Huyu jamaa hajui siri kubwa iliyopo kwenye huu ulimwengu na walimwengu.
Wapenda madaraka na fedha ni mafirauni wakubwa sana.
Ukiona MTU anapenda saana fedha na madaraka ujue huyo mtu ni firauni na msodoma mkubwa sana.
Na hao wameja kila kona ya dunia hii.
Wanawake wengi wapenda madaraka ni wasagaji na wasagwaji hali kadhalika wanaume wapenda madaraja.
Kwa Afarika wanajifanya kuwa wanaupinga ushoga mana wanajua kuwa wajinga ni wengi watawashangilia na kuona kuwa wanayoyakemea midomoni yanatoka Rohoni.
Afrika wateja wa vitendo viovu ndio wanaojinasibu kuwa wanavipinga ili waaminike machoni mwa watu.
Ndio maana Afrika unakuta mla rusha na mbadhirifu wa mali za umma anajinasibu mbele za macho ya watu kuwa anapinga rushwa.
Anayeiba kura anajinasibu kuwa anafanya uchaguzi huru na haki. Mla rushwa za ngono anajifanya mcha Mungu na mpinga udhalilishaji.
Mshirikina anajifanya anapinga mauaji ya alibino.
Mtupa takataka barabarani anazuia watupa taka na kuwatoza faini.
Afrika Mvunja sheria anajifanya anaisimamia . Afrika Hakimu mla rushwa anatoa huku na kufunga watu waliojaa magerezani.
Afrika Msimamiza wa misitu ana mashine ya kukata miti ndani na ndiye mfanya biashara ya mbao pori.
Mzuia ujangili anajua wateja wa pembe.
Afrika Biashara za msimamizi wa kodi zinakwepa kodi .
Afrika nyumba ya afsa wa Kampuni ya kusambaza umeme imechakachuliwa mita.
Afrika nyumba ya afsa wa idara ya maji haina mita ya maji.
Afrika mhamasishaji wa kuepuka ngono zembe ni kinara wa kufanya ngono zembe.
Afrika mzuia magendo ndiye mvusha magendo.
Afrika mshauri wa mambo ya ndoa ,ndoa yake Imevunjika.
Afrika muuza dawa za kuongeza nguvu za kiume hana nguvu za kiume.
Afriaka mtoa Pete ya bahati hana bahati.
Afrika mtoa dawa ya utajiri ni maskini wa kutupwa.
Afarika anayetatua migogoro ana migogoro.
Afrika ,anayepinga mabeberu ni beberu mkubwa. Anayechukia matajiri yeye anaupenda utajiri na ana Mali alizoficha.
Afrika anayepinga ukabila ni mkabila.
Afrika anayepinga udini ni mdini.
Kifupi Afrika mtu akikuambia kuwa anapinga ushoga mwambie aanzishe kampeni huru ya kupima watu huko kunakofanyiwa huo uchafu na yeye awe wa kwanza kupimwa.
Kulitaja taja hilo suala lenye laana kubwa ni mbinu ya Kifreemason ya kulieneza. Wanajifanya kuwa wanalipinga lakini wanalirudia rudia Mara kwa Mara mana wanajua kuwa hawawezi kuliunga mkono kwa wazi kulingana na mila za kiafrika. Wana mbinu nyingi za kulitangaza na kulijaza kwenye vichwa vya vijana na watoto kwa kulitaja Mara kwa Mara kwa kujifanya kuwa wanalipinga.
Mifumo ya kiserikali haikuanzia Afrika Bali ni zao la mabeberu.
Wakoloni ndio waliotuletea mifumo ya kiserikali barani Afrika na Yale yaliyojificha ndani yake.
Kilichotuumiza zaidi waafrika ni kukosa uwazi na ukweli na kuweka unafiki mbele.
Mwenyezi Mungu akomboe Dunia nzima hasa Bara la Afrika lilolojaa watu wenye ndimi mbili.
Sent using
Jamii Forums mobile app