Picha: Dar es Salaam waonesha uhalisia suala la bandari nchini. Viongozi wajitafakari sana

Picha: Dar es Salaam waonesha uhalisia suala la bandari nchini. Viongozi wajitafakari sana

Suala hapa siyo anko ako...
Suala ni mkataba....unasemaje?

Mbona mnakuwa wagumu kuelewa??

Hakuna anayetilia shaka uwezo wa DP, inawezekana ndiyo kampuni kubwa kabisa Duniani kwenye masuala ya bandari kwa sasa kama siyo ya pili...

Ila Watu wanachohoji ni mkataba...kwahiyo mnapojibu hoja jibuni suala la mkataba na siyo uwezo binafsi wa DP..
Jamami mbona mkataba wa uendeshaji bandari bado?

Hivi ni kipi hamuelewi?
 
Bandarini pale ni wizi mtupu. Usione watu wanapinga ujio wa DP world ukafikiri ni wazalendo. Ukweli ni kwamba wanaopinga mkataba wengi ni wale wezi wa bandarini, wapitisha madawa ya kulevya na vishoka.
Nakwambia, hii rasharasha tu, hata kazi za DP-WORLD hazijaanza rasmi, vitu vya "polomosheni" siku hizi havionekani mitaani kwetu.
 
Wakazi wa Dar na viunga vyake tunazijuwa dursa zitazozalishwa na bandari ya kisasa.

Hao DP WORLD wengine hapa tunawangoja kwa hamu. Tuna vijukuu vyetu tunataka violewe Dubai.

Fursa hizo.
Fursa nyingi zinakuja, but watakaoziona ni wachache ambao akili zao bado hazija athiriwa na wanasiasa uchwara.
 
Saa 8 hii bado upo kitandani unaota. Tatizo la ndoto unaweza kuota kuwa wewe ni tajiri namba 1 duniani, lkn ukija kushtuka unakuta mfukoni huna hata 200 ya kununua muhogo wa kula.
Hahaha, mjukuu wangu siku moja kanizushia ugomvi alipoamka. Anasema kapewa minoti na mama'ke imejaa mifuko yote, nimrudishie.

Nimelipa deni wiki nzima, kila siku buku.
 
Wewe umeolewa?

Kama bado hujaolewa nakushauri itumie fursa, tafuta jihandsome la Kiarabu lenye Dirham zake uolewe Dubai.

Usiziwachie fursa za DP World.

Ngino nje ya ndoa usiisogelee kabisa. Haramu.

Unamshauri akachanganye damu na wauzao wa Mtume SAW? Yuko mmoja alimshauri mkewe. Bahati mbaya mama akashindwa kutofautisha Banyiani na wale wa uzao wa Mtume. Jamaa akaishia kumuuliza mkewe mbona mtoto ananywele za singa. Akajibiwa kitanda hakizai haramu.
 
Habari zenu wana JF na wazalendo wenzangu wote mliopo humu kwa ujumla,

Ndugu zangu wana JF, hapa nchini au duniani tunapozungumzia Mkoa wa Dar es Salaam basi ni ukweli ulio wazi kwamba ni kama vile tunakuwa tumeizungumzia Tanzania nzima. Nasema hivi kwa sababu kuu mbili.

1. Dar es Salaam ndio iliyobeba taaswira halisi ya nchi, ndio maana mkoa huu uliongoza mapambano yote ya kudai uhuru, na mambo mengine mengi ya kiserikali na kijamii yalifanyikia Dar es Salaam, kabla na baada ya uhuru.

2. Dar es Salaam ndio Mkoa uliokusanya makabila yote kutoka mikoa na maeneo mbali mbali ya nchi (kabila langu likiwa moja wapo wa wahamiaji wa Mkoa huu). Hivyo kila linalofanyika mkoa huu linakuwa limegusa kwa kiwango kikubwa mikoa mingine na watu wake kwa ujumla.

