Prof. Tibaijuka: Chato haina sifa kuwa Mkoa
Chato haina sifa hiyo na hata uwanja wa ndege pale zilitumika fedha za watanzania vibaya.
Mfano siku ya mazishi ya mwenda zake, watu tuli lala Kahama, Katoro Geita na hata wengine Mwanza na Shinyanga kutokana na kinacho pendekezwa kuwa mkoa kukosa huduma muhimu. Leo wana taka mkoa.
 
Mwenye uwelewa na vigezo hapa atusidie ili tujue kwa mujibu wa sheria ya Jamuhuri mkoa unatakiwa uwe na sifa zipi
Ati vigezo 🙂 ....kigezo kimojawapo ni 'wazee wanataka mkoa' basi. Ni kama kiuteuliwa cheo kigezo ni kuwa mtoto wa kada mstaafu/aliyeondoka ili 'riziki' iendelee kuingia kwenye malago yaleyale.

Binafsi sio mpenzi wa kusoma vitabu lakini nalazimika kukitafuta kitabu cha hayati Shaaban Robert ili kujua aliposema nchi ya kufikirika alimaanisha kitu gani. Haiwezekani mbali na utashi wa mkoa lakini kwenye jamii hii kuna mbunge hajui kuwa bunge ndicho chombo huru cha kuisimamia serikali bali anapendekeza kuundwe kingine huku mkuu wake akikana kupitisha sheria aliyoipitisha kwa mbwembwe
 
Chato haina vigezo vya kuwa Mkoa, kwanza hii italeta picha mbaya ya ubinafsi kwa JPM, kwa mfano JK nae angetaka Msoga iwe Mkoa, Mkapa angetaka Masasi iwe Mkoa, Mzee Mwinyi angetaka Mkuranga iwe Mkoa, Mwalimu Nyerere angetaka Butiama iwe Mkoa, tungefika wapi? Ili kuwa Mkoa ni vigezo, sio will tu ya Mkuu wa nchi kwa wakati husika. Chato haijakidhi vigezo kabisa kuwa Mkoa. Tusilazimishe
Kuna haja ya kurekebisha Katiba yetu haraka iwezekanavyo. Yaani kila alikotoka mkuu fulani inalazimishwa uwe mkoa, kwa faida ipi watakayoipata? Basi kila watu na Kanda zao wajipe promo maeneo yao yawe mkoa. Morogoro yenyewe kubwa, Kigoma na Tabora zote bado ni kubwa, bila kusahau Kagera ni kubwa sana, kwa nini usianzishwe mkoa wa Biharamulo bali ni Chato? Kwa nini?
 
"Katika mazishi Wazee Chato walimuomba Rais Samia mkoa wakidai ni ahadi ya mtangulizi wake.kwa hekima akasema ataangalia vigezo.Kama Mbunge Mstaafu jirani Muleba Kusini najua vigezo havipo.Wazo halitekelezeki. Wazee jirani na sisi naamini tutapewa nafasi kushauri"Anna Tibaijuka

---
Anaandika PROF. ANNA K. TIBAIJUKA

Ramani inaonyesha Chato ni sehemu ya Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa Kagera. Kiuhalisia. Na kihistoria. Mengine ni kulazimishalazimisha tu.

Naendelea kusisitiza hakuna hoja yoyote ya kiuchumi kuunda mkoa wa Chato. La sivyo basi tuelimishwe.

Ila kama mnapenda siasa za upendeleo wa sehemu fulani ama kwa kuwa mkubwa aliwahi kuzaliwa pale au mtu apewe nafasi kwa sababu ni mtoto wa kiongozi endeleeni kuwabebesha wananchi mizigo ya kulipa kodi kusudi wateule wajichane. Period.

Kwanza ikumbukwe Mkoa wa Geita ulianzishwa kusudi Chato iwe Makao Makuu. Ikakosa vigezo. Geita mjini ikaonekana ndiyo yenye sifa za kuwa Makao Makuu ya Mkoa mpya wa Geita. Hii ilikuwa 2010. Sasa 11 years later Chato ati ina vigezo kuwa Makao Makuu ya Mkoa wake wenyewe? Are we serious with our development? Really? Na Rais wetu mpendwa SSH tunataka kweli kumtwisha zigo la kuamua jambo hili na controversy zake? Elimu haina mwisho. Mimi kama kuna vigezo naomba viorodheshwe. Labda ndiye sina taarifa. Ila so far Hoja ya kuwaletea maendeleo Kakonko, Biharamulo, Ngara na Muleba inayokatwa vipande ninazikataa. Mkoa unaweza kuleta maendeleo gani kwa Wilaya yake wakati Mkoa unategemea bajeti ya Serikali Kuu. Mkoa una mapato gani zaidi ya kutumia kodi? Lets be serious. Maendeleo yanatokana na uwekezaji na uwezeshaji kwa wananchi. Siyo watumishi wa Serikali tena baadhi bila maadili wanaweza kuishia kuwabugudhi wananchi badala ya kuwa msaada.

