Paul Makonda arejea, aibukia Uwanja wa Ndege Arusha uliopo eneo la Kisongo

Paul Makonda arejea, aibukia Uwanja wa Ndege Arusha uliopo eneo la Kisongo

Karibu tena Makonda!

Wakati upo huko ulipokuwa mengi yametokea

Nape na nyodo zake ashaliwa kichwa na kafuta akaunti zake zote za mitandaoni kwa hasira, January naye yuko Bumburi anasugua, Kabudi karejea kwenye System na mengine mengi. Karibu tuendelee kuijenga Tanganyika
 
Uongo mbaya. Tulumiss Makonda.

Karibu sana, naona umetia akili sio kama ulivyokua kabla ya mama Samia kushika madaraka, ulijimwambafai sana kwa kumuiga yule mjinga mwenzako.Tunakuombea aklli yenye manufaa kwa taifa iwe imekuingia. Maana hiyo ilikua huna.
Mjinga mwenzake nani

Ova
 


Updates...

Kumepita ukimya wa takribani mwezi mmoja huku swali kuu likiwa yupo wapi Mkuu wa Mkoa wa Arusha, RC Paul Makonda lakini leo Agosti 16, 2024 swali hilo limejibiwa baada ya kuonekana kwa mara ya kwanza akikagua ujenzi wa Uwanja wa ndege wa Arusha uliopo eneo la Kisongo.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda alipotembelea Uwanja wa Ndege wa Mkoa Arusha na kukagua Ujenzi huo unaondelea kutekelezwa leo Agosti 16, 2024 ameeleza chanzo cha utanuzi wa Uwanja huo.

RC Makonda amelezea kuwa itakuwa chanzo cha utanuzi kwa Uwanja huo wa ndege ni kuongeza kundi kubwa la Watalii wanaoingia nchini kupitia mkoa wa Arusha kwa uwepo wa vivutio mbalimbali vya utalii ambapo itaongeza Uchumi kwa taifa letu na kujitangaza zaidi kupitia utalii.

RC Makonda ameeleza zaidi kuwa ifikapo Septemba Mosi Uwanja kuanza kutumika kuanzia Septemba mosi, 2024 ambapo idadi ya watalii inakadiriwa kuongezeka zaidi.

Mkandarasi
Moja ya Miradi ambayo itafanyika katika uwanja huyo wa ndege ni kufunga taa za kuongozea Ndege kwa sababu uwanja wa ndege uwe kufanya kazi masaa 24.

"Tumeshapata Mkandarasi tayari na tumeshamkabidhi na sasa yupo katika hatua ya kufanya usanifu wa mfumo wenyewe".

"Lakini tatizo ambalo tunalo ni hile ardhi ya kufunga hizo taa za aproch ya kutua ndege, kwa sababu kiwanja chetu kutoka pale mwisho tuna mita 200 na lakini tunahitaji mita 500".

Soma Pia: Bananga: Jana nimeongea na Makonda sasa yupo Arusha, amemaliza likizo yake

Ujinga huungwa mkono zaidi kuliko werevu!!! Kwani kuna agenda gani hadi kuanzisha thread kama hii?
 
Kabisa livypobashiri mkeka wa kina nape na february akaona atembelee hiyo ngekewa ,sasa mara ya pili MUHINDI kamchania MKEKA.
Hahah maana kila mimi nkipekenyua nlikuwa naona kimya
Jamaa naona kajuwa kucheza na akili za watu

Ova
 
1723827691915.png

BAADA ya ukimya wa zaidi ya siku 33, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda amerejea katika kituo chake cha kazi leo tarehe 16 Agosti na kumaliza minong’ono iliyokuwa imeenea mitaani juu ya alipo kiongozi huyo machachari. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Makonda ambaye anafuatiliwa na Watanzania wengi kutokana na matendo na utendaji wake wenye utata, hapo awali iliripotiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu kwamba amekwenda likizo na kukaimisha majukumu yake kwake.

Hata hivyo, minong’ono ilizidi zaidi baada ya watu kuhoji uhalali wa likizo hiyo hasa ikizingatiwa alianza kuitumia nafasi hiyo ya mkuu wa mkoa tarehe 31 Machi mwaka huu, muda ambao kwa taratibu za likizo serikalini, hakuwa ametimiza muda wa miezi nane kazini.

Ukimya wake ulizidi kuibua mjadala huku baadhi ya watu wakihoji kuhusu afya yake baada ya kuibuka madai katika mitandao ya kijamii kwamba yupo nje ya nchi anatibiwa baada kunywesha sumu jambo ambalo hata hivyo hakuna kiongozi wa serikali aliyewahi kulizungumzia.

Leo Ijumaa mkuu huyo wa mkoa wa Arusha, amemaliza minong’ono hiyo baada ya kutua mkoani humo na kufanya ukaguzi wa jengo jipya la Uwanja wa ndege wa Kisongo jijini Arusha.

LIVE: MAKONDA AREJEA AIBUKA NA MAPYA AIRPORT.​


View:
 
Kwenye nchi iliyojaa mambumbumbu kama hii, ni sawa kabisa kumuita PCM akili kubwa.
Acha kuendeshwa na chuki! Hao akina Lisu mnaodai wana akili kubwa wameleta impact gani hapa Bongo!
Mnapenda kujivika akilo kubwa lakini you have nothing to offer!
Makonda yupo na ataendelea kuwepo kwa mapenzi ya Mungu!
 
Back
Top Bottom