Paul Kagame katoa onyo kwa Kiswahili, walengwa mmepata ujumbe?

Paul Kagame katoa onyo kwa Kiswahili, walengwa mmepata ujumbe?


Mibongo ni VIAZI
Sasa kama aliaona anakaribia kukamuliwa mavi ulitaka abaki? Ushaambiwa alikuwa chini ya darubini kali! Tz ni nchi isiyo na ubaguzi, huwezi kuzuiwa ajira kisa una asili ya nchi fulani..., hii ni nchi huru
 
Kagame kama kweli anajiamini kwanini asianzishe hiyo vita anayojitapa kila siku yuko vizuri?

Huku kujisifu kwake kila siku bila vitendo vyovyote pia kunaweza kuwa ni dalili ya mtu asiyejiamini, anajihami tu, ili aachwe aendelee kuharibu amani ya eneo la maziwa makuu.

Huyu naona anaweza kuwa anaongoza kwa mdomo na ujuaji kuwashinda marais wote wa hili eneo, lakini sio zaidi ya hapo, kwasababu kama anaona anachokozwa kila siku kwanini asiwafundishe adabu hao wachokozi?
Kagame anawatishia KENYA ambao wamepeleka jeshi lao kupambana na waasi wa M-23.
Sisi tuliwatimuaga hao m23 wake chapu tu, mbona alinywea? Tukamalizia na oparesheni kimbunga..
 
Rais Paul Kagame alikuwa anaapisha mawaziri wapya hapo jana mapema. Alianza kutoa hotuba yake kwa lugha ya Kinyarwanda, lakini baadae akahamia kwenye lugha ya Kiingereza na baadaye akatoa kitisho kizito kwa lugha ya Kiswahili. Wengi wetu tumeona hicho kipande chenye lugha ya kiswahili kikisambaa huko mitandaoni hasahasa kwa raia wa Tanzania na Kenya. Kitendo cha kusambaa mtandaoni kwa kasi hivi, inaonesha kabisa walengwa wa ujumbe ni watu gani.

Kwenye FASIHI njia moja kuu ya kufikishia ujumbe ni kuifahamu HADHIRA, lakini kubwa zaidi ni kufahamu lugha ambayo HADHIRA hutumia. Siku zote kimetumika Kinyarwanda na Kiingereza, lakini leo hii na Kiswahili juu, tena sehemu ambayo anatoa vitisho. Kwenye Dakika ya 27, ameanza kuwaliza mawaziri wake kama wanafahamu lugha ya kiswahili, wakamjibu wanelewa, ndipo akaanza kuzungumza kiswahili.

Huu ujumbe siyo wa wanyarwanda, wazungumzaji wakubwa wa lugha ya kiswahili wanafahamika, hivyo hicho kitisho ni ujumbe kwenu. Hajataja mhusika, mimi binafsi sitamtaja, lakini naamini walengwa mapema leo, watakuwa washafikiwa na huu ujumbe.

Alichokisema Rais Paul Kagame ni kwamba ukubwa wa pua siyo wingi wa kamasi. Kwamba Rwanda doesn't have the means, but they have the methods (ways). Hivyo kijiografia Rwanda ni nchi ndogo isiyo na rasilimali nyingi, lakini wao siyo migomba mifupi kama wanavyofikiriwa. Binafsi naamini, haivuki miaka miwili (2) kuna mtu kwenye huu ukanda wetu wa maziwa makuu atatoa kilio kikubwa sana.

View attachment 2433276
Nionavyo mm pia Kaghame hajajuwa kuwa nimfupi ila anajiona mrefu. Swali rahisi angejiuliza ni nani anasumbua DRC? Na je ninani anachezesha huu mchezo. Akijuwa hili ataiponya nafsi yake ila asipo lijuwa hili Pagasus yake itakuwa ina mpa wrong taarifa. Ukiniuliza mm nitasema neno moja siku za Marais wa miasha wawili zina soma kama mshale wa saa. Keep silence u shall see maneno ya mtabiri wa kimataifa. Asante
 
Kagame kama kweli anajiamini kwanini asianzishe hiyo vita anayojitapa kila siku yuko vizuri?

Huku kujisifu kwake kila siku bila vitendo vyovyote pia kunaweza kuwa ni dalili ya mtu asiyejiamini, anajihami tu, ili aachwe aendelee kuharibu amani ya eneo la maziwa makuu.

Huyu naona anaweza kuwa anaongoza kwa mdomo na ujuaji kuwashinda marais wote wa hili eneo, lakini sio zaidi ya hapo, kwasababu kama anaona anachokozwa kila siku kwanini asiwafundishe adabu hao wachokozi?
Sasa si ndo vita inaendelea huko Mashariki mwa DRC mkuu? Au huna habari🤣
 
Wacha Bhwanah!
Umezungukaweeee, kidogo nijiondokee zangu!

