Polisi wamenitrack niliokota simu, kesho natakiwa kituoni

Nenda kafungwe kabisa mbwa wewe,

Omba mhusika awe hai kama aliuawawa wewe ndo muuaji wake.

NARUDIA USITHUBUTU KUNUNUA SIMU MKONONI KWA MTU USIYEMJUA,

USITHUBUTU KUOKOTA SIMU NA KUANZA KUITUMIA AU KITU CHOCHOTE UKAANZA KUKITUMIA. IKITOKEA UMEKAMATWA NACHO NA MTU ALIYEIBIWA ALIUAWAWA AU KUSABABISHIWA MAJEREHA BASI WEWE NDO MUUAJI AU NDO MWIZI WAKE HIVYO UTAWAJIBIKA NA MAUAJI HAYO. NDIYO MAANA TUNASAJILI LAINI WANDKUJA MTAANI KWAKO WANAKUNYAKA VZR.
 
Mjinga wa mwshoi
 
Kwanza hakikisha una kadi ya Chama tawala.....haitakuokoa sana lakini itakupunguzia madhila ya kupotea.
HAKI ZAKO NA WAJIBU WA ASKARI HUO HAPO . NAKUTAKIA KAZI NJEMA YA UOKOTAJI. KUNA SHERIA ZA TCRA ZINAKATAZA UOKOTAJI. SITOKUTUMIA ILA ZIPO . MITANO KWA MAMA SAMIA
 
Tulishawapa onyo hayo mambo hamkusikia. Nenda kawape milioni 1 na simu wachukue wakuachie.
Wataitupa tena ili mjinga mwingine aingie King.
Hiyo ni michezo michafu ya polisi. Una bahati hujaambiwa mwenye simu kauwawa mngeuza mpaka nyumba ndo wakuache
 
Miaka 5 jela inakusubiri.

Hakuna mwivi anayeiba simu kisha akaidondosha. Umenunua mali ya wizi na sasa kimewaka
Teh teh teh 😃 😃 hatari kweli kweli
 
Na abadili line kabisa ikiwezekana manake lazima tu kesi imdondokee yeye
Kama alisajili line, jina wanalo tayari hata akibadli line, zima simu mazima, kama Maza ana kitambulisho cha Nida tumia kusajili line mpya....
 
Hebu angalieni ubinadamu ulipofikia! Jitu linaiba samaki wa watu, hujali boda katumwa au vipi kwamba itabidi afidie. Ulivyowala umeshiba mpaka leo?
 
Andaa hela ndefu ya kumlipa mwenye simu na kuhonga polisi. Ukizubaa unakula mvua kama Nyundo. Hizi simu za kuokota unaweza kuunganishwa na kesi ya mauaji unajiona. Kuna misala wanatafuta watu wa kuwaangushia.
Tahadhari usijidanganye kukimbia
 
Pole kwa huo msala, hapo watakufinya utaongea hadi vitu ambavyo hata wewe mwenyewe huvijui
 
Kwa mfano hao samaki wangekuwa wametiliwa sumu anapelekewa mtu.

Hapo Mungu kamlinda boda kawadondosha ,

Wewe umeokota ukala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…