Open Letter: Rais Samia, TRA isiyo na Support yako, ni Kifo cha Taifa

Open Letter: Rais Samia, TRA isiyo na Support yako, ni Kifo cha Taifa

Huyu mleta hoja unaweza kudhani ni raia mwenye nia njema! Lakini huyu anaweza kuwa mmoja wa watumishi vi.laza wa TRA waliokuwa wanapata rushwa kubwa kutokana na mfumo haramu wa Task force kukusanya kodi! Mhe .Rais Mama Samia kuwa macho sana na hawa "_Majambazi" waliojificha TRA.
Kodi ni sheria (Tax law Act) ,kila kitu kuhusu aina za mapato( taxable income) zimeainishwa vizuri na namna ya kutoza kodi! Sasa shida inakuja wapi kama sheria hiyo inafuatwa?!
Huyu ni mmoja wa watoza kodi walioxoea kutumia NGUVU badala ya AKILI!
Sasa anaona mfumo uliokuwa unawapa rushwa kubwa kubwa unakufa na wao walishazoea kujinufaisha!
Cha msingi sana wigo wa walipakodi uongezeke( tax base) na sheria ya kodi ifuatwe, kodi itakusanywa kwa wingi tu na malengo ya trillion 2 kwa mwezi yatafikiwa.

Kunyanyasa wafanyabiashara kwa vitisho na ubabe siyo njia endelevu ya kuongeza mapato ya Serikali.
Mtu anapoleta hoja kinyume ya unavyofikiri wewe usimuattack yeye kama yeye, attack hoja zake. Btw mimi sio mfanyakazi wa TRA na sio mnufaika kwa namna yoyote ile. Ila nimetoa experience baada ya kuona realities na mjadala wa baadhi ya maafisa wa TRA ambao tupo nao mtaani.

In simple terms, I am doing this not for personal gain rather for National Interest.
 
Mara ya kwanza nilipotoka Tanzania kwenda Switzerland na baadaye Australia, nilijiuliza sana kama na sisi huku Tanzania ni wanadamu kamili.

Nchi za wenzetu, wanaheshimu sana utu na ubinadamu wa watu wote. Hiyo haijalishi mwanadamu huyo ni kiongozi, raia wa kawaida au mtuhumiwa.

Kuna wakati nilikuwa Switzerland, ikaja kujulikana kuwa kuna Wasudan waliingia kwa kupitia mataifa mengine bila kufuata taratibu. Kwa vile Wasudan ni weusi, hivyo kila mweusi alitiliwa mashaka.

Nakumbuka wakati huo nikiwa kijana kabisa, polisi waliponijia, waliniambia:

English, French, Germany? Nikawaambia, English. Kisha wakaendelea:

"Excuse me Sir, my name is ---------, accompanied by ------ and ------. Our main duty is to enforce the law. We want to clear ourselves. We would like to confirm - you are in a country after having met all the immigration requirements. If you don't mind, can we see your passport?

Baada ya kuwaonesha passport yangu, wakatizama sehemu ilipogongwa visa yangu, wakanirudishia. Kisha wakaniambia. We are done. Thank you for your cooperation.

Kisha wakaniuliza, is Tanzania a nice country? Nikawaambia Yes. Mmoja akauliza, do you know Zanzibar, nikawajibu. Wakaniuliza, it is in which part of Africa, nikawajibu. Hapo niling'amua kuwa ingawa tulikuwa tunaendelea na mazungumzo ya kawaida, hawa bwana walikuwa bado kazini. Walikuwa wanataka kujua kama kweli mimi ni Mtanzania, na hiyo passport ni halali, na wala sijapata, pengine kwa njia za panya.

Baadaye, wakaniomba msamaha kwa kunipotezea muda. Mmoja akanipa business card yake, na kusema, feel free to contact me in case you have uncomfortablly been treated by any one while in the country.
Lovely
 
