Paul Makonda informer wa Benard Membe katika ya Utawala Magufuli

Paul Makonda informer wa Benard Membe katika ya Utawala Magufuli

Wapi kwenye andiko langu nimeandika Magufuli mbaya?!

Magufuli alimuona BM ni kikwazo kwenye Utawala wake na ningeweza kumzuia?!

Kwangu mimi JPM ni Rais bora kabisa kutokea katika Bara letu Afrika na kama ni mapungufu anayo kama ilivyo kwa binadamu yeyote.
This is a very honest post umebalance mapenzi yako na uhalisia. Safi sana
 
Ipo habari msisimko isiyofahamika na wengi kumhusu Aliyewahi kuwa W NJ ndugu Benard Membe aliyetangulia mbele za haki mapema juzi na ndugu Paul Makonda aliyepata kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Nyuma ya pazia, wawili hao wana hadithi nzuri na yenye fundisho ndaniye. Kwa sababu wahusika wakuu hatunao tena, yaani JPM na BM acha leo niwashirikishe.

Ikumbukwe, Makonda kabla ya ujio wa kishindo wa Magufuli Mamlakani alikuwa timu Membe tena mwandani kabisa! Na Membe ndiye aliye mshawishi Kikwete amteue Makonda kuwa DC wa Kinondoni. Lengo la BM kumwombea uteuzi mtoto mpendwa tena kwenye Wilaya yenye hadhi ya Jiji ilikuwa kumwandalia/ kumsafishia njia bwana Makonda ili baadae imuwie u rahisi kugombea Jimbo la Kinondoni mwaka 2015 kwenye Uchaguzi Mkuu. Na ndoto ilikuwa BM angefanikiwa kuwa Rais ndiposa angelimteua Makonda kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ( W MNN) ndoto iliyoyeyushwa na ujio wa bahati wa JPM.

Kutokana na JPM kutoka Kanda pendwa kama ilivyo kwa Makonda na kuelewana lugha, na kwa sababu nyingine ambayo ni nyeti aliyomtonya JPM na baada ya tonyo lile kuja kuwa la kweli; bwana Makonda akaaminiwa na JPM hakika. Hali ya kuaminiwa ghafla na Boss mpya ilipelekea ateuliwe kuwa RC wa Jiji Kuu la Dar es Salaam. Kilichofuatia baina ya wawili hao ni historia!

Sasa basi, pamoja na uswahiba wa kufa na kuzikana baina ya Makonda na JPM, bado Makonda alikuwa mwaminifu kwa BM. Lakini, baada ya JPM na BM kuwa maadui wakubwa BM alimpa uhuru Makonda wa kumponda huku akiendelea kumtonya za ndaniii kabisa ambazo JPM alikusudia kumtendea BM.

Hatari zote ambazo zilipangwa za kumhusu BM zilianzia kwa mtoto pendwa na kabla ya utekelezaji wake mtoto pendwa alimtonya BM kupitia namna ya mawasiliano yao waliyokuwa wameyafanya kuwa rasmi.

Mlishajiuliza kwa nini BM alikuwa anasanua kila mpango pangwa kwake? Jibu ni mnyetishaji alikuwa mtoto pendwa na JPM asingeweza kung'amua hilo kwa namna alivyokuwa anamwamini dogo na ilifikia wakati hata alikuwa anaenda mwenyewe kutekeleza mission bila awaye na kupitia mwanya huo alikuwa akikutana na mtu kati baina yake na BM kumpa mpango utarajiwao kumuumiza ili ajinasue.

ULISHAJIULIZA KWA NINI BM ALIKUWA AKIMZODOA JPM KWAMBA CHOCHOTE ANACHOKIPANGA IWE USINGIZINI AMA NDOTONI YEYE ANAKIFAHAMU?! JIBU NI MTOTO PENDWA ALIKUWA ANAVUJISHA SIRI.

Pamoja na mikakati yote iliyopangwa kwa ajili ya kumnyamazisha BM alikuwa mshirika, lakini dogo alihakikisha BM anatonywa ili aweze kujinasua. Hiyo yote ilitokana na wema aliotendewa na BM kabla ya JPM kuibuka ghafla.

