Profesa Ndalichako aongoza viongozi na wananchi wa Dodoma kutoa heshima za mwisho kwa marehemu John Kijazi

Profesa Ndalichako aongoza viongozi na wananchi wa Dodoma kutoa heshima za mwisho kwa marehemu John Kijazi

Tapeli kajificha kwenye mawe tena,
Yupo anaangalia clip za wale Wapambe wake wanaojiita chawa wa Magufuli.
 
Mwigulu Nchemba alimdanganya Magufuli akapewa zawadi ya uwaziri. Sasa hii Covid21 inakwenda kuwavua nguo yeye na bosi wake. Tanzania ndio nchi pekee ukiwa muongo na mnafiki anapewa cheo.
 
Boss wake aliyekuwa anaripoti kwake hajaweza kuhudhuria kutoa heshima za mwisho?
Masharti ya mganga na makafara ni mabaya sana. Halafu kila siku eti anadai anamwamini Mungu na kanisani kiti cha mbele...ushirikina mtupu.

Hata mkewe akifariki anaweza kutoa execuse na asiende japo msiba utakuwa nyumbani kwake.
 
Najiuliza yule bingwa wa maombi duani nzima yuko wapi?
Hivi kuna kitu unaweza kumpa rafiki yako wa karibu aliyefariki zaidi ya kuhudhuria safari yake ya mwisho hapa duniani?

Masikini Kijazi hakujua kama mtu waliyeshibana na mwandani wake hivi anaweza kukacha msiba wake.
 
Hivi kuna kitu unaweza kumpa rafiki yako wa karibu aliyefariki zaidi ya kuhudhuria safari yake ya mwisho hapa duniani?

Masikini Kijazi hakujua kama mtu waliyeshibana na mwandani wake hivi anaweza kukacha msiba wake.
Ataenda kuzika jamani. Sema leo kamiss kutoa heshima tu ila makaburini atakuwepo jama
 
Isaya 5:8; kisha nikasikia sauti ikisema nimtume nani na nani atakaekwenda kwa ajili yetu? Nami nikajibu nipo Bwana nitumie.

Joyce amekua isaya anatumwa sehemu ngumu.
 
Jiwe kajificha, kala kona teh teh teh!
Zenji hajaenda wala Dom hayupo
Labda yuko kwenye "handaki" lake kajikunyata tuli!
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

[emoji2307][emoji2307][emoji2307][emoji2307][emoji850][emoji850][emoji850][emoji850][emoji850]
 
Poleni watanzania wenzangu
Pole kwa rais John Pombe Magufuli kwa kumpoteza msaidizi wake
Sio rahisi kwake Mungu aendelee kutupa imani, tuchukue tahadhari na kumwomba sana yeye
tuchukue tahadhari ya nini?
 
Viongozi wa serikali na wananchi wa Dodoma wanatoa heshima za mwisho kumuaga marehemu John Kijazi chuo kikuu UDOM.

Prof Ndalichako ambaye ni waziri wa elimu ndio anaongoza watumishi na wananchi katika tukio hili.
Dr Kijazi rip atazikwa siku ya Jumamosi huko Korogwe Tanga.

Tukio hili liko mubashara TBC

Maendeleo hayana vyama!
Jiwe linatuambia hakuna corona,msiba ukitokea haliendi kuzika,linajificha,

Sent from my TECNO CD6 using JamiiForums mobile app
 
Viongozi wa serikali na wananchi wa Dodoma wanatoa heshima za mwisho kumuaga marehemu John Kijazi chuo kikuu UDOM.

Prof Ndalichako ambaye ni waziri wa elimu ndio anaongoza watumishi na wananchi katika tukio hili.

Dr Kijazi (RIP) atazikwa siku ya Jumamosi huko Korogwe, Tanga.

Tukio hili liko mubashara TBC

Maendeleo hayana vyama!
Hivi waswahili nani alitutenda?? Yaani wote tunajua huyu ndugu yetu ametwaliwa kwa Covid....we all know...yet...we are exposing our people in the name of heshima za mwisho….
 
Back
Top Bottom