Polepole: Nilitegemea kuona kuna Mawaziri watajitokeza na kulaani ile kauli ya kula kwa urefu wa kamba

Polepole: Nilitegemea kuona kuna Mawaziri watajitokeza na kulaani ile kauli ya kula kwa urefu wa kamba

Polepole hata wewe ulikula kwa urefu wa kamba enzi zako...
 
AGAIN mkuu hii ni mada tunaijadili na hatuwezi wote tukawa na mawazo sawa,wewe umeona ni kosa kwa CDM kumchukua Mr.Lowasa kuwa presidential candidate wao ni kosa(ni absolute your right)mwingine ataona CDM waliamua kwa busara kumchukua Mr.Lowassa na wana facts zao,kuja kwa Mr.Lowassa CDM walifanikiwa kupata kura zaidi ya 6M za urais(hii ni rekodi hata Mr.Mrema hakuifikia),walipata wabunge wengi wa kuchaguliwa bungeni,na walifanikiwa kuchukua almost majiji yote hapa Tanzania,sasa why wewe uwanyoshee kidole kwa mafanikio yote haya!sometimes we need to relax kidogo ili kuonyesha demokrasia tuliyokua nayo humu..JF
Anachohoji huyu ndugu hapo kwamba Leo Polepole anaonekana mnafiki akikosoa kisa alikuwa hakosoi enzi za JPM. Jamaa anahoji Chadema walimtukana Lowasa nchi nzima kuwa fisadi papa enzi za JK hadi akajiuzulu Kwa makashfa kibao ambayo hakuna mtanzania asiye yajua lakini baadae Chadema hao hao tena chini ya mwenyekiti yule yule Mbowe wakamchukua kuwa mgombea wao wa urais na kumnadi majukwaani!! Je huu sio unafiki? Mbona Leo Mbowe akikosoa hasemwi vibaya kuwa ni mnafiki wakati hapo awali alishakula matapishi yake yeye mwenyewe na viongozi wenzeke wa Chadema?

Kwanini Polepole ahukumiwe kwa makosa yaliyopita hadi sasa anyimwe uhalali wa kukosoa?

Hayo mambo ya mafanikio tuyaache pembeni kwanza la sivyo unambie kuwa ni halali kutumia mafisadi kisa tu yanaleta faida Fulani.
 
Me siwezi kuiwaza chadema wakati ninamaisha yangu kauli yangu nikuonesha tuwache double standard PolePole katoa hoja mjibuni kwa hoja sio kufanya personal attack huo unafiki mnaosema anao mbona 99.9% wanasiasa pia ni wanafiki kuanzia wa chadema mpaka CCM
Comrade Punguza jazba
 
Unafikri kila mtu aliunga mkono ujio wa lile zee tapeli la siasa ndani ya CDM? Tafuta popote nilipounga mkono ujio wa Lowassa ndani ya CDM. Polepole anaongea ukweli sasa sio kwa mantiki ya ukweli, bali ni sehemu ya yeye kusaka kurudishwa kwenye ulaji.

Halafu ww kama wewe hujawahi kuwaunga mkono CDM, maana CDM tayari ina wapiga kura wa kutosha. Na isitoshe CDM haihitaji uungwaji wako mkono kwa lolote. Hiyo hoja vya polepole ipambanie ww maana akipata ulaji ww utafaidika.


Halafu we jamaa ni bogus sijapata kuona ingawa mwenyewe unajiona 'machinowa'

Kwamba haukukubaliana na ujio wa lowassa CDM ,lakini mpaka leo bado upo humo humo CDM na hao viongozi waliomleta lowassa bado wapo kama viongozi,na daily unawapigania humu,kwani hiko chama ni Baba/Mama yako? na hao viongozi wake wana 'uspesho' gani kwako mpaka kuwang'ang'ania hivyo?


Sasa kama unazo akili jiulize kwa nini ulipinga ujio wa lowassa CDM, ukishapata jibu jiulize tena kama akili zako zina akili (unaishi kwa principles au unaishi tu kama bendera?)
 