Sasa ukiona kiongozi au mtu maarufu anakataliwa katika mkoa wa Dar es Salaam, basi anatakiwa ajitafakari vizuri, kuliko kukimbilia kuwapa vijana vijihela na data za kuja mitandaoni kumsafisha na kutunga propaganda mbalimbali, sababu kuna uwezekano mkubwa wa kukataliwa nchi nzima.

Mwaka 2020 katika kampeni za uchaguzi mkuu, kuna chama kilimsimamisha mgombea kutoka ulaya, kwa kufikiri labda wana Dar es Salaam na watanzania kwa ujumla watadanganyika, watetemeke na kumpa kura mgombea huyo. Lakini kumbe hali ikawa tofauti kwa kuanza kupuuzwa na wana Dar es Salaam na watanzania kwa ujumla, hivyo kupelekea mgombea huyo kutoka ulaya kuangukia pua katika uchaguzi ule.

Na yeye kwa aibu siku mbili tatu baada ya uchaguzi akakimbilia ulaya kwa kudanganya umma kuwa anasakwa na serikali ili iwe rahisi yeye kupewa hifadhi ya ukimbizi na pia kujitoa katika kashfa ya aibu ya kushindwa uchaguzi.

Watu wenye akili tulijiuliza, kama kweli alitakiwa kuuwawa, kwanini asingeliuwawa wakati wa kampeni, badala yake aje auwawe baada ya uchaguzi, tena uchaguzi ambao yeye ndo ameshindwa!

Hilo likapita, sasa likaja hili la bandari chama hicho kilichoangukia pua Dar katika uchaguzi mkuu, kikalivalia njuga na swala hili wakiamini kuwa lingewabeba katika mkoa huo wenye mamilioni ya watu.

Cha kushangaza, pamoja na kualika viongozi njaa wa dini, wanasheria uchwara na wanasiasa wachumia tumbo kutoka maeneo mbali mbali ya nchi lakini bado wana Dar es Salaam wakaendelea kukiadhibu chama hicho na genge lake bila huruma.

Ndio maana nashauri viongozi wa chama hicho wajitafakari upya kuhusu kuelekeo wao. Kuruhusu wapitisha madawa ya kulevya, wezi, wakwepa kodi na ushuru wa bandari wawatumie katika ajenda zao kwa sababu ya malipo madogo tu yanayoliwa na viongozi wachache wa chama lilikuwa ni kosa la kiufundi.

Pia hii style ya kusambaza vijana wenye ID kumi kumi mitandaoni, kwani katika mkutano huonekana watu na sio wingi wa ID zao. Mfano humu tulitangaziwa mkutano wa bandari pale temeke, masham masham mitandaoni yakawa mengi, lakini siku ilipofika watu hawakujitokeza kama ilivyodhaniwa.

Hii ni dalili kuwa hii pinga pinga ya bandari ni ya mitandaoni tu lakini mitaani na nchini hakuna anaepinga.

View attachment 2699597
Acha unaa na fitina chawa wa🍀. watanzania ni waelewa na waungwana.Ila usisahau ahadi yenu feki,Kuwa fitina kwenu mwiko,na pia mnasema rushwa ni adui wa haki,isije Kuwa mengi ya mitazamo yako inaongozwa kwa nguvu ya mlungulatu,ili kuwaandama wazalendo wa kweli,na kuwaomba mafisadi🤔
 
Mpaka mtumie makalio kuongea ndio mtaeleweka kwa sasa tunasema bandari haiuzwi
 
Unamshauri akachanganye damu na wauzao wa Mtume SAW? Yuko mmoja alimshauri mkwewe. Bahati mbaya mama akashindwa kutofautisha Banyiani na wale wa uzao wa Mtume. Jamaa akaishia kumuuliza mkewe mbona mtoto ananywele za singa. Akajibiwa kitanda hakizai haramu.
Kitanda toka lini k8kazaa? Anaezaa anaelalia kitanda.

Huyo afanye toba, uzinzi ni haramu.
 
Ni kama unachanganyikiwa!! Pole
Nichanganyikiwe kwa lipi?

