Paul Makonda akutana na Viongozi wa madhehebu na Taasisi za dini, asema anayoyafanya Rais Magufuli yanazidi maelekezo ya ilani ya CCM

Paul Makonda akutana na Viongozi wa madhehebu na Taasisi za dini, asema anayoyafanya Rais Magufuli yanazidi maelekezo ya ilani ya CCM

Ukisikia mawazo mgando ndio haya. Sasa mtu akikuambia ana degree nne utasema amekutukana.
 
Lakini kwani amemaanisha nini?

Hata hivyo ni machinjio ya vingunguti wala sio machinjio ya imani yoyote ile ya kidini.
 
VP kuhusu viwanda vya nyama?? huko kunamashekhe?? mbona mwala nyama za kwenye makopo??
 
Kwani hayo machinjio ni ya Bakwata au ujenzi wake unafadhiliwa na Bakwata? Kwa nini msijenge machinjio yenu ambamo mtatumia hizo taratibu?

Mnakula sana Mahotelini na kwa mama Ntilie. Mnakula Chips Kuku mitaani. Mna uhakika gani kwamba hao Mifugo wamechinjwa kwa utaratibu wenu?
 
Na huyu Ni msemaji was chama au Sirikali?
 
Ni katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.

Karibu!

Kardinali Pengo na Sheikh wa mkoa kwa niaba ya Mufti wanauombea mkutano huo.

Sasa viongozi wa dini wanaangalia mkanda wa video unaomuonyesha RC Makonda akitolea ufafanuzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

------
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kasi ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo inayofanywa na Rais wa Tanzania, John Magufuli inazidi maelekezo ya ilani ya CCM.

Makonda ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Novemba 18, 2019 katika mkutano wake na viongozi wa dini unaofanyika katika ukumbi wa Julius Nyerere (JNICC) ambako anawaeleza mambo yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kipindi cha miaka minne.

Amesema kasi ya kiongozi mkuu huyo wa nchi ni kubwa kuliko ilani hiyo, kwamba amefanikiwa kwa kuwa amemtanguliza Mungu mbele.

Amesema uchapakazi huo ndio umewafanya watendaji wengine kumuiga.

“Kawafanya hata viongozi wa Serikali wanaotumia hirizi kumtaja Mungu kwanza. Mara nyingi ameweka wazi kuwa mambo yanavyokwenda kasi hata yeye mwenyewe anamshangaa Mungu,” amesema Makonda.

Amesema ameamua kukutana na viongozi wa dini ili kuwaeleza miradi inayotekelezwa katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Chanzo: Mwananchi
maajabu ya Musa hivi Rais anajuwa kile kinafanyika au ndio ameamua kijana afanye yake.... Mungu tuepushe yajayo yanafurahisha. Kumpa Mamlaka kijana asie juwa wajibika niatari sana.
 
Back
Top Bottom