Profesa Lipumba ashangazwa na Rais Samia kumuachia mtu aliyekula njama katika wizi wa shilingi zaidi ya bilion 300 za Escrow kwa kutoa bilion 26 tu

Profesa Lipumba ashangazwa na Rais Samia kumuachia mtu aliyekula njama katika wizi wa shilingi zaidi ya bilion 300 za Escrow kwa kutoa bilion 26 tu

Duh! Miongoni mwa vitu alivyokuwa akishtumiwa JPM hapa ni kuwafunga hao akina Seth, leo maza kamtoa Seth nje, watu hao hao wameanza kumgeuka maza kwa kitendo hicho cha kumtoa Seth.

Ngoja nimshauri mama labda atasikia: Mama hakuna chochote alichofanya JPM ambacho hakikupaswa kufanywa kwa mazingira ya nchi yetu ilivyokuwa. Na ukifikiri waliokuwa anti-Magufuli wanakusifia genuinely, hilo litakuwa kosa la kwanza tena kubwa kimkakati. Wanakusifia kama Chatu amvutiavyo mbwa, na mara tu uingiapo kumi na nane zao watakurarua bila huruma. Kama walifanya hivyo kwa miti mibichi, je kwako wewe mti mkavu itakuwaje? Stuka!

Sisi tupo tu hapa tunakucheck moves zako zote.
 
Wanaomlaumu Lipumba kupambana na Maalimu Seif ndani ya CUF hawamjui vizuri Maalim. Maalim ndiye alitemsaliti Jumbe, na Maalim ndiye aliyeuza ramani kwa kukubali kuingia ndani ya Serikali ya Hussein Mwinyi licha ya Mauaji na wizi wa kutisha wa kura ambao CCM waliufanya mwaka jana.

Lipumba aliamua kugangamala bdani ya CUF baada ya kukasirishwa na kitendo cha Maalimu kuamua kumuunga mkono Lowasa akishirikiana na Juma Duni hulu akimbypass yeye kama mwenyekiti wa chama. Hiyo ni dharau na Lipumba aliamua kukunjua makucha ili apewe heshima yake!.
 
Akiongea na waandishi wa habari leo profesa Lipumba ameonyesha kushangazwa na hatua ya Rais Samia kumuachia huru mtu aliyekula njama za kukwapua zaidi ya shilingi bilion 350 za Escrow kwa kulipa shilingi bilion 26 tu, Profesa anahoji hizo pesa nyingine sasa zinakwenda wapi, na tutazipataje?

Akiongea kwa utulivu na kwa data, profesa Lipumba pamoja na kutambua baadhi ya mambo mazuriambayo rais Samia ameyafanya ndani ya siku 100 za uongozi wake, Profesa Lipumba ameendelea kusisitiza kuwa Demokrasia ndiyio msingi wa uchumi shirikishi, kwamba huwezi kujenga uchumi shirikishi wenye kunufaisha wananchi bila demokrasia.

Profesa anasema kuwa licha ya rais Magufuli kufungia shughuli za kisiasa kwa madai hayohayo ya kukuza uchumi kwanza lakini takwimu zinaonyesha kuwa thamani yote ya pesa za uwekezaji nchini ilipungua kutoa zaidi ya dola bilion 2 mwaka 2015 hadi dola milion 800 tu mwaka 2019 tena kabla ya gonjwa la korona halijaikumba dunia, Profesa anahoji kuwa kama kuzuia shughuli halali za kisiasa ndiyo kukuza uwekezaji mbona basi uwekezaji ulishuka kipindi cha Magufuli?

Profesa akaendelea kusema kuwa uwekezaji ulishuka nchini kwa sababu Magufuli alikuwa haheshimu sheria, kitu ambacho Rais Samia amekionyesha kuwa naye atakuwa siyo mheshimu sheria baada ya kutoa tangazo la kuzuia shughuli halali za kisiasa kama zinavyoruhusiwa na sheria za nchi. Kutoheshimu sheria kunaua confidence ya wawekezaji na wenye mitaji yao!

Profesa Lipumba anasema kuna uwezekanao Wahafidhina ndani ya Chama cha Mapinduzi wanamshauri vibaya rais Samia ili asikutane na wapinzani na kuchukua hatua kama hizo tunazoanza kuona akichukua.