BM alishamwepusha na hatari nyingi Makonda zilizokuwa zikipangwa na timu mamvi na R kipindi akiwashambulia kwa tuhuma za ufisadi. Lowasa na Rostam walichukizwa mno na Makonda kwa namna ambayo kwao ilikuwa inawachafua na walishuhudia kupitia mashambulizi ya Makonda twasira yao kisiasa, inaharibiwa. Ikumbukwe, bwana Lowasa alikuwa kinara wa mbio za kuutaka u Rais.

Pamoja na uswahiba wa yeye ( Makonda) na JPM lakini bado kwa namna yeyote aliapa kulipa fadhira kwa kumwepusha BM na dhahama yeyote ile.

Ujanja wote wa Membe na kiburi chote ndani ya Utawala wa JPM ulihisaniwa na Makonda ambaye ndiye alikuwa mwandani wa kufa na JPM.

Paul haishi Masaki kwa bahati mbaya. Paul ni CHUNGU NA TAMU KWA WATAWALA! Paul yupo, atakuwepo hadi mwenyezi Mungu ATAKAVYOAMUA VINGINEVYO.

Na siku USA watakapomwondolea Makonda tuhuma walizo mtuhumu, amini nawaambia mtoto pendwa atarejeshwa kesho yake katika Ufalme wa [emoji1241].

IMANI YA JPM KWA MAKONDA NDIYO ILIYOMWEPUSHA NA HATARI NYINGI BM.

NB: ZIMWI LIKUJUALO....
Hili nalo mkalitizame,,
 
Ipo habari msisimko isiyofahamika na wengi kumhusu Aliyewahi kuwa W NJ ndugu Benard Membe aliyetangulia mbele za haki mapema juzi na ndugu Paul Makonda aliyepata kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Nyuma ya pazia, wawili hao wana hadithi nzuri na yenye fundisho ndaniye. Kwa sababu wahusika wakuu hatunao tena, yaani JPM na BM acha leo niwashirikishe.

Ikumbukwe, Makonda kabla ya ujio wa kishindo wa Magufuli Mamlakani alikuwa timu Membe tena mwandani kabisa! Na Membe ndiye aliye mshawishi Kikwete amteue Makonda kuwa DC wa Kinondoni. Lengo la BM kumwombea uteuzi mtoto mpendwa tena kwenye Wilaya yenye hadhi ya Jiji ilikuwa kumwandalia/ kumsafishia njia bwana Makonda ili baadae imuwie u rahisi kugombea Jimbo la Kinondoni mwaka 2015 kwenye Uchaguzi Mkuu. Na ndoto ilikuwa BM angefanikiwa kuwa Rais ndiposa angelimteua Makonda kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ( W MNN) ndoto iliyoyeyushwa na ujio wa bahati wa JPM.

Kutokana na JPM kutoka Kanda pendwa kama ilivyo kwa Makonda na kuelewana lugha, na kwa sababu nyingine ambayo ni nyeti aliyomtonya JPM na baada ya tonyo lile kuja kuwa la kweli; bwana Makonda akaaminiwa na JPM hakika. Hali ya kuaminiwa ghafla na Boss mpya ilipelekea ateuliwe kuwa RC wa Jiji Kuu la Dar es Salaam. Kilichofuatia baina ya wawili hao ni historia!

Sasa basi, pamoja na uswahiba wa kufa na kuzikana baina ya Makonda na JPM, bado Makonda alikuwa mwaminifu kwa BM. Lakini, baada ya JPM na BM kuwa maadui wakubwa BM alimpa uhuru Makonda wa kumponda huku akiendelea kumtonya za ndaniii kabisa ambazo JPM alikusudia kumtendea BM.

Hatari zote ambazo zilipangwa za kumhusu BM zilianzia kwa mtoto pendwa na kabla ya utekelezaji wake mtoto pendwa alimtonya BM kupitia namna ya mawasiliano yao waliyokuwa wameyafanya kuwa rasmi.

Mlishajiuliza kwa nini BM alikuwa anasanua kila mpango pangwa kwake? Jibu ni mnyetishaji alikuwa mtoto pendwa na JPM asingeweza kung'amua hilo kwa namna alivyokuwa anamwamini dogo na ilifikia wakati hata alikuwa anaenda mwenyewe kutekeleza mission bila awaye na kupitia mwanya huo alikuwa akikutana na mtu kati baina yake na BM kumpa mpango utarajiwao kumuumiza ili ajinasue.

