Pre GE2025 Paul Makonda: Gambo usitake umaarufu wa kijinga, uwe unahudhuria vikao vya maendeleo Mkoa wa Arusha

Pre GE2025 Paul Makonda: Gambo usitake umaarufu wa kijinga, uwe unahudhuria vikao vya maendeleo Mkoa wa Arusha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

BabaMia

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2024
Posts
270
Reaction score
554
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda akiambatana na Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha Lami ya Mianzini-Olemringaringa amemtaka Mbunge wa Arusha Mjini Mhe. Mrisho Gambo kuwa anahudhuria vikao mbalimbali vya maendeleo ndani ya Mkoa wa Arusha, badala ya kuwasubiri Viongozi wa Kitaifa na kuzungumzia kero mbalimbali ndani ya Jimbo lake.

Mhe. Makonda ameeleza kuwa kufanya hivyo ni kutafuta huruma ya wananchi kinyume cha taratibu, akiziita kuwa ni siasa zisizokuwa za maendeleo kwa wananchi, akiagiza kuwa ni muhimu kwa Viongozi wateule na wa kuchaguliwa kushiriki vikao vya kupanga na kuamua kuhusu maendeleo ya Mkoa wa Arusha.

Kauli ya Mhe. Makonda inafuatia maombi ya Mhe. Gambo aliyeomba kwa Waziri wa Ujenzi kujengewa barabara ya Kilombero pamoja na ufungaji wa taa kwenye barabara mbalimbali za Jiji la Arusha, masuala ambayo kulingana na Mhe. Makonda yalishajadiliwa na maamuzi kutolewa kwenye vikao mbalimbali vilivyofanyika chini ya Maagizo ya Mawaziri mbalimbali wa Kisekta ikiwemo Kikao cha mapema leo asubuhi kilichohudhuriwa na Waziri wa ujenzi Mhe. Abdallah Ulega na Waziri wa fedha Mhe. Mwigulu Nchemba.
 
Duh! Hii kali.
Mbona yeye ni mpenda kuongea public katika mambo mengi?

Anajisahaurisha kuwa huwa anaitisha mikutano ya hadhara na kuanza kuhoji watendaji juu ya mambo ambayo tayari yapo serikalini?

Huyu Makonda lazima ana matatizi ya kiakili Leo hii kageuka ghafla kuwa muumini wa vikao? Hataki tena habari za mambo hadharani?
 
Mbona yeye ni mpenda kuongea public katika mambo mengi?
Anajisahaurisha kuwa huwa anaitisha mikutano ya hadhara na kuanza kuhoji watendaji juu ya mambo ambayo tayari yapo serikalini? Huyu Makonda lazima ana matatizi ya kiakili Leo hii kageuka ghafla kuwa muumini wa vikao? Hataki tena habari za mambo hadharani?
Alisha taja wale waliokuwa wanamtukana raisi mitandaoni? Wale mawaziri? Mbona hakusubiri vikao...!!
 
CCM mmeanza kukanyagana wenyewe kwa wenyewe. Kuna mtu alisema Serikali ya CCM ikimaliza kuwashughulikia wapinzani ndio hapo watarudi kushughulikiana wao wenyewe kwa wenyewe, ndio hii sasa taratibu tuna anza kuona yakitimia
 
Hehehe dah huku kuaibishana sasa haya maccm yameanza kupaluana makucha yenyewe kwa yenyewe kugombania uchawa wa bi kiremba.
 
Back
Top Bottom