Njia pekee kumuenzi Hayati Magufuli ni kurekebisha mambo ambayo kama binadamu hakufanya vizuri. Mengine yote ni ubinafsi. Na kufifisha sifa zake katika historia ya nchi hii. Tumuache apumzike.

Miundombinu iliyowekwa Chato siyo kigezo kuunda mkoa hapo. Tuikamilishe na kuitafutia matumizi mbadala ya kitaifa. Mfano Airport ya Chato inaweza kufanywa Hub ya kilimo cha contract floriculture na horticulture...(kilimo mkataba cha maua na mboga) ili tuwe na ndege za mizigo kuja kubeba. Na maziwa .

Hospitali ya Kanda Chato.... naomba tutathmini kwanza maendeleo ya hospitali ya Mloganzila. State of the Art buildings only 40km away from Dar City Centre na Muhimbili. Mojawapo ya mafanikio makubwa ya Awamu ya nne. Lakini Angalia changamoto zake. Uhaba wa madaktari hadi leo. Sasa hao specialist doctors watakaokubali kuishi Chato mtawalipa fedha kiasi gani?. A hospital is not just buildings. Its manpower resources and the economy surrounding it. Katika dhana ya mipango miji na maendeleo ya makazi lazima vigezo vyote hivyo kuangaliwa. Kwa uelewa wangu Chato haina vigezo. Tusidanganyane.
We Mama sindo ulitupandishia Kodi za ardhi bila huruma? Au nakufananisha
 
Nyerere Nae angesema Butiama, Makutano Na Ikizu uwe Mkoa??
 
Kanda ipi kungali na Bugando?
Kanda ni hadhi tu technically ni hospitali ya rufaa. Kwa ivyo uwepo wa Bugando kanda hiyo sio kigezo wa kutokuwa na nyingine inategemea hospitali inahudumia watu wangapi.

Ndio maana hapo unaona nimeweka criteria ni population density and being centre of gravity.

Chato aina watu hao na wala sio centre of Gravity; hospitali ya kanda (rufaa) maeneo yale inahitajika Geita mjini kwa sababu kwanza population yake karibu 1 millioni yenyewe tu, bado inaweza hudumia watu kutoka Mwanza, Mara, Chato, Kigoma na maeneo ya Bukoba.

Sehemu zingine zenye sifa ya kuwa centre of gravity either Bukoba, Kigoma au Tabora; kuhudumia hiyo population, lakini siyo Chato.
 
Hivi huwa mna nini vichwani mnapotoa statements kama hizi! Wewe ni Samia? Na ikiwa mkoa aibu utaziweka wapi?
Na wewe vipi izo aibu utazuweka wapi hicho kimkoa chenu kisipotangazwa?
 
Mama pumzika zako makongo Dar ya huko waachie wana Chato na Mama Mkoa Geita wameshakubali .....acha iwe utaambiwa ya kuambiwa wilaya mojawapo au 2 Kagera itamegwa kwenda Chato....pambana na wajukuu mama awamu 6 hii sukuma gang wanalia huko legacy ......ya kulazimishia
hapana,mama ana haki ya kutoa maoni yake kwanza kama raia,pili kama mbunge mstaafu ambaye eneo la jimbo lake linahusishwa na na mpango huo na tatu kama mtaalam wa mipango miji ambaye alikua Mkurugenzi Mkazi wa UN Habitat.

Asifumbwe midomo kwani kuwa na wajukuu wa kulea si hoja ya kumfanya asishauri kile alicho nacho kichwani mwake.
 
Naomba niwe mtu was mwisho kusema...
Hakuna na hakutakua na mkoa was chato.
 
Kiukweli lipo tatizo la kufikirika,ni Bora kuongeza halmashauri na kupandisha hadhi palipo na vigezo, ofisi ya RC Haina impact kubwa kwa ustawi wa Jamii. Kwa dunia ya leo mawasiliano hata wazo la kuhamia Dodoma halina tija Bora fungu like lingetumika boresha sector kilimo, SGR ingepata mizigo ya kutosha mbeleni.
"Iwapo nia ni kuunda mkoa unaosogeza huduma jirani na wananchi ni busara mkoa huu kuundwa kwa kuweka makao makuu Biharamulo.

