Polisi: Vijana wawili waliouawa Vingunguti, Dar ni Panyaroad

Polisi: Vijana wawili waliouawa Vingunguti, Dar ni Panyaroad

Ila polisi wamezingua.

1. "Walijeruhi watu wawili ambae ni Shommy maarufu Paka Pori na Beka."

2. "Miili miwili imetambuliwa kuwa ni Shommy na Beka ila wa tatu ambae ni Paka Pori hajatambuliwa"

Maelezo yanakinzana.

SItetei uhalifu ila kitengo cha mawasiliano cha polisi kiwe kina hariri habari zao ili kuondoka mkanganyiko na kuleta sintofahamu.
 
Nilileta uzi huku juzi kwa namna ambavyo jeshi letu linafanya kazi bila weledi, yaani watu wanamapanga nyie mnawapiga risasi.

Hii inauzi sana
Sana sana ndugu lakini kwa sababu wanajua wabongo wanashabikia wahalifu kuuawa basi wamekuja na story za panya white etc. Hao panya wangewasweka ndani woteee
 
Inasikitisha sana kwa watu wasiokuwa na watetezi bingo,tutaweka wakili haki zao waliodhulumiwa uhai wao,ukiangalia comment ni uthibitisho watu walivo na chuki kwa jamii ambayo sio yao.
Majitu hayana akili , awamu ya tano tulilia sana kuhusiana na matendo ya kishenzi ya utekaji , utesaji na mauaji ya kishenzi yaliyokuwa yanafanywa na jeshi la polisi na vibaka wa usalama wa taifa .
Leo hii utakuta ndio hao hao wanashabikia ushenzi kama huu
Hii nchi ina sheria na mahakama , hao hata kama waliua ,walipaswa kupelekwa katika mfumo wa sheria na sheria kuwashughulia na si kuwateka na kuenda kuwafanyia torture mbaya kama hiyo na kuwatoboa macho na kuwaua
Huu ni ushenzi
 
Ila polisi wamezingua.

1. "Walijeruhi watu wawili ambae ni Shommy maarufu Paka Pori na Beka."

2. "Miili miwili imetambuliwa kuwa ni Shommy na Beka ila wa tatu ambae ni Paka Pori hajatambuliwa"

Maelezo yanakinzana.

SItetei uhalifu ila kitengo cha mawasiliano cha polisi kiwe kina hariri habari zao ili kuondoka mkanganyiko na kuleta sintofahamu.
Si ujanja ujanja
 
Kwa hiyo polisi haiwezi kukamata mhalifu bila kuua? Yaani vijana sita wenye mapanga imekua tabu kukamata au hawataki mambo za mahakamani! Very sad kuambiwa tu fulani panya road just like that afu unakula chuma!
Ni mambo ya ovyo sana hii nchi yanafanyika
 
Kama ni panya road wamestahili walichokipata,mambo ya utawala bora yaishie huko huko
Na siku uingie mtaani uwe na bifu na mtu wakusaikizie wewe ni panya road then waende wakufanyie hicho walichofanya hao madogo ndio utaona utamu wake .
Taifa la wapumbavu , illiterates wasio na akili wala elimu .
Hivi mnajua maana ya nchi kuweka mifumo ya sheria na haki ?
 
Mtoto wako/ndugu yako akiwa mhalifu utakubali apigwe chuma? Au ushabiki maandazi.

Wahalifu washungulikiwe kwa mujibu wa sheria sio kuwajaza hao polisi kichwa waanze kuua watu hovyo! THIS IS NOT A POLICE STATE. Ni nchi ina sheria zake sema ujinga ujinga umetujaa wabongo
Kama hukai Dar Es Salaam una haki ya kusema hivyo. Ila mkazi yeyote wa Dar es salaam ambaye ameshakutana na kadhia ya hawa Panya road akisikia wamekula chuma roho yake inasuuzika.

Hawa Panya hamna kitu wanaelewa kichwani kwao hata wakikukuta na mama yako mzazi au mkeo wanaweza mshika makalio mbele yako hapo hapo sasa chaguo ni lako zingua ufe au utulie wafanye yao.

Na ukichagua kufa wala hawajali. Wana-kubless mapanga tu
 
Chapa shaba panya rodi wote.

Tatizo kubwa ni uaminifu wa hili jeshi letu, oparesheni kama hizi hutumiwa vibaya na hao polisi kwa kuua, kutesa au kukamata watesi wao binafsi kwa kisingizio kua ni panya rodi.
 
Na siku uingie mtaani uwe na bifu na mtu wakusaikizie wewe ni panya road then waende wakufanyie hicho walichofanya hao madogo ndio utaona utamu wake .
Taifa la wapumbavu , illiterates wasio na akili wala elimu .
Hivi mnajua maana ya nchi kuweka mifumo ya sheria na haki ?
Hakika ni ujinga ndo maana ukimuona polisi mkwepe sana hata ukigombana nae itatengenezwa hiyo story hutakaa uaamini
 
Wangekamatwa wakalime huko jela sio kuua hovyo. Hawa polisi wamepewa mamlaka ya kuua ndo maana wakikuta na vimilioni vyako unakula chuma utasikia tulikua tunamkamata akatuponyoka!
Mage dada yangu kama kweli polisi waligundua ni waovu naona pia wameuawa kistaarabu sana, nafikiri hujawahi kuona unyama wa hali ya juu wanaofanya hawa vibaka sio?