Kwa kweli unastahili kupewa nishani ya Mzalendo mkereketwa! Mungu akubariki sana! Wafanyabiashara ni watu muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa. Tatizo ni kwamba watanzania hatuna elimu ya kodi kama sehemu ya uzalendo. Tangu chekechea mpaka chuo kikuu hakuna mahali elimu ya kodi na umuhimu wake inafundishwa!
Kwa hiyo karibu wafanyabiashara wote hawalipi kodi kwa hiari! Ukiwapa mwanya watakwepa kodi au watatoa kodi kwa udanganyifu! Kwa sababu ya mazoea ya kukwepa kodi, wafanyabiashara wakifuatiliwa vilivyo kuhusu kodi wanahisi wanaonewa! Wakitoa kodi wanahisi faida inapungua maana walizoea kuifanya kodi iliyopaswa kulipwa kama sehemu ya faida!
Kwa sasa hivi TRA watakuwa na wakati mgumu sana wa kufuatilia kodi, maana wametafisirika kama vile walikuwa wanabambikiza kodi! Mama huu ushauri uliopewa ni wa muhimu sana! Wasaidizi wako wengine wanaweza wasikushauri huku wakitazamia ukwame halafu waseme hakuwa anakubali ushauri! Kwa mazingira ya Tanzania hiki kizazi chetu ni cha kulipa kodi kwa lazima wala katika hili tusidanganyane! Tuwekeze kwenye elimu ya kodi tangu chekechea ili vizazi vijavyo vione fahari ya kulipa kodi!! Mama kaza buti kabisa kwa habari ya kodi ikiwezekana katika hili uwe mkali kuliko mtangulizi wako. Ukikamata mkwepa kodi mfilisi kabisa ili wengine waogope! Vinginevyo we are bound to fail!
Asante
 
Labda nikuulize swali mkuu,umetumia njia zote za kiungwana ili mfanyibiashara alipe kodi na halipi,what do you do,a straight answer please.

Unajua,nilitegemea Rais asisitizie juu ya umuhimu wa wafanyibiashara kulipa kodi kama sheria inavyowataka kufanya.Then nilitegemea aseme kwamba kwa mfanyi biashara yeyote ambaye hatapenda kulipa kodi kwa hiari,sheria itachukua mkondo wake,kwa kuwa zipo sheria.

Mkuu huwezi kumbembeleza mfanyibiashara asiyetaka kulipa kodi kwa hiari.Ukimbembeleza hata lipa.Lazima sheria zimbane ili alipe.
Watu wanataka kulipa kodi halali na rafiki badala ya kutegemea harrassment kama njia ya kukusanya kodi pamoja na faini.Badala ya TRA kumshauri Rais kuhusu maeneo mapya ya kodi ili kupanua wigo wao wanasusa ni kwa vile wamefika mwisho wa kufikiri. Waangalie vyanzo vipya eg kuna taxi bubu nchi nzima hazilipi kodi mbona hawajashauri walipe wao wanakazania traditional methods tu.Rushwa !Rushwa!
 
Mhe Rais, naomba utumie dakika chache kusoma barua hii wewe mwenyewe, na kama hautapata muda naomba wasaidizi wako wakusaidie kuusoma na kukufikikishia.

Naandika haya kama Raia aliye na wasiwasi baada ya kutafakari kwa kina juu ya "TONE" yako uliyokwishaitoa hadharani kuhusu taasisi hii nyeti inayokusanya mapato ya nchi.

Pia ni baada ya kukaa na baadhi ya maafisa kodi ambao wanakiri kwamba toka kauli yako kazi yao imekuwa ngumu kupindukia ni kama wamewekwa benchi!

Mhe. Rais, kwa sasa kuna mambo makuu mawili yanayotokea ambayo sidhani kama umeshayajua.

i) Wafanyabiashara wameacha kutoa risiti za EFD na ukiwadai wanasema kabisa WASISUMBULIWE maana Rais wao ameshatoa maelekezo hayo. Wapo HOLIDAY!

Hata TRA wenyewe wamecancel mazoezi ya ku-enforce utoaji risiti. Maana wanajua wakienda watabagazwa!

Swali kubwa hapa, Je, Kodi gani itakusanywa na nchi bila watu kutoa risiti? Unawezaje kutrack mauzo ya mlipa kodi bila kutoa risiti ya EFD?

ii) Wafanyabiashara hawapeleki tena malipo ya kodi kwa kama kasi ya awali, kila mmoja ameset mind ya kupinga kodi maana anaona kama kile alichokadiriwa si sahihi baada ya kauli ya Rais.

Wataalam wenyewe wanasema impact yake itaonekana katika taarifa za mapato mwezi huu na ijayo!

Mhe Rais, katika taasisi zote chini yako zinazohitaji Top Level Presidential Support ya moja kwa moja ni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Bila TRA yenye support ya Rais, Taifa linakufa, na hakika litashindwa kufikia malengo yake.