Kwa hili la wana Dar es Salaam kushtuka na kukataa kutumiwa na wanasiasa uchwara kwenye ajenda zao na kupelekea mkutano wa bandari kudoda?

Au kwa hili la watu kutumia ID kumi kumi mitandaoni ili kuwahadaa wasiojua kinachoendelea afu mikutanoni wanahudhuria watu wawili watatu?
 
Aheri hata papai lina faida, unaweza kulila.

Uwe na majitu yenye upungufu wa akili kama mleta mda halafu utegemee maendeleo! Laana kubwa ya nchi yetu ni aina ya watu ilio nao.
Siku zote chizi (mtu asiekuwa na akili) humuona mzima kuwa ndio chizi. So sishangai wewe kuniona mimi sina akili, ilihali kiuhalisia wazima tunajua kuwa wewe ndio huna akili.
 
Habari zenu wana JF na wazalendo wenzangu wote mliopo humu kwa ujumla,

Ndugu zangu wana JF, hapa nchini au duniani tunapozungumzia Mkoa wa Dar es Salaam basi ni ukweli ulio wazi kwamba ni kama vile tunakuwa tumeizungumzia Tanzania nzima. Nasema hivi kwa sababu kuu mbili.

1. Dar es Salaam ndio iliyobeba taaswira halisi ya nchi, ndio maana mkoa huu uliongoza mapambano yote ya kudai uhuru, na mambo mengine mengi ya kiserikali na kijamii yalifanyikia Dar es Salaam, kabla na baada ya uhuru.

2. Dar es Salaam ndio Mkoa uliokusanya makabila yote kutoka mikoa na maeneo mbali mbali ya nchi (kabila langu likiwa moja wapo wa wahamiaji wa Mkoa huu). Hivyo kila linalofanyika mkoa huu linakuwa limegusa kwa kiwango kikubwa mikoa mingine na watu wake kwa ujumla.

Sasa ukiona kiongozi au mtu maarufu anakataliwa katika mkoa wa Dar es Salaam, basi anatakiwa ajitafakari vizuri, kuliko kukimbilia kuwapa vijana vijihela na data za kuja mitandaoni kumsafisha na kutunga propaganda mbalimbali, sababu kuna uwezekano mkubwa wa kukataliwa nchi nzima.

Mwaka 2020 katika kampeni za uchaguzi mkuu, kuna chama kilimsimamisha mgombea kutoka ulaya, kwa kufikiri labda wana Dar es Salaam na watanzania kwa ujumla watadanganyika, watetemeke na kumpa kura mgombea huyo. Lakini kumbe hali ikawa tofauti kwa kuanza kupuuzwa na wana Dar es Salaam na watanzania kwa ujumla, hivyo kupelekea mgombea huyo kutoka ulaya kuangukia pua katika uchaguzi ule.

Na yeye kwa aibu siku mbili tatu baada ya uchaguzi akakimbilia ulaya kwa kudanganya umma kuwa anasakwa na serikali ili iwe rahisi yeye kupewa hifadhi ya ukimbizi na pia kujitoa katika kashfa ya aibu ya kushindwa uchaguzi.

Watu wenye akili tulijiuliza, kama kweli alitakiwa kuuwawa, kwanini asingeliuwawa wakati wa kampeni, badala yake aje auwawe baada ya uchaguzi, tena uchaguzi ambao yeye ndo ameshindwa!

Hilo likapita, sasa likaja hili la bandari chama hicho kilichoangukia pua Dar katika uchaguzi mkuu, kikalivalia njuga na swala hili wakiamini kuwa lingewabeba katika mkoa huo wenye mamilioni ya watu.

Cha kushangaza, pamoja na kualika viongozi njaa wa dini, wanasheria uchwara na wanasiasa wachumia tumbo kutoka maeneo mbali mbali ya nchi lakini bado wana Dar es Salaam wakaendelea kukiadhibu chama hicho na genge lake bila huruma.

