Pamoja na Maumivu Makali Mbona Hatuwezi Kama Wenzetu?Tumelishwa Nini?

Pamoja na Maumivu Makali Mbona Hatuwezi Kama Wenzetu?Tumelishwa Nini?

Mkuu kuandama ni tofauti na kufanya fujo vurugu. Na mara nyingi waleta fujo ni polisi wakitumiwa na wanaharamu!!!

⚖️Justice for Asimwe#
Kweli kabisa, maandamano siyo fujo.
Hata hivyo, kupandishwa kwa kodi ni maumivu kwa walalahoi na raha kwa viongozi na watumishi wa uma wanaoishi kwa kutegemea sehemu ya kodi hizo.
Watu wenye maumivu hawaoneshi hisia na vitendo vya kupinga kinachowaumiza kwa utulivu.
 
Huko Kenya katika budget yao iliyosomwa siku moja na sisi kuna vitu vimetangazwa kama ongezeko la kodi nk mambo ambayo yana maumivu kwa raia.
Tofauti na tabia zetu, wao ASAP wakaingia barabarani bila kujali chama au sura na kupinga kwa nguvu moja hadi Serikali imesalimu amri na kutangaza kufuta kodi hizo.
Kwanini wenzetu wanaweza sisi hata tuwekewe kodi ya kuvuta oxygen hatuta goma zaidi ya kusifu kuwa "anaupiga mwingi"?
Jee ni uchawi gani umetumika kutuloga hadi kuwa taifa la mazombie?
Kwa aina ya vijana kama Lucas Mwashambwa unategemea nini?hapo bado hujaangalia vyombo vya habari uone mapambio na sifa kedekede ambazo ukiwa kama raia wa kawaida kabisa unaona ni urongo ila watu wazima na familia zao kwa kutetea matumbo yao wapo radhi kujitoa ufahamu
 
Tanza ni taifa la wakata UNO
We waambie mambo ya mziki,udaku, mipira

Ova
 
Huko Kenya katika budget yao iliyosomwa siku moja na sisi kuna vitu vimetangazwa kama ongezeko la kodi nk mambo ambayo yana maumivu kwa raia.
Tofauti na tabia zetu, wao ASAP wakaingia barabarani bila kujali chama au sura na kupinga kwa nguvu moja hadi Serikali imesalimu amri na kutangaza kufuta kodi hizo.
Kwanini wenzetu wanaweza sisi hata tuwekewe kodi ya kuvuta oxygen hatuta goma zaidi ya kusifu kuwa "anaupiga mwingi"?
Jee ni uchawi gani umetumika kutuloga hadi kuwa taifa la mazombie?
Mkuu kweli kabisa unauliza tumelishwa Nini?
Umewahi kusikia jamaa anayeitwa Forojo Ganze mchawi maarufu Afrika yote.
Huyu Ganze kwenye zindiko huko Bagamoyo lengo lake umewahi kusikia lilikuwa na lengo gani?
 
Huko Kenya katika budget yao iliyosomwa siku moja na sisi kuna vitu vimetangazwa kama ongezeko la kodi nk mambo ambayo yana maumivu kwa raia.
Tofauti na tabia zetu, wao ASAP wakaingia barabarani bila kujali chama au sura na kupinga kwa nguvu moja hadi Serikali imesalimu amri na kutangaza kufuta kodi hizo.
Kwanini wenzetu wanaweza sisi hata tuwekewe kodi ya kuvuta oxygen hatuta goma zaidi ya kusifu kuwa "anaupiga mwingi"?
Jee ni uchawi gani umetumika kutuloga hadi kuwa taifa la mazombie?
Tumelogwa, vijana wakitanzania wanaota uteuzi muda wote na siyo maslahi ya nchi yao
 
Lakini mapambano ya Nairobi juu ya kodi wakenya wamesema watajiongoza bila vyama vya siasa na wamefanikiwa.
Hapa wapinzani wakiitisha maandamano mnawaambia walete watoto wao, na wakileta kinazuka kiroja kingine!
Sisi hatuko serious na lolote
Tuna laana kubwa haswa
 
ELIMU, ELIMU, ELIMU...UJINGA,UJINGA,UJINGA;
Sisi tukobize na kina babalevo na mwijaku,nchi zinazojitambua hata wachekeshaji wao huwa na point sio kusifusifu kijinga na kujikomba Kwa matakjiri
 
Huko Kenya katika budget yao iliyosomwa siku moja na sisi kuna vitu vimetangazwa kama ongezeko la kodi nk mambo ambayo yana maumivu kwa raia.
Tofauti na tabia zetu, wao ASAP wakaingia barabarani bila kujali chama au sura na kupinga kwa nguvu moja hadi Serikali imesalimu amri na kutangaza kufuta kodi hizo.
Kwanini wenzetu wanaweza sisi hata tuwekewe kodi ya kuvuta oxygen hatuta goma zaidi ya kusifu kuwa "anaupiga mwingi"?
Jee ni uchawi gani umetumika kutuloga hadi kuwa taifa la mazombie?
Nyie ni maiti acording to Jomo Kenyata
 
IMG_20240620_065440_352.jpg


🇰🇪 1. Vijana wameingia barabarani kupinga muswada wa sheria ya fedha (finance bill 2024) ambayo ilikiwa inakwenda kuongeza tozo na ushuru katika bidhaa mbalimbali.

