Pamoja na hasara kubwa waliyoipata Hamas lakini Israel imeukosa ushindi

Pamoja na hasara kubwa waliyoipata Hamas lakini Israel imeukosa ushindi

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Siku ya leo Jumapili Januari 19 vita vya Gaza vinaingia hatua muhimu ambapo kutakuwa na usitishwaji wa vita kwa muda na ambao unaelekea kuwa wa kudumu baada vita vya zaidi ya mwaka mmoja.

Vita hivyo ni kati ya taifa kubwa kijeshi la Israel na washirika wake ambao ni mataifa makubwa dunia dhidi ya vikundi vya wanamgambo ndani ya Gaza vinavyoongozwa na Hamas.

Katika vita hivyo ambavyo huenda ndio vita vibaya zaidi kwa teknolojia za kisasa watu karibu nusu laki wameuliwa sambamba na majengo karibu yote ya ghorofa kuporomoshwa.

Hata hivyo Israel imeshindwa kuupata ushindi iliotangaza kuutafuta.

Vita vilipoanza Israel ilitangaza kutaka kuimaliza Hamas na kuwarudisha nyumbani mateka wote waliokuwa wakishikiliwa ndani ya Gaza.

Siku ya leo ni muhimu sana kwa pande zote zilizokuwa zikipigana. Israel kwa upande wake baada ya kushindwa kuwaokoa mateka wake itakabidhiwa baadhi yao kutoka kwa Hamas ambao watarudishwa nyumbani.

Kwa upande mwengine watu wa Gaza watapata nafuuu ya kuuliwa kwa kasi ya watu wasiopungua 100 kwa siku.

Kilichowazi kwa kila mfuatiliaji wa vita hivi ni kuwa Israel imefanya makubaliano na wale wale ilioazimia kuwamaliza na wasiwepo kabisa Gaza na kwamba mateka imebidi wawapate kwa njia za makubaliano na haikuwa wa kubebwa kibabe kama ilivyowahi kufanyika kuleta Entebe ambalo ndili lililokuwa lengo la awali.
 
Hamas wametakiwa kuorodhesha majina ya mateka watakaowaachia, wameshindwa, kwa hiyo uwezekano wa kutokuwepo mateka hai wa ki israel ni mkubwa, hivyo ceasefire inaweza isifikiwe leo wala kesho.
Hilo ndio tangazo la kushindwa vita kwa Israel.
Tujaalie hakuna mateka wa kubadilishwa kosa itakuwa ni la nani na Israel nayo itafanya nini baada ya kuporomosha majengo ya Gaza.Jee wataendelea kuuwa wapalestina waliobaki kwenye makambi au itachukua uamuzi gani mwengine?
 
Siku ya leo Jumapili Januari 19 vita vya Gaza vinaingia hatua muhimu ambapo kutakuwa na usitishwaji wa vita kwa muda na ambao unaelekea kuwa wa kudumu baada vita vya zaidi ya mwaka mmoja.
Vita hivyo ni kati ya taifa kubwa kijeshi la Israel na washirika wake ambao ni mataifa makubwa dunia dhidi ya vikundi vya wanamgambo ndani ya Gaza vinavyoongozwa na Hamas.
Katika vita hivyo ambavyo huenda ndio vita vibaya zaidi kwa teknolojia za kisasa watu karibu nusu laki wameuliwa sambamba na majengo karibu yote ya ghorofa kuporomoshwa.Hata hivyo Israel imeshindwa kuupata ushindi iliotangaza kuutafuta.
Vita vilipoanza Israel ilitangaza kutaka kuimaliza Hamas na kuwarudisha nyumbani mateka wote waliokuwa wakishikiliwa ndani ya Gaza.
Siku ya leo ni muhimu sana kwa pande zote zilizokuwa zikipigana.israel kwa upande wake baada ya kushindwa kuwaokoa mateka wake itakabidhiwa baadhi yao kutoka kwa Hamas ambao watarudishwa nyumbani.Kwa upande mwengine watu wa Gaza watapata nafuuu ya kuuliwa kwa kasi ya watu wasiopungua 100 kwa siku.
Kilichowazi kwa kila mfuatiliaji wa vita hivi ni kuwa Israel imefanya makubaliano na wale wale ilioazimia kuwamaliza na wasiwepo kabisa Gaza na kwamba mateka imebidi wawapate kwa njia za makubaliano na haikuwa wa kubebwa kibabe kama ilivyowahi kufanyika kuleta Entebe ambalo ndili lililokuwa lengo la awali.
waisraeli hawajaanza leo kuwapiga wapelestina na miaka yote hawajawahi kushinda,dawa wawarudishie ardhi yao na waishi kwa amani
 
