Polisi watoa tamko tukio la jaribio la utekaji Kiluvya, wasema uchunguzi umeanza toka aliporipoti Novemba 11, 2024


Wapo wengi ,wengine wana hadi rasta
 
Wanaharakati tayari Mungu kashawaonyesha nani hasa wanaoteka na kuua wapinzani wa serikali,sasa kazi kwenu kulifikisha mbali kwa wazungu ili hao watekaji/wasiojulikana wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.

Hao ndiyo baadhi ya genge la waliomuua Kibao ,waliomteka sativa ,soka ,wasipochukuliwa hatua inabidi wananchi tujilinde wenyewe.
 
Mkingojea hao watekaji wakamatwe mtangojea sana. Hawa dawa yao ni ile aliyoitumia yule mfanyabiashara wa Musoma ZAKARIA aliyewafyatulia risasi na kuwaua walipotaka kumteka
 





Utendaji ulioonekana hivi karibuni katika "kumteka" au kumtia nguvuni mwananchi anayeitwa Tarimo huko Kiluvya, unatia mashaka makubwa juu ya weledi kiutendaji wa sehemu za jeshi letu la Polisi.

Polisi ni chombo kinachotakiwa kujiendesha kisheria kwa kutumia PGO-Police General Orders.
Kumtia nguvuni raia yeyote kuna utaratibu ulioelezwa kisheria katika PGO.

Sasa kwa kituko kilichoonekana hivi karibuni kinaifedhesha jeshi la Polisi, na zaidi ya hapo kinamfedhehesha sana Mkuu wa Polisi nchini IGP Camillius Wambura.

Polisi wanaooperate kama hooligans wa Haiti, hii haileti picha nzuri mbele ya wananchi.

Kulikuwa na ulazima gani kutumia style ya kwa kweli kihuni, kama polisi walioenda kumu arrest, na wanajua kwamba huyu ni mhalifu, kwenda na arrest warrant, tafuta viongozi wa mtaa kwa ushahidi, kumweleza huyo Tarimo makosa yake, na mwisho kumpandisha Defender?

Nahisi kuna maafisa chini wa IGP wanamtengenezea zengwe kumuaibisha IGP aonekane hafai kwenye cheo chake.

All in All, jeshi la Polisi kwa vitendo kama hivi halionyeshi proffessionalism kazini, bali wanonekana kama hooligans!
 
Unayemtetea ndiye kinara wa hizo mbanga
 

Nimekusoma na kukuelewa. Hongera kwa kuanzisha uzi.
Niseme tu
Hili jeshi siyo la IGP hili jeshi ni la watanzania. Jeshi linapofanya vizuri, tunapata sifa watanzania woote. Na linapofanya mambo ya aibu. Aibu inakuja kwetu watanzania wote. Sasa kwa haya mambo ya aibu yanayotokea, ni wakati muafaka sasa kuanzia Waziri mwenye dhamana na jeshi letu la polisi pamoja na IGP wake wapishe. Maana tumechoka kupakwa matope kila kukicha na mambo yale yale. Hii ni nchi yenye watu wanaojitambua na utashi. Huwezi kututukana matusi ya mwilini kupitia chombo chetu adhimu jeshi la polisi halafu uendelee kuwepo ofisini. Utupishe, binafsi naona haya yanayotokea katika jeshi la polisi yanawafanya waonekane taasisi ya ajabu mbele ya jamii. Unakiua chombo chetu mahiri huku tukikuangalia. Hilo halikubaliki.
Nahitimisha.
 
Ni aibu kubwa kwa IGP Wambura, maafisa wake kufanya kazi kihuni!
Waziri na IGP wanatuchafulia chombo chetu waondoke. Maana hatua tunayofuata sasa ni jamii kukosa kukiamini chombo chao cha usalama. Hilo ni janga kubwa sana.

Tuitishe maandamano ya kulaani wale ambao wameazimia kukichafua na kukiua chombo chetu jeshi la polisi
 
Sina maana kwamba waliomteka Big ni polisi,lakin wapo polisi wenye tatoo,Rasta,Ndevu na nywele ndefu n.k inategemeana na kitengo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…