Pigo la mwisho kwa Thadei Ole Mushi: Katoliki wakataa kumzika kwa kuwa aliwapinga TEC kuhusu DPW

Pigo la mwisho kwa Thadei Ole Mushi: Katoliki wakataa kumzika kwa kuwa aliwapinga TEC kuhusu DPW

Kwani kutoendesha ibada ya mazishi ndio kuhukumu? Kuna kitu hamuelewi hapa. Kanisa Katoliki hutoa huduma za kiroho kwa Wakatoliki tu. Kwa mujibu wa taratibu za kiroho, Ole Mushi hakuwa Mkatoliki
Kwakua alipinga walaka?
 
Kuwepo kwa habari hii ni dalili tosha kuwa marehemu amepungukiwa. Angekuwa hajapingukiwa, isingekuwa habari
Aliepungukiwa ni kanisa kwa kumpiteza kondoo wake wala marehemu hana haja nao. Imeandikwa, mchunga kondoo mwenye kundoo kumi, akimpoteza mmoja, ataawacha wale tisa na kumtafuta yule aliepotea mpaka ampate. Akipatikana atamkumbatia na kumrejesha kundini na wenzie.

Soma maandiko tajiri. Achana na utapeli wa ukatoliki wa kisasa.
 
Hii article imeandikwa kichochezi.Wengi walipinga ule waraka lkn hii haujawahi kuwa sababu ya wao kutengwa na kabisa.Kanisa Katoliki ni tooo liberal na linaamini katika hoja ndo maana waamini wake wako huru kuchangua aina ya maisha wayatakayo.

Ni kweli Kanisa halishiriki mazishi ya mtu ambaye alikua hashiriki katika mambo ya kanisa ikiwemo kuhudhuria Ibada. Hii ni sahihi kabisa.Mtu ana Uhuru wa kuchagua aishije na akifa tutatumia aina ya maisha yake kuamua alitaka azikweje (Mode of life test). Aliamua kutoshiriki na kanisa hence sio busara kumpeleka kanisani wakati kafa mtakua mmemtemdea marehemu kinyume na matakwa yake.
Ni kweli mkuu kanisa Katoliki hailimtengi mtu ila halilazimishi mtu kulifuata. Kama alijitenga akiwa hai, kwa nini kanisa limlazimishe akiwa ameshakufa na bila kujua sababu ya yeye kujitenga huko.

Suala la Waraka inaweza isiwe sababu ila maisha yake ya ukatoliki, ndoa n.k hatuyajui yanaweza kuwa ni sababu pia.

Wapo wengi mfano bilionea Mrema wa Arusha (Ngurudoto na Nauru Spring) nae hakupata ibada ya mazishi ya kanisa Katoliki. Nyie mnaosema haina umuhimu wowote kwa nini mnalalamika na kuleta uzi?

Ile ni Ibada/ Misa ya kuonesha ushindi katika kuiishi imani katoliki (Ukristo) katika maisha yako hapa duniani. Kwamba "Nimevipiga vita vilivyo vizuri mwendo nimeumaliza na Imani nimeilinda."
 
Kanisa Katoliki lagoma kuendesha Ibada ya misa ya mazishi ya Thadei Ole Mushi kwa sababu ALIPINGA WARAKA WA BARAZA LA MAASKOFU WA KANISA KATOLIKI TANZANIA (TEC) Uliopinga uuzwaji wa Bandari, uliotolewa tarehe 18 August 2023 na TEC.

Thadei Ole Mushi alipinga hadharani waraka wa TEC, kupitia andiko lake la tarehe 18 August 2023 lenye kichwa cha Habari "WARAKA WA MAASKOFU SIO ITHIBATI ZA MAONI YA WATANZANIA"

Juzi ndugu na msemaji wa familia Bwana Victor Tesha, alitangazia dunia kwamba ibada ya mazishi ya kumuaga ndugu yetu Thadei Ole Mushi kwa Dar es Salaam ingefanyika katika kanisa la St. Peter - Oysterbay.

Lakini watu wengi ikiwemo mimi tulipofika kanisa la St. Peter's Oysterbay, tulikuta milango ya kanisa imefunga na hakuna dalili ya kuwepo kwa misa yoyote.

