Passport ya Tundu Lissu iliibwaje akiwa Ujerumani?

Passport ya Tundu Lissu iliibwaje akiwa Ujerumani?

Kwani waliotaka kumtoa uhai Lissu ilikuwa ni misingi gani? Sasa we unashangaa kumkatalia passport?
Kwa hiyo serikali anayoiongoza Samia ndo wanaomkatalia Lissu pasipoti yake?
 
Tundu Anthipas Lissu ni mwanasheria na msomi. Sina wasiwasi kuwa alishafuatilia taratibu zote, lakini mamlaka zinazohusika haziwezi kufanyia kazi maombi yake kwa hofu iliyojengwa na watawala hasa utawala uliopita wa ile awamu ya giza.

Waliomwibia Lissu passport yawezekana walitumwa kumdhuru na/au kumwibia nyaraka mbalimbali anazofanyia kazi. Nina imani kuwa hizo nyaraka na passport zipo Tanzania zimekaa tu mezani kwa mtu.

Kwa mazingira hayo, ilifaa Lissu apeleke ombi lake kwa Rais ambaye anaweza kutoa tamko tu na wahusika wakaondoa hayo mambo machafu yanayoendelea kuiweka Tanzania katika zama za ujinga na giza.
I conquer [emoji848]
Bongo noma sana,Lisu sio mjinga amuombe rais.
 
Kwamba huelewi anaposema ameibiwa passport? Kama aliibiwa mkoba wenye passport, leseni, pesa, nguo za ndani, kitabu cha katiba ya chama chake na vitu vingine, je alipaswa avitaje vyote?

Suala la nani aliiba passport anajua aliyeiba. Inawezekana ni wale ambao hawataki arudi Tanzania.

Kuhusu kumwambia Rais, ukiacha kuwa Rais ni taasisi, anayeshika nafasi ni mtu. Kila mtu huomba msaada kwa mtu mwenye connection na kitu fulani. Kama wewe una jamaa uhamiaji kwani ni shida kuomba msaada? Sasa yeye kakutana na mtu mwenye nafasi ya juu, na inawezekana alikuwa anakataliwa kupewa passport nyingine. Kaomba msaada kwa mtu mwenye connection naye.
Ni kweli kabisa. Ameomba msaada kwa mtu ambaye anaona ni wa msaada kwake na si kwa sababu ni Rais. Ikumbukwe kuwa hata kabla Mama hajawa Rais, alienda kumjulia hali Mh. TL kule Hospital Nairobi.
 
Afrika kuna ukiritimba.

Miguna Miguna alikua deported kwa madai ameishi Kenya kama raia wa Canada.

Inawezekanaje mtu aliyezaliwa Kenya na kuishi uhamishoni miongo miwili kwa kukimbia utawala dhalimu unasema sio raia?

Miguna alipoenda tofauti nao wakatumia loophole sasa kumfanyia deportation kwa madai ameukana uraia wa Kenya hivyo afanye kuomba upya.

Katiba mpya ya Kenya ya 2010 inaruhusu uraia pacha sasa kwanini hawamruhusu?

Katika majaribio yake 2 ya kurudi yamegonga mwamba kuanzia 2018 mpaka 2021, na mahakama zimeruhusu aingie ila serikali inakataa hii ndio Afrika na anaambiwa akiingia ataingia kwa tourist visa.

Kuomba hati ya kusafiria mpya inapopotea ya zamani inajulikaka , Lissu na Miguna Miguna ni wanasheria na raia halali wa mataifa yao na hatua hizo wan

Tatizo kubwa wamawekewa ngumu sababu ni wakosoaji wakubwa na wa wazi kwa serikali na Africa taasisi zinanyenyekea serikali sio kufuata sheria.
Halafu kuna watu hapa wanahoji kana kwamba wao wana akili kuliko Lissu!
 
Kwenye hili Lissu kaibiwa au kapoteza kwa uzembe wake na anapaswa kuwajibika kwa uzembe wake huu!
Passport ni kama kitambulisho kinapaswa kutunzws kwa umakini mkubwa na anayepoteza hati ya kusafiria huchukuliwa kama mtu mzembe na asiyejali!
Lissu kwenye hili ameonesha udhaifu mkubwa sana kushindwa kutunza kitu muhimu kama hiki labda itaonekana sio mzembe kama ana ushahidi alivamiwa na kuibiww hiyo hati!

Pengine Sukuma gang wa ujeremani wamemuibia[emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Na aliponyimwa hela ya matibabu pia alikuwa mzembe. Omba ya sikukute.
 