Basi yeyote ambaye aliwahi kukutwa na dhahama ya vibaka atakushangaa sana sana ,jamaa yangu mpaka leo haongei vizuri walitaka kumchinja bahati nzuri watu wakatokea wakiwa washaanza ,hao sio wa kwenda kulimishwa hawastahili kuishi.
 
Sio mtoto wangu tu, hata mzazi wangu kama ni muhalifu anapaswa kupigwa chuma. Wao wakija kukuibia wanatumia sheria ipi?? au unakaza fuvu tu madam??
Una uhakika gani hao vijana waliouawa ni panya road ?
Au unaandika usenge tu hapa kimhemuko bila kutumia akili ?
 
Kama hukai Dar Es Salaam una haki ya kusema hivyo. Ila mkazi yeyote wa Dar es salaam ambaye ameshakutana na kadhia ya hawa Panya road akisikia wamekula chuma roho yake inasuuzika.

Hawa Panya hamna kitu wanaelewa kichwani kwao hata wakikukuta na mama yako mzazi au mkeo wanaweza mshika makalio mbele yako hapo hapo sasa chaguo ni lako zingua ufe au utulie wafanye yao.

Na ukichagua kufa wala hawajali. Wana-kubless mapanga tu
Nakaa kimara labda sababu sipo vingunguti!
 
Mimi nafikiria kwa kutumia Ubongo, sifikirii kwa kutumia makalio kama ulivyo wewe.

Do you know the meaning of Administrative Laws and the Rule of Laws??? The Principle of Natural Justice?
Upo msingi wa Sheria unaosema kwamba "No one is to be Condemned Unheard."
Nimekuja kugundua watu wengi ni wajinga sana nchi hii
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha kuwapiga risasi zilizopelekea vifo vyao Vijana wawili Bakari Ismail (21) na Shomari Kacheuka maarufu Babuu (22) Wakazi wa Vingunguti Jijini Dar es salaam ambapo wamesema Vijana hao walikuwa Wahalifu (Panya Road) na kwamba mwenzao wa tatu bado mwili wake upo Amana Hospital na wenzao wengine wamekimbia.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Jumanne Muliro amesema “December 27,2023 lilipokea taarifa kutoka kwa Wananchi wanaochukia uhalifu meneo ya Vingunguti kuwa kuna kundi la Watu vijana akiwemo Panya White kama kiongozi wao wanajiandaa kukufanya matukio ya kihalifu maeneo ya Vingunguti ambapo ufuatiliaji ulianza na Polisi walipofika maeneo ya Vingunguti darajani majira ya saa 2:00 usiku waliwakuta Watu sita wakiwa na silaha za jadi (mapanga) wakiwa wamekusanyika”

“Polisi waliwataka wajisalimishe ili wakamatwe, kinyume chake wakataka kuwashambulia Polisi kwa mapanga, Polisi walijihami na kufyatua risasi hewani lakini mazingira yalivyozidi kuwa ya hatari zaidi Polisi walilazimika kuwajeruhi kwa risasi miguuni na hapo watatu miongoni mwao walifanikiwa kukamatwa huku wakiwa na mapanga matatu yaliyopatikana eneo hilo la tukio”

“Polisi waligundua baadaye kuwa waliokuwa wamejeruhiwa eneo hilo ni pamoja na Paka Pori maarufu Shommy ambaye baadae alijulikana kwa jina la Shomari Salehe Kucheuka na Beka aliyejulikana baadaye kama Bakari Athumani, waliokimbia ni Panya White na mwingine ambaye hajafahamika, hao waliokamatwa baada ya kujeruhiwa walipelekwa Hospitali ya Amana kwa matibabu lakini baada ya kufikishwa pale Madaktari walibaini kuwa tayari walikuwa wamepoteza maisha”

“Maiti mbili za Shomy na Beka tayari zimetambuliwa na Ndugu zao na maiti moja ya Paka Pori bado ipo Hospitali ya Amana haijatambuliwa na Ndugu na upelelezi wa tukio hili na matukio mengine ya eneo hilo unaendelea”.

Pia soma: Dar es Salaam: Vijana wawili wafariki mikononi mwa polisi

View attachment 2858621

©Millardayo
Mchuma janga hula na wa kwao.
 
Kwa kiasi Fulani, Kuna chembechembe Fulani za ukweli kwenye hii hoja yako. Kuna jamaa mmoja ana jina la utani (a.k.a) la "Mkata Umeme," nilipojaribu kuchimbua kiini cha huyo mtu kuitwa kwa jina hilo, nikagundua "mambo mazito sana" juu ya jina lake hili.
Mkata umeme ,mkata moto Ina maana jamaa jambaka muuaji🤔
 
Back
Top Bottom