Yeye ameshavimbiwa atulie na wenye njaa nao wale zam yao
 
Anachohoji huyu ndugu hapo kwamba Leo Polepole anaonekana mnafiki akikosoa kisa alikuwa hakosoi enzi za JPM. Jamaa anahoji Chadema walimtukana Lowasa nchi nzima kuwa fisadi papa enzi za JK hadi akajiuzulu Kwa makashfa kibao ambayo hakuna mtanzania asiye yajua lakini baadae Chadema hao hao tena chini ya mwenyekiti yule yule Mbowe wakamchukua kuwa mgombea wao wa urais na kumnadi majukwaani!! Je huu sio unafiki? Mbona Leo Mbowe akikosoa hasemwi vibaya kuwa ni mnafiki wakati hapo awali alishakula matapishi yake yeye mwenyewe na viongozi wenzeke wa Chadema?

Kwanini Polepole ahukumiwe kwa makosa yaliyopita hadi sasa anyimwe uhalali wa kukosoa?

Hayo mambo ya mafanikio tuyaache pembeni kwanza la sivyo unambie kuwa ni halali kutumia mafisadi kisa tu yanaleta faida Fulani.
Bora umenisaidia maana kuna wengine wanavichwa vigumu
 
Halafu we jamaa ni bogus sijapata kuona ingawa mwenyewe unajiona 'machinowa'

Kwamba haukukubaliana na ujio wa lowassa CDM ,lakini mpaka leo bado upo humo humo CDM na hao viongozi waliomleta lowassa bado wapo kama viongozi,na daily unawapigania humu,kwani hiko chama ni Baba/Mama yako? na hao viongozi wake wana 'uspesho' gani kwako mpaka kuwang'ang'ania hivyo?


Sasa kama unazo akili jiulize kwa nini ulipinga ujio wa lowassa CDM, ukishapata jibu jiulize tena kama akili zako zina akili (unaishi kwa principles au unaishi tu kama bendera?)
Mwamba anaushabiki wa kisiasa unaosababisha ajitoe ufahamu
 
Tulimwambia hakusikia na sasa hayupo!!Uzi wa Tumiaakili huo kausome!! Pole pole anasema kama alivyoelekezwa kusema!! pole pole alikaa kimya hakuwa na la kufanya angefanya nini??ili na yeye afe??sio kila mtu Anaweza kufia wengine ila kusemea wengine!!!

Anavyoongea hivi sasa haogopi kufa? Kama alikalia kimya mambo maovu, leo hiyo kula usawa wa kamba yake ndio inamtisha?
 
Kuna kitu kimoja mkuu hujaelewa hapo hapingi kwasababu ya uwana harakati ila alicho nacho ni chuki na kumkomoa Kwa kupinga kila kitu anachosema ata kama ni cha kweli kwasababu tu alikuwepo awamu ya Tano.

NB. Punguza maneno makali tujadili na kutoa maoni yetu bila kuvunjiana heshima.

Kama hiyo awamu ya tano alipinga kila zuri lililo nje ya utashi wa mlo wake, mnatoa wapi nguvu ya kutaka sisi tuunge mkono hayo mnayoita mazuri sasa? Huyo Polepole hapigi kelele kwa ajili ya uzalendo, bali ni kukosa mlo. Akipewa mlo na kauli hiyo ikatolewa hawezi kujiuzulu. Nyinyi wenye upendo na yeye muungeni mkono, sisi wenye chuki na yeye kwasababu alikuwa kwenye awamu ya tano, msimamo wetu ndio huohuo. Hatuungi mkono muhuni yoyote no matter what.
 
Kama hiyo awamu ya tano alipinga kila zuri lililo nje ya utashi wa mlo wake, mnatoa wapi nguvu ya kutaka sisi tuunge mkono hayo mnayoita mazuri sasa? Huyo Polepole hapigi kelele kwa ajili ya uzalendo, bali ni kukosa mlo. Akipewa mlo na kauli hiyo ikatolewa hawezi kujiuzulu. Nyinyi wenye upendo na yeye muungeni mkono, sisi wenye chuki na yeye kwasababu alikuwa kwenye awamu ya tano, msimamo wetu ndio huohuo. Hatuungi mkono muhuni yoyote no matter what.
Hiki unachokisema hapa kinaondoa ukweli wa kauli ya Polepole ?

