Profesa Shivji ashangazwa na uteuzi wa wafanyabiashara kwenye uongozi wa TANESCO

Profesa Shivji ashangazwa na uteuzi wa wafanyabiashara kwenye uongozi wa TANESCO

Msomi wa kiwango cha kimataifa wa Tanzania, Profesa Shivji ameshangazwa na kitendo cha wafanya biashara kuchaguliwa kuongoza taasisi za umma.

Shivji anasema sekta ya umma haiwezi kuchangamana na sekta binafsi.

Sisi wengine tumeshangazwa na uteuzi wa wafanya biashara na watu wenye maslahi binafsi kwenye bodi ya TANESCO. Yule mama Balozi ndie mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Rex Attorneys ambao wanaiwakilisha Dowans na Symbion kwenye kesi ambazo TANESCO inashitakiwa na hayo makampuni halafu anateuliwa kuwa board member.

"Pamoja na kushirikiana na sekta binafsi, huwezi kuwaingiza wafanyabiashara jikoni wakupikie chakula cha umma!
Sekta ya umma na sekta binafsi hazilinganiki. Ni kweli huwezi kuendesha biashara kama idara ya serikali; pia ni kweli huwezi kuendesha serikali kama kitengo cha biashara."

Unaweza kusoma mwenyewe hapa.

Mwambie Prof. Shivji atulie tutaona mengi huko tuendako. Subiri siku Mama akimaliza muda wake ndo mtashangaa zaidi mtakaokuwepo. Huu mwendo hakuna anayeweza kuuzia hata aingie yeyote tunaelekea vita vya hamegedoni kama dunia.Hali itakuwa mbaya kuliko sasa.
 
Naomba nielimishwe kidogo, hilo lipo katika katiba au ni mawazo binafsi ya Shivji? Yule Trump aliyekuwa Rais wa Marekani ana biashara dunia nzima, Vipi nchi iliathirika na ubiashara wake au ya kule nisiyahusishe na huku kwetu wenye nyeusi ngozi?

Mbowe ni mfanyabiashara na aliwahi kugombea uraisi, vipi km angepata Prof Shivji angekuja na maoni haya pia?!!
Kule ukiwa na bishara ukigombea serikarini biashara yako unakabidhi kwa mtu akusimamie na pia kwenye tenda za serikari unaweza usipewe nafasi kwa kupitia cheo chako
 
Mkuu labda unisaidie, hivi bodi inaweza amua mambo tu kiholela bila hata waziri au Rais/vyombo vya usalama kushauri otherwise prior to maamuzi? Mbona wakiboronga huwa wanatimuliwa? Maadam wanafanya kazi ndani ya sheria na kanuni basi wakizivunja watatimuliwa tu.

2. Ni kheri uchukue wafanya biashara wanaojua soko linahitaji nini na market patterns ni zipi kuliko profesa wa UDSM ambaye anajua theories tu lakini hana practical experience ya kuendesha taasisi pana kama TANESCO!!

3. Kingine Tanzania na dunia nzima inaendeshwa kwa ubepari ama market economy lakini ni ngumu sana kuchora mstari kati ya private sector na public sector.
Mfano tunajua kuna mawaziri ambao wana biashara na hisa kwenye sekta binafsi je Mwigulu au Jenista wawe disqualified kuwa viongozi serikalini kisa wana biashara binafsi? Au double standards ni pale mfanya biashara mkubwa tu anapokua kwenye bodi ya TANESCO ila akiwa mwanasiasa ni halali ???

VERDICT: Mimi siungi mkono mafisadi kuwepo kwenye bodi ila naunga mkono 100% kujaza watu wa private sector kwenye taasisi za umma ili waweze kuongeza ufanisi. Imagine TTCL inavyoendeshwa!! leo hii wakihamisha management nzima ya Vodacom/Tigo kwenda TTCL unadhani ufanisi hautongezeka?

kikubwa ni sheria za kudhibiti bodi, manunuzi, tenda, matumizi n.k ziangaliwe na zisimamiwe 100% trust me kutakua hakuna madhara hata Seth akipewa TANESCO!!
U.M.E.M.A.L.I.Z.A👍😍
 
Ndio maana nikahoji mbona hata mawaziri ni share holders wa baadhi ya kampuni huko private sector ila hawazuiwi kuwa mawaziri/wabunge??

Ndio maana nimeuliza ni wakati gani unachora mstari wa private sector na public sector ilihali waliopo public sector zaidi ya 50% wanamiliki biashara/investments/hisa huku uraiani??
Hapo ndio tatizo lipo na ngumu kutoka hapo.
unaona kila siku yanaibuka mapya, unakuta waziri wa ujenzi ana kampuni ya ujenzi, anajipa tender kwa gharama kubwa .
Mwanasheria wa shirika ana hisa kwenye kampuni inayofanya kazi na shirika
Ni ngumu sana hii nchi kuja kuendelea
 
Yes kwenye uadilifu kuna hoja ya msingi ila sio eti kwa kuwa wapo private sector au ni wafanya biashara basi hawafai kuongoza bodi za taasisi ya umma?
Kwa mfano ungekuwa na bucha ungempa fisi aisimamie?
 