🇹🇿 1. Tanzania, mawaziri wanalipa mazombi posho kusukuma hashtag na bungeni waziri anataja jina la Rais mara 40, bajeti inapita. Wabunge wanaruka sarakasi na miluzi.

🇰🇪 2. Maandamano ya kupinga muswada wa sheria yameratibiwa na wananchi wenyewe, hakuna chama cha siasa kilichoshiriki kuandaa. Hiyo inaitwa nguvu ya umma.

🇹🇿 2. Serikali ya Tanzania inapitisha tozo na kodi nyingi kwa watanzania, Waziri wa fedha anatoka hadharani anasema asiyekubaliana na kulipa tozo hizo ahamie Burundi.

🇰🇪 3. Baada ya kuingia barabarani, Rais William Ruto imebidi awaite wabunge wa upande wa Serikali (Kenya Kwanza) wajadili na kukubaliana kuondoa jumla ya tozo 14.

🇹🇿 3. Wananchi wanalalamika lakini wanaendelea kulipa. Baadae Rais anasema hajawahi kuona Waziri wa fedha, Mwigulu Nchemba anasifiwa. Ni kulaaniwa, apige kazi tu.

🇰🇪 4. Ruto amesema mapendekezo yameondolewa kufuatia zoezi la ushirikishwaji wa umma ambalo lilishuhudia Wakenya wakiibua upinzani dhidi ya mapendekezo hayo.

🇹🇿 4. Wananchi hata wakishirikishwa, hawaelewi nguvu zao, bado kuna wengine wanasema siasa haiwahusu, hawajui kuacha kushiriki ndiyo ahueni kwa serikali ya CCM.

🇰🇪 5. Awali Ruto aliwaita wabunge wa Kenya Kwanza, Ikulu ili kuwashinikiza kupitisha muswada huo wa sheria ya fedha, wabunge hao wamemkatalia baadhi ya tozo.

🇹🇿 5. Watanzania wao wanaamini ni wajibu na jukumu la CHADEMA wakiongozwa na Freeman Mbowe na Tundu Lissu kuwapambania kuhusu ugumu wa maisha yao.

🇰🇪 6. Wabunge hao wamemueleza Rais Ruto kwamba, watapitisha muswada wa sheria ya fedha ikiwa kelele za wakenya zitazingatiwa. Serikali imeondoa tozo 14 tata.

🇹🇿 6. Wabunge wa Tanzania wao kila linapotajwa jina la Rais wanapiga makofi, hawasomi vifungu vya bajeti, wanaunga kila hoja mkono na wanapitisha. Hawakuchaguliwa.

🇰🇪 7. Tozo zilizoondolewa; 16% ya VAT kwenye mkate na usafirishaji sukari, huduma za fedha na miamala ya kigeni, mafuta ya kula, bidhaa za ndani, kusajili biashara. Etc.

🇹🇿 7. Tanzania bado tozo zipo nyingi na katika bajeti ya 2024/25 zimeongezwa tozo nyingine na waliongezewa tozo na kodi hawana habari wao ili mradi wanapumua tu.

🇰🇪 8. Wananchi wa Kenya hawaogopi polisi, maandamano wameitisha wenyewe na wameingia barabarani hadi Rais na wabunge wake wamewasikiliza hoja zao.

🇹🇿 8. Pamoja na kwamba polisi wa Tanzania ni katili lakini hata katika maandamano ya ambayo yanalindwa na polisi vizuri watanzania wanapunga mkono kwa mbali.

🇰🇪 9. Kenya, unawaona vijana wadogo wa kike na wa kiume barabarani, wamebeba mabango yenye maandishi yanayotaka serikali iondoe muswada huo wa sheria ya fedha.

🇹🇿 9. Tanzania, wasichana na vijana wamejazana katika kumbi za starehe wanashindana kuvuta shisha hawajui kama bajeti ya nchi yao imepitishwa na tozo na kodi kibao.

