Paul Makonda kuitetemesha na kuitikisa mikoa kumi mfululizo bila kupumzika

Paul Makonda kuitetemesha na kuitikisa mikoa kumi mfululizo bila kupumzika

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Makonda Mwenezi.jpg

Paul Makonda, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo

Ndugu zangu Watanzania,

Fahamu ya kuwa Ndugu Paul Makonda Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Taifa, yule mwamba wa siasa za majukwaani na ambaye anachukuliwa kama sauti ya wanyonge na ambaye alitangaziwa Mwisho na maadui zake lakini Mungu akatangaza Mwanzo,ambaye kwake zege halilali,na ambaye anatajwa kama kijana jasiri sana katika ukanda huu wa Afrika mashariki na kusini mwa Afrika.

Ambaye akizungumza na kuanza ziara basi nchi yote husimama,vyombo vyote vya habari hushindana kupamba picha zake kurasa za mbele na mitandao yote hutekwa na habari zake na ambaye amekuwa kiboko ya CHADEMA anakwenda kuitikisa na Kuitetemesha mikoa kumi mfululizo kwa ziara ambayo inasubiriwa kwa hamu sana na mamilioni ya watanzania ambao walikuwa wanamsubiri kwa hamu kuwafikia huko waliko ili wamueleze kero zao kusudi azipeleke serikalini.

Sasa kama ulikuwa na shughuli yako au biashara yako unataka kuitangaza kupitia vyombo vya habari au mitandao ya kijamii,basi nakushauri usipoteze muda, ni bora usubili huyu mwamba amalize ziara yake ,maana kwa sasa anakwenda kuiteka nchi yote kimijadala na watu wote wanakwenda kutega masikio yao kusikiliza nini anazungumza na nini kinajiri katika ziara zake.

Kama wewe ni msanii na ulipanga kutoa wimbo wako basi ni bora uuweke kwanza pembeni mpaka Mheshimiwa amalize ziara zake,maana akishaingia mitaani huyu basi wimbo utakuwa ni mmoja tu ambao ni Makonda na utekelezaji wa ilani ya CCM tu.

Endeleeni kutulia Watanzania wenzangu maana najuwa mlimkumbuka sana na mlikuwa na hamu ya kumsikiliza mwamba akiunguruma kama Simba majukwaani.sasa amewasikia na anakuja kwa kishindo.

Watendaji wa serikali na wateule wa Mheshimiwa Rais andaeni majibu ya kila kitu juu ya kazi mnazofanya na kusimamia katika utekelezaji wa ilani ya CCM Katika maeneo yenu.Maana huyu mwamba huwezi kujuwa atakupiga wapi. Kumbuka huyu ni msemaji wa chama na mjumbe katika vikao vyote muhimu vya CCM. Sasa wewe lete nyodo zako huko uone kitakachokupata atakaporejea kupeleka mrejesho kwa chama juu ya aliyoyabaini mikoani huko na akina nani wanakichonganisha chama na wananchi au wanatesa wananchi au hawatoi huduma stahiki kwa wananchi au wanapuuza wananchi au hawawasikilizi wananchi.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.

========For English Audience Only========
Paul Makonda, the National Secretary for Ideology and Publicity of CCM, sets off on a national tour covering ten regions. To lend a listening ear to the concerns and issues of our fellow citizens.

Makonda, is embarking on this extensive tour with the sole purpose of connecting with Tanzanians from diverse regions.

As he crisscrosses the country, Makonda aims to create an open platform for dialogue, encouraging citizens to express their grievances, share their aspirations, and contribute to the discourse on national development. it is said that this tour is not just a political spectacle; it's an opportunity for every Tanzanian to be heard.

The ten regions are poised to become the stage for Makonda's interactive sessions, where he will engage with communities, listen to their stories, and gather insights that will be crucial in shaping policies and strategies. The tour is a testament to his commitment to inclusivity, ensuring that the concerns of every Tanzanian, regardless of their location, are taken into consideration.

However, the public has criticized this act as a CCM propaganda for the upcoming elections this year and 2024 and it is not an act of service delivery to the citizens of Tanzania.
 
amekuwa kiboko ya CHADEMA

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Punguza Shobo basi hapa nimekuona wewe ni Kibaraka na unatumikishwa kama Punda, mkate wako wa kila siku unaupata katika mazingira magumu sana. Yaani mpaka uwataje CHADEMA ndio ulipwe ? Kuna ACT, TLP, UDP CUF, SAU mbona hivyo vyama hujavitaja? Kichefuchefu sana we jamaa
 
Huyo ni takataka, dhulumati wa jengo la GSM, magari ya watu, na marekani wamem blacklist kwa kudhulumu haki ya kuishi
Weka ushahidi acha kuchafua watu hapa wewe. Marekani siyo Mungu.hao hao Marekani ndio walimuua Saddam Husseni kwa kisingizio kiwa anamiliki silaha za nyukilia.je uliziona au kuonyeshwa silaha hizo? Marekani waliuonyesha ulimwengu shehena ya silaha hizo? Vipi kuhusu muamari Gadaffi si hao hao walimuua kwa visingizio vya uongo baada ya kuona maono yake yanahatarisha maslahi yao na uwepo wao katika bara la Afrika? Hujawahi kusikia hata Barack Obama akikili Hadharani kuwa walifanya makosa kumuua Gadaffi? Sasa unaanzia wapi kuwaona kama miungu watu na kuwaamini kwa kila kitu? Za kuambiwa changanya na za kwako ndugu yangu.usiwe na akili kama kasuku au nyumbu.
 