Uamuzi wa haraka kutaarifu watu waelekee Muhimbili katika kanisa la Pamoja (siyo Katoliki) ukafanyika na pakaendeshwa ibada na mapadre ambao ni marafiki wa karibu wa Thadei Ole Mushi na siyo Paroko anayehusika katika parokia yake ya Muhimbili.

Leo familia imekwaa tena kisiki kingine Mkoani Kilimanjaro, Uru nyumbani kwa Thedei Ole Mushi baada ya Parokia ya Uru nyumbani kwa marehemu kugomea kuendesha mazishi na kufunga milango kiasi cha kupelekea kutafutwa kwa wachungaji wa madhehebu ya Kipentekoste pale Uru.

Baadae ibada ikaendeshwa na kasisi akiwa amevaa t-shirt nyeusi na sio mavazi halisi ya ibada kwa mujibu wa taratibu. Na wala hakukuwa na kwaya ya Kanisa.

Wajuzi na wasomi wa kanisa Katoliki wanasema ukipinga Waraka wa Maaskofu ni sawa na kuasi kanisa kwa kukataa mafundisho yake, hivyo kama utafariki kabla ya kurudishwa kundini utakuwa umefariki kama muasi nje ya kanisa na hivyo kanisa halitohusika na mazishi yako.

Hili ni Somo kubwa na funzo kwa wanasiasa na watu wote ambao tulikuwa hatujui uzito na maana ya waraka wa baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) ambao hutolewa na kusomwa makanisa yote ya waumini wao.

Kama na wewe ni muuumini wa kanisa katoliki na unajua uliropoka na kupinga lolote kuhusu waraka ule wa TEC fanya haraka urudishwe kundini.

VIJANA🙄
Kanisa katoliki ni ovyo mnooo
 
Hapa ndio dini yangu huwa inanichosha kabisa!

Hata wakatae kumsalia, what difference does it make to a dead man?🧟‍♂️ AbsoFREAKINGlutely NONE!!!!
Sio siri mimi nimebakia kuwa Mkatoliki kwa ajili wa watoto tu ila kiuhalisia hili dhehebu sio kabisa
 
Hapa ndio dini yangu huwa inanichosha kabisa!

Hata wakatae kumsalia, what difference does it make to a dead man?[emoji3446] AbsoFREAKINGlutely NONE!!!!
Ulichokiona ndio difference yenyewe.
Huwezi kupinga ule waraka ambao umenyooka vile na umejikita kwenye mapugufu ya mkataba wa kibwege kabisa achilia mbali kwamba waliotoa ni jopo la viongozi wako wa kiroho alafu watu wakuchekee...
Bandari ni future ya Watanzania wote na vizazi viijavyo.
Thadei alikosea sana simuhukumu ila atapambana na Muumba wake.
Usaliti, Roho mbaya ..Ubinafsi ndio umeleta haya yote.
Waliokula hela ya Dp wanajijua.
Nasimama na Viongozi wangu wa kiroho always...siwezi kusimama kamwe na wanasiasa uchwara na wezi NEVER.
 
Aliepungukiwa ni kanisa kwa kumpiteza kondoo wake wala marehemu hana haja nao. Imeandikwa, mchunga kondoo mwenye kundoo kumi, akimpoteza mmoja, ataawacha wale tisa na kumtafuta yule aliepotea mpaka ampate. Akipatikana atamkumbatia na kumrejesha kundini na wenzie.

Soma maandiko tajiri. Achana na utapeli wa ukatoliki wa kisasa.
Sasa kama marehemu hana hoja na Kanisa, malalamiko yaliyomo kwenye uzi huu yanahusu nini? Au ni kiherehere cha watu kujidai kumtetea marehemu wakati yeye hana hoja na Kanisa? Tangu lini ukaona Kanisa Katoliki likashughulika na kondoo aliyeamua mwenyewe kwa akili zake timamu kujipoteza?
 
Kanisa Katoliki lagoma kuendesha Ibada ya misa ya mazishi ya Thadei Ole Mushi kwa sababu ALIPINGA WARAKA WA BARAZA LA MAASKOFU WA KANISA KATOLIKI TANZANIA (TEC) Uliopinga uuzwaji wa Bandari, uliotolewa tarehe 18 August 2023 na TEC.