Profesa anasema kuwa rais Samia anayo nafasi adhimu ya kukumbukwa kwa kuacha urathi (legacy) ya maana iwapo atawaachia wananchi katiba mpya, Profesa anasema kwamba kwamba hoja ya rais Samia kwamba tusubiri ajenge uchumi kwanza ndo tuzungumze habari za katiba ni ya kushangaza, ni ya kushangaza kwa sababu wao wanasema sisi tayari tuko katika uchumi wa kati, Profesa anahoji anasema au Samia anataka hadi tuwe uchumi wa juu ndo afikirie habari za katiba mpya?

Profesa Lipumba pia ametoa maoni yake pia kuhusu bajeti ya nchi, Amesema kwamba bajeti ya shilingi trilion 36 iliyosomwa bungeni haitekelezeki, anasema haoni means ambazo seriakli itaweza kupata fedha za kutosheleza bajeti hiyo

MY TAKE:
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Profesa ameongea mambo mazito sana leo na ni fact tupu!

1.Tunataka tujue ni nini hatma ya pesa za wananchi za Escrow, Habinder Seth ameachiwa , kwa nini kalipa bilion 26 tu, zilizobaki zitalipwa na nani?

2. Bila Political reforms na economic reforms vikienda kwa pamoja rais Samia atashindwa kukidhi mahitaji ya wananchi, ajiandae ama kuwa dikteta kuzidi Magufuli ili kunyamazisha watu, au aonyeshe leadership kwa kuachana na wahafidhina ndani ya CCM wanaomshauri afuate njia zilizofeli za kutoheshimu sheria na kuminya haki za makundi mbali mbali ya kijamii

3. Samia kuendelea kukumbatia baraza la mawaziri la Magufuli na baadhi ya wateule wa Magufuli akidhani kuwa atawamudu kwa kuwa yeye ni rais, bila shaka ni ishara ya kuendeleza status quo, na kwa kuwa hawa ndiyo washauri wake wakubwa basi tutegemee mambo ya Kimagufulimagufuli yakirudi polepole maana hiyo ndiyo njia pekee wanayoijua ya kulinda vyeo vyao, hawawezi kumshauri awe fair kwa wapinzani wake hawa maana fairness inahitaji kujiamini na kujenga hoja za ushawishi mbele ya wananchi badala ya ujanjaujanja tuliouona katika miaka 5 iliyopita

4. Hii ya kumuachia mtu anayetuhumiwa kula njama za kuiba mabilioni ya fedha za wananchi, na ile tuliyoishuhudia kutoka kwa mtangulizi wa rais Samia ya kufunga watu kiuonevu ni Uthibitisho usioyumba kuwa wananchi tunahitaji katiba mpya ili tuweze kuondoa abuse hii ya mamlaka, kinyume cha hapo, kwa katiba hii hata ukiujenga uchumi ukawa kama Singapore bado inatoa mwanya mchwa kuutafuna kifisadi huku wakilindwa na katiba!
Lipumba aende mahakamani
 
Cha kujiulza hizo 200 Bil zimerudishwa kweli ama ni changa la macho tu? Wadanganyika safari hii kazi mnayo.
 
Mama Samia ndio kamuachia huyo Habinder? nilidhani kaachiwa kwa vigezo vya Plea bargain? Halafu acheni roho za chuki na ukatili, kama mnaamini aliiba hela za uma serikali yenu iliyokua chini ya huyo mungu mtu wenu ilishindwa nini kudhibitisha na kumtia hatiani? Mngemhukumu na kumpa adhabu mnayoona anastahili na sio kumweka mtu mahabusu miaka minne eti uchunguzi unaendelea! mnachunguza nini miaka minne kama sio udhaifu, uzandiki, uonevu, chuki na roho za kishetani! kama mtu kaiba unahitaji miaka minne ya nini kuchunguza

Mambo mengine ya kipumbavu sana ndio maana mungu alisikia kilio chetu sisi tusiopenda chuki na ushetani

Mwacheni Mama achape kazi na mtulie kama wengine tulivyotulia wakati nchi ikiendeshwa kwa chuki na U#45$$!
 
