Prof. Samuel Manyele wa Tume ya vinyesi vya Ng'ombe Mto Mara

Habari ya chuo weka pembeni, habari ya utalaam weka pemben, 25kg + 21 L ng'ombe mmoja kwa siku moja?

Halafu bado tunaagiza mbolea toka nje ya nchi? Kweli?
 
Huyu Prof,nadhani ndiye huwa akifika kwao,anafikia loji hadi anasepa,kule Msanzi,Sumbawanga,au nimechanganya?Kama niyeye,sijui anatumiaga theory ipi kufanya hivyo,anyway.... tumeipokea ripoti kwa hisia tofautitofauti.
Yes, anatokea Sumbawanga huyu jamaa, tulikua nae kipindi fulani nikiwa UDSM.

Ana mambo ya utamaduni mno hasa imani za kishirikina japo ni msomi.
 
Nimekinga mkojo na mavi ya ng'ombe hapa.

Mkoja lita 21,kinyesi 25kg.

Naongeza maji lita kumi kumi.. inakuja kama biogas.

Kadiri maji yanavyoongezeka naona ile concentration inapungua.

Sasa huko mtoni iliwezaje ikatokea.


Hao ng'ombe walikaa wapi wakaanza kukojoa na kunya.
 
Mkuu, anaweza kuwa kama Kabudi, ama Chief Justice
 
 
Ni shida sana!

Niko kwenye group ambalo lina maprof kutoka SUA chuo kinachojielewa wamegoma kuikubali hiyo report!

Hii sasa ndiyo ilitakiwa kuitwa kama alivyosema Tundu Lissu kwamba ni professorial rubbish!

Wasomi wa Tanzania ni hopeless kabisa, yaani hata yule mkurugenzi wa Bodi ya Bonde la Ziwa Victoria ameshindwa kuwasaidia kuungana na kile walichobaini mwanzoni?
 
Currently ni Chemical and Process engineering Department
 

Kuishia kunong'ona kwenye ma group ya WhatsApp kunaitwa kufichama. Wanasemezana huko wao kwa wao? Haitoshi!



Si watoke huko nao wapaze sauti?
 
Reactions: Ame
Currently ni Chemical and Process engineering Department

Asante kwa maboresho.

Ninarejea kurekebisha pale.

Ndipo ilipo tofauti baina ya background check na facts check.

Ninakazia shukurani kwa maboresho.
 
Bado ripoti yake ina ukakasi.

Kwani ngombe wameanza leo kinyesi cha ya sumu katika mto Mara?
 
Un
Inanikumbusha kichekesho kimoja ndugu walimpekua mgonjwa hospitalini akiwa mahututi.

alivyofikishwa kwa daktari daktari akasema ndugu yenu ameshafariki kwa bahati nzuri mgonjwa ile kauli akasikia ingawa kwa mbali sana basi akajibu mimi bado sijafa.

wale jamaa zake wakamwambia we kua na Adabu unambishia mpaka daktari
 
Mnaopinga ripoti yake kuhusu mto Mara na nyie toeni yenu sio maneno tu.
 
Teh teh teh 😂😂...kumvaa msomi kama huyu tena kwenye fani yake lazima ujipange haswa....lasivyo utaonekana kituko tu.
 
Wewe unayemtetea uwezo wako ni kama wake wa kuhongwa hela kubadili ripoti.

Of course hata ningekuwa mimi ndiyo professor ningechukua hela ili kulinda uhai wangu.

Kipindi hiki serikali inalinda wawekezaji kuliko uhai wa watanzania.

Prof angeshupaza shingo wangemuua.

Hivyo tumuelewe hiki ndicho kipindi cha hivyo.

Hata akina Prof Kabudi au Prof Luoga asingekuwa Dkt Magufuli wangeuawa na ripoti zao za madini na makinikia etc.

Kwa ufupi Prof tusimlaumu ila tuwalaumu kundi la mafisadi lililokumbatiwa na serikali.

Prof kafanya hivyo kutetea uhai wake.
 
Mnaopinga ripoti yake kuhusu mto Mara na nyie toeni yenu sio maneno tu.

Unaweza kuwa umeona katika maandiko yangu kwenye uzi huu. Ripoti ya Professor ina ukakasi wa kutosha. Ila sasa namna ya kumwingia inabidi kujipanga.

Ndiyo maana kumekuwa na background checks, fact checks na maboresho ya hapa na pale kila ilipobidi (credit kwako fizoG).

Hizi hapa ni facts:

"Ng'ombe wa beberu aliyenona vilivyo (540kg) anakula takribani 15kg tu kwa siku.

Determining How Much Forage a Beef Cow Consumes Each Day

Hawa Ng'ombe wa Prof Manyele wenye vinyesi vya kufikia 25kg kwa siku anawapata wapi?


Wanakua vipi ng'ombe hao?"

Kimsingi hadi sasa zipo inputs za kutosha na hatimaye tunaweza kuyasema haya tukiwa na macho makavu:

Ripoti ya Vinyesi vya Ng'ombe mto Mara haishawishi

Hoja hujibiwa kwa hoja. Profesa Manyele anahitajika kutoa ufafanuzi zaidi.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…