Ni sawa na katika taasisi za kawaida, kitengo ambacho kinaleta mapato kwa taasisi, ndicho Mkurugenzi Mkuu hukitolea macho na kukipa support yote inayohitajika ili aweze kufikia malengo yake kibiashara.

Mhe Rais, sitaki kurejea katika maagizo yako ya nyuma kuhusu namna TRA wanavyofanya kazi ambayo uliyatoa hadharani, ila ningekuwa mmoja wa washauri wako ningeshauri usiongee sentensi zile hadharani bali uongee moja kwa moja na Viongozi na Wafanyakazi wa TRA indoors.

Kwa nini??. Kwa sababu nature ya mfanyabiashara ni kulalamika na kuficha mapato yake halisi. Hakuna mfanyabiashara hata mmoja aliye genuine ya kipato chake, Popote duniani. Hakuna!

Mhe. Rais, unaweza kukuta mfanyabiashara anafanya biashara yenye mauzo ya Billioni 2 anadeclare faida ya milioni 4, Seriously?

Katika mazingira hayo unahitaji Taasisi yenye nguvu na mamlaka ili iweze kutafuta wapi mtu huyu alipodanganya ili Serikali iweze kukusanya kodi yake. Otherwise, utachukua hio hio Milioni 4 alafu maisha yanaendelea wakati kwa hakika labda mtu huyo alipaswa kulipa milioni 50.

Mwisho:
Natambua kupitia maneno ya Makamu wako, Mhe. Mpango, umeweka malengo ya Trillion 2 kwa Mwezi, lakini ukweli ni kwamba hata kama sheria zitabadilika na baadhi ya kodi kupungua lazima kuna nyingine zitapanda ili kufikia lengo la Trillion 2. Sasa nani atatumika kuenforce ukusanyaji huo? Je ni hao hao TRA? Je wataweza ku-enforce huo ukusanyaji bila support yako? Au kuna watu wanaku-sabotage ili ushindwe kufikia malengo hayo?

Naomba kuhitimisha kwa kukushukuru kwa muda wako.

Wako,
Raia aliye na wasiwasi.
15 April, 2021

Nyongeza muhimu kutoka kwa baadhi ya wadau 👇






Postscriptum (PS):
Kuna baadhi ya wachangiaji katika uzi huu wana attack mleta mada wakisema alikuwa mnufaika wa utaratibu wa awali i.e mfanyakazi TRA, alikuwemo kwenye taskforce n.k.

Inasikitisha sana pale mtu badala ya kusikiliza na kuijibu hoja anadhani wewe ni mnufaika, umehongwa, kibaraka sababu tu umenena jambo tofauti na aloamini. Ni legacy mbaya sana hii.

Niseme tu, mimi sio mfanyakazi wa TRA na sio mnufaika wa mfumo. ILA nimetoa experience yangu baada ya kuona realities mtaani (mfano suala la risiti limenikuta mimi kama mimi si mara moja) na pia katika mijadala yetu sisi wananchi pamoja na maoni ya baadhi ya maafisa wa TRA ambao tupo nao mitaani maana nao ni binadamu wa kawaida tunaishi nao.

So in simple terms, I did this not for any personal gain rather, I decided not to keep quite for National Interest.
Mama alishasema hata makusanyo yakiyumba kwa muda mfupi si hoja wakati utaratibu mzuri ukitafutwa. Au ulitaka nyie TRA muendelee kuwa miungu watu?...
 
Mhe Rais, naomba utumie dakika chache kusoma barua hii wewe mwenyewe, na kama hautapata muda naomba wasaidizi wako wakusaidie kuusoma na kukufikikishia.

Naandika haya kama Raia aliye na wasiwasi baada ya kutafakari kwa kina juu ya "TONE" yako uliyokwishaitoa hadharani kuhusu taasisi hii nyeti inayokusanya mapato ya nchi.

Pia ni baada ya kukaa na baadhi ya maafisa kodi ambao wanakiri kwamba toka kauli yako kazi yao imekuwa ngumu kupindukia ni kama wamewekwa benchi!

Mhe. Rais, kwa sasa kuna mambo makuu mawili yanayotokea ambayo sidhani kama umeshayajua.

i) Wafanyabiashara wameacha kutoa risiti za EFD na ukiwadai wanasema kabisa WASISUMBULIWE maana Rais wao ameshatoa maelekezo hayo. Wapo HOLIDAY!