Mama Samia ndio kamuachia huyo Habinder? nilidhani kaachiwa kwa vigezo vya Plea bargain? Halafu acheni roho za chuki na ukatili, kama mnaamini aliiba hela za uma serikali yenu iliyokua chini ya huyo mungu mtu wenu ilishindwa nini kudhibitisha na kumtia hatiani? Mngemhukumu na kumpa adhabu mnayoona anastahili na sio kumweka mtu mahabusu miaka minne eti uchunguzi unaendelea! mnachunguza nini miaka minne kama sio udhaifu, uzandiki, uonevu, chuki na roho za kishetani! kama mtu kaiba unahitaji miaka minne ya nini kuchunguza

Mambo mengine ya kipumbavu sana ndio maana mungu alisikia kilio chetu sisi tusiopenda chuki na ushetani

Mwacheni Mama achape kazi na mtulie kama wengine tulivyotulia wakati nchi ikiendeshwa kwa chuki na U#45$$!
Habinder kakiri kosa, kwa hiyo ni kweli aliktenda kosa
 
Mzigo ulitoka wewe
“Mzigo ulitoka”hilo unajua wewe

Sisi wananchi tumeambiwa hii ni cospiracy

Lipumba kasema hii ni conspiracy

Wanasheria (hujiita learned brothers) wamesema hii ni conspiracy

Ukishtakiwa kwa conspiracy ya mauaji ina maana hakufa mtu.

Angekufa ungeshtakiwa kwa mauaji, murder case!

Singa Singa alijipanga kupiga lakini hakufanikiwa, inaitwa conspiracy, kula njama.
 
Habinder kakiri kosa, kwa hiyo ni kweli aliktenda kosa
Hata ingekua mimi ningekiri kosa hata kama sina kosa... Haiwezekani mtu ukae mahabusu miaka minne eti uchunguzi unaendelea? unachunguza nini Miaka minne? na kwa nini umshike mtu wakati bado huna ushahidi? Huwezi kuniweka jela miaka minne bila hukumu wala kudhibitisha kosa langu, Kama kukiri kosa ndio njia pekee ya mimi kua huru nitakiri tu.. its that simple, na msijitoe akili na kushabikia tawala za kidhalimu zisizojali sheria wala haki za binadamu!
 
Nimemuelewa sana mzee lipumba.

Sasa hapa ilitakiwa wawepo watu wa kumsemea raisi wajibu hoja kwa hoja wanamchi tunaewa mbivu na mbichi.

Sio huyu anaongea alafu hoja inakuwa haijibiwi.

Ningekuwa mimi ndo samia nawapa teuzi hawa akina zito,mbowe,lipumba,lissu alafu nawachooraaa tuuuuu wasimamie sheria katika maeneo niliyowachagua
Sio wakati wote watu ni wabaya.ata hao uliowasema kwa jinsi mfumo wa nchi ulivyo ata wao wanaweza wasiwe na mchango mkubwa bila kwanza kufanya mapinduzi ya mfumo wetu wa utendaji kama nchi.Ata uko ccm sio viongoz wote ni wabaya lakini hawawezi kufikia matarajio makubwa kwa hali kama hiyo niliyoitaja.Sasa swala lakufanya mapinduzi yakimfumo sio swala la mtu moja mmoja mmoja.
 
Lipumba nae haeleweki mbele wapi nyuma wapi.

Leo kaongea hivi kesho ataongea lingine
 
Akiongea na waandishi wa habari leo profesa Lipumba ameonyesha kushangazwa na hatua ya Rais Samia kumuachia huru mtu aliyekula njama za kukwapua zaidi ya shilingi bilion 350 za Escrow kwa kulipa shilingi bilion 26 tu, Profesa anahoji hizo pesa nyingine sasa zinakwenda wapi, na tutazipataje?

Akiongea kwa utulivu na kwa data, profesa Lipumba pamoja na kutambua baadhi ya mambo mazuri ambayo rais Samia ameyafanya ndani ya siku 100 za uongozi wake, Profesa Lipumba ameendelea kusisitiza kuwa Demokrasia ndiyio msingi wa uchumi shirikishi, kwamba huwezi kujenga uchumi shirikishi wenye kunufaisha wananchi bila demokrasia.

Profesa anasema kuwa licha ya rais Magufuli kufungia shughuli za kisiasa kwa madai hayohayo ya kukuza uchumi kwanza lakini takwimu zinaonyesha kuwa thamani yote ya pesa za uwekezaji nchini ilipungua kutoa zaidi ya dola bilion 2 mwaka 2015 hadi dola milion 800 tu mwaka 2019 tena kabla ya gonjwa la korona halijaikumba dunia, Profesa anahoji kuwa kama kuzuia shughuli halali za kisiasa ndiyo kukuza uwekezaji mbona basi uwekezaji ulishuka kipindi cha Magufuli?

