Paul Makonda amtaka mwandishi kumuuliza mama yake baada ya kumhoji tuhuma za kumshambulia Lissu

MTU ALIYE MUULIZA KAKOSEA KUULIZA KAENDA DIRECTY HAKUNA MTU MWENYE AKILI KAMA MAKONDA ANAWEZA KUJIBU UTUMBO HUO

Makonda angekuwa na busara angefanya haya

1. Angelaani tukio lile.

2. Angempa pole Lissu.

3. Angekanusha kuhusika.

4. Angempigia simu IGP na kumuuliza uchunguzi umefika wapi.

5. Angetoa maelekezo kwa IGP uchunguzi ikamilike ndani ya siku 30 kama alivyotoa maelekezo kwa Waziri Mkuu.
 


Kumtania?! Wewe Una utani na Makonda? Kuanzia lini?

Unadhalilisha utu wa mtu halafu unauita utani??

Hiyo busara mnayotaka Makonda aitumie ninyi mmeitumia kwa kiasi gani?

Uwepo wa Makonda unafanya tunawaona rangi zenu halisi.
 
Hili takataka lilikuwa limetupwa dampo, huyo aliyelirudisha aliona amefanya la maana?
 
..ameshindwa kukanusha.

..ameshindwa kutoa pole.

..ameshindwa kulaani tukio lile.

..ameshindwa kutumia vizuri nafasi hiyo kuushawishi umma kuwa hahusiki.


Akanushe tuhuma ambazo wanabambikwa watu tofauti kila kukicha kulingana na upepo wa kisiasa?

Kutoa pole ni lazima? Ni sheria?

Kulaani tukio kwa msingi upi?

Kuushawishi ummah kwamba hausiki? Kuna sheria inamuelekeza kufanya hivyo?
 
Hivi unadhani ana jibu jingine zaidi ya hilo? Sasa hapo tu mwandishi wa habari kamuuliza katoa hilo boko, siku akiulizwa na wapelelezi wa DCI si atawataja akina Mabeyo, Kapilimba na Sirro na tarehe na mahali kikao kilipofanyika cha kumuua Lissu chini ya Magufuli.

Frustration yake kubwa ni pale waliposhindwa kutoa roho ya Lissu kwa kuwa Kapilimba na Mabeyo walimuonya Makonda kwenye kikao kuwa inaweza ika abort, yeye na Musalika Makungu (RAS Tabora 2018-20) wakasema hawatafeli.

Ndipo hata taratibu za kuchimba kaburi Ikungi zikawa zimeandaliwa chap.

Ila take it from me huyu PIMBI Zerobrain Bashite atakufa kifo kibaya sawa na Samuel Doe wa Liberia
 
Akanushe tuhuma ambazo wanabambikwa watu tofauti kila kukicha kulingana na upepo wa kisiasa?

Kutoa pole ni lazima? Ni sheria?

Kulaani tukio kwa msingi upi?

Kuushawishi ummah kwamba hausiki? Kuna sheria inamuelekeza kufanya hivyo?

1. Tuhuma zimetoka moja kwa moja kwa mhanga wa tukio.

2. Kutoa pole sio lazima lakini ni uungwana.

3. Kulaani tukio kwa misingi kwamba ni tukio la kinyama na halistahili kwa yeyote yule.

4. Hakuna sheria inayomlazimisha kushawishi umma kuwa hahusiki.

5. kama kiongozi wa umma si sahihi kwa Makonda kuacha kukanusha tuhuma mbaya dhidi yake.
 


Huyo muhanga kisha wataja wangapi kwa tuhuma hizo hizo mpaka sasa?

Uungwana hufanyiwa waungwana, wahuni ufaidi uhuni.

Mtazamo wako hauwezi kuwa Sawa na wake kuhusu unyama ama ubinaadam kwenye tukio lolote.


Unapotuhumu mtu ni kazi yako wewe mtoa tuhuma kuthibitisha pasipo shaka tuhuma zako dhidi yake na sio kazi ya mtuhumiwa kutumia muda wake kukanusha tuhuma zako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…