Watu wa TISS ni kwanini mnashindwa kumwamba Boss wenu Rais Samia kuwa huyu mtu Paul Makonda hafai na kama anampenda sana basi amtupe tu huko Ubalozini akapumzike? Nimeangalia Video Clip yake akiwa anajitambulisha huko Mkoani Arusha alikotupwa baada ya Kufeli katika Uenezi nikagundua kuwa Kisaikolojia ana tatizo Kubwa mno la Kiakili na huenda Yeye hajijui na hata Wanamzunguka nao hawajui.
Makonda hakuna Mkoa ambao unatakiwa uwe nao makini na uende nao kwa Step kama huo wa Arusha ulipo. GENTAMYCINE pamoja na Usela Nnya wangu wote, Ujanja na Ubabe wa Kimusoma (Mkoani Mara Kwetu) nikienda huko huwa nakuwa Mpole hutoamini kwani nimeishi huo Mkoa, naujua na Watu wa huko Kiasili huwa HAWABIPIWI na UKIWABIPU tu haraka sana wanakupigia.
Ukiwa Mwenezi nilikuambia na Uzi upo kuwa hutodumu hapo hata ndani ya Miezi Sita na kama Kawaida yao au Kawaida yenu baadhi ya watu hapa JamiiForums yakanipuuza GENTAMYCINE lakini kile kile nilichokitabiri juu ya Paul Makonda kimetokea.
Haya Makonda na leo tena nakwambia kuwa hata huko Arusha ulikopelekwa ni Kimkakat zaidi ili Watu wamalize Shughuli mapema kwani tayari umeshaonekana ni tatizo halafu umeshajulikana kuwa kuna Mtu huwa unajifanya Kumpenda mbele za Mic za Media ila ukikaa Vijiweni Kwako na Washkaji pale Mbezi Beach na Masaki huwa Unamkashifu na Unamdharau hakuna mfano na ukimsifia Baba yako wa Hiari aliyemaliza safari yake 2021.