Precision Air yafuta Safari zote za kwenda Kenya licha ya Kenya kuruhusu Safari zake

Huyu mpumbavu wa kenya asitusumbue
 
And that weak demand is because Kenyans in Tanzania have all come back so there are no people to carry. Watanzania hawapandangi ndege.
Ha ha ha hii analysis ni ya kibera. Tanzania hatujazuia raia wa kenya, tumezua ndege tu. The shirika lenye makazi tzania linafuta safari za nairobi siyo za kutoka huko kuja dsm, arusha na Zanzibar. Sasa hapo nani wanapanda ndege kati ya Kenya na tzania?

Precision wamekosa biashara kwa kuwa abiria wa kutoka Tanzania wana compulsory 14 daya quarantine, nani aende huko? So routes ni mahali pasipo na ujinga huo
 
Hawa jirani zetu walikua wanasemaga watanzania wako nyoronyoro sana.
Ati hata jambazi la kitanzania likitaka kukuibia linakuomba ".....tafadhali naomba ulale chini nikuibie" 😁😁😁
Ndugu zangu watanzania tuliokua tumehamia Kenya turudi nyumbani kumenogaaaa
 
Magu yupo yupo sana mpk 2030,mungiki huyo mamluki wenu anajipotezea muda tu
 
ni kwanini asilimia kubwa ya watanzania waliopo JF wanapenda shari/ugomvi kati ya Tz na kenya ?
 
ATCL ilikuwa na route ya Kenya [emoji1139] tangu lini?
 
Watalii wanaotaka kuja Tanzania watafanya direct booking za kuja huku kupitia mashirika ya ndege mengine kama klm etc. Kwani KQ hao watalii inawatoa ulaya kuwaleta Tanzania au Kenya kuja Tanzania? Pia kuna mashirika mengine yana hizo flight mfano Ethiopia airline, Rwanda air wana ndege ya kuzunguka almost nchi zote za eac. Hii pin ni msiba kwa KQ sababu wakijua haiji Tanzania wazungu ni ngumu tena kuja kuwaaminisha inakuja huku kwetu
 
Bakini huko huko msituletee Corona
 
Baada ya serikali ya Kenya kusema kuwa haitafuta haki za usafiri za kampuni hiyo, wakati huu kukiwa na mvutano baina ya nchi hizo mbili, gazeti la Business Daily limeandika.

Taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wake wa twitter, imesema inaahirisha mipango hiyo kwasababu ya idadi ndogo ya wateja wanaotaka kusafiri, ikiahidi kuwa tarehe nyingine ya safari kuelekea Nairobi itapangwa na kuchapishwa kwenye tovuti yao hivi karibuni.

Tanzania ilizipiga marufuku kampuni tatu za ndege kutoka Kenya kuingia nchini humo kama hatua ya kulipiza kisasi vita vya kibiashara ambavyo vimekuwepo kati ya mataifa hayo .

Hatua hiyo iliochukuliwa na Tanzania inajiri baada ya Nairobi , kwa mara ya pili mfululizo, kuiweka Tanzania miongoni mwa mataifa ambayo sio salama kutokana na virusi vya corona.

Hatua hiyo ina maana kwamba wasafiri kutoka Tanzania wataendelea kukabiliwa na masharti ya lazima ya kuwekwa katika karantini kwa wiki mbili wanapowasili Kenya ili kuzuia maambukizi ya maradhi hayo.

Wasafiri kutoka mataifa 130, hatahivyo wako huru kuingia nchini Kenya bila masharti yoyote kufuatia hatua ya pili ambapo serikali iliongeza mataifa mengine 90 katika orodha yake ya mataifa yanayostahili kuingia nchini humo.

Mvutano huu umeathiri biashara kati ya mataifa hayo mawili. Afisa mkuu mtendaji wa shirika la ndege la Kenya Airways Allan Kilavuka alisema kwamba njia ya kuelekea Tanzania inasalia kuwa muhimu kutokana na idadi ya wateja inaowaleta Kenya kwa safari nyingine za kimataifa kwa kutumia ndege za kampuni hiyo.
Tunatumai kwamba tatizo hili litatatuliwa haraka iwezekanavyo , alisema bwana Kilavuka.

Precision Air itarajiwa kuanza safari kutoka Dar es Salaam kupitia Zanzibar kuelekea Nairobi na kurudi.
BBC Swahili
 
Kenya wanashangaza Sana. Na hiyo EAC ivunjike tu sioni umuhimu wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…