Profesa akaendelea kusema kuwa uwekezaji ulishuka nchini kwa sababu Magufuli alikuwa haheshimu sheria, kitu ambacho Rais Samia amekionyesha kuwa naye atakuwa siyo mheshimu sheria baada ya kutoa tangazo la kuzuia shughuli halali za kisiasa kama zinavyoruhusiwa na sheria za nchi. Kutoheshimu sheria kunaua confidence ya wawekezaji na wenye mitaji yao!

Profesa Lipumba anasema kuna uwezekanao Wahafidhina ndani ya Chama cha Mapinduzi wanamshauri vibaya rais Samia ili asikutane na wapinzani na kumshawishi kuchukua hatua za kuvunja sheria kama hizi tunazoanza kuona akichukua.

Profesa anasema kuwa rais Samia anayo nafasi adhimu ya kukumbukwa kwa kuacha urathi (legacy) ya maana iwapo atawaachia wananchi katiba mpya, Profesa anasema kwamba kwamba hoja ya rais Samia kwamba tusubiri ajenge uchumi kwanza ndo tuzungumze habari za katiba ni ya kushangaza, ni ya kushangaza kwa sababu wao wanasema sisi tayari tuko katika uchumi wa kati, Profesa anahoji anasema au Samia anataka hadi tuwe uchumi wa juu ndo afikirie habari za katiba mpya?

Profesa Lipumba pia ametoa maoni yake pia kuhusu bajeti ya nchi, Amesema kwamba bajeti ya shilingi trilion 36 iliyosomwa bungeni haitekelezeki, anasema haoni means ambazo seriakli itaweza kupata fedha za kutosheleza bajeti hiyo

MY TAKE:
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Profesa ameongea mambo mazito sana leo na ni fact tupu!

1.Tunataka tujue ni nini hatma ya pesa za wananchi za Escrow, Habinder Seth ameachiwa , kwa nini kalipa bilion 26 tu, zilizobaki zitalipwa na nani? (By the way Profesa kasema Habinder Seth kalipa shilingi milioni 200 tu kwa hiyo hata hiyo bilioni 26 nayo ina question mark)

2. Bila Political reforms na economic reforms vikienda kwa pamoja rais Samia atashindwa kukidhi mahitaji ya wananchi, ajiandae ama kuwa dikteta kuzidi Magufuli ili kunyamazisha watu, au aonyeshe leadership kwa kuachana na wahafidhina ndani ya CCM wanaomshauri afuate njia zilizofeli za kutoheshimu sheria na kuminya haki za makundi mbali mbali ya kijamii

3. Samia kuendelea kukumbatia baraza la mawaziri la Magufuli na baadhi ya wateule wa Magufuli akidhani kuwa atawamudu kwa kuwa yeye ni rais, bila shaka ni ishara ya kuendeleza status quo, na kwa kuwa hawa ndiyo washauri wake wakubwa basi tutegemee mambo ya Kimagufulimagufuli yakirudi polepole maana hiyo ndiyo njia pekee wanayoijua ya kulinda vyeo vyao, hawawezi kumshauri awe fair kwa wapinzani wake hawa maana fairness inahitaji kujiamini na kujenga hoja za ushawishi mbele ya wananchi badala ya ujanjaujanja tuliouona katika miaka 5 iliyopita

4. Hii ya kumuachia mtu anayetuhumiwa kula njama za kuiba mabilioni ya fedha za wananchi, na ile tuliyoishuhudia kutoka kwa mtangulizi wa rais Samia ya kufunga watu kiuonevu ni Uthibitisho usioyumba kuwa wananchi tunahitaji katiba mpya ili tuweze kuondoa abuse hii ya mamlaka, kinyume cha hapo, kwa katiba hii hata ukiujenga uchumi ukawa kama Singapore bado inatoa mwanya mchwa kuutafuna kifisadi huku wakilindwa na katiba!
Confidence wanayotaka wawekezaji wengi sio utawala wa sheria kama anavyobainisha profesa. Confidence wanayotaka ni uwepo wa hali ya kuwawezesha wao kuvunja sheria za nchi za uwekezaji bila kushikwa. Hali ya wao kuweza kuepa kodi hali ya wao kuweza kuhonga hali ya wao kuweza kufanya udanganyifu bila ugumu. Kwa hivyo wawekezaji waliyokuepo kwa magufuli hawajumlishi hao wababaishaji. Hao ndio wale nzi mzee mwinyi alisema ukifungua milango na madirisha wanaingia. Mmojawapo wa nzi ni huyo kalasinga aliyetia hasara mabilioni. Aliingia enzi ya jk. Sasa mama samia anamtoa kwa kulipa shs milioni 200 wakati kachota shs bilioni 350 Utawala wa mama utaona kalasinga na wababaishaji wa kila aina wakija kwa fujo kuwekeza.
 
