#COVID19 Propaganda za Chanjo ya COVID-19: Askofu Gwajima apuuzwe
Sasa kama mtu unaweza ukapatiwa chanjo ya COVID na bado uko kwenye hatari ya kupata COVID na pengine kupoteza maisha kwa COVID sasa mantiki ya chanjo ni ipi.....??
Chanjo haikufanyi usiambukizwe bali ni kinga ya ugonjwa ukiupata usidhurike,mbona pia wapo watu ambao wana chanjo ya surua but waliugua surua? wapo wenye chanjo ya TB na waliugua TB?
 
Yaani Gwajima ndio wa kupingana na Kauli ya Amiri Jeshi Mkuu? Eti Askari wasichanjwe? Eti Madaktri wasichanjwe? Eti Rais amepokea pesa ili akubali Chanjo?
Ile chanjo ni hiari na hata Rais kasema hilo. Pia Serikali imeshadeclare kwamba unachanjwa at your own risk na litakalokukuta, usimuulize mtu.

Kamsikilize vizuri Gwajima. Hapingani kindezi tu. Ametoa sababu zake ambazo wataalamu wetu wa afya wanapaswa kutolea maelezo na sio kubwabwaja huku JF
 
Kwanini mambo makubwa na ya msingi kama chanjo yanaachwa na kuzungumziwa na watu ambao hawana taaluma ya utabibu?

Halafu kwanini mtu anatisha madaktari kuwa watakufa kama wataiunga mkono hiyo chanjo wakati huyo mtu siyo daktari?, huu si ni uganga wa kienyeji!

Sitaki kuamini kuwa eti Serikali imekuwa katili kiasi hicho kwa wananchi mpaka iruhusu chanjo yenye sumu ya kuwaua raia. Hapana serikali ya namna hiyo haipo duniani.

Naomba Serikali itoe tamko juu ya upotoshaji huu unaofanywa kwa makusudi kabisa. Watanzania wengi wataaminishwa huu uongo.
 
Samahani Mwmeshimiwa, Tukichanjwa hatupati korona??
Tukichanjwa hatuvai mask???
Hata ukipata jabs tatu, lazima uendelee kuvaa mask. Ukicheza vibaya tena, corona inakutandika tena na tena. Hakuna mwenye uhakika hizo chanjo zitaisha lini nguvu (kama zinazo) ili ukachanjwe tena

Sasa sijui kazi ya hizo vaccines ni nini?
 
Ile chanjo ni hiari na hata Rais kasema hilo. Pia Serikali imeshadeclare kwamba unachanjwa at your own risk na litakalokukuta, usimuulize mtu.

Kamsikilize vizuri Gwajima. Hapingani kindezi tu. Ametoa sababu zake ambazo wataalamu wetu wa afya wanapaswa kutolea maelezo na sio kubwabwaja huku JF
Hakika mkuu tunataka muongozo na maelezo kwa wataalamu wetu wa afya kuhusu usalama wa hii chanjo miili yetu isiwe majaribio
 
Kwanza nilitamani sana huyu mtu anayejiita Askofu akamatwe na vyombo vya dola kisha ahojiwe kuhusu tabia yake ya kwenda kanisani na kwenda kuwadanganya Watanzani kua chanjo si salama wakati anajua kabisa kua kila chanjo inayotolewa na serikali imejiridhisha.

Huyu mtu anarudisha juhudi za serikali nyumba ikiwa Mhe Rais alitamka wazi kua sisi siyo kisiwa hatuwezi kujitenga na na dunia, mpotoshaji moja anasoma na kumdhihaki Mama eti anashadadia pesa za Bilgate kweli?

Eti anaombea madaktari wanahimiza na kuchanja watu wafe,huyu mtu ni chizi si mzima. Na atakufa yeye kwanza Corona tunamuombea kama yeye anavyoombea watu.

Gwajima anajifanya yeye mtu wa Mungu wakati ameiba kura za ubunge mchana kweupe dunia inajua, anapata wapi Moral authority ya kunyooshea watu vidole mtu huyu wakati anakula vya halamu? Chama tunajua kuwa aliiba kura na ushindi wake ni haramu tumemnyamazia na akiendelea tutamuumbua.

Huyu mtu ni wa kupuuza anaendelea kurudisha mapambano ya serikali nyuma, lakini akiendelea hivi akamatwe. Hawa ndio waliompotosha mzee kwa kiasi kikubwa tukajikuta tumeingia katika matatizo makubwa. Hivyo kabisa na wapuuzwe. Pesa za Bilgate ndio nini? Kwani Corona haipo?
Askofu wa wajinga.
 
Samahani Mwmeshimiwa, Tukichanjwa hatupati korona??
Tukichanjwa hatuvai mask???
Mkuu wangu.....

Kazi ya hiyo chanjo ni kuushtua mwili uzalishe KINGA ya kupambana na UVIKO ...kila binadamu ameumbwa tofauti na hata nguvu ya zile kinga zinazozalishwa/kushtuliwa huwa pia ziko tofauti(potency).....