Hakuna kitu hapo mkuu, asipoangalia huu ndio utakuwa mwisho wa Bwana Fito. M23 ni jiwe litakalomwangamiza.

Lakini kinachonifurahisha ni kuona unafiki/utapeli wa baadhi ya mataifa ya ukanda huu wa kujitwisha mzigo kwa jina la Jumuia, halafu wanafanya ghelesha kupeleka jeshi huko eti kulinda maslahi yao (ya nchi yao) kwa mgongo wa Jumuia.

Haya, jeshi linafika eneo la mapambano, hapo hapo hadithi inabadilika, eti wao wamekuja kulinda amani na siyo kuimarisha amani! M23 anawaangalia tu na kucheka.

Nisitoe hadithi ndefu, lakini sasa ni wazi, waCongo wenyewe sasa wameamua, hawataki kuchezewa na hivi vikaragosi na vinyago.

Kinachonipa moyo kwa upande wetu, ni kutofuata mkumbo wa hao wanaotumia jina la Jumuia kujiingiza na kutumika kama 'tissue' bila ya kujitambua.
Lakini ifahamike, tukiona maslahi yetu yanachezewa, tusisite kuyalinda.
Eneo lenye maslahi makubwa kwa Tanzania ni jimbo la zamani la Katanga. M23 hawana nia yoyote ya kwenda hadi jimbo la Katanga.
Bidhaa tunazouza nyingi zinakwenda jimbo la Katanga kutumika katika shughuli za uchimbaji wa madini. Bidhaa nyingi za transit zinazopitia bandari zetu na kubebwa na magari ya Kitanzania na Kitanzania-Zambia, zinaenda katika jimbo la Katanga zamani. Siku hizi ni majimbo mawili.
Kwa uchache wa maslahi yetu mashariki mwa DRC ukilinganisha na Uganda, Rwanda na Kenya, sioni sababu ya kumwaga damu ya vijana wetu kwa ajili hiyo.
Sisi tukae macho, usumbufu wowote usitokee kusini na kusini mashariki mwa DRC. Sisi maslahi yetu yapo sana katika Copper Belt ya Zambia na DRC ambayo pia ina madini mengine lukuki.
 
Leo nimeanza kusikia tone imebadilika Jeshi la Afrika ya Mashariki linasema linataka kudili na Vikundi vyote ikiwemo vya Kihutu lakini swali linabaki palepale kwa Cogolese Tutsis 23 iwapo watanyang'anywa silaha kuna hatari ya Genocide nyingine ikatokea huko Congo dhidi yao.

Waingizwe kwenye Jeshi la Kongo na Rank zao halafu wabakizwe kwenye Command ya North Kivu tena watasaidia kuiondoa ADF ya Magaidi.
Kuna makundi mengi sana ya kikabila yenye silaha mf Codeco ya walendu, maimai ya wabembe na vingine vingi tu.

Kupokonywa silaha ni muhimu kwa amani ya kudumu ya Drc
 
Eneo lenye maslahi makubwa kwa Tanzania ni jimbo la zamani la Katanga. M23 hawana nia yoyote ya kwenda hadi jimbo la Katanga.
Bidhaa tunazouza nyingi zinakwenda jimbo la Katanga kutumika katika shughuli za uchimbaji wa madini. Bidhaa nyingi za transit zinazopitia bandari zetu na kubebwa na magari ya Kitanzania na Kitanzania-Zambia, zinaenda katika jimbo la Katanga zamani. Siku hizi ni majimbo mawili.
Kwa uchache wa maslahi yetu mashariki mwa DRC ukilinganisha na Uganda, Rwanda na Kenya, sioni sababu ya kumwaga damu ya vijana wetu kwa ajili hiyo.
Sisi tukae macho, usumbufu wowote usitokee kusini na kusini mashariki mwa DRC. Sisi maslahi yetu yapo sana katika Copper Belt ya Zambia na DRC ambayo pia ina madini mengine lukuki.
Hapana, sikubaliani nawe kamwe kwamba maslahi ya Tanzania yanaishia Katanga.

In fact, maslahi makubwa zaidi yapo huko kati na kaskazini mwa DRC. Kushindwa kwetu hadi sasa kutumia fursa isiwe sababu ya kutoendelea kutafuta fursa hizo.

Kwa nini uwepo wa Ziwa Tanganyika kati yetu ndiyo kiwe kikwazo kwetu badala ya kufanya kuwe fursa baina yetu?

Usinielewe vibaya, sichochei tujitumbukize kichwa kichwa kwenye mgogoro wa waKongo. Sisi tulishafanya kazi ya aina hiyo, ya kupigania wenzetu siku nyingi sana, na hakuna anayehoji heshima hiyo kwetu. Hiyo kazi tuliimaliza, wakati huu tusilaumiwe kwa kutojihusisha na maswala ya namna hiyo, lakini ni wajibu wetu mkubwa wa kujihusisha na mashirikiano ya kiuchumi baina yetu. Kama ni upatanishi, sawa; na kama hatuchokozwi, sioni sababu ya kwenda kupambana.

