Nioroedheshèeee kwenda no 15777
Niliombwa niende nikamwone mtu kumbe huyo mtu aliandaa vitendea kazi vya kuniua . 1. Nilikuta kisu, 2. Kitambaa cha dawa . Ila sijaingia ndani alinikaribisha akajisahau kuficha eh jamani alipona nimeona alikasirika akaanza kunikimbiza na taulo . Cha ajabu niliwahi toyo fulani tena mdada aliniwahia toyo kupanda mbele namuona kawa kama shetani ai yaani niliogopa sana mwisho wa siku nikaamua kumkemea nikafika nyumbani kwa shida .
Alikuwa akipaa angani kama nini ananinisukumia magari , toyo zinipe ajali. Tulitaka kwenda kugonga mti ila haikuwezekana kwa imani .
Nikafika nyumbani ile nimelala akanza kuniita wakaja na watu wawili wamevalia makanzu meupe , wananiita wananipiga na mijeledi , aisee nilipigwa hadi basi . Nikaamka nimekatwa ,nimechapwa nimevimba . Nikaona niongee na majamaa zangu wakanipeleka kwa shekhe akaniombea akanipa dawa .
Mwingine akaanza kuniandama wewe nilipomkubalia akaanza kujionesha ananipenda kumbe uongo nilipomtumia picha nikaanza kuota makaburi majeneza , aisee nikaona utani kila mahali nakutana na majeneza misafara ya misiba nilipo enda tena kwa shekhe akaniombea akanipa dawa yakuofa nakunywa nilitoa vitu vingi tu sisemi kuanzia hiyo siku nikasema ngoja nipunguze kutaka wanaume humu .
Aisee kumbe nikaombwa tena sana sana nipendwe , nikapendwa weh huyo ndio mkali sasa alikuwa ananiuguza na vitu vingi siwezi sema hapa nabado sijamwona . Aisee nilipewa heka heka hadi nilipopona ni kazi kweli nilitapika tena shanga , sibenge , hirizi 3 na nyoka wawili . Na alitajwa jina lake aisee mpaka sasa nimekoma sitaki tena hawa watu wajf bora nikae zangu pembeni nisije nikafa kwa sababu ya hawa viumbe wa humu kuna huyu au ngoja nikae kimya
Ila nimeteswa humu kuna huyu mlokole tukaanza powa akaanza kunionyesha dalili yakuja home .
Ila nilivyokuwa nimeshakamilika mbwa huyu akanza vibwangwa nikawa naota ndoto niko kanisani mbele ya mimbara wa tu wanaimba mie napigwa miti namchungaji halafu hao watu waumini wako kama wanashangilia nikaona nimuache nakujiombea nakumkana sijamwonaga tena nikaanza kulala vizuri na nilikuwa namka nimechoka na kama mananiliiu ya mwanaume kabisa unayakuta naupo kama ulitumiwa kweli.
Acha tu. Na visa hadi basi