Nchi inarud kuwa kichaka cha wapigaji, tangu lini wafanyabiashara wakajali maslahi ya umma zaidi ya kutaka kutumia ofisi za umma kwa maslahi binafsi.....
 
Naomba nielimishwe kidogo, hilo lipo katika katiba au ni mawazo binafsi ya Shivji? Yule Trump aliyekuwa Rais wa Marekani ana biashara dunia nzima, Vipi nchi iliathirika na ubiashara wake au ya kule nisiyahusishe na huku kwetu wenye nyeusi ngozi?

Mbowe ni mfanyabiashara na aliwahi kugombea uraisi, vipi km angepata Prof Shivji angekuja na maoni haya pia?!!
Trump aliwaachia management zote za kampuni watoto / familia yake, hata kama ilikuwa ni theoretically lakini ni katika avoidance ya conflict of interests
 
Haiwezi kutokea hapa, kwanza ibinafsishe ndo iendeshwe kibiashara, kinyume na hapo, ni utaratibu tu wa kuwapiga waTz.

Hakuna shirika litakalomilikiwa kwa 100% na serikali lenye machineries kubwa kubwa likaweza kujiendesha kibiashara, HAKUNA.
Usiseme hakuna wakati bado haijafanyika hebu punguza pressure kunywa maji mengi alafu tafakari upya kiongozi
 
Kule ukiwa na bishara ukigombea serikarini biashara yako unakabidhi kwa mtu akusimamie na pia kwenye tenda za serikari unaweza usipewe nafasi kwa kupitia cheo chako
Ahsante sana!
 
Huyu bibi huwa hata hausiki kwenye teuzi, yeye kazi yake ni kusaini tu, nadhani ingekuwa vyema angejiuzulu kabisa maana hakuna kitu cha maana anafanya
Rubber stamp.

CS na mkwe ndo kila kitu
 
Naomba nielimishwe kidogo, hilo lipo katika katiba au ni mawazo binafsi ya Shivji? Yule Trump aliyekuwa Rais wa Marekani ana biashara dunia nzima, Vipi nchi iliathirika na ubiashara wake au ya kule nisiyahusishe na huku kwetu wenye nyeusi ngozi?

Mbowe ni mfanyabiashara na aliwahi kugombea uraisi, vipi km angepata Prof Shivji angekuja na maoni haya pia?!!
Hivi akili huwa zinakwenda mapumziko?.

Yaani kiongozi wa kiafrika umlinganishe na Marekani kweli?, Au demokrasia ya ulaya uilinganishe na Tanzania?.

Huyo Trump anajua fika akigusa maslahi ya Marekani kupitia biashara zake leo usingeandika ulichoandika.

Nadhani jifunze kutoka afrika kusini kupitia sheria zao dhidi ya viongozi kama Jacob.
 
Hivi akili huwa zinakwenda mapumziko?.

Yaani kiongozi wa kiafrika umlinganishe na Marekani kweli?, Au demokrasia ya ulaya uilinganishe na Tanzania?.

Huyo Trump anajua fika akigusa maslahi ya Marekani kupitia biashara zake leo usingeandika ulichoandika.

Nadhani jifunze kutoka afrika kusini kupitia sheria zao dhidi ya viongozi kama Jacob.
Sawa nimekuelewa lakini si kwa kuirejea afrika kusini. Niirejee nchi ambayo fisadi Zuma anafungwa miezi 15?!!! Utofauti uko wapi na kutofungwa?
 
Huyu bibi huwa hata hausiki kwenye teuzi, yeye kazi yake ni kusaini tu, nadhani ingekuwa vyema angejiuzulu kabisa maana hakuna kitu cha maana anafanya
Dah....Kama awamu ya kwanza ya Vasco....enzi za mamvi ....uzuri Vasco ni mtoto wa mjini...akamtengenezea mamvi zengwe akapigwa chini....Sasa Bibi yetu sijui itakuwaje ,🤭😂😂😂
 
Taratibu utamkubali tu!

Ni suala la muda tu
Magufuli alikuwa shetani ameondoka na damu nyingi sana za watu adhabu yake anatakiwa maiti yake imwagiwe tindikali au ichomwe na gesi ipotee kabisa kwa ardhi ya nchi hii.
 
WaTanzania hamueleweki!! Kuna thread ipo humu ikidai TANZANIA inahitaji watu wa private sector wenye exposure ndio wasimamie taasisi za umma ili ziwe na ufanisi. Leo tena oooh wafanya biashara wasiwe kwenye kusimamia hizi taasisi? Which is which.

Muda mwingine naona Magufuli alikua sahihi tu kufanya alichojisikia yeye hata kama ni mistake sababu waTZ hawaeleweki wanataka nini.
Ni hakika kabisa watu walio na exposure wanastahili lakini suala la conflict of interest lina angalizo la kipekee katika jicho la maadili
 
Back
Top Bottom