🇰🇪 10. (GDP) ya Kenya ni $113.4 billion (2022). GDP per capita ni $2,099.30 (2022). Wananchi wa Kenya wameingia barabarani, uchumi mkubwa wa nchi, hauwagusi wananchi.

🇹🇿 10. GDP ya Tanzania ni $75.7 bilioni (2022). GDP per capita ni $1,192.77 (2022). Kenya wapo juu kiuchumi na wameingia barabarani, watanzania wanamwaga pongezi kwa Rais.

Martin Maranja Masese, MMM.
 
Huko Kenya katika budget yao iliyosomwa siku moja na sisi kuna vitu vimetangazwa kama ongezeko la kodi nk mambo ambayo yana maumivu kwa raia.
Tofauti na tabia zetu, wao ASAP wakaingia barabarani bila kujali chama au sura na kupinga kwa nguvu moja hadi Serikali imesalimu amri na kutangaza kufuta kodi hizo.
Kwanini wenzetu wanaweza sisi hata tuwekewe kodi ya kuvuta oxygen hatuta goma zaidi ya kusifu kuwa "anaupiga mwingi"?
Jee ni uchawi gani umetumika kutuloga hadi kuwa taifa la mazombie?
Nikukumbushe llabda umesahau au hukuwahi kusikia Rais wa kwanza wa Kenya Jomo Kenyata aliwahi kusema kuwa:
Waganda ni sawa na wagonjwa wanaweza kupona na kudai haki zao. Wakenya ni sawa na waliolala usingizi wanaweza kuamka wakati wowote na kudai haki zao. Watanzania ni sawa na maiti hawawezi kamwe kudai haki zao.
 
Mmefanyiwa divide and rule , mkipanga kufanya maandamno na kuisema serikali ,mkitokea mikoa ya waislamu mnaitwa magaidi , mkitokea kaskazini mnaitwa wakabila , Mkitoea kanda ya kati mnaitwa waharibifu wa amani ya nchi ...
 
Kwa aina ya vijana kama Lucas Mwashambwa unategemea nini?hapo bado hujaangalia vyombo vya habari uone mapambio na sifa kedekede ambazo ukiwa kama raia wa kawaida kabisa unaona ni urongo ila watu wazima na familia zao kwa kutetea matumbo yao wapo radhi kujitoa ufahamu
Kuna wakati Kenya vilianzishwa vikundi kama Mungiki. Kazi yake ilikuwa kukomesha watu individual waliokuwa wanatumia nafasi zao kukandamiza au kuunga mkono viongozi wafanyapo uovu.
Watu kama Kitenge na genge lake wanarudi nyumbani wanakuta mke na watoto wamecharazwa viboko with a message "acha unoko tusirudi tena".
Unadhani kuna unoko tena hapo? Au kafatwa kijijini baba au mama kawambwa makofi akiulizwa mbona mwanao hana adabu ndivyo umemfundisha?
Kwa adhabu hizo huwezi endelea kufanya ujinga hata upewe pesa kiasi gani.
Tukianza kwenye shina jamii ya vijana machawa watajitambua na kugeuka kuwa GENERATION Z kama wa Kenya.
 
Huko Kenya katika budget yao iliyosomwa siku moja na sisi kuna vitu vimetangazwa kama ongezeko la kodi nk mambo ambayo yana maumivu kwa raia.
Tofauti na tabia zetu, wao ASAP wakaingia barabarani bila kujali chama au sura na kupinga kwa nguvu moja hadi Serikali imesalimu amri na kutangaza kufuta kodi hizo.
Kwanini wenzetu wanaweza sisi hata tuwekewe kodi ya kuvuta oxygen hatuta goma zaidi ya kusifu kuwa "anaupiga mwingi"?
Jee ni uchawi gani umetumika kutuloga hadi kuwa taifa la mazombie?
Fanya kazi dogo. Tanzania hakuna maisha magumu. Mi nauA chipsi hapa stand kwa siku nauza elfu 50. Kina wenye degree wanalipwa laki 2 shuleni kwa mwezi, huu ni uninga.
 
Huko Kenya katika budget yao iliyosomwa siku moja na sisi kuna vitu vimetangazwa kama ongezeko la kodi nk mambo ambayo yana maumivu kwa raia.
Tofauti na tabia zetu, wao ASAP wakaingia barabarani bila kujali chama au sura na kupinga kwa nguvu moja hadi Serikali imesalimu amri na kutangaza kufuta kodi hizo.
Kwanini wenzetu wanaweza sisi hata tuwekewe kodi ya kuvuta oxygen hatuta goma zaidi ya kusifu kuwa "anaupiga mwingi"?
Jee ni uchawi gani umetumika kutuloga hadi kuwa taifa la mazombie?
Mwenge wa uhuru!
 
Back
Top Bottom