Ndio maana nashauri viongozi wa chama hicho wajitafakari upya kuhusu kuelekeo wao. Kuruhusu wapitisha madawa ya kulevya, wezi, wakwepa kodi na ushuru wa bandari wawatumie katika ajenda zao kwa sababu ya malipo madogo tu yanayoliwa na viongozi wachache wa chama lilikuwa ni kosa la kiufundi.

Pia hii style ya kusambaza vijana wenye ID kumi kumi mitandaoni, kwani katika mkutano huonekana watu na sio wingi wa ID zao. Mfano humu tulitangaziwa mkutano wa bandari pale temeke, masham masham mitandaoni yakawa mengi, lakini siku ilipofika watu hawakujitokeza kama ilivyodhaniwa.

Hii ni dalili kuwa hii pinga pinga ya bandari ni ya mitandaoni tu lakini mitaani na nchini hakuna anaepinga.

View attachment 2699597
Wewe waonyesha ni msomi wa hali ya juu.Unatuelezea,na kukuelewa ki urahisi sana.Mengi ilikuwa siyajui,lakini nimeyajua kupitia uzi huu wako.
 
Wadau wenyewe wa bandari wanasubiri muwekezaji aanze kazi waanze kufaidi matunda.

Ni Tanzania tu nchi ambayo uagizaji wa bidhaa na uuzaji nje ya nchi unasumbuliwa na urasimu mwingi, sehemu nyingine zote hakuna kupotezeana muda kwa maana ya meli kusubiri pale nje kwa wiki nzima.

Mdau halisi wa bandari hana muda wa kumpinga DP World, wengi wa hawa wanaotumia ID kumi ni vibaraka tu wanaolipwa na mafisadi wa bandari wanaosababisha foleni na wizi pale TPA.
Huu ndio ukweli.Endeleeni kutuelimisha wananchi wa kawaida.
 
Kuna anko wangu alileta mzigo kutoka China figisu figisu alizokutana nazo pale bandarini bado nusu auziwe mbuzi kwenye gunia kwa kubadilishiwa mzigo.

Bahati nzuri anko nae mkorofi ileile ivyo jamaa wakanywea. Imagine kama angekuwa ni mtu kutoka Zambia au Rwanda hali ingekuaje
Ni kweli kabisa.
 
Suala hapa siyo anko ako...
Suala ni mkataba....unasemaje?

Mbona mnakuwa wagumu kuelewa??

Hakuna anayetilia shaka uwezo wa DP, inawezekana ndiyo kampuni kubwa kabisa Duniani kwenye masuala ya bandari kwa sasa kama siyo ya pili...

Ila Watu wanachohoji ni mkataba...kwahiyo mnapojibu hoja jibuni suala la mkataba na siyo uwezo binafsi wa DP..
Sasa wewe shuleni unawezaje kujibu swali ambalo haulioni?

Wanaokudanganya kuhusu mapungufu ya mkataba huwa hawakuwekei mkataba wenyewe uuone na kuona mapungufu. Badala yake huishia kukwambia tu porojo kwamba sijui bandari imeuzwa, sijui mkataba mbovu nk bila kuonesha kifungu kinachoonesha mauziano ya bandari wala ubovu wa mkataba.

Na wanafanya hivyo makusudi kwa sababu wana amini bado kuna baadhi ya watanzania ni wajinga, namaanisha wale wanaoamini chochote wanachoambiwa hata kama hakina ushahidi.

Weka mkataba hapa uoneshe mapungufu kifungu kwa kifungu na wajuzi wakujibu kifungu kwa kifungu.
 
Fursa nyingi zinakuja, but watakaoziona ni wachache ambao akili zao bado hazija athiriwa na wanasiasa uchwara.
Kuna mtu amenambia DP World wakishaanza kazi wataleta vichwa vya trucks (tractor) 300 na trailers 1,000 na kuwako pesha transporters wadogo wadogo bila riba ili mizigo yao ifike kwa wateja wao kwa wakati.

Hii ni fursa kubwa sana.
 
Back
Top Bottom