Hata ingekua mimi ningekiri kosa hata kama sina kosa... Haiwezekani mtu ukae mahabusu miaka minne eti uchunguzi unaendelea? unachunguza nini Miaka minne? na kwa nini umshike mtu wakati bado huna ushahidi? Huwezi kuniweka jela miaka minne bila hukumu wala kudhibitisha kosa langu, Kama kukiri kosa ndio njia pekee ya mimi kua huru nitakiri tu.. its that simple, na msijitoe akili na kushabikia tawala za kidhalimu zisizojali sheria wala haki za binadamu!
Naona unatetea ufisadi wa ESCROW
 
Akiongea na waandishi wa habari leo profesa Lipumba ameonyesha kushangazwa na hatua ya Rais Samia kumuachia huru mtu aliyekula njama za kukwapua zaidi ya shilingi bilion 350 za Escrow kwa kulipa shilingi bilion 26 tu, Profesa anahoji hizo pesa nyingine sasa zinakwenda wapi, na tutazipataje?

Akiongea kwa utulivu na kwa data, profesa Lipumba pamoja na kutambua baadhi ya mambo mazuri ambayo rais Samia ameyafanya ndani ya siku 100 za uongozi wake, Profesa Lipumba ameendelea kusisitiza kuwa Demokrasia ndiyio msingi wa uchumi shirikishi, kwamba huwezi kujenga uchumi shirikishi wenye kunufaisha wananchi bila demokrasia.

Profesa anasema kuwa licha ya rais Magufuli kufungia shughuli za kisiasa kwa madai hayohayo ya kukuza uchumi kwanza lakini takwimu zinaonyesha kuwa thamani yote ya pesa za uwekezaji nchini ilipungua kutoa zaidi ya dola bilion 2 mwaka 2015 hadi dola milion 800 tu mwaka 2019 tena kabla ya gonjwa la korona halijaikumba dunia, Profesa anahoji kuwa kama kuzuia shughuli halali za kisiasa ndiyo kukuza uwekezaji mbona basi uwekezaji ulishuka kipindi cha Magufuli?

Profesa akaendelea kusema kuwa uwekezaji ulishuka nchini kwa sababu Magufuli alikuwa haheshimu sheria, kitu ambacho Rais Samia amekionyesha kuwa naye atakuwa siyo mheshimu sheria baada ya kutoa tangazo la kuzuia shughuli halali za kisiasa kama zinavyoruhusiwa na sheria za nchi. Kutoheshimu sheria kunaua confidence ya wawekezaji na wenye mitaji yao!

Profesa Lipumba anasema kuna uwezekanao Wahafidhina ndani ya Chama cha Mapinduzi wanamshauri vibaya rais Samia ili asikutane na wapinzani na kumshawishi kuchukua hatua za kuvunja sheria kama hizi tunazoanza kuona akichukua.

Profesa anasema kuwa rais Samia anayo nafasi adhimu ya kukumbukwa kwa kuacha urathi (legacy) ya maana iwapo atawaachia wananchi katiba mpya, Profesa anasema kwamba kwamba hoja ya rais Samia kwamba tusubiri ajenge uchumi kwanza ndo tuzungumze habari za katiba ni ya kushangaza, ni ya kushangaza kwa sababu wao wanasema sisi tayari tuko katika uchumi wa kati, Profesa anahoji anasema au Samia anataka hadi tuwe uchumi wa juu ndo afikirie habari za katiba mpya?

Profesa Lipumba pia ametoa maoni yake pia kuhusu bajeti ya nchi, Amesema kwamba bajeti ya shilingi trilion 36 iliyosomwa bungeni haitekelezeki, anasema haoni means ambazo seriakli itaweza kupata fedha za kutosheleza bajeti hiyo

MY TAKE:
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, Profesa ameongea mambo mazito sana leo na ni fact tupu!