Huu Uzi umenifanya niwafahamu watu upeo wa akili zao,nilidhani wana akili ni ma great thinker kumbe hata Ku reason kitu kidogo hiki wameshindwa![emoji848][emoji848]
 
Taratibu za kupata passport mpya kama uliyokuwa nayo imepotea, zipo wazi.

Kwanini uombe msaada wa Rais?

Kama alikuwa anakataliwa, alikuwa anakataliwa kwa misingi gani?

Bado sielewi aisee!
Unajua kusoma na kuandika ?
 
Ninachokiona hapo ni kuwa Tudu Lissu hakutegemea kama mama atakutana nae, alipoomba kukutana nae alikuwa katupa turufu na alishakuwa na jibu la kukataliwa kuonana nae kwa 100%, ili apayuke kisiasa. Mama kamziba mdomo na akawa hana la kusema hajui amwambie nini, akaanza kubwabwaja.
Wewe haya uliyoyaandika umebwabwaja.

Mnapenda sana wenzenu wafikwe nimatatizo huku mkicheka na kutoa kejeli na kila siku unajifanya ulamaa wa dini humu kumbe buyu tupu.

Ulichokiona tu?????
 
Kwamba huelewi anaposema ameibiwa passport? Kama aliibiwa mkoba wenye passport, leseni, pesa, nguo za ndani, kitabu cha katiba ya chama chake na vitu vingine, je alipaswa avitaje vyote?

Suala la nani aliiba passport anajua aliyeiba. Inawezekana ni wale ambao hawataki arudi Tanzania.

Kuhusu kumwambia Rais, ukiacha kuwa Rais ni taasisi, anayeshika nafasi ni mtu. Kila mtu huomba msaada kwa mtu mwenye connection na kitu fulani. Kama wewe una jamaa uhamiaji kwani ni shida kuomba msaada? Sasa yeye kakutana na mtu mwenye nafasi ya juu, na inawezekana alikuwa anakataliwa kupewa passport nyingine. Kaomba msaada kwa mtu mwenye connection naye.
Umemjibu nadhani harudii kuhuliza tena kitu cha kijinga kama Kigogo2014 mwenziye
 
Na kwa mtu ambaye hana connection na amepoteza pasport utaratibu ukoje?
Je wanaopoteza pasport wote huwa wanaenda kumuomba raisi awasaidie kuzipata au ya kwake ni special?
Usiombe upoteze passport wakati wewe ni number one enemy of state.
 
Inaweza kuwa kweli passport yake imeibiwa au imepotea, Hilo analijua yeye. Lakini kitendo Cha kukaa kimya bila kutoa taarifa Hadi alipokutana na Rais na kumuomba msaada amsaidie hakijakaa vizuri.

Vinginevyo angesema amepata vipingamizi Gani na akiba nani wanamkwamisha kupata passport yake.
Ninani aliyekuwa tayar kumsaidia bila ya kumuambia rais kwa vile ameonanae.

Ni mara ngapi alippkkuwepo nchi kabla ya shambulio kama anafuatiliwa Ni watu waovu mpaka namba za gar akataja ni kiongozi aliyejali hayo mwisho wake akapigwa risasi 38 na hela matiababu hakupewa na ubunge akafukuzwa sasa aende wapi unakokutaka ili asikilizwe bila ya kuongea na rais?

Kwani ameelzea moja hayo matatzo yanayomkumba yeye?
 
Sijaelewa kabisa!

Tundu Lissu kasema kuwa amemuomba Rais Samia amsaidie kupata passport mpya kwa sababu aliyokuwa nayo iliibwa mwezi uliopita huko Ujerumani.

Aliyeiiba hiyo passport ni nani? Na iliibwa au yeye aliipoteza na anachanganya kupoteza na kuibwa?

Na kama iliibwa, kwa nini hilo liwe suala la Rais kumsaidia yeye aipate tena passport yake?

Kwani hakuna taratibu za kufuata pale passport yako inapoibwa au inapopotea mpaka yeye amtumie Rais kuipata mpya?

Kwa kweli kwenye hili sijamuelewa!
Kuibiwa passports kwenye hizo trains za Europe kitu cha kawaida sana. Kuna Waturuki wengi tu wanaiba bags hasa za laptop na ukiweka passport humo inakwenda.

Sasa Lissu kaenda kuomba passport mpya na wanamzungusha tu. kumbuka huyo Sokoine alipoteza cheo kwa kwenda kumuona Lissu hospitali .
 
Back
Top Bottom