Pamoja na kulamba Asali, Mbowe alaani utitiri wa magari, msafara wa Rais hauendani na kubana matumizi

Pamoja na kulamba Asali, Mbowe alaani utitiri wa magari, msafara wa Rais hauendani na kubana matumizi

Adai ni matumizi mabaya ya pesa za umma.

Mwigulu Nchemba auchuna.
Mbowe ahoji utitiri wa magari msafara wa Rais

=======
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema utitiri wa magari katika msafara wa Rais Samia Suluhu Hassan hauendani na dhana ya serikali ya kubana matumizi.

Amesema, gharama za maisha zinatesa wananchi huku serikali ikionekana kutodhihirisha kwa vitendo mkakati wake wa kubana matumizi

Mbowe aliyasema hayo juzi mkoani Shinyanga alipokuwa akihutubia wanachama wa chama hicho katika maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani iliyoandaliwa na Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA).

Alisema hivi karibuni alimwandikia ujumbe Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba kumweleza kodi na tozo wanazotoza kwa wananchi haziakisi uhalisia na kuchochea umaskini miongoni mwao.

“Kodi hutozwa matajiri ili kuwasaidia maskini, unategemea nini kwa wananchi hawa unapowatoza kipato chao kidogo? Sasa wenzetu hawa hawaelewi, nilimuandikia barua Dk Mwigulu kuhusu hili mpaka sasa sijapata majibu” alisema

Alisema: “Gharama za kuendesha serikali kila siku zinapanda, Rais anatembea na msafara wa magari karibu 70 hadi 80 Land Cruiser za kazi gani? Hivi kweli nchi hii na umaskini wake unatumia magari yote haya, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais.”

Mbowe alitolea mfano Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na Naibu wake wawili, Salum Mwalimu (Z’bar) na Benson Kigaila (Bara) wote watatu wametumia gari moja kutoka Dar es Salaam hadi Shinyanga ili kubana matumizi.

Kiongozi huyo wa upinzani ametoa kauli hiyo wakati Rais Samia akiendelea na ziara za kikazi mkoani Iringa akitokea Mkoa wa Njombe na Mbeya alikoanzia.

Lengo la ziara hiyo iliyoanza Agosti 5 mwaka huu ni kukagua, kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi.

Chanzo: Mwananchi
Ndio kazi ya upinzani makini uko kwa ajili ya watu kwa maendeleo ya watu.

Kongole Mh Mbowe.
 
“Kodi hutozwa matajiri ili kuwasaidia maskini, unategemea nini kwa wananchi hawa unapowatoza kipato chao kidogo? Sasa wenzetu hawa hawaelewi, nilimuandikia barua Dk Mwigulu kuhusu hili mpaka sasa sijapata majibu” alisema
Sikio la kufa halisikii dawa
 
Alisema: “Gharama za kuendesha serikali kila siku zinapanda, Rais anatembea na msafara wa magari karibu 70 hadi 80 Land Cruiser za kazi gani? Hivi kweli nchi hii na umaskini wake unatumia magari yote haya, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais.”
Mbowe usilalamike, haya yamesababishwa na wewe mwenyewe kuuza timu 2015
 
Ha ha 😂😂 hata yule wa Ubeligiji alipolipwa mafao akatulia, yamekata kwa madeni kaanza kuongea ongea. Kweli kungulu hafugiki. Siku izi wakiona mambo hayasomeki wanamtuma Heche kubeep Mfumo ili wakumbukwe
Unakita mtu kama wewe uko bize na ukarani wa sensa. Yaanimkiwa mitandaoni mnaonekana mko vizuri sana.
 
Lile faili lipo, ni kuonesha tu nia ya kuendelea na case, sijui DPP anasubiri nini??? Ningekuwa mi ndiye DPP huyu Mbowr ningehakikisha namfunga maisha au hukumu ya kifo, hafai kabisa kwa demokrasia ni dikiteta na muuaji
DPP aanze kumfunga mumeo kwanza
 
Hizo V8 zina sound proof ya malalamiko ya matatizo yanayowakabili wananchi.

Wakishastaafu ndio wanakumbuka walichokifanya na kuandika vitabu..

