Polisi Wapelekwe Shule. Hawana Mamlaka ya Kuzuia Mikutano ya Vyama vya Siasa.

Polisi Wapelekwe Shule. Hawana Mamlaka ya Kuzuia Mikutano ya Vyama vya Siasa.

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Kuna tatizo kubwa la weledi ndani ya Jeshi la Polisi.

POlisi wa nchi hii, bila shaka hawana weledi wa kutosha, na wala hawajishughulishi kujua sheria ili wafanye kazi zao kwa weledi. Lakini pia yawezekana wanajua sheria inataka nini ila kwa kiburi na kwa makusudi wanaamua kuikanyaga sheria kwa kuamini kuwa hakuna wa kuwawajibisha. Wengi wao ni kama wanaamini kuwa Polisi wana uwezo wa kufanya chochote bila ya kuzingatia katiba, sheria na kanuni. Ndiyo maana mara kadhaa tumeshuhudia Polisi wakifanya mambo ya ajabu yanayozuiwa na katiba na sheria za nchi, na hata kanuni za utendaji kazi za Jeshi la Polisi.

Mara kadhaa tumesikia kuwa eti jeshi la polisi limezuia mkutano wa chama cha siasa au limetoa kibali!! Ni mambo ya ajabu sana.

Kuhusiana na suala la mikutano ya vyama vya siasa, chama cha siasa kinachotaka kufanya mkutano, kinawajibika kuwapa taarifa Polisi. Chama hakiombi kibali, bali kinatakiwa kutoa tu taarifa ili kupatiwa ulinzi wa polisi. Kama kuna mazingira yoyote yale ambayo Polisi wanaona ni changamoto kwenye suala la usalama, mamlaka yao yanaishia kwenye kushauriana na chama husika juu ya namna bora ya kufanya ili kujihakilishia usalama. Polisi hawana mamlaka ya kufuta mkutano wa chama cha siasa. Chama husika kama baada ya kushauriana na polisi, kinaona ni aheri kuuahirisha mkutano huo, basi ndicho kitakachokuwa na mamlaka ya kuufuta mkutano kilichokuwa kimepanga kuufanya.

Kufuta shughuli zozote za kisiasa, kama kuna ulazima wa kufanya hivyo, kunaweza tu kufanywa na Rais kwa kutangaza hali ya hatari kwa kuzingatia sheria inasema ni mazingira gani Rais atalazimika kutangaza hali ya hatari.

Watanzania tuungane katika kuzifanya hizi taasisi za ulinzi na usalama, hasa Polisi, zifanye kazi kwa mujibu wa sheria, na siyo kwa matakwa ya mtu mmoja, ambaye yawezekana moyoni mwake akawa na dhamira chafu au akatumiwa na watu wenye dhamira chafu dhidi ya nchi.

Kila itakapotokea Polisi ametoa tangazo au kutenda jambo lolote lililo kinyume na katiba, sheria za nchi au kanuni, basi mara moja polisi huyo ashtakiwe kama yeye kwa kosa la kutumia madaraka vibaya (japo tunajua kuwa mahakama zetu nazo zinaiingiliwa).

OCD wa Ngorongoro afunguliwe mashtaka haraka sana kwa kuvunja sheria.
 
Acha umbumbumbu wako hapa.wewe umezuiwa kufanya mikutano na mikusanyiko ya aina yoyote ile na kupewa sababu za kuzuiwa halafu unataka ulazimishe? Kwanini usielewe wakati Umeambiwa ni sababu za kiusalama? Watu wakiumia au kuumizwa utamlaumu nani wakati umepewa tahadhari? Kwanini ninyi watu mnakuwa na vichwa vigumu kiasi hicho? Hata hivyo sikulaumu maana najuwa uwezo wako na upeo wako ulivyo.
 
Unataka litumie weledi wakati lenyewe linaitwa police force ,utapatikana weledi likiitwa police service

Majina huumba , jiite matatizo au SHIDA utaona habari yake
 
Polisi wasivunje Katiba na Sheria wao kazi zao ni kinyume chake.
 
