Professor Jeffrey Sachs: Marekani inapigana vita vya Netanyahu

Professor Jeffrey Sachs: Marekani inapigana vita vya Netanyahu

We bakia na ngano zako uzuri historia ya wayahudi/Israel ipo vizuri sana na haina konakona hata kidogo kwa anayetaka kuijua na kuithibitisha katika vipimo vyovyote vile. Ila kwa anayetaka kulishwa matango pori kama wewe, matango pori yamejaa kibao na ndiyo hayo unayoandika humu jukwaani mara kwa mara.
Fanya hivi iweke hapa hiyo historia ya Wayahudi ukimaliza ya Wayahudi njoo ya Israel
 
Israel sio Tanzania, pia Wapalestina wengi ni waarabu wahamiaji kutoka Jordan.
Wewe ni Mtanzania lakini nauhakika sio Mtanzania kama ilivyo kwangu mimi na kwa watu wengi katika hii nchi inayoitwa Tanzania.
 
Wewe ni Mtanzania lakini nauhakika sio Mtanzania kama ilivyo kwangu mimi na kwa watu wengi katika hii nchi inayoitwa Tanzania.
Mimi ni Mtanzania,ninachofahamu babu zangu hadi wa kizazi cha nne wamekuwepo hapa Tanzania na sijawahi kuambiwa walifika Tanzania wakitokea wapi au walifikaje. Hao Wapalestina walioko hapo Israel/Palestina wapo waliokuwa hapo Israel muda wote na wapo wengi pia wamehamia kutoka Jordan.
 
Mimi ni Mtanzania,ninachofahamu babu zangu hadi wa kizazi cha nne wamekuwepo hapa Tanzania na sijawahi kuambiwa walifika Tanzania wakitokea wapi au walifikaje. Hao Wapalestina walioko hapo Israel/Palestina wapo waliokuwa hapo Israel muda wote na wapo wengi pia wamehamia kutoka Jordan.
Ibrahim alihamia kutokea wapi ?
 
Mimi ni Mtanzania,ninachofahamu babu zangu hadi wa kizazi cha nne wamekuwepo hapa Tanzania na sijawahi kuambiwa walifika Tanzania wakitokea wapi au walifikaje. Hao Wapalestina walioko hapo Israel/Palestina wapo waliokuwa hapo Israel muda wote na wapo wengi pia wamehamia kutoka Jordan.
Umekubaliana na huo Utanzania wako wa kurithi hivyo hujaona haja ya kujua wewe ni wa kuja kutoka wapi hivyo endelea hivyo hivyo na huo Utanzania wako wa kurithi mpaka siku utakapo ona umuhimu au uhitaji wa kujua uliko toka.
 
Umekubaliana na huo Utanzania wako wa kurithi hivyo hujaona haja ya kujua wewe ni wa kuja kutoka wapi hivyo endelea hivyo hivyo na huo Utanzania wako wa kurithi mpaka siku utakapo ona umuhimu au uhitaji wa kujua uliko toka.
Hakuna umuhimu huo kwangu, hakuna watu ninaogombana nao kwa msingi huo, wanaonichukia kikabila kwamba nimevamia nchi yao au wanaodai hii sio nchi yangu na kwamba nirudi nchini kwetu.
 
Kwani kuwa wahamiaji ni tatizo au kuwa wahamiaji kutoka Jordan kunaondoa haki yao ya umiliki wa ardhi yao?
Kwa hiyo na wamarekani na wakanada hawana haki na ardhi ya nchi hizo kwa sababu na wao ni wahamiaji kutoka Ulaya?
Tatizo la Palestina sio la umilikaji ardhi tu, mgogoro mkubwa wa Mashariki ya kati sio hata kuhusu ardhi, ni utaifa wa Israel na existence yao hapo Mashariki ya kati. Tangu mwanzo Waarabu wengi mashariki ya kati walikuwa hawataki taifa la Israel, baada ya miaka mingi kupita huku wakiona hilo wazo lao limeshindwa na hakuna namna ya kuliondoa taifa la Israel ndipo ikabidi wakubaliane na hilo jambo kwa shingo upande tu huku wakiwaacha solemba Wapalestina bila muelekeo wowote.
 