Ila wakiwa madarakani hawawezi tuelewa tunaposema maisha magumu.
Yeye anahudumiwa kila kitu bure + posho nono tupu hawezi kujua matatizo ya wananchi
 
Alivyofariki mwamba JPM si walikunywa bia hao jamaa, sasa analalamika nini kwa huyu tena wakati ndo waliona anawafaa wao wenye kujua kula nchi.
 
Adai ni matumizi mabaya ya pesa za umma.

Mwigulu Nchemba auchuna.

Mbowe ahoji utitiri wa magari msafara wa Rais

=======
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema utitiri wa magari katika msafara wa Rais Samia Suluhu Hassan hauendani na dhana ya serikali ya kubana matumizi.

Amesema, gharama za maisha zinatesa wananchi huku serikali ikionekana kutodhihirisha kwa vitendo mkakati wake wa kubana matumizi

Mbowe aliyasema hayo juzi mkoani Shinyanga alipokuwa akihutubia wanachama wa chama hicho katika maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani iliyoandaliwa na Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA).

Alisema hivi karibuni alimwandikia ujumbe Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba kumweleza kodi na tozo wanazotoza kwa wananchi haziakisi uhalisia na kuchochea umaskini miongoni mwao.

“Kodi hutozwa matajiri ili kuwasaidia maskini, unategemea nini kwa wananchi hawa unapowatoza kipato chao kidogo? Sasa wenzetu hawa hawaelewi, nilimuandikia barua Dk Mwigulu kuhusu hili mpaka sasa sijapata majibu” alisema

Alisema: “Gharama za kuendesha serikali kila siku zinapanda, Rais anatembea na msafara wa magari karibu 70 hadi 80 Land Cruiser za kazi gani? Hivi kweli nchi hii na umaskini wake unatumia magari yote haya, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais.”

Mbowe alitolea mfano Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na Naibu wake wawili, Salum Mwalimu (Z’bar) na Benson Kigaila (Bara) wote watatu wametumia gari moja kutoka Dar es Salaam hadi Shinyanga ili kubana matumizi.

Kiongozi huyo wa upinzani ametoa kauli hiyo wakati Rais Samia akiendelea na ziara za kikazi mkoani Iringa akitokea Mkoa wa Njombe na Mbeya alikoanzia.

Lengo la ziara hiyo iliyoanza Agosti 5 mwaka huu ni kukagua, kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi.

Chanzo: Mwananchi
Rais akienda ziara wahusika wote lazima wawepo,kubana matumizi kwenye event kama hizo haiwezekani.
 
Asali ikipungua kidogo DJ akili inamrudia. Aongezewe asali huyu kamanda uchwara.
 
Lile faili lipo, ni kuonesha tu nia ya kuendelea na case, sijui DPP anasubiri nini??? Ningekuwa mi ndiye DPP huyu Mbowr ningehakikisha namfunga maisha au hukumu ya kifo, hafai kabisa kwa demokrasia ni dikiteta na muuaji
Madai mazito sana!

Ila Kama una ushahidi wa madai yako mbona hujachukua hatua stahiki za kumfungulia kesi??!!
 
Rais akienda ziara wahusika wote lazima wawepo,kubana matumizi kwenye event kama hizo haiwezekani.
Ni wa kazi gani? Kuna maswali yanayoruhusiwa kutoka kwa wananchi ili waziri mwenye dhamana ayajibie? Misuse of resources tu. Kuna wakati msafara wa IGP itabidi ma RPC wote wawepo 😁😁 kama ni mhimu wote wawepo, tunazo wizara ngapi na je wote wapo au ni uhuni tu wachache ndo wanastahili kuwepo?
 
Ni wa kazi gani? Kuna maswali yanayoruhusiwa kutoka kwa wananchi ili waziri mwenye dhamana ayajibie? Misuse of resources tu. Kuna wakati msafara wa IGP itabidi ma RPC wote wawepo 😁😁 kama ni mhimu wote wawepo, tunazo wizara ngapi na je wote wapo au ni uhuni tu wachache ndo wanastahili kuwepo?
Ujinga wako hauwezi kuwa mzigo Kwa wengine beba mwenyewe..
 
Back
Top Bottom