Hata TRA wenyewe wamecancel mazoezi ya ku-enforce utoaji risiti. Maana wanajua wakienda watabagazwa!

Swali kubwa hapa, Je, Kodi gani itakusanywa na nchi bila watu kutoa risiti? Unawezaje kutrack mauzo ya mlipa kodi bila kutoa risiti ya EFD?

ii) Wafanyabiashara hawapeleki tena malipo ya kodi kwa kama kasi ya awali, kila mmoja ameset mind ya kupinga kodi maana anaona kama kile alichokadiriwa si sahihi baada ya kauli ya Rais.

Wataalam wenyewe wanasema impact yake itaonekana katika taarifa za mapato mwezi huu na ijayo!

Mhe Rais, katika taasisi zote chini yako zinazohitaji Top Level Presidential Support ya moja kwa moja ni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Bila TRA yenye support ya Rais, Taifa linakufa, na hakika litashindwa kufikia malengo yake.

Ni sawa na katika taasisi za kawaida, kitengo ambacho kinaleta mapato kwa taasisi, ndicho Mkurugenzi Mkuu hukitolea macho na kukipa support yote inayohitajika ili aweze kufikia malengo yake kibiashara.

Mhe Rais, sitaki kurejea katika maagizo yako ya nyuma kuhusu namna TRA wanavyofanya kazi ambayo uliyatoa hadharani, ila ningekuwa mmoja wa washauri wako ningeshauri usiongee sentensi zile hadharani bali uongee moja kwa moja na Viongozi na Wafanyakazi wa TRA indoors.

Kwa nini??. Kwa sababu nature ya mfanyabiashara ni kulalamika na kuficha mapato yake halisi. Hakuna mfanyabiashara hata mmoja aliye genuine ya kipato chake, Popote duniani. Hakuna!

Mhe. Rais, unaweza kukuta mfanyabiashara anafanya biashara yenye mauzo ya Billioni 2 anadeclare faida ya milioni 4, Seriously?

Katika mazingira hayo unahitaji Taasisi yenye nguvu na mamlaka ili iweze kutafuta wapi mtu huyu alipodanganya ili Serikali iweze kukusanya kodi yake. Otherwise, utachukua hio hio Milioni 4 alafu maisha yanaendelea wakati kwa hakika labda mtu huyo alipaswa kulipa milioni 50.

Mwisho:
Natambua kupitia maneno ya Makamu wako, Mhe. Mpango, umeweka malengo ya Trillion 2 kwa Mwezi, lakini ukweli ni kwamba hata kama sheria zitabadilika na baadhi ya kodi kupungua lazima kuna nyingine zitapanda ili kufikia lengo la Trillion 2. Sasa nani atatumika kuenforce ukusanyaji huo? Je ni hao hao TRA? Je wataweza ku-enforce huo ukusanyaji bila support yako? Au kuna watu wanaku-sabotage ili ushindwe kufikia malengo hayo?

Naomba kuhitimisha kwa kukushukuru kwa muda wako.

Wako,
Raia aliye na wasiwasi.
15 April, 2021

Nyongeza muhimu kutoka kwa baadhi ya wadau 👇






Postscriptum (PS): Kuna baadhi ya wachangiaji katika uzi huu wana attack mleta mada wakisema alikuwa mnufaika wa utaratibu wa awali i.e mfanyakazi TRA, alikuwemo kwenye taskforce n.k.

Inasikitisha sana pale mtu badala ya kusikiliza na kuijibu hoja anadhani wewe ni mnufaika, umehongwa, kibaraka sababu tu umenena jambo tofauti na aloamini. Ni legacy mbaya sana hii.

Niseme tu, mimi sio mfanyakazi wa TRA na sio mnufaika wa mfumo. ILA nimetoa experience yangu baada ya kuona realities mtaani (mfano suala la risiti limenikuta mimi kama mimi si mara moja) na pia katika mijadala yetu sisi wananchi pamoja na maoni ya baadhi ya maafisa wa TRA ambao tupo nao mitaani maana nao ni binadamu wa kawaida tunaishi nao.

