Panya road katika matukio yao ni lazima wajeruhi kila mtu?

Panya road katika matukio yao ni lazima wajeruhi kila mtu?

Kwanza kabisa lazima tukubaliane kimsingi kuwa panya road ni school drop out hasa shule ya msingi na secondary, lakini wengi pia ni wale waliolelewa Kwa style ya single mothers hii nimeongea sio kukejeli lakini ni kutokana na mahojiano waliyofanya wenzao kituo Cha polisi.

Jana Tarehe 11.02.23 siku ambayo Simba ilifungwa huko Ugenini, Panya road walifanya matukio ya uvamizi na uporaji katika maeneo ya Bunju B.

Mimi najiuliza kwanini Hawa vijana wamekuwa wakatili kiasi hiki, yaani wakifanya uvamizi lazima wakuchororonge mapanga hata kama utakuwa mtiifu na kuwapa wanachotaka tofauti na majizi mengine.

Wao wakikufikia wanaanza na panga Halafu ndo wanadai Hela , simu, etc, pia wakishindwa kuchukua kitu wanakiharibu either Kwa kukipiga nyundo au kukikatakata.

Pia katika video hii hapa chini utaona Bado kuna Watanzania wachache wanakaa na hela ndani , mfano mmoja kuna mtu kakutwa na laki sita ndani, sijui ilikuwa ya matumizi ya kawaida sijui.

Pia najiuliza Hawa vijana walitumia mbinu gani kuweza kujikusanya wengi vile na kuunda timu yaani genge la wahalifu, hiyo sio kazi ndogo, huyo Kiongozi wao ana upeo fulani wa kipekee. Tunaita team building skills


Kwa jicho langu la kiusalama: Panya road ni kikundi cha kihalifu kinachofanya shughuli za ujambazi kwa low scale.. lakini pia baada ya kusikiliza hii clip nimechambua maelezo ya wahanga kwa jicho la usalama nimegundua kuwa hawa panya road ni biashara inayosukumwa na baadhi ya viongozi wasio waaminifu kuwakomoa wananchi kwa kile kinachodaiwa kuwa wananchi wamekuwa wazito au kukataa kulipa hela ya ulinzi shirikishi..

Nashauri: Wananchi washinikize kazi ya ulinzi shirikishi irudishwe kwenye mtaa wao pia wao kama wananchi watoe ushirikiano wa kutosha kwa kuhakikisha wanatoa michango yote inayohitajika na taarifa zote zinazohitajika hiyo itakuwa ni njia pekee ya kugundua nani anawatuma panya road na kumwajibisha kiongozi/viongozi wa mtaa huo kama matukio hayo bado yatakuwa yanaendelea .. waswahili wanasema Mchawi mpe mwanao akulelee, mwanao akifa tu ujue mchawi ndio kamuua..
 
Kwa saikolojia yangu ; Panya road sio wahalifu/watukutu wa kuzaliwa
kuna maisha wamepitia ya kukosa fursa ilihali wanakua wakiona wengine wanapata fursa ya kuwa watu fulani au kufanya vitu fulani...
Sasa kwenye maisha yao kuna swali! Hao wanaopata fursa ni nani hasa na sisi ni nani tukose?
Hapo ndipo chuki inapozaliwa ambayo inapelekea kujeruhi watu wenye nacho na kuvunja ambavyo havibebeki ili upate hasara ujiskie na ww uchungu walionao...
kuwa nacho ni chochote tu kwa mfano; We kwanini unamiliki smartphone?? tayari unakatwa panga!
na jamii hii iko sana uswazi ndo mana huskii panyaroad wamezuka Masaki, masaki washajitosheleza hawawezi kuwa na chuki!
Ambao wanajiunga kwa kufata mkumbo wachache sana.


Ni mtazamo wangu.
 