1.Tunataka tujue ni nini hatma ya pesa za wananchi za Escrow, Habinder Seth ameachiwa , kwa nini kalipa bilion 26 tu, zilizobaki zitalipwa na nani? (By the way Profesa kasema Habinder Seth kalipa shilingi milioni 200 tu kwa hiyo hata hiyo bilioni 26 nayo ina question mark)

2. Bila Political reforms na economic reforms vikienda kwa pamoja rais Samia atashindwa kukidhi mahitaji ya wananchi, ajiandae ama kuwa dikteta kuzidi Magufuli ili kunyamazisha watu, au aonyeshe leadership kwa kuachana na wahafidhina ndani ya CCM wanaomshauri afuate njia zilizofeli za kutoheshimu sheria na kuminya haki za makundi mbali mbali ya kijamii

3. Samia kuendelea kukumbatia baraza la mawaziri la Magufuli na baadhi ya wateule wa Magufuli akidhani kuwa atawamudu kwa kuwa yeye ni rais, bila shaka ni ishara ya kuendeleza status quo, na kwa kuwa hawa ndiyo washauri wake wakubwa basi tutegemee mambo ya Kimagufulimagufuli yakirudi polepole maana hiyo ndiyo njia pekee wanayoijua ya kulinda vyeo vyao, hawawezi kumshauri awe fair kwa wapinzani wake hawa maana fairness inahitaji kujiamini na kujenga hoja za ushawishi mbele ya wananchi badala ya ujanjaujanja tuliouona katika miaka 5 iliyopita

4. Hii ya kumuachia mtu anayetuhumiwa kula njama za kuiba mabilioni ya fedha za wananchi, na ile tuliyoishuhudia kutoka kwa mtangulizi wa rais Samia ya kufunga watu kiuonevu ni Uthibitisho usioyumba kuwa wananchi tunahitaji katiba mpya ili tuweze kuondoa abuse hii ya mamlaka, kinyume cha hapo, kwa katiba hii hata ukiujenga uchumi ukawa kama Singapore bado inatoa mwanya mchwa kuutafuna kifisadi huku wakilindwa na katiba!
Kwani Lipumba alikuwa wapi wakati hizo hela zilikuwa zinabishaniwa bungeni? CCM walisema ni hela za IPTL. Seth kanunua IPTL na kachukua hela zake. Aliibaje hela benki kuu? Alivunja benki na kuondoka nazo? Huu ni usanii tu wanatufanya watoto wadogo. Wampe wenyewe hela halafu warudi mlango wa nyuma na kutuambia Seth kaiba hela!!!!
 
Kwani Lipumba alikuwa wapi wakati hizo hela zilikuwa zinabishaniwa bungeni? CCM walisema ni hela za IPTL. Seth kanunua IPTL na kachukua hela zake. Aliibaje hela benki kuu? Alivunja benki na kuondoka nazo? Huu ni usanii tu wanatufanya watoto wadogo. Wampe wenyewe hela halafu warudi mlango wa nyuma na kutuambia Seth kaiba hela!!!!
Mnufaika wa pesa za wizi naye anahesabika kuwa ni sehemu ya wizi
 
Prof na wewe tunakudai bado usifikiri tumesahau zile mlikuwa mnakwapua mkishirikiana na ofisi ya msajili mnagawaniana pale magomeni NMB.
 
Mnufaika wa pesa za wizi naye anahesabika kuwa ni sehemu ya wizi
Mlimpa wenyewe. Mbona nyie mko huru? Ingependeza sana waliosema ni hela ya IPTL, waliotoa kibali cha kutoa hizo hela, na waliozitoa kumpa wote mgeunganishwa tungesema kweli kuna justice. Mumpe wenyewe halafu mseme kaiba?
 
Mlimpa wenyewe. Mbona nyie mko huru? Ingependeza sana waliosema ni hela ya IPTL, waliotoa kibali cha kutoa hizo hela, na waliozitoa kumpa wote mgeunganishwa tungesema kweli kuna justice. Mumpe wenyewe halafu mseme kaiba?
Alikamatwa yule ili awataje wenzie, Samia kamuachia!
 
Back
Top Bottom