ULISHAJIULIZA KWA NINI BM ALIKUWA AKIMZODOA JPM KWAMBA CHOCHOTE ANACHOKIPANGA IWE USINGIZINI AMA NDOTONI YEYE ANAKIFAHAMU?! JIBU NI MTOTO PENDWA ALIKUWA ANAVUJISHA SIRI.

Pamoja na mikakati yote iliyopangwa kwa ajili ya kumnyamazisha BM alikuwa mshirika, lakini dogo alihakikisha BM anatonywa ili aweze kujinasua. Hiyo yote ilitokana na wema aliotendewa na BM kabla ya JPM kuibuka ghafla.

BM alishamwepusha na hatari nyingi Makonda zilizokuwa zikipangwa na timu mamvi na R kipindi akiwashambulia kwa tuhuma za ufisadi. Lowasa na Rostam walichukizwa mno na Makonda kwa namna ambayo kwao ilikuwa inawachafua na walishuhudia kupitia mashambulizi ya Makonda twasira yao kisiasa, inaharibiwa. Ikumbukwe, bwana Lowasa alikuwa kinara wa mbio za kuutaka u Rais.

Pamoja na uswahiba wa yeye ( Makonda) na JPM lakini bado kwa namna yeyote aliapa kulipa fadhira kwa kumwepusha BM na dhahama yeyote ile.

Ujanja wote wa Membe na kiburi chote ndani ya Utawala wa JPM ulihisaniwa na Makonda ambaye ndiye alikuwa mwandani wa kufa na JPM.

Paul haishi Masaki kwa bahati mbaya. Paul ni CHUNGU NA TAMU KWA WATAWALA! Paul yupo, atakuwepo hadi mwenyezi Mungu ATAKAVYOAMUA VINGINEVYO.

Na siku USA watakapomwondolea Makonda tuhuma walizo mtuhumu, amini nawaambia mtoto pendwa atarejeshwa kesho yake katika Ufalme wa [emoji1241].

IMANI YA JPM KWA MAKONDA NDIYO ILIYOMWEPUSHA NA HATARI NYINGI BM.

NB: ZIMWI LIKUJUALO....
Hili nalo mkalitizame,,
 
Ila Makonda katika watu ambao walikuwa na njia nyeupe ya kufika mbali ila wakaharibu upepo wao kwasababu ya Kiburi, majivuno na ufahari wa kupitiliza basi Makonda atafunga hesabu.

Huyu bwana angeweza kuzicheza karata zake vema miaka ya JPM na kumaintain low profile nina uhakika saa hii angekuwa ameshapata unaibu waziri au uwaziri kamili.

Kimsingi jamaa hakujua kwenda na zali lake. Ushamba mwingi.
 
nachojua kijana pendwa,ni kijana wa jk,na jk alikabishiwa huyo kijana kutoka kwa Pius msekwa,Basi jk akapewa ombi la kumlea kijana pendwa,jk akaja kumuamini kijana pendwa pale alipomsaidia kuzima Moto wa warioba wa rasimu ya katiba ,hapo jk akaona huyu kijana anamfaa Sana ,Basi jk akaona haoni mtu mwingine wa Kum train kijana aive haswa awe kachero wa kitengo ambaye atamtumikia yeye jk na maswahiba wake Kama BM,na ndipo akamkqbidhi kwa kachero mbobezi namba 3 (ambaye ni BM) ,jk akampa maagizo na ombi BM amnoe kijana aive haswa .BM akampokea kijana pendwa na kumuweka chini yake na hapo ndipo unaona ukaribu wa Siri Kati ya kijana pendwa ,BM ,na JK.

maigizo yote aliyoyafanya kijana pendwa kwa jp ,Hadi akakubalika na kuaminiwa na jp ,darasa alikuwa akilipata kwa BM . huyu kijana pendwa ni kachero undercover aliyei a haswa kwa Sasa ,japo Kuna vipengere alikuwa bado hajapitiahwa na mwal.wake Wa ukachero BM.