Alitetemesha nchi wakati ule wa operation toa roho ya lissu na masandarusi ya miili ya watu ufukweni.

Sasa hivi labda acheze na akili za wajinga wajinga kama wewe.
Weka ushahidi wako hapa na siyo kuropoka tu kama hayawani ndugu yangu.
 
Punguza Shobo basi hapa nimekuona wewe ni Kibaraka na unatumikishwa kama Punda, mkate wako wa kila siku unaupata katika mazingira magumu sana. Yaani mpaka uwataje CHADEMA ndio ulipwe ? Kuna ACT, TLP, UDP CUF, SAU mbona hivyo vyama hujavitaja? Kichefuchefu sana we jamaa
 
Punguza Shobo basi hapa nimekuona wewe ni Kibaraka na unatumikishwa kama Punda, mkate wako wa kila siku unaupata katika mazingira magumu sana. Yaani mpaka uwataje CHADEMA ndio ulipwe ? Kuna ACT, TLP, UDP CUF, SAU mbona hivyo vyama hujavitaja? Kichefuchefu sana we jamaa
Hivyo vyama ambavyo unasema sijavitaja nimekuachi wewe uvitaje na kuviimba kama kasuku.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Fahamu ya kuwa Ndugu Paul Makonda Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Taifa,yule mwamba wa siasa za majukwaani na ambaye anachukuliwa kama sauti ya wanyonge na ambaye alitangaziwa Mwisho na maadui zake lakini Mungu akatangaza Mwanzo,ambaye kwake zege halilali,na ambaye anatajwa kama kijana jasiri sana katika ukanda huu wa Afrika mashariki na kusini mwa Afrika.

Ambaye akizungumza na kuanza ziara basi nchi yote husimama,vyombo vyote vya habari hushindana kupamba picha zake kurasa za mbele na mitandao yote hutekwa na habari zake na ambaye amekuwa kiboko ya CHADEMA anakwenda kuitikisa na Kuitetemesha mikoa kumi mfululizo kwa ziara ambayo inasubiriwa kwa hamu sana na mamilioni ya watanzania ambao walikuwa wanamsubiri kwa hamu kuwafikia huko waliko ili wamueleze kero zao kusudi azipeleke serikalini.

Sasa kama ulikuwa na shughuli yako au biashara yako unataka kuitangaza kupitia vyombo vya habari au mitandao ya kijamii,basi nakushauri usipoteze muda ,ni bora usubili huyu mwamba amalize ziara yake ,maana kwa sasa anakwenda kuiteka nchi yote kimijadala na watu wote wanakwenda kutega masikio yao kusikiliza nini anazungumza na nini kinajiri katika ziara zake.

Kama wewe ni msanii na ulipanga kutoa wimbo wako basi ni bora uuweke kwanza pembeni mpaka Mheshimiwa amalize ziara zake,maana akishaingia mitaani huyu basi wimbo utakuwa ni mmoja tu ambao ni Makonda na utekelezaji wa ilani ya CCM tu.

Endeleeni kutulia Watanzania wenzangu maana najuwa mlimkumbuka sana na mlikuwa na hamu ya kumsikiliza mwamba akiunguruma kama Simba majukwaani.sasa amewasikia na anakuja kwa kishindo.

Watendaji wa serikali na wateule wa Mheshimiwa Rais andaeni majibu ya kila kitu juu ya kazi mnazofanya na kusimamia katika utekelezaji wa ilani ya CCM Katika maeneo yenu.Maana huyu mwamba huwezi kujuwa atakupiga wapi.kumbuka huyu ni msemaji wa chama na mjumbe katika vikao vyote muhimu vya CCM. sasa wewe lete nyodo zako huko uone kitakachokupata atakaporejea kupeleka mrejesho kwa chama juu ya aliyoyabaini mikoani huko na akina nani wanakichonganisha chama na wananchi au wanatesa wananchi au hawatoi huduma stahiki kwa wananchi au wanapuuza wananchi au hawawasikilizi wananchi.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Maokoto yameshaidhinishwa!
 
Aina yako ya uandishi, sehemu zenye ccm ukiweka chadema na sehemu zenye samia, makonda n.k ukiweka Mbowe, Lissu n.k bc huwezi kutofautisha na uandishi wa Erythrocyte
 
Maokoto yameshaidhinishwa!
Chama cha Mapinduzi ni chama kikubwa kilichokamilika kila idara na chenye kila kitu.hakiwezi kukwama kwa chochote kwa sababu ya chochote ka vilivyo vyama kama CHADEMA ambavyo kupata mafuta tu ya helikopta inakuwa ni mgogoro wa kukata na shoka.
 
 
Kibaraka asiyelipwa.
Wenzie wako mezani wanakula yeye Yuko chini ya meza anasubiri mifupa.
Mimi sifanyi kazi kwa ajili ya malipo na sipo CCM kwa ajili ya kulipwa.nipo CCM kwa sababu ni chama kinachojali na chenye uchungu na maisha ya watu na chenye itikadi inayoeleweka na yenye kugusa maisha ya watanzania. Sasa mavyama kama CHADEMA hayawezi hata kuandaa ilani yake. Rejea 2015.
 
Back
Top Bottom