Panya road ni ujambazi wa low scale.. lakini pia baada ya kusikiliza hii clip kwa jicho la usalama nimegundua kuwa hawa panya road ni biashara inayosukumwa na baadhi ya viongozi wasio waaminifu kuwakomoa wananchi kwa kile kinachodaiwa kuwa wananchi wamekuwa wazito au kukataa kulipa hela ya ulinzi shirikishi..
Umeeleweka mkuu
 
Kwa saikolojia yangu ; Panya road sio wahalifu/watukutu wa kuzaliwa
kuna maisha wamepitia ya kukosa fursa ilihali wanakua wakiona wengine wanapata fursa ya kuwa watu fulani au kufanya vitu fulani...
Sasa kwenye maisha yao kuna swali! Hao wanaopata fursa ni nani hasa na sisi ni nani tukose?
Hapo ndipo chuki inapozaliwa ambayo inapelekea kujeruhi watu wenye nacho na kuvunja ambavyo havibebeki ili upate hasara ujiskie na ww uchungu walionao...
kuwa nacho ni chochote tu kwa mfano; We kwanini unamiliki smartphone?? tayari unakatwa panga!
na jamii hii iko sana uswazi ndo mana huskii panyaroad wamezuka Masaki, masaki washajitosheleza hawawezi kuwa na chuki!
Ambao wanajiunga kwa kufata mkumbo wachache sana.


Ni mtazamo wangu.
Umechambua vizuri.

Umeitazama hiyo video?
 
Kwamba anaweza kuwa Mstaafu wa moja kati ya vyombo vya ulinzi?

Dhumuni lake ni nini mkuu?
Hilo la ustaafu umelisema ww bosi. Ila kuhusu dhumuni inawezekana ni maslahi ya kisiasa zaidi kuliko maslahi ya kifedha sababu ya aina ya wizi wanaofanya na tabia ya kudhuru mwili.
 
Si rahisi kuunda kundi la kihalfu TZ. Jaribu utaamini. Ila huyu wa Panya ameweza. Ni watu wachache wenye uwezo huo na lazima awe anafahamu mtindo wa utawala au na yeye ni sehemu ya utawala.
Wewe umemaliza mjadala. Kwa tunaoijua vizuri nchi hii uwepo wa Panya Road haumake sense.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Serikali/polisi wakitaka waweze kuwakamata au kuwadhibiti hawa panya road unabidi wawakamate hawa watu wote wanaojiita matembo kwenye vituo vya daladala/mitaani, hawa ndo wanawajua vizuri. Nasema hivi kwa sababu nishakaa nao mtaani vijana hawa, hawa wanaojiita matembo ndo wanajua kila kitu kuhusu panya road
waulizwe polisi wajumbe nyumba 10 watendaji serikali za mitaa lazima hawa watu wanawajua tu wanawafuga

kuna polisi tangu wameanza kazi mika 20 ilio pita wako kwenye vituo vio via kazi kazi yao kubwa kuzuiya uarifu inakuwaje wasiwajue waalifu? wakamatwe polisi wa kawe goba tegeta wapelekeni rugalo jeshini kwa mp wajieleze hawa ndio wanao fuga ujinga huo
 
Hilo la ustaafu umelisema ww bosi. Ila kuhusu dhumuni inawezekana ni maslahi ya kisiasa zaidi kuliko maslahi ya kifedha sababu ya aina ya wizi wanaofanya na tabia ya kudhuru mwili.
Kwamba ni wanasiasa wa eneo husika? Hao wanasiasa wanachafuliwa au wanufaika na tabia hii? Mbinu hii ni maarufu kwenye mataifa kama Congo DR, Burundi, Somalia ili uchaguzi sifanyike waendelee kushikiria nafasi zao.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
How? Mnataka wafanye nini?
polisi yuko kituoni zaidi ya miaka 20 kazi yake kupambana na vibaka inakuwaje asiwajue? mpaka wanavamia watu na kuwaumiza alafu unauliza polisi wafanyeje?
 