Kwa hiyo unapochanjwa haina maana kuwa huwezi tena kuupata huo UGONJWA...mathalani ukipata tena UVIKO kwa mara ya pili ,tatu ,nne ,tano hapo MWILI WAKO utakuwa na "kumbukumbu" ya kupambana ile mara ya kwanza kwa hiyo hautaweza kupata MADHARA MAKALI Kama yale yaliyokupata mwanzo.......

Hoja ya kuvaa ama kutokuvaa mask unaweza kupata mifano tele.....mathalani tuwatazame waingereza katika mashindano ya "EURO"....baada ya kuitikia mwito wa KUCHANJWA waliruhusiwa kuingia VIWANJANI(WEMBLEY)bila ya BARAKAO(haikuwa shuruti).....

Kwetu sisi hapa ,tuko zaidi ya milioni 60(jumla na watoto)....Sasa chanjo iliyopokewa kwa kuanzia ni milioni 1 tu....hata wakichanjwa wote milioni 1 bado wengi watabaki bila ya chanjo sasa tunawakingaje HAWA?!!!

USHAURI WANGU: Kwa kipindi hiki TUVAE BARAKOA KWA "WALE" AMBAO HAWAJACHANJWA

#TujiandaeKuchanjwa
#NchiKwanza
#KaziIendelee
 
Hata ukipata jabs tatu, lazima uendelee kuvaa mask. Ukicheza vibaya tena, corona inakutandika tena na tena. Hakuna mwenye uhakika hizo chanjo zitaisha lini nguvu (kama zinazo) ili ukachanjwe tena

Sasa sijui kazi ya hizo vaccines ni nini?
Sawa mkuu.....

Mathalani chanjo dhidi ya PEPOPUNDA huwa ni moja tu?!!!
 
Ile chanjo ni hiari na hata Rais kasema hilo. Pia Serikali imeshadeclare kwamba unachanjwa at your own risk na litakalokukuta, usimuulize mtu.

Kamsikilize vizuri Gwajima. Hapingani kindezi tu. Ametoa sababu zake ambazo wataalamu wetu wa afya wanapaswa kutolea maelezo na sio kubwabwaja huku JF
Sababu kila MTU anaweza kutoa sababu, hata hivyo mambo ya corona si mlisema ni waziri ndio anapaswa kuongelea? Take it or not huyo msukuma atakuja kuwagharimu
 
Sababu kila MTU anaweza kutoa sababu, hata hivyo mambo ya corona si mlisema ni waziri ndio anapaswa kuongelea? Take it or not huyo msukuma atakuja kuwagharimu
Wewe nenda kachome. Asiyetaka kuchoma maamuzi yake yaheshimiwe. But fact is, aliyechanjwa na ambaye hajachanjwa wote watapigwa na corona tu wakicheza vibaya
 
Msimamo wa Gwajima kama mtumishi wa Mungu tangu enzi za Mwendazake ulikuwa unajulikana na ndio huo huo , msijaribu kupotosha!
 
Gwajima yeye sasa atupe solution ya Tatizo..watalaam wametengeneza chanjo kwa uwezo wao kunusuru watu wasife na kuugua..Gwajima anaipinga chanjo na kutuambia tusichanjwe huku tatizo lipo linamaliza watu kila siku, atupe basi yeye solution watu wasife au kuugua...
 
Mbona yule rabi wa kiyahudi wa kiothodox kaichana chanjo waziwazi na kusema inageuza watu mashoga ni mbinu ovu hajashambuliwa na wayahudi wenzake? Halafu hukohuko wamekazana na chanjo mpaka ya vidonge wametengeneza. Gwajima ana haki ya kutoa maoni kwa chanjo inayotiliwa mashaka dunia nzima.
 
Kwanza nilitamani sana huyu mtu anayejiita Askofu akamatwe na vyombo vya dola kisha ahojiwe kuhusu tabia yake ya kwenda kanisani na kwenda kuwadanganya Watanzani kua chanjo si salama wakati anajua kabisa kua kila chanjo inayotolewa na serikali imejiridhisha.

Huyu mtu anarudisha juhudi za serikali nyumba ikiwa Mhe Rais alitamka wazi kua sisi siyo kisiwa hatuwezi kujitenga na na dunia, mpotoshaji moja anasoma na kumdhihaki Mama eti anashadadia pesa za Bilgate kweli?

Eti anaombea madaktari wanahimiza na kuchanja watu wafe,huyu mtu ni chizi si mzima. Na atakufa yeye kwanza Corona tunamuombea kama yeye anavyoombea watu.

Gwajima anajifanya yeye mtu wa Mungu wakati ameiba kura za ubunge mchana kweupe dunia inajua, anapata wapi Moral authority ya kunyooshea watu vidole mtu huyu wakati anakula vya halamu? Chama tunajua kuwa aliiba kura na ushindi wake ni haramu tumemnyamazia na akiendelea tutamuumbua.

Huyu mtu ni wa kupuuza anaendelea kurudisha mapambano ya serikali nyuma, lakini akiendelea hivi akamatwe. Hawa ndio waliompotosha mzee kwa kiasi kikubwa tukajikuta tumeingia katika matatizo makubwa. Hivyo kabisa na wapuuzwe. Pesa za Bilgate ndio nini? Kwani Corona haipo?
tunategemea serikal ibane viongozi wangemtoa kwenye ubunge
 
Back
Top Bottom