Hara hivyo sioni maana/mantiki ya wakazi wa wilaya za Ngara na Kakonko kuvuka wilaya ya Biharamulo wakienda Chato ambayo ni wilaya itakayokuwa pembeni mwa mkoa huu mpya.

Mkoa huu badala ya kunufaisha wakazi wake wengi, utawaumiza.

Pia sioni manufaa atakayoyapata mkazi wa Buseresere na Katoro kwa kuwa ataongeza umbali wa kwenda makao makuu ya mkoa.

Hata hivyo nashauri serikali badala ya kuwaza kuongeza mikoa, ijikite kupunguza ukubwa wa vijiji na kata.
Hili liende sambamba na kuwarahisishia utendaji wa kazi zao viongozi wa vijiji na kata kwa kuwapa usafiri, vifaa vya kazi kama kompyuta mpakato, simu zinazoweza kupata matukio [picha] vema.

Hapa Ngara kwenye kata ya Muganza, umbali kutoka Kitongoji cha Nyakafandi hadi makao makuu ya Kijiji chao cha Mukubu ni km.15.
Kutoka kitongoji hicho hadi makao makuu ya kata ni zaidi ya km.30.

Mtendaji wa kata na kijiji hawana usafiri wowote.
Huko hakuna umeme.
Wangeweza kusaidiwa kupewa umeme wa jua kwenye ofisi zao ili wachaji simu zao ambazo Kwa sehemu kubwa zinafanya kazi za ofisi.

Wananchi hatuna hitaji la mikoa na wilaya.
Tunahitaji zaidi huduma bora za vijiji na kata.

Ikumbukwe miaka michache iliyopita ukubwa wa vitongoji uliongezwa badala ya kupunguzwa.
Kuna sehemu mitaa/vitongoji vitatu viliungwa kuwa kimoja.
Mzigo uliongezeka."
 
Hiyo Bukoba wakati inapewa hadhi ya makao makuu ya mkoa ilikuwa ni pori tu lakini leo ni mji mkubwa.

Mama Tibaijuka wala asiwe na hofu Chato itajengeka kadri muda unavyokwenda.
Ilikua wakati huo na vigezo vya wakati ule vilitosha kufanya Bukoba kuwa Makao makuu ya mkoa na Ziwa magharibi kuwa mkoa
 
"Iwapo nia ni kuunda mkoa unaosogeza huduma jirani na wananchi ni busara mkoa huu kuundwa kwa kuweka makao makuu Biharamulo.

Hara hivyo sioni maana/mantiki ya wakazi wa wilaya za Ngara na Kakonko kuvuka wilaya ya Biharamulo wakienda Chato ambayo ni wilaya itakayokuwa pembeni mwa mkoa huu mpya.

Mkoa huu badala ya kunufaisha wakazi wake wengi, utawaumiza.

Pia sioni manufaa atakayoyapata mkazi wa Buseresere na Katoro kwa kuwa ataongeza umbali wa kwenda makao makuu ya mkoa.

Hata hivyo nashauri serikali badala ya kuwaza kuongeza mikoa, ijikite kupunguza ukubwa wa vijiji na kata.
Hili liende sambamba na kuwarahisishia utendaji wa kazi zao viongozi wa vijiji na kata kwa kuwapa usafiri, vifaa vya kazi kama kompyuta mpakato, simu zinazoweza kupata matukio [picha] vema.

Hapa Ngara kwenye kata ya Muganza, umbali kutoka Kitongoji cha Nyakafandi hadi makao makuu ya Kijiji chao cha Mukubu ni km.15.
Kutoka kitongoji hicho hadi makao makuu ya kata ni zaidi ya km.30.

Mtendaji wa kata na kijiji hawana usafiri wowote.
Huko hakuna umeme.
Wangeweza kusaidiwa kupewa umeme wa jua kwenye ofisi zao ili wachaji simu zao ambazo Kwa sehemu kubwa zinafanya kazi za ofisi.

Wananchi hatuna hitaji la mikoa na wilaya.
Tunahitaji zaidi huduma bora za vijiji na kata.

Ikumbukwe miaka michache iliyopita ukubwa wa vitongoji uliongezwa badala ya kupunguzwa.
Kuna sehemu mitaa/vitongoji vitatu viliungwa kuwa kimoja.
Mzigo uliongezeka."
 
"Katika mazishi Wazee Chato walimuomba Rais Samia mkoa wakidai ni ahadi ya mtangulizi wake.kwa hekima akasema ataangalia vigezo.Kama Mbunge Mstaafu jirani Muleba Kusini najua vigezo havipo.Wazo halitekelezeki. Wazee jirani na sisi naamini tutapewa nafasi kushauri"Anna Tibaijuka

---
Anaandika PROF. ANNA K. TIBAIJUKA

Ramani inaonyesha Chato ni sehemu ya Wilaya ya Biharamulo Mkoa wa Kagera. Kiuhalisia. Na kihistoria. Mengine ni kulazimishalazimisha tu.

