Prof. Tibaijuka: Chato haina sifa kuwa Mkoa
"Katika mazishi Wazee Chato walimuomba Rais Samia mkoa wakidai ni ahadi ya mtangulizi wake.kwa hekima akasema ataangalia vigezo.Kama Mbunge Mstaafu jirani Muleba Kusini najua vigezo havipo.Wazo halitekelezeki. Wazee jirani na sisi naamini tutapewa nafasi kushauri"Anna Tibaijuka

---
Anaandika PROF. ANNA K. TIBAIJUKA

Ramani inaonyesha Chato ni sehemu ya Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa Kagera. Kiuhalisia. Na kihistoria. Mengine ni kulazimishalazimisha tu.

Naendelea kusisitiza hakuna hoja yoyote ya kiuchumi kuunda mkoa wa Chato. La sivyo basi tuelimishwe.

Ila kama mnapenda siasa za upendeleo wa sehemu fulani ama kwa kuwa mkubwa aliwahi kuzaliwa pale au mtu apewe nafasi kwa sababu ni mtoto wa kiongozi endeleeni kuwabebesha wananchi mizigo ya kulipa kodi kusudi wateule wajichane. Period.

Kwanza ikumbukwe Mkoa wa Geita ulianzishwa kusudi Chato iwe Makao Makuu. Ikakosa vigezo. Geita mjini ikaonekana ndiyo yenye sifa za kuwa Makao Makuu ya Mkoa mpya wa Geita. Hii ilikuwa 2010. Sasa 11 years later Chato ati ina vigezo kuwa Makao Makuu ya Mkoa wake wenyewe? Are we serious with our development? Really? Na Rais wetu mpendwa SSH tunataka kweli kumtwisha zigo la kuamua jambo hili na controversy zake? Elimu haina mwisho. Mimi kama kuna vigezo naomba viorodheshwe. Labda ndiye sina taarifa. Ila so far Hoja ya kuwaletea maendeleo Kakonko, Biharamulo, Ngara na Muleba inayokatwa vipande ninazikataa. Mkoa unaweza kuleta maendeleo gani kwa Wilaya yake wakati Mkoa unategemea bajeti ya Serikali Kuu. Mkoa una mapato gani zaidi ya kutumia kodi? Lets be serious. Maendeleo yanatokana na uwekezaji na uwezeshaji kwa wananchi. Siyo watumishi wa Serikali tena baadhi bila maadili wanaweza kuishia kuwabugudhi wananchi badala ya kuwa msaada.

Njia pekee kumuenzi Hayati Magufuli ni kurekebisha mambo ambayo kama binadamu hakufanya vizuri. Mengine yote ni ubinafsi. Na kufifisha sifa zake katika historia ya nchi hii. Tumuache apumzike.

Miundombinu iliyowekwa Chato siyo kigezo kuunda mkoa hapo. Tuikamilishe na kuitafutia matumizi mbadala ya kitaifa. Mfano Airport ya Chato inaweza kufanywa Hub ya kilimo cha contract floriculture na horticulture...(kilimo mkataba cha maua na mboga) ili tuwe na ndege za mizigo kuja kubeba. Na maziwa .

Hospitali ya Kanda Chato.... naomba tutathmini kwanza maendeleo ya hospitali ya Mloganzila. State of the Art buildings only 40km away from Dar City Centre na Muhimbili. Mojawapo ya mafanikio makubwa ya Awamu ya nne. Lakini Angalia changamoto zake. Uhaba wa madaktari hadi leo. Sasa hao specialist doctors watakaokubali kuishi Chato mtawalipa fedha kiasi gani?. A hospital is not just buildings. Its manpower resources and the economy surrounding it. Katika dhana ya mipango miji na maendeleo ya makazi lazima vigezo vyote hivyo kuangaliwa. Kwa uelewa wangu Chato haina vigezo. Tusidanganyane.
Huu mkoa hauna tija.
Kazi na iendelee kwa mambo mengine yenye tija kwa ustawi na mustakabali wa nchi.
 
Yaan nimekuelewa vizuri sana hapa aliposema ( Njia pekee kumuenzi Hayati Magufuli ni kurekebisha mambo ambayo kama binadamu hakufanya vizuri. Mengine yote ni ubinafsi. Na kufifisha sifa zake katika historia ya nchi hii. Tumuache apumzike.

Miundombinu iliyowekwa Chato siyo kigezo kuunda mkoa hapo. Tuikamilishe na kuitafutia matumizi mbadala ya kitaifa. Mfano Airport ya Chato inaweza kufanywa Hub ya kilimo cha contract floriculture na horticulture...(kilimo mkataba cha maua na mboga) ili tuwe na ndege za mizigo kuja kubeba. Na maziwa . )
Unajua Mama ni msomi sana hivyo hata anachoongea lazima tuwaangalie vizuri.

Kweli kabisa chato haiwezi kuwa Mkoa bado sana sana sana.
 