So in simple terms, I did this not for any personal gain rather, I decided not to keep quite for National Interest.
TRA ni taasisi muhimu sana. Ila waajiriwa wake wengi wamefanya kama ndio biashara yao binafsi. Wameua biashara halali za watu kwa kisingizio cha kukusanya kodi, huku wakineemeka na rushwa isiyosemekana.
TRA inajitaji kusukwa upya. Waende kuajiri watu wengine waadilifu na wanaolewa maana ya umuhimu wa kuwa na private sector.
Wanaodhani kama bila wao TRA haitakuwepo, ni wakati sasa wa kujitafakari. Wasituharibie nchi yetu kwa kuendeleza dhuluma kwa kiini macho cha kukusanya kodi
 
Watu wanataka kulipa kodi halali na rafiki badala ya kutegemea harrassment kama njia ya kukusanya kodi pamoja na faini.Badala ya TRA kumshauri Rais kuhusu maeneo mapya ya kodi ili kupanua wigo wao wanasusa ni kwa vile wamefika mwisho wa kufikiri. Waangalie vyanzo vipya eg kuna taxi bubu nchi nzima hazilipi kodi mbona hawajashauri walipe wao wanakazania traditional methods tu.Rushwa !Rushwa!

Kuna watu pale wamekaa ofisi za umma kama wako nyumbani kwao. Wakitaka kuongeza nyumba wanachukua mafaili na kuhangaika na wafanyabiashara ambao pengine hawana tatizo lolote, ili tu wapatiwe rushwa
 
Kwa mtu niliye na tajiriba na IRS [TRA ya Marekani], naona kama vile Watanzania bado hatuko serious na ukusanyaji kodi!

IRS ni moja ya tax collecting agencies zisizo na mzaha.

Ukitaka kukusanya mapato kupitia kodi, basi ni lazima uwe thabiti.

Upole haufai.

Lakini pia haina maana kuwa ndo uonee watu, ingawa ni kawaida ya binadamu kuona anaonewa hata kama si kweli.
 
Kulipa kodi ni takwa la sheria, hao wafanyabiashara wanatakiwa kulipa kodi kutimiza wajibu wao, wakigoma wacha sheria ichukue mkondo wake, hao maafisa wa TRA unaosema wameamua kukaa pembeni kwa kuogopa kubagazwa ni wazembe wanatakiwa kuadhibiwa.
Point.
 
Rais hajawazuia TRA kukusanya Kodi. Alichosisitiza mh.Rais ni weledi katika kutekeleza zoezi hilo.
Hata mimi nilielewa zile task force za kutumia mabavu kutoka DC. DSO. Takukuru and alike ndizi zisizotakiwa lakini kama mpaka enforcement ya kawaida tu ya TRA wenyewe nayo haitakiwi basi hapo shughuli ipo tena si ndogo.
 
Mkuu watu wanapotaka kukukopa awaangalii sana unadaiwa kiasi, wanachochali wao ni ratios zako mfano; debt interest to income ratio, interest cover and so forth.

Na ratio zina bench mark zake wewe kama serikali yako gearing ratio zake ni over 70% hakuna mtu atakupa hela yake kirahisi.

Basically kinachofanywa na IMF or any other international lender kwenye risk assessment za national financing is just basic financial accounting wamebadili tu terminologies to fit economics.

Kingine serikali ni ‘going-concern’ akitoka mmoja akija mwingine alichokuta kiko mezani ni mzigo wake as far as the world is concerned.

Kama ni miradi ambayo ipo kwenye pipeline aijaanza bado raisi akiona terms sio nzuri it’s OK kuzifuta. Lakini kama ni project ambazo zipo nusu ni jukumu lake kumaliza, kama ni madeni ya nchi ni yake kuyalipa.

Sasa ata kama Magufuli alikopa sana kaondoka anauwezo wa kulipa, na wewe ukafika ukashindwa kulipa madeni ina maana viatu vya kazi havikutoshi.

Na kama kuna miradi ambayo ipo tayari ya kimkakati ukashindwa kuimaliza kisa kukosa mapato kazi imekushinda.

Usione hao maraisi wengine wanashangaa hayati kawezaje kutimiza mengi kwa muda mfupi, kukopesheka sio kazi raisi kama unavyodhani; you need to improve your collection. Vinginevyo tusahau maendeleo watanzania, turudi kwenye vicious povert cycle tuliyoizoea tangia dunia iumbwe.