Thadei Ole Mushi alipinga hadharani waraka wa TEC, kupitia andiko lake la tarehe 18 August 2023 lenye kichwa cha Habari "WARAKA WA MAASKOFU SIO ITHIBATI ZA MAONI YA WATANZANIA"

Juzi ndugu na msemaji wa familia Bwana Victor Tesha, alitangazia dunia kwamba ibada ya mazishi ya kumuaga ndugu yetu Thadei Ole Mushi kwa Dar es Salaam ingefanyika katika kanisa la St. Peter - Oysterbay.

Lakini watu wengi ikiwemo mimi tulipofika kanisa la St. Peter's Oysterbay, tulikuta milango ya kanisa imefunga na hakuna dalili ya kuwepo kwa misa yoyote.

Uamuzi wa haraka kutaarifu watu waelekee Muhimbili katika kanisa la Pamoja (siyo Katoliki) ukafanyika na pakaendeshwa ibada na mapadre ambao ni marafiki wa karibu wa Thadei Ole Mushi na siyo Paroko anayehusika katika parokia yake ya Muhimbili.

Leo familia imekwaa tena kisiki kingine Mkoani Kilimanjaro, Uru nyumbani kwa Thedei Ole Mushi baada ya Parokia ya Uru nyumbani kwa marehemu kugomea kuendesha mazishi na kufunga milango kiasi cha kupelekea kutafutwa kwa wachungaji wa madhehebu ya Kipentekoste pale Uru.

Baadae ibada ikaendeshwa na kasisi akiwa amevaa t-shirt nyeusi na sio mavazi halisi ya ibada kwa mujibu wa taratibu. Na wala hakukuwa na kwaya ya Kanisa.

Wajuzi na wasomi wa kanisa Katoliki wanasema ukipinga Waraka wa Maaskofu ni sawa na kuasi kanisa kwa kukataa mafundisho yake, hivyo kama utafariki kabla ya kurudishwa kundini utakuwa umefariki kama muasi nje ya kanisa na hivyo kanisa halitohusika na mazishi yako.

Hili ni Somo kubwa na funzo kwa wanasiasa na watu wote ambao tulikuwa hatujui uzito na maana ya waraka wa baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) ambao hutolewa na kusomwa makanisa yote ya waumini wao.

Kama na wewe ni muuumini wa kanisa katoliki na unajua uliropoka na kupinga lolote kuhusu waraka ule wa TEC fanya haraka urudishwe kundini.

VIJANA🙄
Kama ni kweli basi kanisa limepotoka kwani wao ni mungu!
 
Kwani wao ndo wenye uamuzi wa nani aingie mbinguni au hapana. Wanaona jamaa mchochezi kama TL alivyokuwa anasakamwa? Waache utoto
Kwani unaombewa ili uingie mbinguni. Hizo taratibu zimeshawekwa. Ukikosea, utahukumiwa kidunia, hata kama umekufa, ili liwe fundisho kwa walio hai.
 
Kanisa Katoliki lagoma kuendesha Ibada ya misa ya mazishi ya Thadei Ole Mushi kwa sababu ALIPINGA WARAKA WA BARAZA LA MAASKOFU WA KANISA KATOLIKI TANZANIA (TEC) Uliopinga uuzwaji wa Bandari, uliotolewa tarehe 18 August 2023 na TEC.

Thadei Ole Mushi alipinga hadharani waraka wa TEC, kupitia andiko lake la tarehe 18 August 2023 lenye kichwa cha Habari "WARAKA WA MAASKOFU SIO ITHIBATI ZA MAONI YA WATANZANIA"

Juzi ndugu na msemaji wa familia Bwana Victor Tesha, alitangazia dunia kwamba ibada ya mazishi ya kumuaga ndugu yetu Thadei Ole Mushi kwa Dar es Salaam ingefanyika katika kanisa la St. Peter - Oysterbay.

Lakini watu wengi ikiwemo mimi tulipofika kanisa la St. Peter's Oysterbay, tulikuta milango ya kanisa imefunga na hakuna dalili ya kuwepo kwa misa yoyote.