Ukiwaona polisi basi umewaona CCM hawa ni watoto mapacha kwenye kukandamiza raia Kwa makusudi...
Siku CCM wakiondoka madarakani na polisi nao wataanza kufuata sheria
 
Acha umbumbumbu wako hapa.wewe umezuiwa kufanya mikutano na mikusanyiko ya aina yoyote ile na kupewa sababu za kuzuiwa halafu unataka ulazimishe? Kwanini usielewe wakati Umeambiwa ni sababu za kiusalama? Watu wakiumia au kuumizwa utamlaumu nani wakati umepewa tahadhari? Kwanini ninyi watu mnakuwa na vichwa vigumu kiasi hicho? Hata hivyo sikulaumu maana najuwa uwezo wako na upeo wako ulivyo.
Wewe ni mpiga kelele usiye na uwezo wa kuchangia mada yoyote kwa hoja. Hapa tunaongelea sheria inasema nini, na polisi wanafanya nini. Siyo kuleta hadithi za eti Polisi wametoa sababu.

Umeelezwa wazi kuwa kama kuna sababu zozote za msingi kama vile shida ya usalama, polisi wanatakiwa kuwaita waliotoa taarifa ya mkutano na kushauriana nao, na wao ndio wana uwezo wa kufuta au kuahirisha mkutano kama wataona sababu za polisi zina mantiki. Polisi hawana mamlaka ya kufuta mkutano wowote wa chama cha siasa.
 
Polisi wasivunje Katiba na Sheria wao kazi zao ni kinyume chake.

Jeshi la Polisi ambalo kwa mujibu wa sheria, ndilo linatakiwa kusimamia sheria, na kila wakati linawataka wananchi watii sheria bila shuruti, lilitakiwa lenyewe kutembea juu ya kauli zake, lakini cha ajabu, jeshi hili ndilo linaoongoza katika uharamia wa kuvunja sheria na kutofuata katiba.
 
Wewe ni mpiga kelele usiye na uwezo wa kuchangia mada yoyote kwa hoja. Hapa tunaongelea sheria inasema nini, na polisi wanafanya nini. Siyo kuleta hadithi za eti Polisi wametoa sababu.

Umeelezwa wazi kuwa kama kuna sababu zozote za msingi kama vile shida ya usalama, polisi wanatakiwa kuwaita waliotoa taarifa ya mkutano na kushauriana nao, na wao ndio wana uwezo wa kufuta au kuahirisha mkutano kama wataona sababu za polisi zina mantiki. Polisi hawana mamlaka ya kufuta mkutano wowote wa chama cha siasa.
Acha ujinga wako hapa wewe. Wawaite washauriane nao nini tena wakati umeshaambiwa sababu zake.acha umbumbumbu wako kwa Masuala yanayohitaji akili wewe unatumia na kuleta hisia zako.
 
Kuna tatizo kubwa la weledi ndani ya Jeshi la Polisi.

POlisi wa nchi hii, bila shaka hawana weledi wa kutosha, na wala hawajishughulishi kujua sheria ili wafanye kazi zao kwa weledi. Lakini pia yawezekana wanajua sheria inataka nini ila kwa kiburi na kwa makusudi wanaamua kuikanyaga sheria kwa kuamini kuwa hakuna wa kuwawajibisha. Wengi wao ni kama wanaamini kuwa Polisi wana uwezo wa kufanya chochote bila ya kuzingatia katiba, sheria na kanuni. Ndiyo maana mara kadhaa tumeshuhudia Polisi wakifanya mambo ya ajabu yanayozuiwa na katiba na sheria za nchi, na hata kanuni za utendaji kazi za Jeshi la Polisi.

Mara kadhaa tumesikia kuwa eti jeshi la polisi limezuia mkutano wa chama cha siasa au limetoa kibali!! Ni mambo ya ajabu sana.

Kuhusiana na suala la mikutano ya vyama vya siasa, chama cha siasa kinachotaka kufanya mkutano, kinawajibika kuwapa taarifa Polisi. Chama hakiombi kibali, bali kinatakiwa kutoa tu taarifa ili kupatiwa ulinzi wa polisi. Kama kuna mazingira yoyote yale ambayo Polisi wanaona ni changamoto kwenye suala la usalama, mamlaka yao yanaishia kwenye kushauriana na chama husika juu ya namna bora ya kufanya ili kujihakilishia usalama. Polisi hawana mamlaka ya kufuta mkutano wa chama cha siasa. Chama husika kama baada ya kushauriana na polisi, kinaona ni aheri kuuahirisha mkutano huo, basi ndicho kitakachokuwa na mamlaka ya kuufuta mkutano kilichokuwa kimepanga kuufanya.