Mwisho miradi yote ya kimkakati aliyofanya Magufuli kwenye infrastructures iliyoisha na ambayo ipo njiani ina multiplier effect kubwa sana kwenye uchumi, kuacha hiyo miradi ni sawa na kusema tumezaliwa maskini na tufe maskini tu; “ponda mali, kufa kwaja” wajao watajijua wenyewe.
Ku- abandon atafanya tu ikiwa anaona haina tija kwa taifa. Mbona A Mwinyi hakuendeleza viwanda vya Tanganyika Packers vya Shinyanga na Mbeya. Hata mwenywe Mwendazake ali abandon bomba la gas ya Mtwara na kuchagua STIGLERs.

Sidhani kuwa eti kigezo cha viatu kukutosha ni ku implement miradi blindly?? Mtu anaanzisha daraja la Mwanza Busisi wakati liko nje ya Mpango, unashindwaje kuliacha kama hilo.

I expect atafanya anayoweza kwa wakati wake na tutapiga hatua.
 
Kwa kweli unastahili kupewa nishani ya Mzalendo mkereketwa! Mungu akubariki sana! Wafanyabiashara ni watu muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa. Tatizo ni kwamba watanzania hatuna elimu ya kodi kama sehemu ya uzalendo. Tangu chekechea mpaka chuo kikuu hakuna mahali elimu ya kodi na umuhimu wake inafundishwa!
Kwa hiyo karibu wafanyabiashara wote hawalipi kodi kwa hiari! Ukiwapa mwanya watakwepa kodi au watatoa kodi kwa udanganyifu! Kwa sababu ya mazoea ya kukwepa kodi, wafanyabiashara wakifuatiliwa vilivyo kuhusu kodi wanahisi wanaonewa! Wakitoa kodi wanahisi faida inapungua maana walizoea kuifanya kodi iliyopaswa kulipwa kama sehemu ya faida!
Kwa sasa hivi TRA watakuwa na wakati mgumu sana wa kufuatilia kodi, maana wametafisirika kama vile walikuwa wanabambikiza kodi! Mama huu ushauri uliopewa ni wa muhimu sana! Wasaidizi wako wengine wanaweza wasikushauri huku wakitazamia ukwame halafu waseme hakuwa anakubali ushauri! Kwa mazingira ya Tanzania hiki kizazi chetu ni cha kulipa kodi kwa lazima wala katika hili tusidanganyane! Tuwekeze kwenye elimu ya kodi tangu chekechea ili vizazi vijavyo vione fahari ya kulipa kodi!! Mama kaza buti kabisa kwa habari ya kodi ikiwezekana katika hili uwe mkali kuliko mtangulizi wako. Ukikamata mkwepa kodi mfilisi kabisa ili wengine waogope! Vinginevyo we are bound to fail!
Ukikamata mkwepa kodi mfilisi kabisa ili wengine waogope! Vinginevyo we are bound to fail!

Na ukikamata mwenye kuonea mlipakodi kwa makusudi kwa lengo la rushwa NYONGA KABISA ili nchi iende smoothly.
 
Hii ni hatari sana.

KODI NDIO usalama na UHAI wa TAIFA bila kukusanya KODI basi tena ndio tunaenda kuzimu.

wafanya biashara walio wengi ni wa kwepa KODI kamwe hawawezi kulipa kodi bila kushurutishwa.

Kwenye suala la KODI viongozi wetu wawe imara.
 
Watu wanataka kulipa kodi halali na rafiki badala ya kutegemea harrassment kama njia ya kukusanya kodi pamoja na faini.Badala ya TRA kumshauri Rais kuhusu maeneo mapya ya kodi ili kupanua wigo wao wanasusa ni kwa vile wamefika mwisho wa kufikiri. Waangalie vyanzo vipya eg kuna taxi bubu nchi nzima hazilipi kodi mbona hawajashauri walipe wao wanakazania traditional methods tu.Rushwa !Rushwa!
Hayo yote ni sawa kabisa mkuu,TRA wabuni new revenue sources,hilo halina ubishi,ila under scrutiny here are President Samias' statement ambayo ina potential ya kupunguza mapato.
 
Rais hajawazuia TRA kukusanya Kodi. Alichosisitiza mh.Rais ni weledi katika kutekeleza zoezi hilo.
Hakustahili kabisa kuwaambia pale hadharani,kwa kuwa alikuwa keshateua Kamishna mpya,angekaa naye pamoja na wataalamu wengine wazungumze
 
Mbona Mapema sana nchi imeishamshinda Mama mtanipa majibu baada ya mwaka mmoja
 
Back
Top Bottom