Kabisa mkuu
Hilo la ustaafu umelisema ww bosi. Ila kuhusu dhumuni inawezekana ni maslahi ya kisiasa zaidi kuliko maslahi ya kifedha sababu ya aina ya wizi wanaofanya na tabia ya kudhuru mwili.
Yaani wewe umeliangalia kama mimi ninavyoliangalia suala hili. Hii nchi toka tulipoamua kufanya siasa chafu na kundi fulani kutumia kila njia kulinda maslahi yao tulijimaliza. Sasa hivi tunapiga hatua moja baada ya nyingine kwenda kujiangamiza.

Siku hiyo ikifika tusitafute mchawi aliyeko nje, ni sisi wenyewe tulipandikiza misingi ya kuliangamiza hili taifa.
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Yaani wewe umeliangalia kama mimi ninavyoliangalia suala hili. Hii nchi toka tulipoamua kufanya siasa chafu na kundi fulani kutumia kila njia kulinda maslahi yao tulijimaliza. Sasa hivi tunapiga hatua moja baada ya nyingine kwenda kujiangamiza.

Siku hiyo ikifika tusitafute mchawi aliyeko nje, ni sisi wenyewe tulipandikiza misingi ya kuliangamiza hili taifa.
Kweli mkuu
 
Polisi wakiamua mtaanza piga kelele
Paka akiingia kwenye nyumba yenye panya waharibifu mwenye nyumba anafurahi hata majirani wakipiga kelele hawataki kuona paka.
 
Kwanini hao majeruhi hawakupewa PEP ya kujilinda na VVU ,nawashauri wapewe badi wapo ndani ya 72hrs,hayo mapanga wameyatumia kwa watu wangapi kuwakata?

Kama Polisi wameshindwa kuthibiti Panya Road waseme ili JWTZ waingie mtaani ,pia majeruhi hapo ametoa ushauri mzuri ,polisi wanakuwa wengi sana mchana kufanya deal zao za kukamata magendo ambayo sio kazi yao lakini usiku wanakuwa wachache sana,wajaribu kubadili utendaji ,usiku wawe wengi na pia viongozi wa serikali za mitaa waamasishe wananchi kulipa hela ya ulinzi kila mwezi ili vijana wawe wanalinda kuanzia saa tatu mpaka 11 na 30 alfajiri.
 
Kwanza kabisa lazima tukubaliane kimsingi kuwa panya road ni school drop out hasa shule ya msingi na secondary, lakini wengi pia ni wale waliolelewa Kwa style ya single mothers hii nimeongea sio kukejeli lakini ni kutokana na mahojiano waliyofanya wenzao kituo Cha polisi.

Jana Tarehe 11.02.23 siku ambayo Simba ilifungwa huko Ugenini, Panya road walifanya matukio ya uvamizi na uporaji katika maeneo ya Bunju B.

Mimi najiuliza kwanini Hawa vijana wamekuwa wakatili kiasi hiki, yaani wakifanya uvamizi lazima wakuchororonge mapanga hata kama utakuwa mtiifu na kuwapa wanachotaka tofauti na majizi mengine.

Wao wakikufikia wanaanza na panga Halafu ndo wanadai Hela , simu, etc, pia wakishindwa kuchukua kitu wanakiharibu either Kwa kukipiga nyundo au kukikatakata.

Pia katika video hii hapa chini utaona Bado kuna Watanzania wachache wanakaa na hela ndani , mfano mmoja kuna mtu kakutwa na laki sita ndani, sijui ilikuwa ya matumizi ya kawaida sijui.

Pia najiuliza Hawa vijana walitumia mbinu gani kuweza kujikusanya wengi vile na kuunda timu yaani genge la wahalifu, hiyo sio kazi ndogo, huyo Kiongozi wao ana upeo fulani wa kipekee. Tunaita team building skills


Hao panya waangamizwe mara moja ni hatari.
 
Back
Top Bottom