Uzinduzi ulifanyika lini mbona iyo hospital ya wilaya ipo tok kitambo tukio la mwisho ilikuwa ni kuweka jiwe la msingi kwenye hospital ya rufaa ya kanda iliyojegwa CHATO nadhan nipo sahii
Uko sahihi mkuu, kuna hospitali ya wilaya ambayo ni kongwe na kuna nyingine kubwa zaidi ya rufaa kikanda inajengwa hapo Chato.... Haijakamilika.
 
Basi wilaya zote ziwe mikoa zijengeke kadri muda unavyoenda
Hiyo Bukoba wakati inapewa hadhi ya makao makuu ya mkoa ilikuwa ni pori tu lakini leo ni mji mkubwa.

Mama Tibaijuka wala asiwe na hofu Chato itajengeka kadri muda unavyokwenda.
 
Mama pumzika zako makongo Dar ya huko waachie wana Chato na Mama Mkoa Geita wameshakubali .....acha iwe utaambiwa ya kuambiwa wilaya mojawapo au 2 Kagera itamegwa kwenda Chato....pambana na wajukuu mama awamu 6 hii sukuma gang wanalia huko legacy ......ya kulazimishia
apumzike ile muharibu nchi. hatuwezi kufanya ujinga ili kumfurahisha marehemu
 
Serikali isipowekwa wazi vigezo vinavyotumika kuunda mikoa ugawanyaji wa mikoa utaendelea kuwa utata mtupu
Tunaomba orodha ya sifa zinazotakiwa kwa sehemu ya Jamhuri ya Muungano Tanzania kufuzu kuitwa mkoa. Tukizipata hizo sifa itaturahisishia kujua kama Chato inakidhi vigezo kwa sasa ama la!
 
Hiyo Bukoba wakati inapewa hadhi ya makao makuu ya mkoa ilikuwa ni pori tu lakini leo ni mji mkubwa.

Mama Tibaijuka wala asiwe na hofu Chato itajengeka kadri muda unavyokwenda.
Kwanza Chato irudi Kagera then ule mkoa wa Geita ufanyiwe tathimini upya. Kulazimisha ujinga. Naungana na Prof Tibaijuka kwenye hili.
 
Kama huo ndio utaratibu basi kila wilaya itakuwa mkoa
Chato tayari ni mkoa wananchi kupitia madiwani wao wameshamaliza kutoa mawazo yao na wengi wameshapendekeza wilaya za mkoa wao sasa huyo Prof. alikuwa wapi wakati wa kutoa maoni? Haturudi nyuma tunasonga mbele. Tarehe 14/10/2021 wakati wa sherehe za kuzima Mwenge hapa Chato tunategemea Rais wetu mpendwa Samia atangaze rasmi kuwa Chato ni mkoa. Sasa wasiotaka wajiandae kisaikorojia wasije wakafa na stress bure.
 
Wazee Wa Chettle Mupo
Mnaona Sasa Hivi Watu Wale Wale Wanawakataa Kweupe
Kuku Wanaona 😆😅😄😃😂😁😀
 
Tufahamishe sifa za eneo kuwa mkoa
Watu wameingia vitani tena.

Sasa hivi wanagombea kama Chato iwe mkoa ama la. Ndani kabisa ya wahusika wa huu ugomvi ni walewale wa 'legacy' na 'yule hana legacy yoyote'

Kwa urahisi zaidi nasema ni upuuzi unaendelea. Huu ni ushindani bado wa kupimana kama marehemu alikua au hakua sahihi, cha kufurahisha ni kwamba pande zote hazijui na hazitaki kujua sifa za eneo kua mkoa.

Watanzania tupo kwenye mtego, watu hawataki kusonga mbele wameganda zama iliyopita na kuna dhihaka kwa waliobaki huko.

Ni upuuzi unaendelea.
 
Vigezo vya eneo kuwa mkoa ni vipi?
Huo utakuwa mkoa. Sisi wa Ngara na maeneo hayo tunaelewa maana ya Chato kuwa mkoa. Tunaelewa maana ya wilaya kadhaa kuunganishwa pamoja ukapatikana mkoa mpya.

Wengi humu wanapinga kwa sababu ya kupinga mengi aliyokuwa akiyafanya hayati JPM, wanazo hoja za kisiasa zaidi kuliko uhalisia.
 
Kijiografia unaposema kuanzisha mkoa wa chato na chato iwe makao makuu ili kusogeza huduma karibu na wananchi huo ni uongo wa kupingwa kwa nguvu zote,

kama tuko serious Nyakanazi ndio eneo liliopo katikati ya Biharamulo, Ngara, Kakonko na Wilaya ya Bukombe,

kwanini isiundwe wilaya ya nyakanazi kisha tukatengeneza mkoa wa nyakananzi utakaoundwa na wilaya za Biharamulo, Nyakanazi, Ngara, Kakonko na Bukombe?

kwanini tunagangania chato kutoka kakonko na ngara kwenda chato bado ni mbali sana,


kama ajenda iliyopo ni kuwasogezea wananchi huduma za karibu basi uanzishwe mkoa wa nyakanazi ila kama kuna ajenda nyingine ya kijinga basi endeleeni na chato yenu
 
Back
Top Bottom