiwa nchi na wakoloni mwaka 1961 na kipindi anaikabidhi kwa mwinyi 1985,viwanda vyote vilikufa,uzalishaji ulisimama,mahitaji muhimu yalipayikana kwa foleni..,
 
Sijaongelea socialism, naongelea Ujamaa. Ujamaa ni tofauti na socialism.
Ujamaa una bond zake tofauti na socialism.
Rudi kafanye utafiti, usikalili ya kuambiwa.
...Usikariri....!
 
Bora angewaacha wamiliki tu maana kungekua na nafuu mara dufu na tulivyo,Leo tusingekua tunakopa matrillion Ili kujengea matundu ya vyoo
Ni aibu alibanaaaaa mwishowe akaachia mwenyewe Tena Kwa kufail kubaya kabisaa!
...Afrika Kusini au Zimbwabwe Kuna Amani?
 
Back
Top Bottom