BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Kundi la Vijana wanaojihusisha na Uhalifu Maarufu kama 'Panya road' wamevamia nyumba moja Kawe mtaa wa Mzimuni usiku wa kuamkia leo Septemba 14, 2022 na kujeruhi watu watano na Kumsababishia kifo Binti aliyetambulishwa kama Maria paschal Basso mwenye umri wa miaka 24.
Eneo la tukio na pameonekana uharibifu walioufanya kwenye nyumba ikiwemo kuvunja milango na kufanikiwa kuingia ndani, na kuwapora simu na fedha na kuharibu vitu mbali mbali ikiwemo TV.
Pia baadhi ya Mashuhuda wa tukio hilo pamoja na Mwenyekiti wa Mtaa huo ambao wameeleza kuwa tukio hilo lilifanyika usiku wa saa 8 na vijana wanaokadiriwa kufikia 30 waliokuwa na silaha mbalimbali yakiwemo mapanga.
Wahalifu hao waliwapiga na kuwajeruhi watu wanne ambapo wawili walikuwa mahututi na kati yao mmoja amefariki huku wengine wakipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Eneo la tukio na pameonekana uharibifu walioufanya kwenye nyumba ikiwemo kuvunja milango na kufanikiwa kuingia ndani, na kuwapora simu na fedha na kuharibu vitu mbali mbali ikiwemo TV.
Pia baadhi ya Mashuhuda wa tukio hilo pamoja na Mwenyekiti wa Mtaa huo ambao wameeleza kuwa tukio hilo lilifanyika usiku wa saa 8 na vijana wanaokadiriwa kufikia 30 waliokuwa na silaha mbalimbali yakiwemo mapanga.
Wahalifu hao waliwapiga na kuwajeruhi watu wanne ambapo wawili walikuwa mahututi na kati yao mmoja amefariki huku wengine wakipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.