Siku ya leo Jumapili Januari 19 vita vya Gaza vinaingia hatua muhimu ambapo kutakuwa na usitishwaji wa vita kwa muda na ambao unaelekea kuwa wa kudumu baada vita vya zaidi ya mwaka mmoja.
Vita hivyo ni kati ya taifa kubwa kijeshi la Israel na washirika wake ambao ni mataifa makubwa dunia dhidi ya vikundi vya wanamgambo ndani ya Gaza vinavyoongozwa na Hamas.
Katika vita hivyo ambavyo huenda ndio vita vibaya zaidi kwa teknolojia za kisasa watu karibu nusu laki wameuliwa sambamba na majengo karibu yote ya ghorofa kuporomoshwa.Hata hivyo Israel imeshindwa kuupata ushindi iliotangaza kuutafuta.
Vita vilipoanza Israel ilitangaza kutaka kuimaliza Hamas na kuwarudisha nyumbani mateka wote waliokuwa wakishikiliwa ndani ya Gaza.
Siku ya leo ni muhimu sana kwa pande zote zilizokuwa zikipigana.israel kwa upande wake baada ya kushindwa kuwaokoa mateka wake itakabidhiwa baadhi yao kutoka kwa Hamas ambao watarudishwa nyumbani.Kwa upande mwengine watu wa Gaza watapata nafuuu ya kuuliwa kwa kasi ya watu wasiopungua 100 kwa siku.
Kilichowazi kwa kila mfuatiliaji wa vita hivi ni kuwa Israel imefanya makubaliano na wale wale ilioazimia kuwamaliza na wasiwepo kabisa Gaza na kwamba mateka imebidi wawapate kwa njia za makubaliano na haikuwa wa kubebwa kibabe kama ilivyowahi kufanyika kuleta Entebe ambalo ndili lililokuwa lengo la awali.
Kwa taarifa yako hamas hard kwenye utawala Gaza ndio makubaliano na Israel anatoa jesh maeneo maalum ya watu sio Gaza. Huu ujinga ni kama ule mnaolishana kwamba hezbollah ameshinda wakati alipigwa mande kila mahali mpaka akakubali kunyoosha.mikono
 
waisraeli hawajaanza leo kuwapiga wapelestina na miaka yote hawajawahi kushinda,dawa wawarudishie ardhi yao na waishi kwa amani
Sera ya kuuwa viongozi wao na kuwaua wananchi walidhani wapiganaji wataisha na wanachi watavunjika moyo walete fujo.Hakuna kilichofaa.
Viongozi wakuu wamewauwa lakini walio baki wameshika bendera ya vita.
 
Kwa taarifa yako hamas hard kwenye utawala Gaza ndio makubaliano na Israel anatoa jesh maeneo maalum ya watu sio Gaza. Huu ujinga ni kama ule mnaolishana kwamba hezbollah ameshinda wakati alipigwa mande kila mahali mpaka akakubali kunyoosha.mikono
Kama unavyojidanganya wewe mwenyewe.Taifa la kibabe pamoja na kumiliki silaha zote hizo wameshindwa kuwamaliza Hizbullah na Hamas mpaka anakubali kufanya makubaliano.
Hizbullah wanasubiri muda ufike tu waanze kurusha vitu katika ya Israel na kuwatimua watu majumbani mwao
 
Kama unavyojidanganya wewe mwenyewe.Taifa la kibabe pamoja na kumiliki silaha zote hizo wameshindwa kuwamaliza Hizbullah na Hamas mpaka anakubali kufanya makubaliano.
Hizbullah wanasubiri muda ufike tu waanze kurusha vitu katika ya Israel na kuwatimua watu majumbani mwao
Wanarusha wakiwa vilema sio. Sasa hao waarabu wameongeza nini zaid ya kupoteza zaid kule Golan height na west bank. Na Gaza hamas hard. Upuuz mtupu
 
Hamas wasiwepo kiasi kwamba angeingia mitaani tu kuunda serikali isiyo na Hamas na ingekuwa ni tusi kuwaomba Hamas msaada wa kuwapata mateka
Kati ya hamasi na israel ipi iliyoshinda?
 
Thamani ya waisraeli 33 ni sawa na wapalestina 1890??!!!.Hii nimeona kwenye deal la kubadilishana wafungwa!!!
 
1737143826724.jpg
 
Hivi vichwa ndivyo vinavyosapoti Genocide isiishe. Kwani Vita vya dunia viliisha kwa kumalizwa Wajerumani wote?.

Kwa mpaka sasa ulipendezwa wapalestine waendelee kuchinjwa tu kwasababu ya moyo wako neno ushindi.

Sasa Ebu mtaje kiongozi anaeongoza mapambano wa Hamas mpaka sasa.

Aisee.
 
Kiongozi wa Hamas aliyeoongoza kutiliana saini ni Khalid Meshal
 
Hilo ndio tangazo la kushindwa vita kwa Israel.
Tujaalie hakuna mateka wa kubadilishwa kosa itakuwa ni la nani na Israel nayo itafanya nini baada ya kuporomosha majengo ya Gaza.Jee wataendelea kuuwa wapalestina waliobaki kwenye makambi au itachukua uamuzi gani mwengine?
Toa alama za kuuliza utaliona jibu linajitokeza.
 
Wanarusha wakiwa vilema sio. Sasa hao waarabu wameongeza nini zaid ya kupoteza zaid kule Golan height na west bank. Na Gaza hamas hard. Upuuz mtupu
Jiulize na Israel imepata nini katika kuuwa watu zaidi ya 45000 na kuvunja majumba.
Mbona hawajaweza kuwamaliza Hamas.Zaidi imedhihirika kuwa Israel haina uwezo wa kupigana bila msaada wa mataifa makubwa na kwamba wapalestina wakiendelea kukomaa watarudisha heshima zao.
 
Muelewe kuwa vita vilivyopiganwa vilikuwa ni kulenga kundi la wanamgambo tu. Ingekuwa ni kuvumirusha makombora tu israeli ingeifi. agia palestina yote. Vita vya kulenga adui tu ni ngumu sana
 
Back
Top Bottom