Profesa Assad aliumia sana kuvuliwa u-CAG. Mpaka leo namwona bado ana chuki kubwa sana. Tatizo ni nini?

Ukisahakuwa CAG, hakuna nafasi tena. Labda upewe unyekiti wa bodi.
 
Umemuona wapi kama ana chuki? Umejuaje kama aliumia kuvuliwa U CAG au ni mawazo binafsi tu
 
Who is Assad?

Kuna nyakati kabla ya kuanza kumjadili mtu ni vyema ukamjua kiasi ili walau unachoandika kiwe na chembe za fikra yakinifu.

Unamzungumzia Assad ambaye inawezekana ulimjua baada ya kuteuliwa kuwa CAG?

Kabla ya hapo unajua nini kuhusu Assad?

Tuna nafasi ya kuandika lakini sio vyema kujipa majukumu ya kujifanya unamjua mtu ambaye kiuhalisia humfahamu kabisa.

Mawimbi ya kisiasa yasiwafanye vijana kuropokwa kwa kila jambo.

Unamzungumzia Assad ambaye alikuwa Associate Proffesor akifundisha
akiwa na majukumu ya kusimamia MBA dissertations kufanyia ukaguzi wanafunzi wa PhD?

Mtu wa level hizi huwezi kuwa na uwezo wa kumpima na kumjadili kwa masuala makubwa ya kitaifa, Prof Assad anajua anachoongea, ni mwanazuoni, ni mbobevu......
 
Willpower,
Ahsante sana.
 
Alinyang’anywa tonge mdomoni lazima awe na chuki! Muache azidi kusononeka Pengine itamsaidia kupunguza kitambi!
 
Kama unamwona kama ulivyosema, muulize basi.
 
MaCCM Bhana! Kazi kweli! Haishangazi kuona bado masikini kutokana na upigaji wa watawala! Hawataki hata kukaguliwa na kuwajibishwa na watu makini.
 
Midi...
Nina hakika humjui Assad ungelimjua usingeandika hayo.
Itafute historia yake Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam akiwa mwanafunzi hadi mwalimu.
Kwa mujibu wa katiba mzee. Wewe unajua historia tu? Ukasome katiba. Ukishakuwa CAG, ukistaafu huwezi kuteuliwa nafasi nyingine ndani ya JMT. Labda apewe kwa kuvunja katiba.
Nina uhakika unamtetea kwa sababu ni muislamu mwenzio na mna asili ya Tanga wote-homeboy wako.
 
Tatizo ni Magufuli kunilazimisha kustaafu kabla ya muda wake simply alifichua 1.4 trillion aliyoiba shujaa wa Kanda ya ziwa. Inauma sana. Huyu jamaa hata hakwenda msibani
 

Siyo mfano mzuri kwa kizazi kipya.
 
Yule Mzee na midevu yote ile na sijda juu akaufyata akisubiria mtu afe ndiyo aanze kulalamika dhulma.😁!

Hiyo Status ndiyo inamuumiza,CAG ni mtu mzito bwana.

Agange yajayo tu kama ilivyo kwa Dr Dau.
 
Anataka amfufue jiwe kisha aombwe msamaha na kulipwa fidia ya udhalilishaji aliofanyiwa.

Au samia akampigie magoti amwombe msamaha wa kitaifa. Kisha 2025 mama akubali kumwachia Prof Assad nafasi ya kugombea Urais kupitia CCM.
 
Thibitisha ameongea kwa chuki na jazba, kwa data na mifano mahususi tuchambue kwa kina, ili ujue ukweli uko wapi na uongo uko wapi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…