Hajaachia nyumba ya serikali.Ati unasemaje?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hajaachia nyumba ya serikali.Ati unasemaje?
Kweli pepo ni hapahapa na moto ni hapahapa
Hata kuandika hujui!Yaani mnaoteseka ni nyie..! Hakuna kazi ngumu kama kukaa unategemea litamkuta lini usiyempenda..! Mara pah...Barozi🤣🤣 usifute huu uzi
Ndio tunachotegemea yaani !! ili iwe fundisho kwa wengineMalipo ni hapa hapa duniani, mnaweza shangaa akafungwa chap chap asipoweza lipa hiyo gari.
Maisha hubadirika au sioAliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na William Malecela maarufu Lemutuz wamefunguliwa kesi mahakamani kwa tuhuma za uporaji wa gari aina ya Range Rover.
Makonda na Lemutuz wamefunguliwa kesi hiyo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na mfanyabiashara Patrick Christopher Kamwelwe ambaye katika madai yake anataka alipwe fidia ya zaidi ya TZS milioni 240 ambazo ni gharama za kodi na thamani ya gari hilo.
Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, Wakili wa mfanyabiashara huyo, Kung’e Wabeya amesema tayari mahakama hiyo imetoa taarifa kwa wadaiwa kuhusu kesi hiyo na kuwataka wawasilishe mahakamani utetezi wao wa maandishi ndani ya siku 21 tangu kupokea taarifa hiyo.
Ameongeza kuwa endapo wadaiwa watashindwa kuwasilisha mahakamani utetezi wao ndani ya muda huo, mahakama itaweza kutoa hukumu dhidi yao.
Wabeya amesema kesi hiyo ya madai namba 234 ya mwaka 2022 imepangwa kutajwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Oktoba 13, 2022 saa 7 mchana.
View attachment 2379487
Ni kweliMaisha hubadirika au sio
😆😆😆😆DAB ni mwizi, mporaji wa mali za watu. Akishirikiana na mwenda zake wamesababisha makovu makubwa sana kwa watu wengi. Nawashangaa mnaosema eti huyu anafaa kuwa Rais ajaye.
KweliDAB ni mwizi, mporaji wa mali za watu. Akishirikiana na mwenda zake wamesababisha makovu makubwa sana kwa watu wengi. Nawashangaa mnaosema eti huyu anafaa kuwa Rais ajaye.