Naendelea kusisitiza hakuna hoja yoyote ya kiuchumi kuunda mkoa wa Chato. La sivyo basi tuelimishwe.

Ila kama mnapenda siasa za upendeleo wa sehemu fulani ama kwa kuwa mkubwa aliwahi kuzaliwa pale au mtu apewe nafasi kwa sababu ni mtoto wa kiongozi endeleeni kuwabebesha wananchi mizigo ya kulipa kodi kusudi wateule wajichane. Period.

Kwanza ikumbukwe Mkoa wa Geita ulianzishwa kusudi Chato iwe Makao Makuu. Ikakosa vigezo. Geita mjini ikaonekana ndiyo yenye sifa za kuwa Makao Makuu ya Mkoa mpya wa Geita. Hii ilikuwa 2010. Sasa 11 years later Chato ati ina vigezo kuwa Makao Makuu ya Mkoa wake wenyewe? Are we serious with our development? Really? Na Rais wetu mpendwa SSH tunataka kweli kumtwisha zigo la kuamua jambo hili na controversy zake? Elimu haina mwisho. Mimi kama kuna vigezo naomba viorodheshwe. Labda ndiye sina taarifa. Ila so far Hoja ya kuwaletea maendeleo Kakonko, Biharamulo, Ngara na Muleba inayokatwa vipande ninazikataa. Mkoa unaweza kuleta maendeleo gani kwa Wilaya yake wakati Mkoa unategemea bajeti ya Serikali Kuu. Mkoa una mapato gani zaidi ya kutumia kodi? Lets be serious. Maendeleo yanatokana na uwekezaji na uwezeshaji kwa wananchi. Siyo watumishi wa Serikali tena baadhi bila maadili wanaweza kuishia kuwabugudhi wananchi badala ya kuwa msaada.

Njia pekee kumuenzi Hayati Magufuli ni kurekebisha mambo ambayo kama binadamu hakufanya vizuri. Mengine yote ni ubinafsi. Na kufifisha sifa zake katika historia ya nchi hii. Tumuache apumzike.

Miundombinu iliyowekwa Chato siyo kigezo kuunda mkoa hapo. Tuikamilishe na kuitafutia matumizi mbadala ya kitaifa. Mfano Airport ya Chato inaweza kufanywa Hub ya kilimo cha contract floriculture na horticulture...(kilimo mkataba cha maua na mboga) ili tuwe na ndege za mizigo kuja kubeba. Na maziwa .

Hospitali ya Kanda Chato.... naomba tutathmini kwanza maendeleo ya hospitali ya Mloganzila. State of the Art buildings only 40km away from Dar City Centre na Muhimbili. Mojawapo ya mafanikio makubwa ya Awamu ya nne. Lakini Angalia changamoto zake. Uhaba wa madaktari hadi leo. Sasa hao specialist doctors watakaokubali kuishi Chato mtawalipa fedha kiasi gani?. A hospital is not just buildings. Its manpower resources and the economy surrounding it. Katika dhana ya mipango miji na maendeleo ya makazi lazima vigezo vyote hivyo kuangaliwa. Kwa uelewa wangu Chato haina vigezo. Tusidanganyane.
Haka kabibi nako mbona kana kiherehere hivyo!? Kama haina sifa si waipe hizo sifa ili wanachato wapate huduma za kimkoa karibu nao atiiiiiih 😜!
 
Nakubaliana na wewe na kama itawapendeza zaidi basii,makao makuu ya mkoa yawe Nyakanazi ambapo patakua centre hata zaidi ya Biharamulo.

Tunajua kama watakubaliana na ukweli huu ni wazi watakua na nia ya dhati ya kuhudumia wananchi.
 
Tatizo lenu akina Tibaijuka na wenzako mkiwa kwenye system mnakuwa vipofu hamuoni, wenye macho (wapinzani) wakisema mnasema wanatumika na mabeberu, mkitoka kwenye system uziwi unawatoka na upofu unawakimbia.

Haya yote wakati Magufuli yupo mulikuwa hamuyaoni na mulikuwa hamuyasemi, wapinzani wakisema wanatekwa na kupigwa risasi na ninyi mnashangilia utafikri aliyepigwa risasi ni mbwa koko, Magufuli kafa ndio mnasema na kujifanya kuwa mnauchungu na wananchi.
 
Back
Top Bottom