Kwema lakini mkuu!!?
 
Kama hiyo awamu ya tano alipinga kila zuri lililo nje ya utashi wa mlo wake, mnatoa wapi nguvu ya kutaka sisi tuunge mkono hayo mnayoita mazuri sasa? Huyo Polepole hapigi kelele kwa ajili ya uzalendo, bali ni kukosa mlo. Akipewa mlo na kauli hiyo ikatolewa hawezi kujiuzulu. Nyinyi wenye upendo na yeye muungeni mkono, sisi wenye chuki na yeye kwasababu alikuwa kwenye awamu ya tano, msimamo wetu ndio huohuo. Hatuungi mkono muhuni yoyote no matter what.
Kweli kabisa
 
Hiki unachokisema hapa kinaondoa ukweli wa kauli ya Polepole ?

Kwema lakini mkuu!!?

Sina tatizo na kauli ya Polepole kwani ni kauli inayosemwa mara zote na wapenda haki. Nina tatizo na Polepole kusema maneno hayo ili apate support ya kumfungulia njia ya kurejea kwenye mlo.

Mimi niko poa sana, nimerejea mjini toka shamba maana mvua imegoma. Nasikitika kuendelea kupoteza hela zangu kwa kuendelea na kilimo cha kutegemea biblia ili mvua inyeshe. Acha niendelee na biashara yangu wa kuwa wakala wa miamala ya fedha ya kampuni za simu na mabenki hapa mjini.
 
Halafu we jamaa ni bogus sijapata kuona ingawa mwenyewe unajiona 'machinowa'

Kwamba haukukubaliana na ujio wa lowassa CDM ,lakini mpaka leo bado upo humo humo CDM na hao viongozi waliomleta lowassa bado wapo kama viongozi,na daily unawapigania humu,kwani hiko chama ni Baba/Mama yako? na hao viongozi wake wana 'uspesho' gani kwako mpaka kuwang'ang'ania hivyo?


Sasa kama unazo akili jiulize kwa nini ulipinga ujio wa lowassa CDM, ukishapata jibu jiulize tena kama akili zako zina akili (unaishi kwa principles au unaishi tu kama bendera?)

Acha kupanick dogo. Nilipinga ujio wa Lowassa maana nilijua Lowassa ni take away, na ukweli unajua saa hii Lowassa yuko wapi. Viongozi waliomleta bado wako maana wamechaguliwa na wengi kwa kura halali, hata kama sikubaliani na kiongozi yoyote dunia hii kukaa madarakani zaidi ya miaka 10. Mimi nina imani na taasisi na sio mtu. Kama ingekuwa naamini katika mtu basi ningeondoka wakati wa ujio wa Lowassa. Una lingine kwa msaada zaidi?
 
View attachment 2100413
"Wapo watu wanakula urefu wa Kamba na wanavimbiwa, hivi hawa watu wana uhalali wa kutuambia sisi tuishi maisha ya uadilifu? na mimi nitakuwa nauliza na wewe unakula kwa urefu wa kamba? kama ndio basi usiongee na mimi". Polepole

"Mimi nilitegemea kuona kuna Mawaziri watajitokeza na kulaani ile kauli ya kula kwa urefu wa kamba kwamba kuna wenzetu wanakula kwa urefu wa kamba na kauli hii haikubaliki, mimi nilidhani watu watatoka, lakini wapi ni kwa sababu ni wanafiki" Polepole

Pia, soma: Thread 'Rais Samia: Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, lakini mbona mnakula sana mnavimbiwa? Si kweli kama hampati kwenye maeneo yenu. Jipimieni...' Rais Samia: Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, lakini mbona mnakula sana mnavimbiwa? Si kweli kama hampati kwenye maeneo yenu. Jipimieni...
Huyu mzee ni shetani kabisa
 
Back
Top Bottom