Kufuta shughuli zozote za kisiasa, kama kuna ulazima wa kufanya hivyo, kunaweza tu kufanywa na Rais kwa kutangaza hali ya hatari kwa kuzingatia sheria inasema ni mazingira gani Rais atalazimika kutangaza hali ya hatari.

Watanzania tuungane katika kuzifanya hizi taasisi za ulinzi na usalama, hasa Polisi, zifanye kazi kwa mujibu wa sheria, na siyo kwa matakwa ya mtu mmoja, ambaye yawezekana moyoni mwake akawa na dhamira chafu au akatumiwa na watu wenye dhamira chafu dhidi ya nchi.

Kila itakapotokea Polisi ametoa tangazo au kutenda jambo lolote lililo kinyume na katiba, sheria za nchi au kanuni, basi mara moja polisi huyo ashtakiwe kama yeye kwa kosa la kutumia madaraka vibaya (japo tunajua kuwa mahakama zetu nazo zinaiingiliwa).

OCD wa Ngorongoro afunguliwe mashtaka haraka sana kwa kuvunja sheria.
Wapite wasome hapa
FB_IMG_1724903438142.jpg
 
Kuna tatizo kubwa la weledi ndani ya Jeshi la Polisi.

POlisi wa nchi hii, bila shaka hawana weledi wa kutosha, na wala hawajishughulishi kujua sheria ili wafanye kazi zao kwa weledi. Lakini pia yawezekana wanajua sheria inataka nini ila kwa kiburi na kwa makusudi wanaamua kuikanyaga sheria kwa kuamini kuwa hakuna wa kuwawajibisha. Wengi wao ni kama wanaamini kuwa Polisi wana uwezo wa kufanya chochote bila ya kuzingatia katiba, sheria na kanuni. Ndiyo maana mara kadhaa tumeshuhudia Polisi wakifanya mambo ya ajabu yanayozuiwa na katiba na sheria za nchi, na hata kanuni za utendaji kazi za Jeshi la Polisi.

Mara kadhaa tumesikia kuwa eti jeshi la polisi limezuia mkutano wa chama cha siasa au limetoa kibali!! Ni mambo ya ajabu sana.

Kuhusiana na suala la mikutano ya vyama vya siasa, chama cha siasa kinachotaka kufanya mkutano, kinawajibika kuwapa taarifa Polisi. Chama hakiombi kibali, bali kinatakiwa kutoa tu taarifa ili kupatiwa ulinzi wa polisi. Kama kuna mazingira yoyote yale ambayo Polisi wanaona ni changamoto kwenye suala la usalama, mamlaka yao yanaishia kwenye kushauriana na chama husika juu ya namna bora ya kufanya ili kujihakilishia usalama. Polisi hawana mamlaka ya kufuta mkutano wa chama cha siasa. Chama husika kama baada ya kushauriana na polisi, kinaona ni aheri kuuahirisha mkutano huo, basi ndicho kitakachokuwa na mamlaka ya kuufuta mkutano kilichokuwa kimepanga kuufanya.

Kufuta shughuli zozote za kisiasa, kama kuna ulazima wa kufanya hivyo, kunaweza tu kufanywa na Rais kwa kutangaza hali ya hatari kwa kuzingatia sheria inasema ni mazingira gani Rais atalazimika kutangaza hali ya hatari.

Watanzania tuungane katika kuzifanya hizi taasisi za ulinzi na usalama, hasa Polisi, zifanye kazi kwa mujibu wa sheria, na siyo kwa matakwa ya mtu mmoja, ambaye yawezekana moyoni mwake akawa na dhamira chafu au akatumiwa na watu wenye dhamira chafu dhidi ya nchi.

Kila itakapotokea Polisi ametoa tangazo au kutenda jambo lolote lililo kinyume na katiba, sheria za nchi au kanuni, basi mara moja polisi huyo ashtakiwe kama yeye kwa kosa la kutumia madaraka vibaya (japo tunajua kuwa mahakama zetu nazo zinaiingiliwa).

OCD wa Ngorongoro afunguliwe mashtaka haraka sana kwa kuvunja sheria.
Wapite wasome hapaView attachment 3081813
 
Back
Top Bottom