Ninakusihi, hebu chukua ramani tena, na angalia kwa makini sana tulipo (Tanzania) na ushiriki wetu katika eneo husika.
Tanzania ndio lango sahihi la kuingila Mashariki yote ya Congo, tusijirudishe nyuma kwa visingizio visivyokuwepo.
Halafu uje uniambie Mombasa achukue nafasi dhidi yetu? Sikubaliani nawe kabisa.
 
Tena mkuu kwa kipindi kile Kagame Nakumbuka alisema anajua hata shuka la kulalia la kikwete, tena alimwambia nakusubili sehemu sahihi nikupige, tena alidhamilia sana tena sana, Sana tena sana, na kwa kipindi kile alisema kabisa hata michoro wa ikulu ya DSM anaujua , na alikuwa na watu wengi tuu hapa bongo mpk huyo tuliyemsema.
Kwa alifanya nini kipindi kile? Naomba nijibu

Huyo Kagame yeye alifanya nini baada ya kulijua shuka la kulalia la JK? 🤣🤣🤣, machocko wengine bhana...
 
Kuna makundi mengi sana ya kikabila yenye silaha mf Codeco ya walendu, maimai ya wabembe na vingine vingi tu.

Kupokonywa silaha ni muhimu kwa amani ya kudumu ya Drc
Kundi la Wakongo wenye asili ya Kitutsi M23 liingizwe kwenye Jeshi la Kongo halafu Nchi za jumuia za Afrika Mashariki tuli train Jeshi la DRC liwe kwenye Standard kama zetu ili visitokee vikundi vingine tena kutumia Ardhi ya Kongo kushambulia Majirani.
 
Hapana, sikubaliani nawe kamwe kwamba maslahi ya Tanzania yanaishia Katanga.

In fact, maslahi makubwa zaidi yapo huko kati na kaskazini mwa DRC. Kushindwa kwetu hadi sasa kutumia fursa isiwe sababu ya kutoendelea kutafuta fursa hizo.

Kwa nini uwepo wa Ziwa Tanganyika kati yetu ndiyo kiwe kikwazo kwetu badala ya kufanya kuwe fursa baina yetu?

Usinielewe vibaya, sichochei tujitumbukize kichwa kichwa kwenye mgogoro wa waKongo. Sisi tulishafanya kazi ya aina hiyo, ya kupigania wenzetu siku nyingi sana, na hakuna anayehoji heshima hiyo kwetu. Hiyo kazi tuliimaliza, wakati huu tusilaumiwe kwa kutojihusisha na maswala ya namna hiyo, lakini ni wajibu wetu mkubwa wa kujihusisha na mashirikiano ya kiuchumi baina yetu. Kama ni upatanishi, sawa; na kama hatuchokozwi, sioni sababu ya kwenda kupambana.

Ninakusihi, hebu chukua ramani tena, na angalia kwa makini sana tulipo (Tanzania) na ushiriki wetu katika eneo husika.
Tanzania ndio lango sahihi la kuingila Mashariki yote ya Congo, tusijirudishe nyuma kwa visingizio visivyokuwepo.
Halafu uje uniambie Mombasa achukue nafasi dhidi yetu? Sikubaliani nawe kabisa.
Hongera kwa kujibu kwa hoja. Una kiwango fulani cha maturity bila kujua umri wako.
Mimi na wewe tuna mawazo yanayofanana tukichukua concept na kuacha tofauti ndogo ndogo za kibinadamu.
Mfanano wetu uko hivi:
1. Sote tunataka kufaidika kutokana na kuwa jirani muhimu kwetu na kwa Ulimwengu yaani DRC kwa maana ya sisi kuuza na kununua kwao lkn pia na bandari yetu kuwa kama lango muhimu la kuingilia DRC na hivyo nchi yetu na watu wake hasa wafanyabiashara kufaidika.
2. Sote tunakubaliana kwa concept kwamba hatuna sababu ya kumwaga damu ya vijana wetu tena.
3.Nakubaliana na wewe kwamba hatutatakiwi kukaa kuegemea migongo kwenye viti bila kushirikia mchakato wa kutafuta amani mashariki mwa DRC. Hata mimi nashangaa Kenya wamekuwa mstari wa mbele huku sisi ambao ni marafiki wa DRC tukiwa waangaliaji tu, just watchers, not observers.
Lakini natofautiana na wewe juu ya kuangalia jiografia. Mashariki mwa Congo hakuna biashara ya maana kwenye eneo la consumption zaidi ya extraction ambayo ndio hiyo inapambaniwa. Vurugu tupu.
Bado nasisitiza kuwa asali kwetu as we speak ni kusini na kusini mashariki kwa DRC.
 

Sasa hivi tutarudia hii oparesheni!!
 
Back
Top Bottom