Utaona Kuna uswahiba Kati ya kijana pendwa na lemutuz , lemutuz ni mtt wa kachero mbobezi namba 1 ,hapa namzungumzia mzee JM wa kule makao makuu, kachero BM anamkubali Sana kachero mbobezi nba 1 ,mzee JM ,hivyo hata huyu BM alilelewa pia ki kachero na mzee JM(kachero mbobezi no.1) ,hivyo BM katika mishe zake za kikqchero enzi za utawala wa JP ,kachero BM akaona amtafute kijana ambaye pia atamsaidia kijana mpendwa ,na hapa aka muamuru kijana pendwa enzi hizo akiwa RC ,amuamini le bebez mtt wa kachero mbobezi no.1,si unajua mtt wa Simba ni simba tu,si unakumbuka Kuna kipindi le bebez aliwahi kusema JP aliwahi kumwambia anataka ampe uteuzi Ila yy akakataa akasema ,ampe connection tu za kupata pesa na sio teuzi.
Huu ni uongo uliokithiri
 
Ila Makonda katika watu ambao walikuwa na njia nyeupe ya kufika mbali ila wakaharibu upepo wao kwasababu ya Kiburi, majivuno na ufahari wa kupitiliza basi Makonda atafunga hesabu.

Huyu bwana angeweza kuzicheza karata zake vema miaka ya JPM na kumaintain low profile nina uhakika saa hii angekuwa ameshapata unaibu waziri au uwaziri kamili.

Kimsingi jamaa hakujua kwenda na zali lake. Ushamba mwingi.
Ndio maana sikubaliani na dhana ya kwamba alikuwa trained na ofisa ngazi ya juu wa TISS, haonyeshi akili wala mafunzo ya juu ila ngazi ya chini sana. Kilichombeba ni roho yake ilivyo, kuweza kutumika kwenye kazi chafu akawa mkuu wa wilaya. Kwa JPM kilichombeba ni kabila na kama asset ya siasa za majitaka, same thing na Sabaya ila huyu kabila lilimuachia uongozi wa wilaya na experience ya kumpandisha juu ya wadhifa huo hakuwa nayo.
 
Ndio maana sikubaliani na dhana ya kwamba alikuwa trained na ofisa ngazi ya juu wa TISS, haonyeshi akili wala mafunzo ya juu ila ngazi ya chini sana. Kilichombeba ni roho yake ilivyo, kuweza kutumika kwenye kazi chafu akawa mkuu wa wilaya. Kwa JPM kilichombeba ni kabila na kama asset ya siasa za majitaka, same thing na Sabaya ila huyu kabila lilimuachia uongozi wa wilaya na experience ya kumpandisha juu ya wadhifa huo hakuwa nayo.
Anaweza kuwa alikuwa trained kwa kazi moja tu maalum
 
Wapi kwenye andiko langu nimeandika Magufuli mbaya?!

Magufuli alimuona BM ni kikwazo kwenye Utawala wake na ningeweza kumzuia?!

Kwangu mimi JPM ni Rais bora kabisa kutokea katika Bara letu la Afrika! Na kama ni mapungufu basi anayo kama ilivyo kwa binadamu yeyote.
Magufuli ni Rais wa hovyo kuwahi kutokea Tanzania. Alikuwa muuaji, mwizi wa mali ya umma na mwongo, mkandamiza demokrasia na mtu asiyefuata utawala wa sheria. Kama angekuwa bado hai leo hii Taifa letu lingekuwa na mpasuko mkubwa kiuchumi kisiasa na kijamii kuliko zilivyo Yemen na Somalia. Tuendelee kumshukuru Mungu kwa kutuondolea yule shetani.
 
Hatari sana!
kwa JK hapo mkuu nina wasiwasi kama bado ni marafiki maana alimtaja mtoto wake kwenye tuhuma za dawa za kulevya. Au labda ntakuwa nimechanganya mafaili?
Hata kama. JK hawezi kumwacha coz bashite ni kibaka mzoefu na anaejiamini. Ni rahisi kumtumia kwani nj cheap labour.
Akipewa ugali tu, atafanya kazi mia.
 
Magufuli ni Rais wa hovyo kuwahi kutokea Tanzania. Alikuwa muuaji, mwizi wa mali ya umma na mwongo, mkanfaniza demokrasia na mtu asiyefyata utawala wa sheria. Kama angekuwa bado hai leo hii Taifa letu lingekuwa na mpasuko mkubwa kiuchumi kisiasa na kijamii kuliko zilivyo Yemen na Somalia. Tuendelee kumshukuru Mungu kwa kutuondolea yule shetani.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Hii kwa upande wako usilazimishe kila mtu amwone kwa mtizamo wako.
 
Back
Top Bottom