Kwa kifupi sana Utawala wa Trump unaenda kuiparalyse Iran vibaya sana.
Trump anaenda kuhuisha agano kati ya Israel na US ambalo limelegalega sana kipindi cha Biden. US na Israel wanaenda kushikamana kuliko kipindi cha Biden. Migaidi ya M.E itapokea kipigo kibaya sana toka US ya Trump.
Kwa kifupi ile heshima ya US kijeshi itarudi vizuri sana chini ya utawala wa Trump.
Kuhusu Ukraine sijui.
Hapo mbona haijaongelewa Irani, huo ni uzuzu au? ,mwandishi amebalance story Kuna watu wanakuja na mahaba ya kijinga. Hili jukwaa linaheshimika
 
Tatizo la Palestina sio la umilikaji ardhi tu, mgogoro mkubwa wa Mashariki ya kati sio hata kuhusu ardhi, ni utaifa wa Israel na existence yao hapo Mashariki ya kati. Tangu mwanzo Waarabu wengi mashariki ya kati walikuwa hawataki taifa la Israel, baada ya miaka mingi kupita huku wakiona hilo wazo lao limeshindwa na hakuna namna ya kuliondoa taifa la Israel ndipo ikabidi wakubaliane na hilo jambo kwa shingo upande tu huku wakiwaacha solemba Wapalestina bila muelekeo wowote.
Israel ya zamani ilisha futwa na Roma makarne kibao yaliyo pita tatizo lilikuja pale watu walipo taka kurudisha taifa ambalo limesha kufa miaka mingi sana iliyo pita.

Kwa mfano leo hii tukitaka tufufue mataifa yaliyo anguka na kufa miaka mingi iliyo pita hii dunia haiwezi kukalika.
 
Israel ya zamani ilisha futwa na Roma makarne kibao yaliyo pita tatizo lilikuja pale watu walipo taka kurudisha taifa ambalo limesha kufa miaka mingi sana iliyo pita.

Kwa mfano leo hii tukitaka tufufue mataifa yaliyo anguka na kufa miaka mingi iliyo pita hii dunia haiwezi kukalika.
Wanaowatetea waisrael na madai ya kuitaka nchi yao ya ahadi huwa nashindwa kuwaelewa.

Masai kwa mila zao ng'ombe zote zipo kwa ajili yao. Kuna mfugaji au mtu yeyote atakuwa yupo radhi masai aje achukue ng'ombe zake kisa masai na itikadi yao?
and 100 others
 
Yoda karibu kwenye mjadala, mkuu The Boss ametisha sana kuanzisha hii mada, japo itakwenda taratibu lakini kuna mengi ya kujifunza pasipo matusi na kejeli.
Hammaz T14 Armata Bwana Utam , baba mwaju-mwajuma
Wamarekani wengi wanaanza kuamka na kuhoji kwa nini Israel anapewa sana kipaombele kuliko wao raia wa Marekani na Marekani kwa ujumla?

Hii hali Marekani wasipoitafutia dawa mbeleni itazalisha chuki nchini mwao kwa wayahudi kwa sababu wanaona nchi yao kama imetekwa na wayahudi na wao hawana mamlaka.

Tucker Carlson anaendelea kuwaumbua mijadala anayoendelea kuifanya siku baada ya siku.
 
Hapo mbona haijaongelewa Irani, huo ni uzuzu au? ,mwandishi amebalance story Kuna watu wanakuja na mahaba ya kijinga. Hili jukwaa linaheshimika
Ficha ujinga we mzee unanipangia cha kuandika wewe kama nani hasa? hivi umeelewa hata muktadha wa kinachojadiliwa usiwe mjinga kiasi hiki muda mwingine ni busara ukaacha kuandika ubakie kusoma tu.
 
Israel ya zamani ilisha futwa na Roma makarne kibao yaliyo pita tatizo lilikuja pale watu walipo taka kurudisha taifa ambalo limesha kufa miaka mingi sana iliyo pita.

Kwa mfano leo hii tukitaka tufufue mataifa yaliyo anguka na kufa miaka mingi iliyo pita hii dunia haiwezi kukalika.
Hakuna wa kuifuta Israel hata isiwepo milele na ndiyo maana hata sasa ipo. Na si mara ya kwanza wayahudi kutawanyika kwenda uhamishoni na kisha baadae kurudi Israel.
 