Uamuzi wa haraka kutaarifu watu waelekee Muhimbili katika kanisa la Pamoja (siyo Katoliki) ukafanyika na pakaendeshwa ibada na mapadre ambao ni marafiki wa karibu wa Thadei Ole Mushi na siyo Paroko anayehusika katika parokia yake ya Muhimbili.

Leo familia imekwaa tena kisiki kingine Mkoani Kilimanjaro, Uru nyumbani kwa Thedei Ole Mushi baada ya Parokia ya Uru nyumbani kwa marehemu kugomea kuendesha mazishi na kufunga milango kiasi cha kupelekea kutafutwa kwa wachungaji wa madhehebu ya Kipentekoste pale Uru.

Baadae ibada ikaendeshwa na kasisi akiwa amevaa t-shirt nyeusi na sio mavazi halisi ya ibada kwa mujibu wa taratibu. Na wala hakukuwa na kwaya ya Kanisa.

Wajuzi na wasomi wa kanisa Katoliki wanasema ukipinga Waraka wa Maaskofu ni sawa na kuasi kanisa kwa kukataa mafundisho yake, hivyo kama utafariki kabla ya kurudishwa kundini utakuwa umefariki kama muasi nje ya kanisa na hivyo kanisa halitohusika na mazishi yako.

Hili ni Somo kubwa na funzo kwa wanasiasa na watu wote ambao tulikuwa hatujui uzito na maana ya waraka wa baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) ambao hutolewa na kusomwa makanisa yote ya waumini wao.

Kama na wewe ni muuumini wa kanisa katoliki na unajua uliropoka na kupinga lolote kuhusu waraka ule wa TEC fanya haraka urudishwe kundini.

VIJANA🙄
Hakuwa na pesa. Kama anapesa maaskofu wangaligombea mwili kuuombea. Au nasema uongo wadau?
 
Kama ni kweli basi kanisa limepotoka kwani wao ni mungu!
Mnachanganya, nani kasema kanisa ni Mungu. Utaratibu lazima ufuatwe. Mlio hai ndio mjifunze. Kwani mtu akihukumiwa kuua, adhabu anapata yupi? Maiti, funzo kwa walio hai.
 
Duh aiseee wamezingua sana
Mkuu ni sahihi kabisa, watu ni wanafiki sana humu. Utakuta mtu anaanzisha uzi wa kupinga kushiriki jumuiya akidai zinawachangisha hela, halafu mtu huyo huyo anakuja kuanzisha uzi kuwa Kanisa linazingua kukataa kumzika marehemu. Sasa kama wewe unahitaji huduma, kwa nini ukiwa hai hautaki kushiriki na wenzako? Ukiamua kujitenga hutakiwi kuja kuomba huruma siku watakapokukana kuwa sio mwenzao. Yaani wakiwa wanakuhitaji unawakana, wewe ukiwa unawahitaji wakikukana iwe nongwa? Kimsingi unatakiwa kujua umejitenga mwenyewe, wala hujatengwa
 
Hakuwa na pesa. Kama anapesa maaskofu wangaligombea mwili kuuombea. Au nasema uongo wadau?
Kuna msiba uliokuwa na hela kama wa Ruge Mutahaba kwa siku za hivi karibuni? Muulize ndugu yake yeyote kama alizikwa kikatoliki. Ukiishi bila ndoa umejitenga na Kanisa, utazikwa na wahuni
 
Sasa kama marehemu hana hoja na Kanisa, malalamiko yaliyomo kwenye uzi huu yanahusu nini? Au ni kiherehere cha watu kujidai kumtetea marehemu wakati yeye hana hoja na Kanisa? Tangu lini ukaona Kanisa Katoliki likashughulika na kondoo aliyeamua mwenyewe kwa akili zake timamu kujipoteza?
Ni kweli, watu wanasema mara yeye maiti, wengine pigo la mwisho. Somo fuata taratibu za mifumo tuliyojiwekea, kokote kule. Kama hajui hata taratibu za kupinga kanisa, yamkini hakuwa anaenda kanisani kama mimi. Kuzika ni ibada, mbona kama sio ibada hakuna dhehebu linaenda mochwari kubeba miili isiyo na ndugu wakazike.
 
Back
Top Bottom