Ombi kwa Rais Samia: Sheria Mpya ya Uchaguzi Bado ina Ubatili. Haki ya Kuchagua na Kuchaguliwa imeporwa! Irejeshwe kwa Mujibu wa Katiba!

Ombi kwa Rais Samia: Sheria Mpya ya Uchaguzi Bado ina Ubatili. Haki ya Kuchagua na Kuchaguliwa imeporwa! Irejeshwe kwa Mujibu wa Katiba!

Shida nchi imetekwa nyara na CCM wakisaidiwa na JWTZ, Polisi na TISS. As long as hao watu wanaona CCM haina shida hakuna mabadiliko yoyote.
Katika mazingira haya ni wendawazimu kuendelea kushiriki chaguzi za nchi hii. Inatakiwa wananchi wengi wapuuze kupiga kura, hapo tutakuwa na nguvu ya kudai chaguzi za haki. Kinyume na hapo kuendelea kushiriki chaguzi hizi ni kuzipa uhalali usiostahili.
 
Kama ni ombi kwani kuna ulazima kulikubali? Tukisema tudai Katiba MPYA yenye misingi mizuri hamtuelewi, Sasa haya maombi mpaka lini? Kila kitu Rais tunaomba, Rais tunaomba, Hivi Watanganyika tutaamka lini kwenye huu usingizi wa pono? Nchi imeachwa mikononi mwa mtu mmoja anatufanya avyotaka halafu tupo tu kama mazezeta. 🚮🚮🚮
 
Tatizo sheria nyingi zinazohusu siasa, chama Tawala lazma ziwe na manufaa kwa CCM
Uhuru wa kuchagua au kuchagulia lazima suala la mgombea binafsi lizingatiwe. Maana ni haki na uhuru wa mtu (awe mpiga kura au mgombea)
Nakumbuka comredi Mtikila alivyopambambania hili jambo
 
Katika mazingira haya ni wendawazimu kuendelea kushiriki chaguzi za nchi hii. Inatakiwa wananchi wengi wapuuze kupiga kura, hapo tutakuwa na nguvu ya kudai chaguzi za haki. Kinyume na hapo kuendelea kushiriki chaguzi hizi ni kuzipa uhalali usiostahili.

Maamuzi hayo ndio mtaji wa CCM, maana wale wanao susia kupiga kura kisasa madudu ya CCM wanapunguza idadi ya kura kwa wapinzani, sababu CCM wataenda na wataongeza idadi ya kura zao

cha msingi kuwepo na tume huru ya uchaguzi
 
Haki inaombwa kwa Rais Samia! Haki inaombwaga?
Japo haki sio hisani, ni stahiki, lakini kwa mfumo wetu, haki ni hisani, Asante Rais Samia kwa kuwasisitiza watendaji wa vyombo vya haki kuwa haki sio hisani, bali ni stahiki. Watende haki, tubadili Katiba kurudisha haki
20240602_145636.jpg


Pia niliwahi kuuliza Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga. Kuzuiwa bila kifungu, kuruhusu bila Kifungu. Ni hisani ya Rais Samia. Haki kuhisaniwa hadi lini?
P
 
Yaani haki ni hisani kwa watanzania na siyo sharti la kikatiba
Kwa Tanzania, haki ni hisani!, na it's very unfortunately hatuna upinzani wowote wa maana wa kudai haki au kuipigania. Angalia hapa nilichosema
View: https://youtu.be/A_YPEHtM9WM?si=3Cm92lS5twafkRko

Watanzania wanategemea kuhisaniwa haki zao kwa hisani ya Mkuu wa nchi.

Ndio maana alipopiga marufuku mikutano ya vyama, tuliuliza
View: https://youtu.be/Ta0URHvUlko?si=3vP9ZC99u3XU_Sy6

Mama aliporuhusu mikutano ya siasa, pia tumeuliza, Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga. Kuzuiwa bila kifungu, kuruhusu bila Kifungu. Ni hisani ya Rais Samia. Haki kuhisaniwa hadi lini?

Mimi mwenyewe najihesabu ni mtetezi huru wa haki, huu ubatili wa katiba nimeuzungumza sana.

View: https://youtu.be/3a4SjkV46JY?si=rS6X-ttZFwtlbcyy

View: https://youtu.be/PBpjDhH2XiA?si=y3wvuR5p0UBD03cn

View: https://youtu.be/lBC3xKODSvY?si=SNx0DquDv8knTt1p

P
 
Huwezi kusema hakuna upinzania na wakati Lisu na team yake kila siku wanashambulia na CCM wanafanya ziara ambazo hata wao hawajui wanafanya ajili ya nani
 
Wanabodi,

Zawadi yangu kwa Birthday ya Mama nilipanga kumpa wiki ya mwisho ya October 2025,

Ili zawadi hii iwe na manufaa kwake, nikisubiri mpaka hiyo 2025, it might be a bit too little too late, kuna ubaya hiyo zawadi, kutolewa mapema mwaka huu ili iweze kutumika mwaka kesho?.

Zawadi yenyewe ni Salaam tuu za Birthday zenye ki parcel fulani!

HBD Mhe. Rais Samia kwa kutimiza miaka 64!, nakupongeza sana na kukuombea afya njema!.

Mwakani 2025 utakuwa unatimiza umri wa miaka 65 na 2030 utakuwa na umri wa miaka 70, hivyo zawadi yangu ya pekee kwako ni HII na kukusisitizia, sio lazima kuizingatia saana kivile, ila ni muhimu kuisikiliza na kujisikilizia kama na wewe pia uliambiwa kama nilivyoambiwa mimi, kwasababu yule YEYE, sometimes ana tabia na mtindo wa kuwaambia watu wake, kupitia kwa watu wengine!, hivyo just listen and try to make sense of this, a think about it, if makes any sense to you, ikitokea it doesn't make any sense to you, then dismiss it as just another set of crap!.

Ila ikitokea na wewe pia uliambiwa, but you are not very sure kama ni YEYE au ni yeye, then don't take a chance!, usipuuze!, maana hicho kitu chenyewe, is nothing compared!.

If this being the case, then tunakuomba sana sana sana, ututekelezee haya mambo tunayokulilia nayo tangu umeingia kwenye usukani, tekeleza tuu yale yaliyomo ndani ya uwezo wako, maana kusubiria post 2025, it might be too little too late!. Please Mama!.


Na ikitokea wewe hujaambiwa mpaka 2025 inaingia na hujawahi kuambiwa na mtu mwingine yeyote, then ipuuze HII itakuwa sio sauti yake YEYE bali itakuwa ni sauti ya yeye tuu ambaye sio YEYE!.

Hivyo endelea na ule mpango wako wa 2025!, na Watanzania wanaolitakia mema taifa letu hili, wote tutakuwa Tuko nyuma yako,
Tuko pamoja nawe,
Tuko nawe!.

Mungu Akubariki Sana!.
HBD Mamaa!.
Paskali
HBD Rais Samia!.
P
 
Back
Top Bottom