Wamarekani wengi wanaanza kuamka na kuhoji kwa nini Israel anapewa sana kipaombele kuliko wao raia wa Marekani na Marekani kwa ujumla?

Hii hali Marekani wasipoitafutia dawa mbeleni itazalisha chuki nchini mwao kwa wayahudi kwa sababu wanaona nchi yao kama imetekwa na wayahudi na wao hawana mamlaka.

Tucker Carlson anaendelea kuwaumbua mijadala anayoendelea kuifanya siku baada ya siku.
Wamarekani wengi ni wajinga sana pia, kuna Wamarekani wengi sana hawajui jinsi gani serikali yao ya Marekani imefaidika na wanasayansi Waisraeli na pia jinsi inaizuia Israel kuuza teknolojia za silaha kwa mataifa mengi ambayo yangezinunua kwa mabilioni ya pesa.

Kikubwa zaidi Israel ndio mshirika pekee wa kufa na kuzikana wa Marekani mashariki ya kati, ni serikali jinga sana ya Marekani itakayokubali kuipoteza Israel.
 
Wamarekani wengi ni wajinga sana pia, kuna Wamarekani wengi sana hawajui jinsi gani serikali yao ya Marekani imefaidika na wanasayansi Waisraeli na pia jinsi inaizuia Israel kuuza teknolojia za silaha kwa mataifa mengi ambayo yangezinunua kwa mabilioni ya pesa.

Kikubwa zaidi Israel ndio mshirika pekee wa kufa na kuzikana wa Marekani mashariki ya kati, ni serikali jinga sana ya Marekani itakayokubali kuipoteza Israel.
Mkuu, kwa bahati mbaya ama nzuri huwa sihofii wasiyoelewa kutonielewa.
 
Wamarekani wengi wanaanza kuamka na kuhoji kwa nini Israel anapewa sana kipaombele kuliko wao raia wa Marekani na Marekani kwa ujumla?

Hii hali Marekani wasipoitafutia dawa mbeleni itazalisha chuki nchini mwao kwa wayahudi kwa sababu wanaona nchi yao kama imetekwa na wayahudi na wao hawana mamlaka.

Tucker Carlson anaendelea kuwaumbua mijadala anayoendelea kuifanya siku baada ya siku.
Marekani inazitumia Saudi Arabia na Israel kama nchi za kukabiliana na Iran na nchi nyingine hasimu katika eneo hilo mashariki ya kati, kulinda maslahi yao ya mafuta na pia inawatumia kama kambi zao za kijeshi ili kuilinda Suez Canal.
 
Wamarekani wengi ni wajinga sana pia, kuna Wamarekani wengi sana hawajui jinsi gani serikali yao ya Marekani imefaidika na wanasayansi Waisraeli na pia jinsi inaizuia Israel kuuza teknolojia za silaha kwa mataifa mengi ambayo yangezinunua kwa mabilioni ya pesa.

Kikubwa zaidi Israel ndio mshirika pekee wa kufa na kuzikana wa Marekani mashariki ya kati, ni serikali jinga sana ya Marekani itakayokubali kuipoteza Israel.
Marekani ina wanasayansi Wayahudi na si waisirael nyinyi mtu akisha kuwa myahudi basi ni muisrael?
Marekani ana isaport Israel kwa kila namna kwa sababu ya kuitumia kuivuruga na kudhibiti mashariki ya kati basi hakuna zaidi ya hilo.
Hizo hoja za wanasayansi hazina mashiko kwa sababu Marekani ina wanasayansi kutoka karibia kila asili hapa duniani .
Vipi na Ukrain nayo ina wanasayansi wangapi ndani ya Marekani mbona ndo inateketeza pesa za walipa kodi wa Marekani mara 5 ya Israel?
Au Misri na Pakistan wana wanasayansi wangapi nchini Marekani mbona kila mwaka anatoa mabilion ya dora kila mwaka kwa nchi hizo?

Mbona wasomi na wanasayansi wa kiajemi walio jazana Marekani hamuwaiti wairan?
 
Back
Top Bottom